Week Hot newz

Usilete mzaha, ananuka!

Manamuziki Remmy Ongala anakilalamikia kifo pasipo kutushauri tukikabilije: “kifo kifo kifo hakina huruma! Ukitaka kujua ubaya wa kifo, pita hospitalini, utakuta wengine wanalia. Wengine hawana miguu tena, wengine wana vidonda, wengine wana vipele, wengine wana ukurutu, wengine wamezaa watoto wamekufa shauri yako wewe kifo, kifo kwa nini unatusumbua. Tumezaliwa shauri ya kuishi. Ulimwengu bila watu siyo ulimwengu tena. Kifo we! Kifo kifo kifo hakina huruma…. Kifo ni kiboko yao!”

Ni ukweli kabisa, kifo hakina huruma, kifo kinatia uchungu, kifo kinakatisha tamaa ya maisha. Mbele ya kifo watu tunalia machozi. Ongala anakilaani kifo kiasi kwamba anaona hata magonjwa na ajali yanasababishwa na kifo. Ninakipongeza kifo kwa sababu kinatufanya watu wote tulingane! Kinamvaa kila mtu, bila kujali umri, cheo, ukuu, kabila, dini, jinsia. Kifo hakipokei rushwa. Ama kweli kifo ni kiboko kikali! Bahati mbaya na nzuri ya kifo kinawafanya wafiwa wengi wachanganyikiwe na kuanza kumlaani na kumtukana Mungu, kwa wafiwa wengine kinawakomaza kiimani na kimaadili. Hata kama tukilia na kulalalmika namna gani kifo kinabaki palepale na msimamo wake! Kifo ni suala nyeti. Je, haiwezekani kufanya appointment ya kukutana na kifo na kujadiliana naye suala hili nyeti?

Jumapili iliyopita tulitafakari “Ishara” jinsi anavyoita Mwinjili Yohana kuhusu uponyi wa upofu. Jinsi kipofu anavyozawadiwa mwanga au anavyofunguka macho. Ishara ile ilikuwa kama aina mpya ya uumbaji anaofanya Kristo. Lakini hata baada ya huko kufunguka macho, tunabakiwa bado na maswali dodoso ya kujihoji juu ya maisha. Mosi, Kristu anatufungua macho ili tuone nini au twende wapi? Pili, je, lengo la kutufungua macho ni kwa ajili ya kuona tu mambo hapa duniani halafu mwisho wake iwe nini?

Aidha, hata kama Yesu ananifungua macho na kuniwezesha kutembea vyema humu ulimwenguni, Je, maisha haya yana maana gani endapo hayana hatima? Je uzee usioisha na unaoendelea tu bila kwisha utauita ni ushindi dhidi ya kifo? Halafu hali hiyo ya uzee itaishia wapi wakati ulimwengu unaendelea kudumu tu hata bila ya mimi? Je, maisha hayo yanayoendelea tu yatakuwa na maana gani ndani yangu? Maswali kama haya ndiyo tutakayoyatafakari katika injili ya leo.

Tukitaka kuelewa vizuri hali halisi ya maisha tunayoyaishi, hatuna budi kuangalia kwa makini upi ni mwisho wake. Ni sawa na usafiri wa mguu usianze tu kusafiri kichwakichwa bila kujua wapi unaenda na umbali wake. Tunaposema mwisho wa maisha tunamaanisha kifo. Yaani, yabidi kukitafakari kifo, vinginevyo maisha yetu yote yanakuwa ni kutorokatoroka na kukikimbikimbia kifo, kwa kuogopa kukabili ukweli huo wa maisha ambao hatuna budi kuukabili.

Ni utamaduni wa binadamu ambao mara nyingi matendo ya maisha yetu yanajaribu kuepa kupanga ratiba ya kukutana na kifo. Kumbe, unaona kifo kinaendelea kututia wazimu hadi kutukosesha raha kabisa. Muziki wa Ongala unatupa hali halisi ya woga wa binadamu mbele ya kifo. Ni woga mkuu usioleta matumaini. Ama kweli “usilolijua litakusumbua.”

Ni ukweli dhahiri kwamba sisi binadamu tumeumbwa kwa ajili ya maisha ambayo hayana kikomo. Kwa hiyo ni vyema kukumbuka maneno ya mzaburi anayosema: “Ee Bwana utufundishe kuhesabu siku zetu, tujipatie hekima ya moyo” (Zab. 90:12). Tuwe na busara kutambua siyo kwa woga kwamba maisha yetu ni mafupi sana na tujaribu kuyapangilia vizuri.

Leo tumebahatika kuwa na mihadi (appointment) ya majadiliano na kifo kilichomwingia mwenzetu Lazaro. Msemaji mkuu katika mazungumzo hayo ni Yesu pamoja na wafiwa ambao ni dada wa damu wa mfu.

Tukifuatilia kwa makini mazungumzo hayo tutagundua uhondo uliomo katika ishara hiyo na kuelewa kifo ni nini na kina faida au hasara gani kwetu. Awali ya yote tuelewane juu ya matumizi ya msamiati wa neno kufufuka na tunavyolitumia kwa Lazaro. Hilo neno hapa siyo pahala pake kwa sababu neno kufufuka linamaanisha hali ya kupita toka ulimwengu huu na kuingia mbinguni kwenye maisha ya milele ya kukaa na Mungu Baba. Kwa mfano tunazungumza juu ya kufufuka kwa Yesu ikiwa na maana kwamba ameingia mbinguni na kuketi pamoja na Mungu Baba.

Kwa hiyo Yesu amefufuka yaani amepita toka ulimwengu huu na kuingia ulimwengu wa Baba. Kufika mbinguni na kumwona Mungu ni kikomo komesha na “Hakuna aliyemwona Mungu akarudi tena duniani.” Kwa hiyo kama Yesu alimfufua Lazaro ambaye alishaingia katika ulimwengu wa Baba basi alimkatishia mwenzake uhondo wa kukaa na Mungu. Kwa hiyo tunapozungumzia juu ya Lazaro, tusitumie neno kufufuliwa bali tutumie neno kuhuisha. Lazaro alihuishwa kwa sababu hakuwa ameingia katika maisha ya milele mbinguni.

Lazaro alirudishiwa uhai wake na akaendelea kuishi tena hapa duniani, ingawaje hatujui alikuwa wapi kipindi kile alichokufa na kuzikwa. Kati ya miujiza mingi aliyoyaifanya Yesu tendo hili la kuhuisha lilikuwa la pekee sana kwa watu waliolishuhudia, kwani watu walimwona Lazaro ameshafariki na kunuka. Mwinjili Yohani analichukua tendo hili la Yesu kuwa kama ishara, ili kuonesha jinsi gani Yesu ni Bwana wa maisha haya ya kibiolojia.

Hoja ya Yesu kumrudisha tena Lazaro katika ulimwengu huu wa maisha mapya ambayo hayakuwa yameguswa na aina ile ya maisha yenye malengo, yenye hatima, yaani maisha ambayo hayaishii hapa tu, bali yanaendelea na kuishia kwenye maisha ya Baba wa mbinguni. Huu ndio ujumbe mmojawapo ambao mwinjili anataka kutuletea katika ishara anayoifanya Yesu leo.

Sasa tuione kwa karibu ishara hii ya kuhuishwa kwa Lazaro. Masimulizi yanaanza hivi: “Kulikuwa na mtu aitwaye Lazaro.” Huyu Lazaro, alikuwa mwanafamilia ya namna yake. Kwa sababu katika familia hii hatuwaoni wazazi, yaani baba na mama. Tunaona tu kuna kaka na dada wawili Maria na Marta. Maana yake tunaoneshwa jumuia ya wana ndugu, au tungeweza kusema, jumuia ya kikristu. Jumuia ya kaka na dada ambao yabidi wakabiliane na hali halisi ya maisha. Hali halisi ya maisha tuionayo ni ya homa halafu kifo nk.

Katika familia hii tunasikia kuwa kaka mtu anaumwa homa kali inayopelekea kifo. Kabla mambo hayajawaharibikia, akina dada hawa wanatuma ujumbe kumtaarifu Yesu wakiwa na matumaini kuwa angemponya. Wakamwambia: “Bwana, yeye umpendaye hawezi.” Majibu ya Yesu hayaeleweki kirahisi, anaposema: “Ugonjwa huu si wa mauti, bali ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu.” Maana yake, kwa njia ya homa hii kutafumbuliwa kile ambacho Mungu anauwezo nacho na anachotaka kutufundisha. Kwa maneno haya Yesu anataka kusema kwamba yaonekana kuna ugonjwa unaopelekea kifo, na ugonjwa mwingine haupelekei kifo.

Ugonjwa unaopelekea kwenye kifo, ni ule unaoharibu maisha ya kweli ya mtu, yaani maisha yale yasiyo na mwisho. Kama vile isemavyo kwenye kitabu cha Mwanzo. Ukifanya uchaguzi wa mambo kinyume cha yale anayokuagiza Mungu utakufa: “Msile matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.” (Mwa 2:1) Kama hufanyi mambo kadiri alivyoagiza Mungu, unaharibu maisha yako halisi, maisha ya utu, ya binadamu. Huko ndiko kunakoitwa kufa-basi! Lakini kuna homa ambayo inakupeleka kwenye kifo cha kimwili tu (kibaolojia).

Kifo cha kimwili ni kile ambacho Mungu alishakipanga kwa ajili ya binadamu. Kifo cha aina hiyo hatuwezi kamwe kukikwepa. Hiki siyo kifo anachomaanisha Yesu. Ukweli Yesu aliipenda sana familia hii tena ni mapendo ya Kristu yanayotakiwa katika juimuia ya kikristu. Lakini unaona kuwa Yesu anaposikia kwamba Lazaro anaumwa, anabaki alipo na kuchelewa kwa siku mbili zaidi hadi Lazaro anakufa. Je upendo wa Mungu upo wapi pindi anatuacha tufe? Yesu anampenda Lazaro lakini anapomwacha afe anataka kutupa ujumbe. Hapa linaingia suala la ukuu wa Mungu.
Sisi tungependa kwamba Mungu aturuhusu tu tuingie paradisini pasipo kufa. Je, Mungu anaweza kuruhusu jambo hilo? Jibu ni hapana! Mungu angeweza kuruhusu hilo, lakini ingekuwa kama kutudanganya na kutuchanganya, kwamba Mungu anatupatia uhai huu ili aturudishie tena mwili huu wa kibinadamu tuendelee nao bila kwanza kuubadili kidogo. Tatizo ni kwamba, maisha yetu ya kibaolojia, yanahusu ulimwengu huu, lakini kwa vile ndani mwetu tuna maisha ya Kimungu, tunapopaswa kuingia katika maisha ya Mungu, kwa hiyo maisha haya budi yakome. Anayeshiriki maisha ya kimungu hawezi kufa, hawezi kupambana na kifo kile cha kibaolojia. Hadhi yetu ya kibidamu ipo kwa ajili ya kufa ili kuendelea na maisha ambayo Mungu ametuandalia.

Kwa kumwacha Lazaro afe, Yesu anataka kutuonesha waziwazi kwamba yeye hajafika kuzuia kifo hiki cha kibaolojia. Yesu anaacha mambo yafuate mfumo wake wa kimaumbile (wa kibaolojia). Mwanamuziki Mbaraka Mwinshehe anapowalilia wanamuziki waliofariki, anakubali kwamba kifo ni njia ya kila binadamu, anaimba: “Wanamiziki na wanamichezo wote hapa nchini Tanzania, hujiwa na majonzi kila mara tunapowakumbuka waliotutoka. Rambirambi zetu ziwafikie wanandugu. Kifo ni njia ya kila binadamu. Hatuna budi tutoe masikitiko na imani zetu kwa yao mazuri.” Kwa vile “Kifo ni njia ya kila binadamu”, Basi lengo la Yesu likatimia, kwani anapofika Bethania Lazaro alishafariki kitambo na kuzikwa siku nne zimeshapita.

Mandhali anayoikuta Yesu ni ya msiba. Hivi kulikuwa na watu wengi waliofika kuwatuliza wafiwa. Hapa unaalikwa kuvuta taswira (picha) kidogo ya hali halisi inayokuwa msibani, na ya watu wanaotuliza wafiwa. Mara nyingi watuliza wafiwa wanasema: “Poleni na msiba! Mtulizike ni mapenzi ya Mungu! Kazi ya Mungu haina makosa! Marehemu atabaki daima kwenye kumbukumbu ya mioyo yetu! Pengo lake haliwezi kuzibika tena! Sisi tulimpenda, lakini Mungu alimpenda zaidi! Bwana alitoa, na Bwana ametwaa, jina la Bwana na libarikiwe! nk.

Wakati mwingine inawekwa kanda ya muziki wa nyimbo za maombolezo. Pengine zinachapishwa hata kadi za ukumbusho na kuvaliwa sare za msiba nk. Yote hii ni kwa ajili ya kutuliza wafiwa. Lakini hata hivyo unaona wafiwa hawatuliziki sana wanazidi kuwa na majonzi na kubujika machozi. Hiyo ndiyo hali halisi inayoletwa na kifo. Kumbe ingefaa zaidi katika mazingira kama hayo kukitafakari kifo. Na katika misiba ya kikristu yatakiwa kutafakari kuhusu mwanga huu anaotupatia Kristu, yaani tumaini la ufufuko.

Hebu sasa tumfuatilie Yesu anapofika msibani anakabilianaje na mazingira haya magumu ya uchungu na huzuni? Atawatulizaje wafiwa hawa? Aidha wafiwa wenyewe wanamtazamaje Yesu aliyechelewa kufika licha ya kuambiwa hali ya mgonjwa kabla hajafa? Vituko anavyovionesha Marta kwa Yesu vinawakilisha vituko na fikra za wengi wanapokabiliwa na msiba au matatizo mazito. Mara nyingi tunasikia hata watu wa dini wanapokuwa katika matatizo, wanakosa imani, wanamkasirikia Mungu, wanakatishwa tamaa ya kuamini.

Angalia sasa Yesu anapofika pale msibani Marta anaanza kumvaa na kumgombeza bila hata ya kumwamkia: “Bwana kama ungalikuwapo hapa ndugu yangu hangalikufa.” Yesu anamwelewa vizuri tu Marta anajaribu kumtuliza kwa maneno aliyozoea kuyasikia mfiwa kadiri ya fikra za wengi ili aweze baadaye kuyatolea maelezo ya kina anamwambia: “Usijali ndugu yako atafufuka.” Kwa jibu hilo la Yesu, Marta anazidi kuchafuka nyongo tu, kwani haoni jipya kwa sababu alishakeremishwa ukweli huo kwenye imani ya mafarisayo juu ya ufufuko ujao kwa hiyo mara moja anamdakiza Yesu: “Najua ya kuwa atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho.” Ni dhahiri kwamba uelewa huu wa ufufuko ujao hauna maana yoyote.

Ufufuko utakaokuwepo sijui lini, yaani Mungu atuache tufe kisha baada ya kupita miaka mingi aturudishie tena maisha haya. Imani ya mtindo huu haiwezi kumtuliza mtu. Kutokana na udhaifu huo wa hoja ya ufufuko wa siku ya mwisho, Yesu anaongeza maneno yanayoleta maana na yanauyotuliza anamwambia kwa mkazo: “Mimi ndimi huo ufufuo na uzima.” Kumbe kama tuko gizani, basi tunahitaji mwanga toka nje unaoweza kutuangaza. Kujijulisha namna hii kwa Yesu kunafanana na kule alikomwambia yule Msamaritana pale kisimani: “Mimi ninayesema nawe, ndiye.”

Ni mimi niliye hapa ndiye ninayeweza kuhuisha mambo, ninayeweza kuwatuliza, wale waliokata tamaa ya maisha. Hapa mpangilio wa maneno unaanza na ufufuo halafu Uzima. “Mimi ndimi ufufuo na uzima”. Yaani kwanza kuwekwa huru halafu kuishi milele. Ufufuo ndiyo kitu cha muhimu zaidi katika maisha yetu ya sasa. Ufufuo ni mwito hasa kwa walio wazima kimwili halafu kwa waliokufa. Sisi tumeshakuwa wafufuka anavyosema Paulo: “Hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu, alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, mmeokolewa kwa neema. Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu.” (Efeso 2:5-6). Ni kwamba mtu huyu amepata maisha au uzima ambao hauwezi kumtoka kutokana na kufa kibaolojia.

Maisha ya mbinguni ni bora zaidi kuliko maisha ya duniani. Jaribu kupata picha ya watoto pacha walio bado tumboni mwa mama. Humo tumboni watoto hao wanalishwa chakula toka mwilini mwa mama yao. Inapotokea kwamba mmoja anatangulia kuzaliwa, yule aliyebaki tumboni anaweza kuwaza kwamba mwenzangu amekufa. Lakini yule aliyezaliwa na kuona mwanga anaufurahia uso wa mama yake ambao kabla yake hakuujua ulivyo ingawaje mama yake huyo ndiye aliyekuwa anampa uhai alipokuwa bado tumboni. Sasa anauona laivu uso wa mama yake. Vivyo hivyo Yesu anaposema anayenisadiki mimi hatakufa anamaanisha kwamba baada ya maisha haya kuna maisha mengine utakayoyaona laivu.

Dada mwingine, Maria naye anafika kwa mtindo wake. Yeye anafika huku analia. Yesu anapomwona Maria analia anamwelewa kwamba hayo ni mapato ya kifo ndiyo yanayofanya mtu alie. Lakini kilio cha Maria na cha waombolezaje wengine ni kile cha sauti na cha kukata tamaa. Tofauti na kilio cha Yesu baada ya kuuliza: “Mmemweka wapi?” Yesu analia, lakini kilio chake hakikuwa cha kukata tamaa bali yasemwa yalikuwa yanamtoka tu machozi. Kwa hiyo hata mtu mwenye imani yatamtoka tu machozi mbele ya kifo. Baada ya kuelewana hivyo juu ya ufufuo na uzima, sasa Yesu anaanza kufanya vitu vyake ambavyo ndiyo ishara inayoonesha kuwa yeye ni ufufuo na uzima. Hapa Kifo kinakatwa kilimilimi.

Yesu anaagiza kuliondoa jiwe lililofunika pango alimowekwa mfu. Kuliweka jiwe juu ya pango maana yake ni kuliziba. Kitendo hiki cha kufunika kinatafsiriwa kuwa ni cha kusahau. Kwamba kesi ya mtu aliyekufa imeisha. Hebu ifunike! “Funika kikombe mwanaharamu apite”. Kumbe Yesu anaagiza: “Liondoeni jiwe.” Kwa sababu haina maana kuufunika kwa jiwe ulimwengu wa wazima katika shimo la “sahau” na kumtenga na ulimwengu wa watu walio paradizini. Martha anapata bado shida ya kuelewa maana ya kutoa jiwe lile wakati mambo yameishaharibika kabisa na yananuka.

Bado ana mashaka, akdhani kwamba mambo yataweza kumzidi Yesu. Anadadisi: “Ananuka kwa vile amekaa humo siku nne.” Marta hajui kwamba kunuka ndiyo pia ni hali halisi ya kifo. Yesu anamwambia: “Marta kama unasaidiki, utaona utukufu wa Mungu.” Baada ya kufunguka macho yabidi kuangalia mambo kwa undani zaidi na kuona mambo ambayo macho ya kawaida hayawezi kuyaona. Maana yake, kama unasadiki utaweza kuona.

Toka hapa sasa kunafuata mahitimisho ambayo ndiyo uhondo wa Injili yote ya leo. Yesu analia kwa sauti kuu: “Lazaro njoo huku nje.” Hiyo sauti ni kilio cha ushindi. “Mfu akatoka,” huyo anatamkwa jina la mfu na siyo kwa jina la Lazaro. Mfu alitoka aliyeviringishwa sanda miguuni, mikononi na uso umefungwa leso. Mfu huyo hatuoni wala sisi hatumwoni. Ameviringishwa nguo na kufunikwa leso kama vile mtoto mchanga aliyezaliwa.

Hapa ni dhahiri kwamba tunaletewa fundisho muhimu sana la kiteolojia, kwamba hata Lazaro amezaliwa toka tumbo la kaburi. Ni ukweli usiopingika kwamba Yesu amemhuisha Lazaro. Mwinjili anataka kurudia tena ishara ambayo Yesu ameitoa katika kitendo hiki cha kumfufua Yesu kuwa ni Bwana wa maisha, Bwana wa uzima siyo uzima huu wa kibaolojia wa kurudishia uhai Lazaro, la hasha, bali mwuujiza huo tuuchukulie kuwa ni ishara au kichokoo tu cha kutuonesha au kutushirikisha uzima mwingine ambao Yesu amekuja kutuletea hapa ulimwenguni. Mfu anakuwa mzima anazaliwa upya na anabaki katika hali ya mfu ameviringishwa vitambaa. Yaani mfu ambaye Yesu anamwita toka kaburini (pangoni) anabaki bado na alama zote za mzikwa wa kaburini. Kisha Yesu anasema: “Mfungueni, mkamwache aende zake.” Usemi huu nao ni muhimu sana. Tamko hili ni fumbo, kwani Yesu hasemi, “twendeni naye pamoja anakoenda huko”.

Baada ya tamko hili la Yesu na kumfungua mfu na kumwacha aende zake, tungetegemea kuona vituko vingine husika vikiendelea kuorodheshwa. Yaani tungemtegemea Yesu anaendelea kutoa maagizo yafuatayo: “Mfungueni halafu akisha jiweka sawa, ataweza kuja kutusimulia mambo yalivyokuwa kuzimuni alikokuweko siku hizi nne. Kisha tutaenda kumnywea na kufanya sherehe. Ratiba nyingine itaendelea jinsi mambo yatakavyojitokeza.”

Pengine hata Lazaro mwenyewe angeenda kumkumbatia Yesu ikiwa kama ishara ya shukrani. Lakini kumbe Yesu anasema tu “mfungueni na mkamwache aende zake.” Lazaro anaondoka na kwenda zake kimyakimya bila ya kuwahamasisha, au kuwachangamsha waliokuwa wanahuzunika.

Ndiyo mwisho! Ndivyo anavyotutendea Mungu, anayetuumba, anatuacha mahuru tuendelee na maisha bila kutufunga. Hii ni ishara kubwa katika maisha yetu ya kidini, kutomfunga Mungu katika imani, bali kumwacha huru. Ishara hiyo pia ni mwito kwa ndugu wanaolia na kuhuzunika kwa kuondokewa na ndugu, rafiki na mpenzi wao, lakini utakuwa ni ubinafsi mkubwa sana kumshikilia na kumtaka marehemu aendelee kubaki nao.

Yabidi kumwacha “kumfungua na kumwacha aende kwa raha zake.” Ingependeza sana kutanguzana naye kwenda pamoja huko aendako. Kumbe haiwezekani! Sisi tubaki tu kumsindikiza kwa jicho la imani katika hatua mbalimbali za maisha yake. Tumwache aende kwa uhuru wake wote. Ama kweli mwisho wa maisha ni mwanzo wa maisha.

Padre Alcuin Nyirenda, OSB



Kanisa linapania kushiriki kikamilifu katika kudumisha amani na majadiliano ya kidini huko Mashariki ya Kati!

Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu jioni tarehe 7 Aprili 2014 amekutana na kuzungumza na Mfalme Abdullah wa Pili wa Yordan pamoja na ujumbe wake, ambao walipokelewa na Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican, aliyekuwa ameandamana na viongozi kadhaa kutoka Vatican.

Baba Mtakatifu na mgeni wake wamefanya mazungumzo yao kwenye Hostel ya Mtakatifu Martha, iliyoko mjini Vatican. Mazungumzo haya kadiri ya taarifa ya Padre Lombardi yamefanyika wakati viongozi hawa wawili wakiwa wanaendelea kupata chai ya jioni na kwamba, yamedumu kwa takribani dakika arobaini na tano.

Safari ya kikazi iliyofanywa na Mfalme Abdallah wa pili mjini Vatican ni sehemu ya maandalizi ya hija ya kichungaji ya Baba Mtakatifu Francisko huko katika Nchi Takatifu, ambako atapata fursa kwanza kabisa ya kutembelea na kuzungumza na wananchi wa Yordan na kwamba, wananchi wengi wa Yordan wanasubiri kwa hamu hija hii ya kichungaji, itakayomwezesha Baba Mtakatifu kujionea hali halisi ya wananchi wa Yordan.

Kwa upande wake, Baba Mtakatifu ameonesha utashi na nia ya kimaadili ya kutaka kushiriki kikamilifu katika mchakato unaopania kupata amani ya kudumu huko Mashariki ya kati pamoja na kudumisha majadiliano ya ya kidini, kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya wengi. Mwishoni, Baba Mtakatifu amesalimiana na wajumbe waliokuwa kwenye msafara wa Mfalme Abdallah wa pili wa Yordan



Unashangaa nini? Tazama!

Ninatumaini sisi sote tumewahi kuusikia msemo huu: “Funguka macho, Angalia!” Usemi huu hauna maana kwamba mmoja ni kipofu au amefumba macho yake na sasa anaambiwa ayafungue ili aweze kuona, la hasha bali ni “Kufungua Macho” ili kuweza kuona vyema mambo katika maisha. Mathalani, neno hili linaweza kutumika na wazazi wanaomwonya mtoto wao wa kike anayempenda mvulana mwenye matatizo labda ya kubugia unga, au wizi au hana maisha mazuri au mvivu na hataki kufanya kazi.

Mama mtu anaweza kumwangalisha bintiye na kumwambia: “Mwanangu, funguka macho. Je, huioni hali halisi ya maisha ya huyo kijana unayempenda? Angalia sana usije ukajitatiza. Utadhani umepata kumbe umepatikana!” Kwa hiyo, kuna upofu unaotibiwa hospitalini na mganga wa macho, lakini pia kuna upofu mkubwa unaokupotezea mwelekeo wa maisha, upofu unaokuzuia usiweze kuona hatari iliyo mbele unakoenda katika maisha, upofu ambao unakufanya usione na kuchukua uamuzi gani unaofaa wa kufuata. Maisha kwako yanakuwa giza. Unabaki kama kipofu unayeegemea ukuta, au mkongojo, au kuwategemea wazazi. Wakati kumbe mtu anayeona ni huru hamtegemei mtu yeyote yule.

Leo tutapambana na mganga mkuu wa tiba ya upofu wa macho wa aina hii ya pili. Tutapata mwongozo wa kujikwamua na upofu wa maisha kijumla. Mwinjili Yohane anatuletea kituko cha uponyi wa kipofu wa macho kwa namna kama ya tamthilia au mchezo wa kuigiza ili kutufafanulia vizuri maana ya upofu huo wa maisha na uponywaji unaofanywa na Yesu.

Yesu anajionesha kama mganga wa macho, mponyi wa upofu unaotuwezesha kuona vyema njia tunayosafiri katika maisha na kuchagua vyema maisha kadiri ya thamani zitakiwazo. Kuna usemi wa Yesu anaosema: “Pindi niko duniani, mimi ni mwanga wa ulimwengu. Yesu ni jua linalomeremeta na kutuangaza sote.” Kutokana na ukweli huo, Injili ya Yohane inafungua kwa neno hilo la mwanga: “Kulikuja nuru amtiaye nuru kila mtu, akija katika ulimwengu. Yohane mbatizaji hakuwa nuru, bali alikuja kuishuhudia tu ile nuru yenyewe.” (Yoh 1:7-9).

Kristo ni mwanga unaotuwezesha kuona vyema maisha kwa namna inayoipa maana ya maisha yetu. Injili hii daima ilikuwa inatumika jumapili ya leo katika safari ya wakatekumeni watakaobatizwa Jumamosi Kuu. Baada ya kuibuka toka kwenye kisima cha ubatizo wakawa wanaitwa walioangazwa, wanaomeremeta. Yaani wale waliokuwa wamepata zawadi ya mwanga toka kwa Kristu! Waliofunguliwa macho juu ya kuuona vizuri ulimwengu.

Yawezekana kabla yake walikuwa wevi, wadanganyifu, wachakachuaji, wala rushwa, lakini bila kujitambua kuwa ni vipofu wakapotea njia, wakawa wanapuyanga porini tu hata hawajui wanakoelekea. Sasa wanafuata Injili ya Kristo inayowafungua macho yao. Hali ambayo tunaweza kuipata hata sisi, tunapokosea, kufanya uchaguzi usiofaa katika maisha, anafika mmoja na kutufungua macho, anapotuambia “Angalia, Kaa chonjo, Jihadhari,” hapo tunashtuka kwani tungekosea halafu mapato yake yangekuwa mabaya. Huo ndiyo ufunguo wa kuelewa fasuli ya Injili ya leo.

“Yesu alipokuwa anapita alimwona kipofu tangu kuzaliwa.” Hatuambiwi jina la mtu huyo, bali anatajwa tu kuwa ni kipofu, anaweza kuwa mtu yeyote yule. Maana yake hiyo ni hali ya kibinadamu, ya mtu yule ambaye hajakutana na Yesu, amezaliwa kipofu. Mtu wa namna hiyo, hawezi hata kuhitaji mwanga au nuru, kwa sababu haufahamu ulivyo kwa sababu hajauona. Wakati mwingine tunaweza kusikia watu wakisema: Mume wangu haendi kabisa Kanisani kusali, na hana hata wazo la kusoma biblia au kusikiliza mazungumzo ya mambo ya dini. Au unakutana na mtu, anakuambia “mimi sina hamu kabisa na ukristo, yaani sina interest kabisa!”

Hilo si jambo la kushangaza, kwa sababu Mtu ambaye hajauona mwanga, (kipofu) hajakutana na Kristu, itakuwa ni kumdai mno mtu wa namna hiyo (kipofu) atamani kuutazama ulimwengu kwa namna tofauti. Kwa sababu hana wazo, hawezi kufikiri namna nyingine, hawezi kujua, ni kitu gani hiyo nuru. Mtu aina hiyo ni kipofu anahitaji kufunguka macho. Ni sawa na mtu anayekuja kugundua uhondo wa muziki, uhondo wa riadha, uhondo wa kufanya hija, uhondo wa kusoma hesabu, uhondo wa siasa, nk. Kabla yake hakuwa anashabikia chochote, sasa utamkuta anafurahia kwa sababu kuna mtu amemfungua macho – anakuwa limbukeni hana siri.”

Wanafunzi wa Yesu wanapomwona huyo kipofu wanakuwa kama waafrika mbele ya matatizo, wanaanza kumtafuta mchawi, wanamwuliza Yesu: “Rabi, ni yupi aliyetenda dhambi, mtu huyu au wazazi wake hata azaliwe kipofu?” Hebu angalia kwa makini jibu la Yesu ni tofauti kabisa na fikra zetu. Anajibu kifupi tu: Hiyo ni hali halisi ya maisha. Kwamba mtu anazaliwa hivyo. “Hiyo ni kazi ya Mungu.” Mwanga huu unatoka mbinguni, siyo jambo analoweza kulileta binadamu. Yawezekana akaendelea kuwa kipofu hivyo hadi kufa, au kuweza kubahatika kukutana na Kristu anayeweza kukufungua macho kwa neno lake.

Yesu hataki kusikia watu wanazungumza juu ya dhambi kama inavyozoeleka kusikia kwamba, dhambi imeingia duniani kwa njia ya wazazi wetu wa kwanza na hivi sisi sote tuko katika dhambi, la hasha, bali sisi tunazaliwa hivyo. Yesu anatualika kufunguka macho, kuangalia nuru ya Mungu daima, na ni yeye pekee anayeweza kutufungua macho na kuona ulimwengu kwa namna ya pekee.“Baada ya kusema hayo, Yesu alitema mate chini na kufanya tope kwa yale mate. Kisha akampaka kipofu kope za macho”. Tendo hilo ni muhimu sana, kwa vile inarudiwa kusemwa mara tano katika fasuli ya Injili ya leo Yesu alitema mate chini na kufanya tope kwa yale mate.

Tumeshasikia mara nyingi katika Agano la kale, juu ya tope, ya pumzi ya Mungu na mate. Hayo yanamaanisha uhai au uzima. Kitendo kilichofanyika cha Mungu alipomwumba Adamu. Yesu anakirudia kitendo hicho ikiwa kama ni uumbaji upya wa mtu mpya. Sasa mtu mpya anazaliwa kutokana na mwanga wa Kristu. Yaani sasa mtu anaishi kama inavyotakiwa kuwa binadamu. Anajua anakotakiwa kwenda kisha anamtuma huyo kipofu na kumwambia: “Nenda kanawe katika birika ya Siloamu, maana yake aliyetumwa.” Wataalamu wanasema Siloamu maana yake siyo aliyetumwa, neno kutumwa lingekuwa shaluak ambacho ni kisima pekee kilichokuwa katika mji ule wa Yerusalemu.

Hapa kwa neno hilo mwinjili anataka kuonesha maji yale ambayo yanamfungua macho, kama maji ya ubatizo, na yule ambaye anampa mwongozo wa kuyapata hayo maji yaani Roho wa Kristu, yaani maisha ya kimungu ambayo yanakuwezesha kuona hali halisi ya maisha. Baada ya kutoka kisimani kunafuata mfululizo wa vituko vinavyomsibu kipofu huyu aliyepona. Hiyo ni sawa na safari ya mtu anayeona mwanga baada ya kufunguliwa macho na Yesu. Mtu anayesafiri peke yake bila kutegemezwa na Yesu. Safari ya kipofu huyu ni sawasawa na safari yetu wakristu kuelekea mwanga. Unaalikwa kutanguzana kipofu huyu ujifunze kutembea vyema baada ya kupata mwanga wa ubatizo ili kuelekea kwenye mwanga halisi wa maisha.

Kulikuwa makundi kadhaa ya watu waliokuwa wanahoji na kuujadili uponyi wa kipofu huyu kwa namna yao. Kikundi cha kwanza alichopambana nacho huyu kipofu ambaye sasa anaona ni cha majirani waliokuwa karibu sana naye: Watu hao wanaonekana sasa kutokuwa na uhakika kama wanayemwona ndiye aliyekuwa kipofu mwombayala maskini au la, wanaulizana: “Je! Huyu siye yule aliyekuwa akiketi na kuomba? Wengine wakasema ndiye. Wengine wakasema, La! lakini amefanana naye.”

Tunaweza kujiuliza, je, kumetokea nini hadi Mtu huyu hatambulikani tena na jirani zake alioishi nao. Hiyo ndiyo historia ya maisha yetu, hiyo ni hali halisi ya maisha yetu. Historia ya wale waliokuwa vipofu ambao walikuwa wanatembea bila kuelewa wachukua uchaguzi gani mzuri wa maisha. Wanapofunguka macho katika nuru ya Kristu, wanakuwa watu tofauti kabisa hadi kutokutambulikana tena na watu aliozoeana nao kabla.

Yawezekana mtu alikuwa anathamini mambo mengine kabisa ya duniani, magari, nyumba, raharaha, lakini sasa amegundua thamani nyingine bora zaidi za maisha. Labda alikuwa mpiga rushwa, au mchakachuaji, mdanganyifu, sasa ni kinyume chake. Sasa amefunguka macho. Hivi unapokutana na wanaomfahamu, wanaweza kubishana wenyewe kwa wenyewe. Ni yule au siyo yule tunayemfahamu? Maana yake mtu aliyeangazwa kweli, anakuwa tofauti kabisa kwa sababu yuko katika safari kuelekea mwanga.

Wanapomwuliza Kipofu huyo anathibitisha kwamba ndiye: “Mimi ndiye”. Watu hao wanataka kujua “Kulikoni” wanamwuliza “Yalifumbukaje”. Naye anarudia kueleza ilivyokuwa: Mtu yule aitwaye Yesu alifanya tope akanipaka macho akaniambia, Nenda Siloamu ukanawe; basi nikaenda na kunawa, nikapata kuona”. Inakuwa vizuri sasa hata mimi ninapoulizwa swali la mtindo kama huo imekuwaje hadi uwe mkristu, ulipatapataje wito wa ukristo, wa utawa, wa ukatekista au upadre?

Kipofu anaendelea na safari yake ya maisha. Mara anakutana na kikundi cha pili cha watu ambao ni viongozi wa kanisa. Yaani watunzao mapokeo yadini na ambao tungetegemea wangestaajabia kumwona aliyekuwa kipofu sasa anaona. Kumbe hao wanachukizwa na mtu aliyemfungua macho kipofu huyu. Kikundi hicho cha pili siyo cha wengine bali ni cha Mafarisayo: Chuki yao inakuja pale wanapotambua kwamba, huyu kipofu kabla yake alikuwa anafuata amri zao, alikuwa anafanya wanachotaka wao, alikuwa amewategemea kumbe sasa amefunguka macho, anaona mambo kwa namna tofauti.

Hao ni maadui wa nuru, wanawawakilisha wale walio wafungwa wa fikra zao, dhana zao, mawazo yao juu ya Mungu. Wamefungwa katika utamaduni na mapokeo yao na hawataki kubadili kitu. Hapo wanasema mtu aliyemponya kipofu siyo mtu wa Mungu kwani hashiki sheria ya sabato ya mapokeo yetu. Hivi wanamhoji: “Mafarisayo nao wakamwuliza tena jinsi gani alivyopata kuona.” Naye kipofu anatoa majibu yaleyale aliyotoa mwanzoni: “Alinitia tope juu ya macho nami nikanawa, na sasa naona.” Wanapobishana wao kwa wao juu ya mtu huyo wanagawanyika na wanashindwa kupata jibu wanalolitaka, wanamwuliza tena kipofu mara ya pili, “Wewe wasemaje katika habari zake kwa vile alivyokufumbua macho?” Kipofu anatoa jibu linalompa cheo zaidi Yesu: “Mimi kwa binafsi yangu naona kuwa mtu huyu: ‘ni nabii’”.

Kikundi cha tatu ni wazazi wanaoitwa na wafarisayo na kuulizwa maswali: Wazazi wanamfahamu vizuri sana mtoto wao. Viongozi wanawauliza wazazi “Huyu ndiye mwana wenu, ambaye mnasema kwamba alizaliwa kipofu? Amepataje, basi kuona?” Wazazi wanaruka swali la pili na kulijibu la kwanza: “Tunajua ya kuwa huyu ndiye mwana wetu, tena ya kuwa alizaliwa kipofu; lakini jinsi aonavyo sasa hatujui. Wala hatujui ni nani aliyemfumbua macho. Sisi hatumo katika suala la kufunguka kwake macho. - Mwulizeni yeye mwenyewe, yeye ni mtu mzima, atajisemea mwenyewe.” Yaani alizaliwa kipofu, na kuna mwingine amemfungua macho”.

Hapa unaona kama vile wazazi hawa wanaogopa, wana woga wa kuponywa. Wanamwogopa kijana anayeona mambo kwa namna ya pekee kuliko namna ile waliyomfundisha wao. Wazazi wana wasiwasi, kwa sababu wale ambao hawafuati mapokeo wanaweza kufukuzwa toka hekaluni. Hapa unaweza kuwakumbuka watu ambao wametoa mchango mkubwa sana katika jamii, katika siasa lakini hawapokewi vizuri. Mwanga ni hatari, unagombanisha watu.

Kinakuja kikundi kingine cha nne ambacho ni kilekile tena cha mafarisayo, wanamwambia yule kipofu: “Mpe utukufu Mungu.” Ni sawa na kusema: “Umshukuru Mungu”. Maana yake, wewe kiri tu kwamba umekosea, kisha sisi tutajitahidi kuweka mambo sawa. Hasahasa kurekebisha kufuru hii iliyojitokeza kwa sababu “Sisi tunajua ya kuwa mtu huyo ni mwenye dhambi.”

Hapo kipofu anaanza kuitetea hali halisi anayojisikia kuwa nayo, yaani hali ya kuona mwanga mpya wa Kristu aliyemfungua macho hayo. Anawapa ukweli wao: “Kwamba yeye ni mwenye dhambi hilo mimi silijui. Najua neno moja, kuwa mimi nalikuwa kipofu na sasa naona.” Hapo tunajifunza kwamba yabidi kwa haki yote kujiacha kutetewa na matendo na siyo kwa sheria. Unaona wazi kuwa mtu huyu aliyepata mwanga sasa anazidi kuwa na uhakika zaidi wa mambo na kujiamini zaidi.

Wanapomwulizia tena jinsi alivyofumbuka macho wanapomwuliza: “Alikutendea nini? Alikufumbua macho jinsi gani?” Wanataka aendelee kujibu, ili waweze kutafuta mwanya wa kumkosoa. Hapo yule kipofu anawashtukia na kuwapa “makavu laivu”. “Nimekwisha kuwaambia, wala hamkusikia; mbona mnataka kusikia tena? Yawezekana labda na ninyi mnataka kuwa wanafunzi wake?” Ni kitu cha kawaida kutoa majibu haya makavu. Na kutoka hatua hii sasa wanaanza kutupiana lugha za kebehi na matusi ya rejareja. “Wewe ndiye mwanafunzi wake, sisi tu wanafunzi wa Musa. Sisi tunajua ya kuwa Mungu alisema na Musa; bali yule hatujui anakotoka.” Mafarisayo daima wanakimbilia kusema: “Sisi tunajua” na huyu kipofu daima anasema “Mimi sijui”. Watu wanaofikiri kwamba daima wanajua yote hawawezi kupata mwanga, watabaki daima kuwa katika giza.

Wafarisayo wanaposema kwamba hawajui anakotoka Yesu, kipofu anawakebehi tena na kuwaambia: “Hii ni ajabu! Ninyi mnaojua mambo yote, lakini hamumjui anakotoka huyu aliyenifumbua macho!” Ni kama anawaambia: “Tunakichojua sisi wenyeji yaani watu wa kawaida ni hiki kwamba, mcha Mungu (anayemwogopa Mungu) daima anasikilizwa na naye Mungu.

Aidha, haijawai kusikika kwamba kumetokea mtu anayafumbua macho ya mtu aliyezaliwa na hali ya kipofu. Asiyetoka kwa Mungu hawezi kutenda neno lolote.” Kutoka kwenye hali ya kebehi hadi wanafikia kukashifiana na kutoleana lugha chafu. Hawa wafarisayo, wanashindwa kuhimili vishindo wanaamua kumfukuzia nje. Ni namna dhahiri ya kutenda ya mtu asiyetaka kufunguka macho na kuuona mwanga. Ukifuatilia mazungumzo haya utaona jinsi yalivyopanuka kidogokidogo kutoka kwenye ushawishi, kebehi na dharau matusi hadi kuchefuana nyongo na mwisho kumfukuza mtu. Ndiyo mtindo wa kufanya mambo mtu asiyetaka kufunguka macho. Kipofu anaondoka, anajiona kuwa huru anatoka nje.

Katika sehemu ya mwisho ya Injili tunasikia kwamba yule kipofu akakutana tena na Yesu. Lakini ukweli ni kwamba Yesu alimtafuta yule kipofu ndipo walipokutana nje walikofukuziwa wote wawili. Yesu anaenda kumtafuta mwenzake ambaye naye amefukuzwa kama yeye. Anajua kuwa yule anayepokea mwanga, hawezi kutazamwa vyema na watu wa mapokeo. Yesu akamwuliza: “Wewe wamwamini Mwana wa Mungu?” Yaani wewe unajiaminisha kweli kwa mtu aliyekufungua macho? Yule kipofu anajibu “Ni nani, Bwana, nipate kumwamini?”. Yesu anamjibu: “Umemwona, unayesema naye ndiye.” Mtu aliyeangazwa hahitaji tena uwepo wa mwalimu. Alikuwa ameongozwa katika safari yake na ile Injili inayoendelea kumfungua macho. Ndugu yangu, katika safari yako ya maisha funguka macho uongozwe na nuru ya Kristo yaani Neno lake.
Alcuin Nyirenda, OSB.


Tafakari ya neno la Mungu, Jumapili ya Nne ya Kipindi cha Kwaresima

Niko nawe tena katika kipindi tafakari masomo Dominika ya IV ya Kipindi cha Kwaresima, ambapo tunaalikwa kuwa watu wa mwanga. Katika somo la kwanza tunakutana na uteuzi wa kiongozi atakayeongoza taifa la Israeli.

Mpendwa mwana wa Mungu, jambo hili linatokea miaka 1000 kabla ya Kristu wakati ambao Waisraeli walikuwa katika shida na taabu. Ili kuweza kuondokana na taabu hizi walilazimika kutafuta kiongozi atakayewasaidia kuwaongoza ili waweze kupata ushindi toka Wafilistini. Kwa njia ya Samueli Mungu anaonesha kijana mmoja toka Betlehem katika ukoo wa Yese, ambaye atapakwa mafuta kwa ajili ya kuwa mfalme wao.

Basi Nabii atakwenda mpaka Betlehem na kumwambia habari hii Yese ya kwamba mmojawapo wa wanawe amechaguliwa na Mungu kuongoza taifa la Israeli. Yese anapokea habari hii kwa furaha kuu. Katika furaha hiyo, Yese anafikiri na kuona kwa mtizamo wake, kuwa mtoto huyu atakuwa ELIABU. Katika hali ya kawaida, Eliabu alikuwa mrefu na mzuri, tena alikuwa mtoto wa kwanza. Samweli anavutiwa na sura ya Eliabu, lakini Mungu anasema hapana!

Kwa hapana ya Mungu, Yese atalazimika kuwaleta watoto wake wote isipokuwa Daudi aliyekuwa machungani! Mpendwa msikilizaji, kati ya watoto hawa walioletwa hakukuwa na aliyechaguliwa na Mungu na hivi Samueli akamwambia akamlete Daudi. Yese kwa kuamuliwa amlete Daudi alisema bado Daudi ni mdogo kwa utume ambao ni mkubwa namna hii! Lakini Nabii atasisitiza kuwa huyu ndiye chaguo la Mungu.

Mpendwa, katika uchaguzi huu tunagundua kuwa njia za Mungu na njia zetu ni tofauti kabisa. Fikiria kwa kuchagua taifa la Israeli liwe taifa teule aliacha taifa imara kiuchumi yaani Babilonia, akaacha Misri lililokuwa taifa lenye ufundi wa hali juu na lenye watu wa dini, (Deut, 7:7-8). Ni katika mlengo ule ule katika AJ Bwana atawachagua maskini, wadhambi, wanaoteswa, na wanaotengwa kwa ajili ya ufalme wake. Kumbuka pia alipozaliwa watu wa kwanza kushuhudia utukufu wake ni wachungaji waliokuwa kondeni. Mpendwa msikilizaji, ndiyo kusema hatuna mamlaka ya kuingilia mpango wa Mungu, ni vema siku zote tukajisalimisha katika yeye kadiri ya mapenzi yake.

Katika somo la Pili Mtakatifu Paulo anawaandikia Waefeso akisema, kwa njia ya ubatizo wametwaliwa toka giza na kuingizwa katika mwanga. Kwa tendo la kuingizwa katika utawala wa mwanga, wanaalikwa kuishi na kutenda matendo ya mwanga na kuachana na matendo ya aibu. Anasonga mbele akisema lazima kukemea matendo yaliyo ya aibu tena katika uwazi na kuyapatilizia mbali.

Katika Injili tunakutana na picha ya kipofu anayeponywa na Bwana. Jambo la msingi na fundisho la Bwana ni kwamba yeye amekuja kuwaondolea watu upofu wao na hasa upofu wa kiroho. Tunaona kabla ya tendo hilo jema, wafuasi wake watamwuliza wakisema: Bwana, hivi ni nani kati ya mtoto kipofu na wazazi wake aliyetenda dhambi mpaka mtoto yuko hivi?

Wanauliza swali hili kwa sababu kulikuwa na imani kwamba Mungu huwaadhibu wenye dhambi na kuwarehemu wema! Ndiyo kusema magonjwa na mikosi ilikuwa ni tokeo la dhambi! Aidha, aliyezalwa katika shida kama hizo alidhihirisha kuwa dhambi ilitendwa na wazazi pamoja na mababu. Mpendwa mwana wa Mungu, kufikiri hivi ni kinyume cha mapendo ya Mungu kwa watu, kwa hakika Mungu hajui kuadhibu bali kupenda tu. Ndiyo kusema shida zilizopo zinakuja kwa sababu ya uzembe wetu na hivi lazima tutafute suluhisho na namna ya kukabiliana nazo.

Katika sehemu ya pili ya Injili tunaona sasa ukamilifu wa kile alichokifundisha, yaani anakiweka katika matendo. Katia kutenda mwujiza wa kumfanya kipofu aone tena, anatema mate chini na kufanya tope ambalo atampaka kipofu. Baada ya hilo anamwambia nenda kanawe katika birika ya Siloamu na kwa kufanya hivyo kipofu anaona! Mpendwa msikilizaji, kuna nini katika matendo haya? Mambo yako hivi kwa sababu watu wa wakati huo waliamini katika pumzi kuwako na roho na katika mate kulijaa nguvu ya mtu.

Ndiyo kusema Bwana anatumia alama zilezile kutenda kazi yake ya kuleta uhuru kwa kipofu. Bwana haishii tu katika alama hizi za mwanzo bali anamwambia nenda ukanawe katika Siloamu, ndiyo kusema anamtuma. Hapa tunaona Bwana aliyetumwa na Mungu anamwalika mtu kuja kwake ili apate maji ya uzima, maji yanayoponyesha kama alivyomwahidia mwanamke msamaria, na kisha kwenda kutangaza habari njema ya furaha.

Baada ya tendo hili la uponyaji kipofu ataulizwa na watu mbalimbali kuhakikisha ni kwa nguvu ya nani amepona. Wa kwanza ni majirani zake ambao wanajiuliza ni yeye au ni mwingine na baadaye watampeleka kwa Mafarisayo ambao watamlalamikia Bwana badala ya kumsifu, ati kwa sababu alitenda kazi hiyo wakati wa Sabato, na kwa jinsi hiyo Bwana hakutoka kwa Mungu. Katika hili wengine walisema lakini inawezekanaje mwenye dhambi afanye mwujiza huu?

Kwa majirani kipofu atasema mimi ndiye na wala si mwingine. Kwa Mafarisayo atasema yakuwa aliyeniponya ni Nabii. Mpendwa msikilizaji, katika kuendelea kutafuta ukweli, wenye madaraka watawaendea wazazi wake na kuwauliza na wazazi kwa woga wa kutengwa watasema kamwulizeni yeye mwenyewe kwa kuwa ni mtu mzima. Wenye mamlaka watamrudia aliyekuwa kipofu wakitaka akane ukweli na yeye atawaambia ninachojua ni kwamba nilikuwa kipofu na sasa ninaona. Ndugu huyu aliendelea kutetea ukweli huo kwa furaha mpaka mwisho.

Mpendwa, katika hili twajifunza kuwa wakweli na kuwa wenye furaha daima, na hivi kusimamia imani na matendo makuu ya Mungu. Ndiyo kusema furaha na neema za Mungu tulizozipokea kwa njia ya ubatizo na kipaimara twapaswa kuzitunza mpaka mwisho wa nyakati. Tena, katika safari ya kulinda imani kutakuwa na wakati wa furaha na mateso, jambo kuu ni kuweka tumaini katika yeye aliyetuponya.

Mpendwa ninakutakia furaha na matumaini katika maisha yako daima ukimtanguliza Mungu na kwa nguvu zake kukua na kusimamia imani uliyoipokea kama zawadi toka kwake.

Tumsifu Yesu Kristo. Tafakari hii imeletwa kwako na Padre Richard Tiganya C.PP.S.


BAADA YA KUSOTA, BATAROKOTA AULA TUZO ZA KILL MUSIC AWARD


HATIMAYE mwanamuziki  Batarokota amefanikiwa kuingia kwenye tuzo za muziki za Kilimanjaro Music Award mwaka 2014, kwa mujibu wa waandaaji wa tuzo hizo, Batarokota ameingia na wimbo wake Kwejaga nyangisha.

Tayari makundi ya washiriki wa tuzo hizo yameshapangwa hukua akichuana na wanamuziki wengine wenye majina makubwa hapa nchini, makundi hayo yanahusisha wanamuziki maarufu kama Diamond lakini kundi la Batarokota lipo kama ifuatavyo.

Wimbo bora wenye vionjo vya asili ya Kitanzania
1 Kwejaga nyangisha-Batarokota
2 Nalonji-Kumpeneka
3 Bora Mchawi-Dar Bongo massive
4 Tumbo lamsokota-Ashimba
5 Aliponji -Wanakijiji
6 Agwemwana-Cocodo African music band

Batarokota amekuwa katika mafanikio mazuri baada ya kutengenezxa wimbo huo kupitia njia ya video, hivi karibuni alifanya ziara yake ya kimuziki katika nchi za Swaziland na Afrika Kusini.

Diamond awacharukia tuzo Kili


Kutajwa kwa msanii Diamond Platnumz kuwania tuzo sita za Kilimanjaro 2014, hakujatosha kumfunga mdomo msanii huyo asizungumzie kutofurahishwa kwake na maamuzi ya kutoswa katika tuzo hizo kwa nyimbo za wasanii Snura, Madee na Jux.

Nyimbo za wasanii hao 'Nimevurugwa', 'Tema Mate Tuwachape' na 'Uzuri Wako', zimepigwa marufuku kuonekana katika televisheni na kuondolewa katika kinyang'anyiro cha tuzo hizo na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kutokana na video zake "kukosa maadili" ya Mtanzania.

Kupitia kurasa za mitandao yake ya kijamii, Diamond ambaye ameingia katika tuzo hizo kupitia wimbo wake wa 'My Number One', aliandika: "Ikiwa kweli tuna lengo la kutoipotosha kimaadili jamii yetu na vizazi vyetu pendwa, nafikiri ni vyema tungeanza kuzuia video na nyimbo za kutoka nje, kuliko kuzuia nyimbo na video za nyumbani ambazo uchafu wake haufikii hata robo ya uliopo kwenye nyimbo zinazopewa kipaumbele kutoka nje... Hii ni sawa na kuzidi kuukuza muziki wa nje huku tukiudidimiza na kuua muziki wetu... Mikakati ya kufikia malengo yetu itafanikiwa kweli?? #Ni_mtazamo_tu"

Mwanamke Msamaria anakutana na "Kyasaka"



Mwanamuziki Mbaraka Mwinshehe, aliimba: “Ugeni tabu ndugu zangu, unapofika nchi za mbali huwa mashaka. Hapo fikira za nyumbani hukujaa tele na majonzi kukujia mengi. Ugeni tabu mi’ nasema kweli si masihala wasafiri waelewa. Kwani unaweza tafuta kazi ukapata na pakulala ukawa huna. Ukabaki kuhangaika usiku kucha kwa sababu ya ugeni. Kweli nyumbani ni nyumbani nchi za kigeni hazina mazoea.” Wimbo huu unaonesha ukweli anaopambana nao msafiri au unapojikuta katika mazingira mazingira mageni ambayo wenyeji wake wanakushangaa na hawako tayari kukupokea.

Mtu ukiwa mgeni katika mazingira au pahala usipozaliwa yaani katika mazingira ya taifa jingine au hata kabila jingine, unaweza ukaitwa majina mengi sana hata majina ya kebehi, unawezwa ukaitwa mtu wa kuja; kyasaka, mnyamlenge, mpoma, mgeni, nk. Kama ni mgeni katika mazingira ya dini nyingine, hapo unaweza kuitwa kafiri, mromani, likristu, nk. Kwa vyovyote kuwa mgeni ni karaha sana hasa kama hutaki kujipokea na kujikubali kwamba wewe ni mgeni, mnyamlenge, mtu wa kuja, mpoma, kafiri, mkristu, mromani, nk. Unahitaji pia busara au diplomasia ya hali juu sana ili kuweza kuyatawala mazingira hayo, na hatimaye ukaweza kuyaathiri mazingira ambayo kwa mwanzoni yalikuona kwa jicho baya au hayakukupokea.

Leo tutakutana na mwanadiplomasia na mwanasaikolojia mkuu aliyepambana na mazingira mazito sana ya ugeni, lakini akafaulu kuyateka na kuyabadili. Injili inamwonesha Yesu kama mnyamlenge katika nchi ya Samaria. Alikuwa ametoka kusini Judea (Uyahudini) anaelekea nyumbani kwake kaskazini Galilea, hivi kwa vyovyote ilimbidi akatishe kana kupita katikati ya nchi ya Samaria. Hapo ndipo kilipompata kisanga cha kujisikia mgeni kwenye ardhi hiyo. Siyo tu yeye alijisikia mgeni bali alionwa hivi kama mtu wa kuja, mtu wa utamaduni tofauti na wasamaria tena na mwanamke. Watu wa makabila hayo mawili Wasamaria na kabila la Yesu (Wagalilaya) walikuwa hawaivani kabisa kiutamaduni. Zaidi tena Yesu alitazamwa kama mtu mwenye imani au dini tofauti na ile ya wasamaria yaani walitofautiana kiitikadi.

Katika mazingira kama hayo, utaona jinsi Yesu alivyo gwiji wa saikolojia anavyoweza kukabiliana na mazingira magumu, anavyosikiliza, anavyohoji mambo, na kutoa rai zake, hadi anafikia hali ya kuanzisha mazungumzo (dayalogu) mazuri yanayolainisha na kugeuza moyo mwa mpinzani wake. Hali ambayo ni kama kuanzisha “uzao upya”. Mnaweza kirahisi kulinganisha na kutofautisha dayalogu au mazungumzo yalivyokuwa kati ya Ibilisi na Yesu kule jangwani (Dominika ya kwanza kwaresima) na mazungumzo haya ya kati ya mwanamke huyu msamaria na Yesu kwenye kisima (chemchemi) ya maji.

Mapato ya mazungumzo ya hapa kisimani, yanatokana na uhuru aliokuwa nao Yesu, hadi kufanikisha kuathiri mazingira yaliyokuwa magumu sana tena yaliyokuwa dhidi yake. Hali hii inaonesha wazi kwamba Yesu ni mwalimu wa utu kwa wote, mdiplomasia na msaikolojia mkuu. Ni mwalimu kwa sababu anao uweza wa kuvuka vizuizi vinavyopinga majadiliano. Mipaka au vizuizi vile vinavyomtenga mwanaume na mwanamke, mipaka kati ya watu wa eneo moja hadi jingine; kati ya watu wa makabila tofauti. Ukitaka kujifunza utu wema, saikolojia na diplomasia ya kweli na kuweza kuanzisha na kuendesha dayalogu ya aina yoyote hata ile ya kisiasa, basi jaribu kufuatana na Yesu katika Injili ya leo.

Mchokozi rasmi wa majadiliano hayo ni Yesu anayeomba: “Nipe maji ninywe”. Majibu ya mwanamke yule ndiyo yanayoonesha kuwa Yesu ni mtu wa kuja katika kabila jingine: “Imekuwaje wewe mgeni kuniomba mimi maji ya kunywa, nami ni mwanamke Msamaria?” Jibu kama hili linatosha kabisa kukukatisha tamaa na kuendelea kuomba maji. Mwanamke huyu anamwonesha Yesu kuwa hawana mahusiano yoyote kikabila wala kijinsia. Kwani kati ya myahudi rabi na mwanamke haikuwezekana wala haikuruhusiwa kabisa kuzungumzana. Kumbe Yesu akiwa kama mwalimu wa uzima kwa sababu Yeye ni chemchemu unapotoka uzima. Anaanzisha mazungumzo na kukutanisha watu ambao wamekata kabisa mawasiliano, wala kupeana mikono. Yesu anaanzisha mazungumzo na mahusiano kwa kuanza na ufukara wake: “Nina kiu” (Nipe maji ninywe). Tujifunze kutoa kama anavyotoa Yesu. Kama mtu fukara anayepokea, kutoa kwa fukara, kwa watu wa kuja (wageni) na siyo kwa ukuu kama ule wa mtu tajiri, bali kwa unyenyekevu wa watu fukara. Anayejua kuwa anaweza kupokea zaidi endapo anajali utu. Yesu anafaulu kumzaa mwanamke mpya. Anapozungumza na wanawake anawagusa moyo moja kwa moja. Anajua lugha zao, lugha ya kutamani lugha ya vionjo, lugha ya kutafuta hoja nzito za kuishi.

Kuhusu kupambana na ugeni wa mazingira ya imani (dini) tofauti, ni pale Yesu anapokubaliana na kauli ya mwanamke kwamba anaishi na mshikaji wa sita baada ya kuachika na washikaji wengine watano “Hapo umesema kweli.” Hapo mwanamke anaanza kuthibitisha kutofautiana kwao katika imani: “Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia.” Tamko hili la mwanamke linaonesha wazi kwamba wao ndiyo wanaofuata mapokea ya mababu ya kuabudu katika mlima, wakati dini ya Yesu ni maagizo ya watu wa siku hizi waliojijengea tu hekalu Yerusalemu na kuabudu. Yesu anachukua mwanya huu wa kutofautiana kiitikadi za imani na kumfundisha mwanamke yule akisema: “Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi. Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli...” Hapa Yesu anaenda zaidi ya pale anapofahamu mwanamke na kumwongezea uhondo zaidi wa kuabudu, yaani kuabudu Baba katika roho na kweli.
Ndipo sasa unapomwona Yesu anaibuka na namna mpya ya saikolojia, anaweza hata kupendekeza jambo linalohusu maisha binafsi ya mtu anapomwambia mwanamke: “Nenda kamwite mumeo, uje naye hapa.” Hapa ndipo mwanamke akajibu “Sina mume” kwa kweli angetakiwa aseme tu kwamba “Ninaye mshikaji.” Mwanamke huyu ni mithili ya wayahudi waliokuwa wametangaanawakilisha wale wanaoabudu miungu, sanamu, ni sawa na malaya. Mwanamke huyu ni mimi!

Yesu anasema: “Umesema vema, ‘Sina mume’; kwa maana umekuwa na waume watano naye uliye naye sasa siye mume wako; hapo umesema kweli.” Yesu hamhukumu yule mama msamaria tena hamdhalilishi, bali anasisitiza karibu mara mbili kwa kusema “Umesema kweli kabisa”. Yesu alishamtambua mwanamke huyo ni wa aina gani kutoka mwanzo alipofika kuketi pale kisimani mchana. Wanawake wa kawaida wanachota maji asubuhi sana au jioni, kwa hiyo anayeenda kuchota maji mchana tena peke yake anaweza kujulikana ni mwanamke wa aina gani na anatafuta nini. Kwa tamko hilo “Umesema kweli kabisa” Yesu hana nia ya kuharibu mahusiano waliyo nayo, bali anataka kumweka sawa mwanamke huyo kwamba hana budi kujiweka sawa kabla ya kujidhatiti kuyawania hayo maji ya uzima anayoyatamani. Aidha siyo Yesu anayetakiwa kuyapanga maisha ya mbele ya huyo mwanamke – bali ni kama vile angemwambia “Kazi kwako!” Upendo ni mlango wa Mungu na ni Mungu aliye ndani yetu. Ni Mungu anayetujali sana, ni Mungu mwenye utu wa hali ya juu sana, hiyo ndiyo sura nzuri ya Mungu.

Mwanamke alisema kuwa “Kisima kile ni kirefu kimezama sana.” Kiasi Yesu asingeweza kufanikiwa kuchota maji kwa vile hakuwa na kata (nyenzo) ya kuchotea. Endapo kisima hicho ni wewe na mimi, hapa unaona dhahiri kwamba ipo njia moja tu ya kuchota maji ya kisima hicho kilichozama sana cha kila mmoja wetu, nayo siyo kwa njia ya kugombeza, kukashifu, kukosoa, bali kwa njia ya kumfanya mmoja aonje utamu zaidi wa maisha, wa uzuri wa mali au kisima alicho nacho. Angalia Yesu anavyomtamanisha mwanamke huyu hadi anachoka mwenyewe anapomwambia: “Mimi nitakupa maji ambayo yanakuwa chemchemu”. Maji ni uzima, maisha, nguvu ya maisha, ambayo ninaipokea ninapojiunganisha na chemchemi isiyokauka ya maisha ambayo ni Mungu. Yesu anampa Mama Msamaria fursa ya kujiunganisha au kujisogezasogeza karibu na chemchemi yake ili baadaye yeye mwenyewe awe chemchemu.

Hiyo ni picha nzuri sana, picha ya maji yanayotembea, inayobubujika, mto wa uzima ni zaidi ya ule unaozima kiu yako tu, bali ni mto ule unaozima hata kiu ya wengine. Chemchemu haimilikiwi bali inajieneza, inazaa. Kwa ahadi kama hiyo ya Yesu, yule mwanamke msamaria anaelewa kwamba hataweza kutuliza kiu yake kwa kunywa na kusaza, bali kwa kutuliza kiu ya wengine. Kwamba ataangazwa tu kwa kuangaza wengine, atapata furaha kwa kutoa furaha kwa wengine. Kuwa chemchemi: ni mradi mzuri wa maisha, ni chemchemi ya matumaini, ya kupokea, ya upendo. Baada ya kuuelewa ukweli huu juu ya chemchemi, hapo ndipo sasa, mwanamke yule anautelekeza mtungi wa maji pale kama vile ungekuwa kitenge kilichochakaa, anaacha maisha ya zamani, anakimbia kwenda mjini na kumsimamisha kila anayepita barabarani. “Jamani! kuna mtu kisimani huko, anayekuwezesha uzaliwe na kuzaliwa tena upya. Usipozaliwa hujaumbika. Njoni mumtazame mtu aliyeniambia mambo yote niliyoyatenda.” Anakuambia mambo yaliyoko katika moyo wako na kuiibusha chemchemi.

Mwanamke huyu anahaha huku na huku, anakimbiakimbia, anaita, anashuhudia, anafanya unabii, anawachemsha watu wote, na hadi anazungukwa na jumuia mpya ya kwanza ya wafuasi wageni. “Basi wakatoka mjini, wakamwendea.” (Yohane 4:30). Na katika mji ule Wasamaria wengi walimwamini kwa sababu ya maneno ya yule mwanamke aliyeshuhudia kwamba, “aliniambia mambo yote niliyoyatenda.” Basi wale Wasamaria walipomwendea, walimsihi akae kwao; Watu wengi zaidi wakaamini…” (Yoh 4:39-40). Kuna mmoja, Yesu, anayejua na kusema yote juu yako. Yeye anajua kilicho ndani ya mioyo yetu: Jema lina nguvu zaidi kuliko bovu au baya, kuna jema lililo kongwe zaidi kuliko ubaya, kuna jema linawezekana kuwa muhimu zaidi kuliko ubaya wa sasa. Kuna ziwa la nuru na uwepo wake ndani mwetu ndiyo unaokuwa chemchemu.

Kwa hiyo nitaenda wapi ili kuwambudu Mungu? Siyo mlimani, siyo hekaluni au Kanisani!. Bali katika mimi: ni mimi ndiye ule mlima wa Mungu, mimi ni Kanisa. Naye ni chemchemi ya chemchemi zangu. Hata sisi, kama yule mama msamaria, anayeenda kisimani kuchota maji na anarudi ametajirika, kama tukimpokea Mungu ndani yetu anayetufanye tuzaliwe upya, anayebomoa kila kizuizi, mpaka, hapo tutaona kububujika kati ya mikono yetu wimbo wa chemchemu. Pahala popote pageni utakapokuwa, hali yoyote ile chukivu, mtazamo wowote ule mbaya wa maisha utaweza kuubadili kwa mazungumzo ya upendo, bora tu ukijifunza toka kwa Yesu.
Padre Alcuin Nyirenda, OSB.

Siku kuu ya toba, wongofu na upatanisho!


Kama ilivyokuwa kwa Manabii, wito wa Yesu wa toba na wongofu wa ndani haulengi kwanza kazi za nje yaani kuvaa gunia na kujipaka majivu, kufunga na kujitesa, bali wongofu wa moyo unaogusa undani wa mtu mzima. Bila wongofu huu, matendo ya toba hayana nguvu wala ukweli ndani yake. Wongofu wa ndani husukumwa kuonesha ishara zinazoonekana, vitendo vya mwili, na kazi za toba.

Toba ya ndani ni kuelekeza upya kabisa maisha yote, ni kurudi na kumwongokea Mwenyezi Mungu kwa moyo wote, kukataa dhambi na nafasi zake; kuchukua maovu, kwa kujiwekea lengo ka kubadili maisha pamoja na kuendelea kutumainia huruma na neema ya Mungu. Wongofu wa ndani hufumbata maumivu na machungu ya wokovu ambayo Mababa wa Kanisa wameita kuwa ni taabu ya roho au toba ya moyo.

Moyo wa mtu ni mzito na mgumu. Inatakiwa Mwenyezi Mungu ampe mtu moyo mpya. Ikumbukwe kwamba, wongofu wa ndani ni kazi ya neema ya Mungu inayoufanya moyo wa mwanadamu uweze kumrudia tena Muumba wake, kwa kugundua ukuu, huruma na mapendo ya Mungu yasiyokuwa na kifani. Mwamini anapaswa kuonesha masikitiko ya dhambi zake, kwa kumwangalia Yesu aliyeteswa, akafa na kufufuka ili kumkomboa mwanadamu kutoka katika lindi la dhambi na mauti. Kwa Damu yake azizi, Yesu amemkomboa mwanadamu na kuukirimia ulimwengu neema ya toba na wongofu wa ndani.

Mama Kanisa amewawekea watoto wake nyakati za toba zinazojikita katika mazoezi ya maisha ya kiroho, liturujia, hija, kujinyima, kufunga na kusali pamoja na kushiriki katika kazi za matendo ya huruma na kimissionari. Kwa kutambua umuhimu wat oba na wongofu wa ndani, Baba Mtakatifu Francisko, ametenga Ijumaa ya tarehe 28 Machi 2014 kuwa ni siku maalum ya toba na wongofu wa ndani, mwaliko wa kuchuchumilia Sakramenti ya Upatanisho, inayomwonjesha mwamini huruma na upendo wa Mungu usiokuwa na kifani.

Hii ni mikakati ya shughuli za kichungaji inayotekelezwa na Baraza la Kipapa la Uinjilishaji Mpya. Baba Mtakatifu Ijumaa, majira ya jioni ataongoza Ibada ya Upatanisho kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican na baadaye atapata fursa ya kuungamisha baadhi ya waamini watakaoshiriki katika Ibada hii na baadaye kutoa ondoleo la dhambi.

Kuanzia majira ya Saa mbili kamili asubuhi, Kanisa la Mtakatifu Agnes, Bikira Maria, Trastevere na Kanisa la Madonda Matakatifu, yataendelea kutumika kwa ajili ya Ibada ya Kuabudu Ekaristi Takatifu kwa muda wa Masaa 24. Hayo yamesemwa na Askofu mkuu Rino Fisichella, Rais wa Baraza la Kipapa la Uinjilishaji Mpya. Ni tukio ambalo litawahusisha vijana ambao kimsingi ni Wainjilishaji wapya kwa kuwakaribisha vijana wenzao, kuingia ndani ya Kanisa, ili kuonja huruma na upendo wa Mungu kwa waja wake. Ndani ya Makanisa haya, watakutana na Mapadre ambao watakuwa tayari kuzungumza nao na hatimaye, kuwaungamisha.

Tukio hili la kihistoria, anasema, Askofu mkuu Fisichella, litahitimishwa kwa Ibada ya Masifu ya kwanza ya Jioni, Jumapili ya Nne ya Kipindi cha Kwaresima, Ibada itakayofanyika kwenye Kanisa la Santo Spirito in Sassia, Jimbo kuu la Roma.

St. Margaret Clitherow


Image of St. Margaret Clitherow
Feastday: March 26

St. Margaret Clitherow was born in Middleton, England, in 1555, of protestant parents. Possessed of good looks and full of wit and merriment, she was a charming personality. In 1571, she married John Clitherow, a well-to-do grazier and butcher (to whom she bore two children), and a few years later entered the Catholic Church. Her zeal led her to harbor fugitive priests, for which she was arrested and imprisoned by hostile authorities. Recourse was had to every means in an attempt to make her deny her Faith, but the holy woman stood firm. Finally, she was condemned to be pressed to death on March 25, 1586. She was stretched out on the ground with a sharp rock on her back and crushed under a door over laden with unbearable weights. Her bones were broken and she died within fifteen minutes. The humanity and holiness of this servant of God can be readily glimpsed in her words to a friend when she learned of her condemnation: "The sheriffs have said that I am going to die this coming Friday; and I feel the weakness of my flesh which is troubled at this news, but my spirit rejoices greatly. For the love of God, pray for me and ask all good people to do likewise." Her feast day is March 26th.

More about St. Margaret Clitherow from Wikipedia

Saint Margaret Clitherow (1556 – 25 March 1586) is an English saint and martyr of the Roman Catholic Church.[2] She is sometimes called "the Pearl of York".

Contents

  • 1 Life
  • 2 Canonisation
  • 3 Further reading
  • 4 See also
  • 5 References
  • 6 External links
    • 6.1 Margaret
    • 6.2 Children
    • 6.3 Places

Life

She was born as Margaret Middleton,[3] the daughter of a wax-chandler, after Henry VIII of England had split the Church of England from the Roman Catholic Church. She married John Clitherow, a butcher, in 1571 (at the age of 15) and bore him three children. She converted to Roman Catholicism at the age of 18, in 1574. Her husband John was supportive (he having a brother who was Roman Catholic clergy), though he remained Protestant.[4] She then became a friend of the persecuted Roman Catholic population in the north of England. Her son, Henry, went to Reims to train as a Roman Catholic priest. She regularly held Masses in her home in the Shambles in York. There was a hole cut between the attics of her house and the adjoining house, to enable a priest to escape in the event of a raid. A house in the Shambles once thought to have been her home, now called the Shrine of the Saint Margaret Clitherow, is open to the public (it is served by the nearby Church of St Wilfrid's and is part of the Roman Catholic Diocese of Middlesbrough); her actual house (10 and 11, the Shambles) is further down the street.
In 1586, she was arrested and called before the York assizes for the crime of harbouring Roman Catholic priests. She refused to plead to the case so as to prevent a trial that would entail her children being made to testify, and therefore being subjected to torture. As a result she was executed by being crushed to death – the standard inducement o force a plea; on Good Friday 1586.[5] The two sergeants who should have killed her hired four desperate beggars to kill her. She was stripped and had a handkerchief tied across her face then laid out upon a sharp rock the size of a man's fist, the door from her own house was put on top of her and slowly loaded with an immense weight of rocks and stones (the small sharp rock would break her back when the heavy rocks were laid on top of her). Her death occurred within fifteen minutes but her body was left for six hours before the weight was removed. After her death her hand was removed, and this relic is now housed in the chapel of the Bar Convent, York. Following her execution, Elizabeth I wrote to the citizens of York expressing her horror at the treatment of a woman. Because of her sex, she argued, Clitherow should not have been executed.[citation needed]
Commemorative plaque on the Ouse Bridge, York
In 2008, a commemorative plaque was installed at the Micklegate end of Ouse Bridge to mark the site of her martyrdom; the Bishop of Middlesbrough unveiled this in a ceremony on Friday 29 August 2008.[6]

Canonisation

She was beatified in 1929 by Pope Pius XI and canonised in 1970 by Pope Paul VI along with other martyrs from England and Wales. The group of candidates canonised at that time is commonly called "The Forty Martyrs of England and Wales". Her feast day in the current Roman Catholic calendar, together with the other English martyrs, is 4 May. However her feast day in England is 30 August, which she shares with fellow female martyrs St. Anne Line and St. Margaret Ward.
A number of schools in England are named after Margaret Clitherow, including schools at Bracknell, Brixham, Manchester, Nottingham, Thamesmead SE28, Brent, London NW10 and Tonbridge. The Roman Catholic primary school in Nottingham's Bestwood estate is named after Clitherow. In the United States, St Margaret of York Church and School in Loveland, a suburb of Cincinnati, Ohio, is also named after her. Another school named after her is St. Margaret Clitherow RC Primary School, located next to Stevenage Borough Football Club.
She is also the patroness of the Catholic Women's League, an organisation of Catholic women founded in 1906, with small groups (known as branches) and sections (groupings of branches, usually along diocesan lines) across the world. A group of parishes in the Roman Catholic Archdiocese of Liverpool, Sacred Heart in Hindsford, St Richard's in Atherton, Holy Family in Boothstown, St Ambrose Barlow in Astley, St Gabriel's, Higher Folds in Leigh are now united as a single community with St Margaret Clitherow as its patron.[7][8]

Orodha Kamili ya waliongia katika kinyang'anyiro cha Kilimanjaro Tanzania Music Awards 2014:


Wimbo bora wa mwaka
1 Number one-Diamond
2 Joto hasira-Lady Jaydee Ft Prof Jay
3 I love u-Cassim Mganga
4 Yahaya-Lady JayDee
5 Kidela -Abdu Kiba Feat Ali Kiba
6 Muziki gani-Ney ft Diamond

Wimbo bora wenye vionjo vya asili ya Kitanzania
1 Kwejaga nyangisha-Batarokota
2 Nalonji-Kumpeneka
3 Bora Mchawi-Dar Bongo massive
4 Tumbo lamsokota-Ashimba
5 Aliponji -Wanakijiji
6 Agwemwana-Cocodo African music band

Wimbo bora wa kiswahili -Bendi
1 Ushamba mzigo-Mashujaa Band
2 Shamba la Bibi -Victoria Sound
3 Chuki ya nini -FM Academia
4 Yarabi nafsi -Mapacha Watatu
5 Kiapo mara 3 -Talent Band

Wimbo bora wa Reggae
1 Niwe na wewe-Dabo
2 Hakuna Matata-Lonka
3 Tell Me-Dj Aron ft Fidempha
4 Bado nahitaji-Chikaka ft Bless p & Lazzy B
5 Bongo Reggae-Warriors from the east

Wimbo bora wa Afrika Mashashariki
1 Tubonge-Jose Chamelleone
2 Nakupenda Pia-Waire Ft Allain
3 Badilisha-Jose Chamelleone
4 Kipepeo-Jaguar
5 Kiboko Changu-Aman FT Weizal and Radio

Wimbo bora wa Afro pop
1 Number one-Diamond
2 Joto hasira-Jay Dee
3 Kidela-abdul kiba ft Ali Kiba
4 I love you-Kassimu
5 Tupogo-Ommy Dimpoz Ft J Martins
6 Roho yangu-Rich Mavoko

Wimbo bora wa Taarab
1 Wasi wasi wako-Mzee Yusuf
2 Asiyekujua Hakuthamini-Isha Ramadhani & Saida Ramadhani
3 Nipe stara -Rahma Machupa
4 Sitaki shari-Leyla Rashid
5 Fahari ya Mwanamke-Khadija Kopa
6 Mambo bado-Khadija Yusuf
7 Kila muomba Mungu -Mwanahawa Ali

Wimbo bora wa Hip hop
1 Bei ya mkaa-Weusi
2 Nje ya box-Nick wa pili ft Joh Makini and , Gnako
3 Siri ya mchezo-Fid q ft Nature
4 2030-Roma
5 Pesa-Mr Blue Ft Becka Title

Wimbo bora wa R&B
1 Listen-Belle 9
2 Closer -Vanessa Mdee
3 So crazy-Maua ft Fa
4 kama huwezi-rama dee ft jay dee
5 Wa ubani-Ben Pol ft. Alice

Wimbo bora wa kushirikisha/kushirikiana
1 Music Gani-Ney Mitego ft Diamond
2 Joto Hasira-Lady JayDee ft. Prof Jay
3 Kidela -Abdul Kiba ft. Ali Kiba
4 Bila Kukunja Goti-Mwana FA na AY ft. Jay Martins
5 Tupogo-Ommy Dimpoz ft. Jay Martins

Wimbo bora wa Ragga/Dancehall
1 Nishai-Chibwa Ft Juru
2 Sex girl-Dr Jahson
3 My sweet-Jettyman Dizano
4 Feel Alright-Lucky Stone
5 Wine-Princess Delyla

Wimbo bora wa Zouk /Rhumba
1 Yahaya-Lady Jaydee
2 Yamoto-Mkubwa na wanawe
3 Msaliti-Christian Bella
4 Nakuhitaji-Malaika Band
5 Narudi kazini-Beka

Mwimbaji bora wa kike -kizazi kipya
1 Vanessa Mdee
2 Lady Jaydee
3 Linah
4 Maua

Mwimbaji bora wa kiume -kizazi kipya
1 Ben Pol
2 Rich Mavoko
3 Diamond
4 Ommy Dimpoz
5 Cassim Mganga

Mwimbaji bora wa kike -Taarab
1 Khadija Kopa
2 Isha Ramadhani
3 Khadija Yusuf
4 Mwanahawa Ali
5 Leyla Rashid

Mwimbaji bora wa kiume -Taarab
1 Mzee Yusuf
2 Hashimu Saidi
3 Mohamedi Ali aka Mtoto Pori

Mwimbaji bora wa kiume -Bendi
1 Jose Mara
2 Kalala Junior
3 Charz Baba
4 Khalid Chokoraa
5 Christian Bella

Mwimbaji bora wa kike -Bendi
1 Luiza Mbutu
2 Catherine (Cindy)
3 Ciana

Msanii bora wa -Hip hop
1 FID Q
2 Stamina
3 Young killer (Msodoki)
4 Nick wa pili
5 Gnako

Msanii bora chipukizi anayeibukia
1 Young Killer(Msodoki)
2 Walter Chilambo
3 Y Tony
4 Snura
5 Meninah

Rapa bora wa mwaka -Bendi
1 Kitokololo
2 Chokoraa
3 Furguson
4 Canal Top
5 Totoo ze Bingwa

Mtumbuizaji bora wa kike wa Muziki
1 Khadija Kopa
2 Vanessa Mdee
3 Isha Ramadanni
4 Luiza Mbutu
5 Catherine (Cindy)

Mtumbuizaji bora wa kiume wa Muziki
1 Diamond
2 Christian Bella
3 Rich Mavoko
4 Ommy Dimpoz
5 Abdu Kiba

Mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka -Taarab
1 Enrico
2 Ababuu Mwana ZNZ
3 Bakunde

Mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka -Kizazi kipya
1 Marco chali-Mj Records
2 Man Water-Combination Sound
3 Mazoo-Mazoo Records
4 Sheddy Clever-Burnz Records
5 Nahreel -Home Town Record

Mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka -Bendi
1 Allan Mapigo
2 C9
3 Enrico
4 Amoroso
5 Ababuu Mwana ZNZ

Mtunzi bora wa mwaka -Taarabu
1 Mzee Yusuf
2 El-Ahad Omary
3 El-khatib Rajab
4 Kapten Temba
5 Sadiki Abdul
6 Nassoro Seif


Mtunzi bora wa mwaka -kizazi kipya
1 Belle 9
2 Ben Pol
3 Diamond
4 Rama dee
5 Rich mavoko

Mtunzi bora wa mwaka -Bendi
1 Christia Bella
2 Jose Mara
3 Chaz Baba
4 Nyoshi Saadat
5 Kalala Junior

Mtunzi bora wa mwaka -Hip hop
1 Nikki wa Pili
2 Young Killer(Msodoki)
3 Roma
4 FID Q
5 G- Nako

Video bora ya muziki ya mwaka
1 Number one-Diamond
2 Yahaya-lady Jaydee
3 Joto hasira-Lady Jaydee Ft Prof Jay
4 Uswazi takeaway-Chege Ft Malaika
5 Mama Yeyo-Gnako Ft Ben Pol

Bendi ya mwaka
1 FM Academia
2 Mapacha Watatu
3 African Stars(Twanga Pepeta)
4 Akudo Impact
5 Malaika Band
6 Mashujaa Band

Kikundi cha mwaka cha Taarab
1 Jahaz Modern Taarab
2 Mashauzi Classic
3 Five Stars

Kikundi cha mwaka cha kizazi kipya
1 Makomandoo
2 Navy kenzo
3 Weusi
4 Mkubwa na wanawe

Njia ya Msalaba, 2014: mwaliko wa kuiangalia sura ya Kristo katika sura ya mwanadamu anayeteseka!

Tafakari ya Njia ya Msalaba kuzunguka Magofu ya Colosseo mjini Roma, Ijumaa kuu kwa Mwaka 2014 imeandaliwa na Askofu mkuu Giancarlo Maria Bregantini wa Jimbo kuu la Campobasso Boiano, Italia. Ni tafakari ambayo ameifanya kwa niaba ya Baba Mtakatifu Francisko na itafanya rejea kwa vituo kumi na vinne vya Njia ya Msalaba kadiri ya Mapokeo.

Askofu mkuu Bregantini ni mwenyekiti wa Tume ya masuala ya kijamii, kazi, haki na amani ya Baraza la Maaskofu Katoliki Italia. Taarifa hii imetolewa muda mfupi tu tangu Baba Mtakatifu Francisko alipokutana na kusali pamoja na wahanga wa mashambulizi ya kikundi cha kigaidi cha Mafia nchini Italia.

Katika mikakati yake ya kichungaji, Askofu mkuu Bregantini amekuwa akijielekeza zaidi katika majiundo ya dhamiri nyofu, kwa kuwataka waamini na watu wote wenye mapenzi mema kusimama kidete kulinda na kutetea: utu na heshima ya binadamu; haki msingi, amani na utawala wa sheria.

Askofu mkuu Bregantini anasema, amepewa heshima kubwa na Baba Mtakatifu Francisko kuandika tafakari ya Njia ya Msalaba kwa mwaka 2014. Ni tafakari inayoonesha Fumbo la Msalaba katika maisha ya Yesu mintarafu mahangaiko na mateso ya mwanadamu, katika sala na tafakari.

Hapa waamini wanaalikwa kuingalia sura ya Kristo katika sura ya mwanadamu anayeteseka. Yesu anaendelea kumwonjesha mwanadamu huruma na upendo wake wa dhati; anayafuta machozi ya watu wake kama alivyofanya kwa Mtakatifu Petro alipomkana mara tatu. Tafakari ya Njia ya Msalaba pamoja na mambo mengine itagusia athari za myumbo wa uchumi kimataifa, umuhimu wa Neno la Mungu.

Ikumbukwe kwamba, Askofu mkuu Bregantini ni mwanashirika wa Shirika la Madonda Matakatifu, maarufu kama Wasigmatin. Ni mwaliko wa kumwilisha Injili ya Furaha katika uhalisia wa maisha ya mwanadamu anayejikuta daima akisukumizwa pembezoni mwa Jamii. Mama Kanisa anapenda kumwonjesha mwanadamu upendo na huruma ya Mungu isiyokuwa na kifani inayobubujika kutoka kwa Yesu na Kanisa lake!


Ujumbe wa Baba Mtakatifu Francisko kwa Kipindi cha Kwaresima 2014

Mama Kanisa anakianza kipindi cha Kwaresima, yaani siku arobaini za toba na wongofu wa ndani; kusali na kufunga; kusoma na kulitafakari Neno la Mungu pamoja na kumwilisha imani katika matendo, kwa Jumatano ya Majivu. Waamini wanakumbushwa kwamba, wao ni mavumbi na mavumbini watarudi tena.

Hizi ni nyakati za toba na zimewekwa na Mama Kanisa kwa ajili ya mazoezi ya maisha ya kiroho; zinajikita katika liturujia ya toba, kuhiji kama ishara ya toba, kujinyima kwa hiyari kama sehemu ya kufunga na kutoa sadaka kwa maskini na wote wanaosukumizwa pembezoni mwa Jamii; ni mwaliko wa kushiriki kidugu kazi za mapendo na kimissionari zinazotekelezwa na Mama Kanisa.

Ujumbe wa Kwaresima kutoka kwa Baba Mtakatifu Francisko kwa Mwaka 2014 unaongozwa na kauli mbiu “Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, Jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba, ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake”. Huu ni mwaliko kwa waamini kuonesha moyo wa ukarimu kwa jirani zao kama ilivyokuwa nyakati za Mtakatifu Paulo aliyewahimiza Wakorintho kuwasaidia ndugu zao waliokuwa wanateseka mjini Yerusalemu.

Baba Mtakatifu katika tafakari hii anaonesha jinsi ambavyo Mwenyezi Mungu ambaye ni tajiri na mwingi wa rehema kwa njia ya Yesu Kristo, Mwanaye wa pekee amejinyenyekesha na kuwa maskini, ili aweze kuwa karibu na binadamu kwa njia ya Fumbo la Umwilisho. Hiki ni kielelezo cha upendo wa Mungu ambao ni neema na baraka inayotolewa kwa binadamu anayependwa na Mwenyezi Mungu, kiasi cha hata Kristo kujisadaka maisha yake.

Huu ndio upendo unaoshirikisha, unajenga na kuimarisha umoja na udugu kwa kuvunjilia mbali kuta za utengano. Kwa njia ya Fumbo la Umwilisho, Mwenyezi Mungu amefikiri na kutenda kama binadamu katika mambo yote isipokuwa hakutenda dhambi.

Kwa njia ya umaskini wa Yesu, Mwenyezi Mungu amependa mwanadamu aweze kutajirika, hii ndiyo mantiki ya Fumbo la Umwilisho na Fumbo la Msalaba. Alibatizwa mtoni Yordani si kwa vile alikuwa anahitaji toba, wongofu wa ndani na msamaha, bali alipenda kuonesha mshikamano wa dhati na binadamu mdhambi kwa kujitwika dhambi zake mabegani mwake, ili aweze kuwafariji, kuwaokoa na kuwakomboa kutoka katika lindi la dhambi na mauti.

Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake wa Kwaresima kwa Mwaka huu anasema, Yesu alijifanya kuwa jirani na Msamaria mwema, kwa kuguswa na mahangaiko ya binadamu, ili hatimaye, aweze kumwonjesha huruma na mapendo yanayobubujika kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Utajiri wa Yesu unajionesha kwa namna ya pekee kwa kumtegemea Baba yake wa mbinguni, katika kutekeleza mapenzi yake na hatimaye kuvikwa taji la utukufu. Yesu anatambua kwamba, ni Mwana pekee wa Mungu, Masiha anayewaalika wafuasi wake kujitajirisha kutoka kwake na kushiriki udugu na kujitahidi kuchuchumilia utakatifu wa maisha kwa kuishi kama watoto wa Mungu na ndugu zake Kristo.

Kila wakati Mwenyezi Mungu anaendelea kumkomboa mwanadamu kutoka katika umaskini wake kwa njia ya umaskini wa Yesu, kwa kuonja na kuguswa na umaskini wa jirani zao tayari kujifunga kibwebwe kusaidia kupambana na umaskini: wa hali, kipato na maadili. Umaskini ni kielelezo cha kukosa imani, mshikamano na matumaini. Umaskini wa kipato unawakumba wote wanaoishi katika mazingira ambayo ni kinyume kabisa cha utu na heshima ya binadamu.

Hawa ni watu wanaopokonywa haki na mahitaji msingi kama vile: chakula, maji, malazi, huduma bora za afya, fursa za kazi na ajira, maendeleo na ukuaji wa kitamaduni. Kanisa linaendelea kujisadaka kwa ajili ya kupambana na umaskini wa kipato katika mikakati yake ya kichungaji inayopania kumkomboa mtu mzima: kiroho na kimwili. Kanisa linaiona na kuitambua sura ya Kristo miongoni mwa maskini na wote wanaosukumizwa pembezoni mwa Jamii. Kanisa linapania kuhakikisha kwamba, utu na heshima ya binadamu vinaendelea kupewa kipaumbele cha pekee kwa kukomesha ubaguzi ambao wakati mwingine ni chanzo kikuu cha umaskini. Kanisa linahimiza matumizi bora ya rasilimali ya dunia kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya wengi. Jamii iongozwe katika misingi ya haki, usawa, kiasi na ushirikiano.

Baba Mtakatifu Francisko anasema kuna umaskini wa kimaadili, unaomfanya mwanadamu kuwa ni mtumwa wa dhambi, ulevi wa kupindukia, mcheza kamari na mtazamaji wa picha za ngono. Hili ni kundi la watu lililopoteza dira na mwelekeo wa maisha kwa kukata tamaa! Ni watu wanaoogelea katika utupu kwa kukosa fursa za ajira pamoja na kuendelea kudhalilishwa utu na hehima yao kama binadamu: wanakosa chakula na malazi; hawana haki ya kupata huduma bora katika sekta ya elimu, afya na maendeleo. Matokeo yake ni watu kuelemewa mno na umaskini wa kimaadili kiasi hata cha kutema zawadi ya maisha!

Umaskini huu ni chanzo kikuu cha myumbo wa uchumi kimataifa na matokeo yake ni umaskini na utupu wa maisha ya kiroho. Hali hii inajionesha pale mwanadamu anapomn’goa Mwenyezi Mungu katika maisha na vipaumbele vyake, kiasi hata cha kutema upendo na huruma yake. Hapa mwanadamu anadhani kwamba, anaweza kujitegemea mwenyewe na wala haitaji msaada kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Lakini ikumbukwe kwamba, ni Mungu peke yake anayeweza kukomboa na kumwokoa mwanadamu.

Baba Mtakatifu anasema, Injili ni dawa inayoponya umaskini wa maisha ya kiroho, changamoto na mwaliko kwa kila Mkristo kuhakikisha kwamba, anashiriki kutangaza Injili ya Kristo katika medani mbali mbali za maisha, ili watu waonjeshe upendo na huruma ya Mungu; ili hatimaye, waweze kushirikishwa maisha ya uzima wa milele. Waamini wawe ni watangazaji amini wa Injili ya Furaha inayojikita katika huruma na matumaini; mwanga na faraja kwa wote wanaotembea katika giza na uvuli wa mauti. Ni mwaliko wa kumfuasa Kristo aliyethubutu kuwaendea maskini; akaonesha sifa ya kuwa mchunga mwema kwa kumwendea Kondoo aliyekuwa amepotea, ili kumwonjesha upendo wake. Kwa kushikamana na Yesu, waamini wanaweza kuwa na ujasiri wa kushiriki katika mchakato wa Uinjilishaji Mpya na maendeleo endelevu.

Baba Mtakatifu Francisko katika Kipindi hiki cha Kwaresima anawataka waamini na watu wote wenye mapenzi mema kuonesha ushuhuda wa pekee kwa maskini wa hali, maadili na maisha ya kiroho wanaokutana nao kila siku ya maisha yao, ili waweze kuonja huruma na upendo wa Mungu kwa njia ya Yesu Kristo. Kwaresima ni muda muafaka wa kujisadaka kwa ajili ya kuwasaidia wengine, kwa kutambua kwamba, kwa njia hii pia tunafanya toba.

Waamini wanaweza kuwatajirisha jirani zao na hivyo kushiriki katika mchakato wa kuganga na kuponya umaskini unaomwandama binadamu. Ni matumaini ya Baba Mtakatifu Francisko kwamba, waamini wataweza kukitumia kipindi hiki cha Kwaresima ili kupata neema na baraka zinazobubujika kutoka kwa Kristo mwenyewe!

Ujumbe huu umehaririwa na
Padre Richard A. Mjigwa.
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.



KWARESIMA: Muarobaini wa Maisha ya Kikristu


Neno Kwaresima linatokana na neno la lugha ya kilatini Quadragesima; maana yake, namba arobaini. Kwa hiyo, Kwaresima ni kipindi cha siku arobaini katika  Mwaka wa Liturjia au Mwaka wa Kanisa. Mwaka wa Kanisa ni maadhimisho ya mafumbo ya Ukombozi kwa njia ya Kristo, pamoja na Kristo na ndani ya Kristo katika Kanisa. Mwaka wa Kanisa una vipindi vikuu vitano; Majilio, Noeli, Kwaresima, Pasaka na dominika au jumapili za kawaida. Noeli na Pasaka ndivyo vipindi maalum katika Mwaka wa Kanisa na kabla ya kuadhimishwa hufanyika maandalizi maalum. Noeli huandaliwa kwa kipindi cha Majilio; na Pasaka huandaliwa kwa kipindi cha Kwaresima. Kwaresima huanza siku ya jumatano kwa Ibada ya Jumatano ya Majivu na huisha alhamisi jioni inapoanza Misa ya Karamu ya Bwana ya Alhamisi Kuu ambapo Siku Kuu Tatu za Pasaka huanza. Kwaresima ni kipindi pekee katika Mwaka wa Kanisa ambacho huanza kwa amri ya Kanisa (amri ya pili ya Kanisa): “Shiriki liturjia ya Jumatano ya Majivu, ambayo ni siku ya kufunga chakula; na Ijumaa Kuu iliyo siku ya kutokula nyama.”

Maana ya Kwaresima
Kwaresima ni kipindi muafaka cha kufanya toba. Toba ni sharti la msingi kabisa katika kuutafuta uzima wa milele au ufalme wa mbinguni. Mwenyezi Mungu ndiye anayemwalika mwanadamu ashiriki katika ufalme wake; basi mwanadamu naye anaitikia mwaliko huo kwa kufanya toba. Kwa hiyo toba ni kielelezo cha mwanadamu anayekubali mwaliko wa kuingia katika maisha ya imani ili ashiriki katika ufalme wa Mungu (Mk. 1:15): .....Yesu akaenda Galilaya, akiihubiri Habari Njema ya Mungu akisema, “Wakati umetimia na ufalme wa Mungu umekaribia; tubuni na kuiamini Injili.”

Mwaliko wa Yesu kumtaka mwanadamu afanye toba ndiyo mwanzo wa historia mpya ya uhusiano kati ya Mungu na wanadamu. Tendo la toba linajikita katika maana kuu tatu za msingi:
1)    Kuacha njia potovu. Mtu anapotambua kuwa maisha yake ni kinyume na nia ya Mungu na hivyo anakubali na kuamua kubadilika. Hili ni tendo la toba linalompelekea mtu kubatizwa; na kwa mkristo humpelekea kurudi katika maisha ya kushiriki sakramenti za Kanisa.
2)    Kuacha fikra potovu. Ni mabadiliko ya dhati kwa wakristo wenye fikra potovu kuhusu ukombozi. Baadhi ya wakristo wanapotea kwa kuamini kuwa ubatizo peke yake watosha ili kuokoka. Ubatizo ni mwanzo wa maisha ya kumfuasa Kristo na ni ufunguo wa kuingilia kwenye haki na wajibu wa kikristo.  Kuokoka ni tendo la kuishinda dhambi na kuingia mbinguni. Kwa hivyo basi, si sahihi mtu kusema kuwa ameokoka angali bado yuko hapa duniani. Duniani tunaishi kwenye dhambi na wakati wowote tunaweza bado kuanguka katika dhambi hata kama tumeshabatizwa.
3)    Kuongoka. Ni tendo la kila siku kwa mkristo mwenye fikra sahihi juu ya ukombozi. Kuongoka ni kutambua udhaifu wa kibinadamu na kuitumia vema huruma ya Mungu kwa kuungama dhambi. Dhambi ipo duniani na ina nguvu kuliko sisi wanadamu. Lakini, neema ya Mungu ipo pia na ina nguvu kuliko dhambi. Kufanya toba maana yake ni kuitambua dhambi yako na kuiungama kwa Mungu ili upate neema. Neema ya Mungu inatupatia nguvu ya kupambana na dhambi na inatusaidia kukwepa nafasi ya kutenda dhambi tena.

Kwaresima na Pasaka
Uhalisia wa Kwaresima haupo tu katika toba bali hasa upo katika fumbo la Pasaka. Pasaka ndiyo kiini cha Mwaka wa Kanisa; na ndiyo sherehe kubwa kuliko sherehe zote katika liturjia. Ni sherehe inayoadhimisha ukombozi wa wana wa Mungu kutoka katika utumwa dhambi na kufanyika kwa taifa jipya la Mungu. Kimsingi, Kwaresima ni kipindi cha siku arobaini za toba zinayoitayarisha Pasaka. Pasaka huadhimishwa kila mwaka mara baada ya Kwaresima; na huendelea kuadhimishwa kila jumapili kwa mwaka wote (Jumapili zote zilizo ndani ya kipindi cha Kwaresima hazihesabiwi kati ya siku arobaini). Kila jumapili ni Pasaka, ni siku ya Bwana Mfufuka (dominika) ambapo taifa la Mungu hukusanyika ili kusherehekea ukombozi. Kwa umuhimu wake, Pasaka ya kila mwaka ni lazima itayarishwe kwa kipindi maalum; yaani Kwaresima. Pasaka na Kwaresima ni vipindi vinavyotegemezana. Kwaresima ndiyo inayotuandaa ili tustahili kusherehekea Pasaka.

Nguzo za Kwaresima
Siku arobaini za Kwaresima ni kielelezo cha utimilifu wa maandalizi ya Pasaka. Kadiri ya desturi za kibiblia, namba 1, 3, 7, 10, 12, 40 na 50 huitwa namba kamili. 40 ni namba kamili inayoashiria utimilifu wa kitu fulani. Kwa mfano; Musa alikaa siku arobaini mlimani sinai akisubiri kupewa Amri Kumi za Mungu, waana wa Israeli walisafiri jangwani kuelekea nchi ya ahadi kwa miaka arobaini, Yesu alifunga chakula siku arobaini jangwani kabla ya kuanza kuhubiri Habari Njema, Yesu alipaa mbinguni siku ya arobaini baada ya ufufuko wake. Matukio hayo na mengine mengi kuhusu namba 40 yanaashiria ukamilifu wa jambo fulani katika umuhimu na umaana wake.

Utimilifu wa siku arobaini za Kwaresima hujengwa katika nguzo kuu nne: Neno la Mungu, Sala na Sakramenti, Mfungo, na Matendo Mema.
1)    Neno la Mungu: Kipindi cha Kwaresima ni fursa nzuri ya kujipa muda wa kutosha kwa ajili ya kusoma na kutafakari Neno la Mungu. Tukisoma Biblia tutamjua zaidi Mungu wetu, tutajijua sisi wenyewe na hasa tutaijua nia ya Mungu kwetu ili tuweze kuyafanya mapenzi yake.
2)    Sala na Sakramenti: wakati wa Kwaresima ni vema kusali zaidi sala binafsi na sala za Kanisa ili kujitakatifuza na kuzibariki shughuli zetu za kila siku. Tushiriki Misa Takatifu, tushiriki ibada ya Njia ya Msalaba, tushiriki katika jumuiya zetu, tushiriki sakramenti za Kanisa (hasa Kitubio na Ekaristi Takatifu).
3)    Mfungo: Kwaresima ni wakati muafaka wa kujinyima vitu na mambo ya ziada. Kielelezo kikubwa zaidi ni kufunga chakula. Maana ya kufunga haiishii tu kwenye chakula bali pia ni kuacha mazoea mbalimbali yasiyo ya lazima na yasiyofaa. Kujinyima kunatuwezesha kupata fursa ya kusoma Neno la Mungu, kusali na kufanya matendo mema.
4)    Matendo Mema: Kila mmoja wetu ana shida fulani na anahitaji msaada wa mwenzake. Lakini pia wapo wenzetu wengine wenye shida zaidi kuliko sisi. Kile nilichojinyima kwa kufunga ndicho nimpatie mwenye shida zaidi kuliko mimi. Tuwatembelee wafungwa na wanaoishi katika upweke, tuwatibu wagonjwa, tuwazike wafu, tuwasaidie wazee, yatima na wajane, tuwashauri na kuwaombea wanaopotoka.
Umuhimu wa Kwaresima
Amri ya pili ya Kanisa inamtaka kila mkristo kushiriki kipindi cha Kwaresima tangu siku ya kwanza, yaani Jumatano ya Majivu. Toba ndiyo roho ya Kwaresima iliyojengwa juu ya Neno la Mungu, kusali, kushiriki sakramenti, kufunga na kufanya matendo mema. Siku arobaini za Kwaresima ni kielelezo kamili kinachotufundisha kuwa toba ni tendo la kila siku katika maisha ya mkristo. Wakati wa Kwaresima toba husisitizwa zaidi na kwa namna ya pekee ili kumjenga mkristo katika wajibu wa kuiishi imani. Katika kuiishi imani yetu tunapambana na shetani ambaye nia yake ni kuharibu mpango wa Mungu wa ukombozi. Silaha kubwa ya kupambana na shetani ni kuiishi roho ya toba inayojikita katika Neno la Mungu, sala na sakramenti, mfungo na matendo mema. Bwana wetu Yesu Kristo alifunga jangwani kwa siku arobaini kama maandalizi ya kufanya matendo mema ya kumkomboa mwanadamu. Kwa siku arobaini alifunga na kusali akamshinda shetani kwa kulitumia vema Neno la Mungu (Mt. 4:1-11). Kwa mfano huo wa Yesu, mkristo anatakiwa kuiishi toba wakati huu wa Kwaresima ili astahili kuishiriki Pasaka. Mkristo anatakiwa kuiishi kwa dhati toba ya kila siku ili amshinde shetani na hatimaye aingie kwenye Pasaka ya milele mbinguni.
Makala haya yameandaliwa na;
Dk. Padri Leonard Maliva Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustimo Stella Maris Mtwara. simu namba 0754666908