Week Hot newz

Papa ashukuru mapokezi mazuri ya Tirana Albania.

Katekesi ya Papa kwa mahujaji wageni kwa Jumatano hii mjini Vatican, imetafakari safari yake ya kitume katika Mji Mkuu wa Tirana Albania. Ziara ya siku moja lakini aliyoitaja kwamba, ilijaa utajiri mkubwa wa upendo na mshikamano kati ya Jimbo Takatifu na nchi ya Albania.

Katika Maelezo, Papa Francisco amesema, alikwenda Albania, kuonyesha mshikamano wake wa karibu na Kanisa zima na watu wa Albania, taifa ambalo kwa muda wa miaka mingi, liliteswa na kushamiri kwa ukana Mungu , na unyama wa serikali isiyojali uwepo wa Mungu. Baada ya kuangushwa kwa mamlaka hayo, sasa taifa linahitaji kupewa moyo, kwa ajili ya ufanikishaji wa kazi nyingi za kuijenga upya jamii, ili iwe ni jamii yenye kupenda amani na kuheshimiana na kushirikiana katika huduma, kwa ajili ya manufaa ya wote.

Papa ameonyesha kufurahi na kumshukuru Mungu, kwa uwepo wa roho ya mshikamano na mazungumzo kati ya jamii Albania licha ya tofauti za kidini na kitamaduni. Anamwoba Bwana, ili taifa hili lisonge mbela na roho huyo, na kamwe lisirudishwe nyuma katika mateso makali ya ukana Mungu. Papa alieleza kwa kuurejea Mkutano wake na viongozi wa dini mbalimbali, ambamo aliweza mwenyewe kuushuhudia moyo huo wa kuheshimiana na kushirikiana, uliojengwa juu ya utambulisho wa kila mmoja.

Daily Reading for Saturday, September 20th, 2014

Reading 1, First Corinthians 15:35-37, 42-49

35 Someone may ask: How are dead people raised, and what sort of body do they have when they come?
36 How foolish! What you sow must die before it is given new life;
37 and what you sow is not the body that is to be, but only a bare grain, of wheat I dare say, or some other kind;
42 It is the same too with the resurrection of the dead: what is sown is perishable, but what is raised is imperishable;
43 what is sown is contemptible but what is raised is glorious; what is sown is weak, but what is raised is powerful;
44 what is sown is a natural body, and what is raised is a spiritual body. If there is a natural body, there is a spiritual body too.
45 So the first man, Adam, as scripture says, became a living soul; and the last Adam has become a life-giving spirit.
46 But first came the natural body, not the spiritual one; that came only afterwards.
47 The first man, being made of earth, is earthly by nature; the second man is from heaven.
48 The earthly man is the pattern for earthly people, the heavenly man for heavenly ones.
49 And as we have borne the likeness of the earthly man, so we shall bear the likeness of the heavenly one.

Responsorial Psalm, Psalms 56:10-12, 13-14

10 In God whose word I praise, in Yahweh whose word I praise,
11 in God I put my trust and have no fear; what can mortal man do to me?
12 I am bound by the vows I have made, God, I will pay you the debt of thanks,
13 for you have saved my life from death to walk in the presence of God, in the light of the living.

Gospel, Luke 8:4-15

4 With a large crowd gathering and people from every town finding their way to him, he told this parable:
5 'A sower went out to sow his seed. Now as he sowed, some fell on the edge of the path and was trampled on; and the birds of the air ate it up.
6 Some seed fell on rock, and when it came up it withered away, having no moisture.
7 Some seed fell in the middle of thorns and the thorns grew with it and choked it.
8 And some seed fell into good soil and grew and produced its crop a hundredfold.' Saying this he cried, 'Anyone who has ears for listening should listen!'
9 His disciples asked him what this parable might mean,
10 and he said, 'To you is granted to understand the secrets of the kingdom of God; for the rest it remains in parables, so that they may look but not perceive, listen but not understand.
11 'This, then, is what the parable means: the seed is the word of God.
12 Those on the edge of the path are people who have heard it, and then the devil comes and carries away the word from their hearts in case they should believe and be saved.
13 Those on the rock are people who, when they first hear it, welcome the word with joy. But these have no root; they believe for a while, and in time of trial they give up.
14 As for the part that fell into thorns, this is people who have heard, but as they go on their way they are choked by the worries and riches and pleasures of life and never produce any crops.
15 As for the part in the rich soil, this is people with a noble and generous heart who have heard the word and take it to themselves and yield a harvest through their perseverance.

Tafakari ya Neno la Mungu Domonika ya 25 ya Mwaka A,



Mpendwa, tunatafakari masomo ya Jumapili ya 25 ya mwaka wa A wa Kanisa, tukialikwa kuwa na matumaini daima katika kumtafuta Bwana na kutambua kuwa wema wa Mungu ni wa milele kwa watu wote na fikra zake ni tofauti na fikra za kibinadamu. Katika somo la kwanza Waisraeli wako utumwani Babeli kwa sababu hawakutii mausia ya Bwana na zaidi wanaona hawawezi kusamehewa dhambi zao, wamepoteza tumaini na wanaona kana kwamba Mungu amewatupa na kuwaacha kabisa. Zaidi ya hilo wanaongeza kosa jingine tena la kumwona Mungu anayefikiri kama wao, wanafikiri hawezi kuwasamehe tena.


Mpendwa, katika shida yao hiyo Mungu anamtuma Nabii Isaya awaambie kuwa fikra na njia za Mungu ni za juu mno ni tofauti na fikira za kibinadamu kiasi kwamba si rahisi kuzielewa. Zaidi ya hilo Isaya anawakumbusha kuacha njia zao mbaya na kumrudia Bwana. Kumrudia Bwana si tu kuacha dhambi, bali pia kubadili namna ya kumtazama Mungu, Mungu aliye haki na mkamilifu. Mawazo haya yatajitokeza waziwazi katika Injili ambapo tunaona Mungu anayewapenda wote wadhambi kwa wema.

TB Joshua awakosoa waandishi walioandika ghorofa 6 za kanisa lake zimeporomoka, aeleza kilichotokea



Kanisa la mhubiri maarufu wa Nigeria, TB Joshua linalojulikana kama The Synagogue Church of All Nations limetoa tamko rasmi kuhusu tukio la kuporomoka kwa jengo la ghorofa sita la kanisa hilo, tukio lililoripotiwa kuua watu kadhaa na kujeruhi, Ijumaa.
Katika tamko hilo lililowekwa kwenye ukurasa wao wa Facebook, wamewakosoa waandishi walioripoti kuwa kanisa zima limeporomoka na kwamba sio kanisa wanalotumia kwa ibada bali ni jengo.
“Hili ni tamko rasmi kutoka The Synagogue, Church Of All Nations kuhusu habari zinazoripotiwa hivi sasa na vyombo vya habari kufuatia tukio lililotekea leo. Ni jengo na sio kanisa (tunalotumia kwa ibada) kama ilivyoripotiwa. Watu wachache waliokuwa mule wameokolewa. Unachotaka kitokee kwa wenzako, Mungu anakutakia wewe. Hakuna kinachotufanya sisi kumpenda mtu kama kumuombea. Kadiri navyokupenda, ndivyo kadiri nitakavyokuombea.” Limesomeka tamko hilo.
Ingawa hawakuzungumzia kabisa kuhusu watu kupoteza maisha au la..taarifa za awali zimeeleza kuwa watu makumi wamepoteza maisha. Baadhi ya mashuhuda walisema kuwa wameona miili ya watu waliopoteza maisha ikitolewa katika jengo hilo.
Hata hivyo bado hakuna uthibitisho wa daktari kuhusu taarifa hizo za watu kupoteza maisha.
Inaelezwa kuwa zaidi magari ya wagonjwa (ambulance) 20 yalionekana yakitoka katika eneo hilo yakiwa na majeruhi.


Daily Reading for Thursday, September 4th, 2014

18 There is no room for self-delusion. Any one of you who thinks he is wise by worldly standards must learn to be a fool in order to be really wise.
19 For the wisdom of the world is folly to God. As scripture says: He traps the crafty in the snare of their own cunning
20 and again: The Lord knows the plans of the wise and how insipid they are.
21 So there is to be no boasting about human beings: everything belongs to you,
22 whether it is Paul, or Apollos, or Cephas, the world, life or death, the present or the future -- all belong to you;
23 but you belong to Christ and Christ belongs to God.

Responsorial Psalm, Psalms 24:1-2, 3-4, 5-6

1 [Psalm Of David] To Yahweh belong the earth and all it contains, the world and all who live there;
2 it is he who laid its foundations on the seas, on the flowing waters fixed it firm.
3 Who shall go up to the mountain of Yahweh? Who shall take a stand in his holy place?
4 The clean of hands and pure of heart, whose heart is not set on vanities, who does not swear an oath in order to deceive.
5 Such a one will receive blessing from Yahweh, saving justice from the God of his salvation.
6 Such is the people that seeks him, that seeks your presence, God of Jacob.Pause

Gospel, Luke 5:1-11

1 Now it happened that he was standing one day by the Lake of Gennesaret, with the crowd pressing round him listening to the word of God,
2 when he caught sight of two boats at the water's edge. The fishermen had got out of them and were washing their nets.
3 He got into one of the boats -- it was Simon's -- and asked him to put out a little from the shore. Then he sat down and taught the crowds from the boat.
4 When he had finished speaking he said to Simon, 'Put out into deep water and pay out your nets for a catch.'
5 Simon replied, 'Master, we worked hard all night long and caught nothing, but if you say so, I will pay out the nets.'
6 And when they had done this they netted such a huge number of fish that their nets began to tear,
7 so they signalled to their companions in the other boat to come and help them; when these came, they filled both boats to sinking point.
8 When Simon Peter saw this he fell at the knees of Jesus saying, 'Leave me, Lord; I am a sinful man.'
9 For he and all his companions were completely awestruck at the catch they had made;
10 so also were James and John, sons of Zebedee, who were Simon's partners. ButJesus said to Simon, 'Do not be afraid; from now on it is people you will be catching.'
11 Then, bringing their boats back to land they left everything and followed him.

Barua

BARUA KWENDA KWA MWENYEZI MUNGU:
MAHABUSU GEREZA LA KEKO SELO NO: 2
TAREHE 10/07/2013
MWENYEZI MUNGU,MUNGU WA IBRAHIMU, MUNGU WA ISLAEL,
MUNGU WA ISAKA,MUNGU WANGU  LEO NIMEISIKIA SAUTI YAKO,
NAFANYA BIDII KUTUNZA NA KUFANYA MAAGIZO YAKO,
MUNGU WANGU UNITUKUZE JUU YA MATAIFA YOTE,
BARAKA ZAKO ZOTE ZINIJALIA,
NIZIDISHIE BARAKA NIBARIKIE MJINI NIBARIKIWE SHAMBANI,
MUNGU UNIFANYA NIWE WA HERI KATIKA UZAO WA TUMBO LANGU NA KATIKA NCHI BWANA ULIYONIPATIA,
MUNGU BABA MUNGU MTAKATIFU SANA MUNGU MWANZO NA MWISHO,
MUNGU BABA WA MWANA YESU KRISTO NA ROHO MTAKATIFU UNIBARIKI NIINGIAPO NA NANITOKAPO,
UWAFANYE  ADUI WAINUKAO JUU YANGU KUPIGWA MBELE YA MACHO YANGU,
WAMENITOKEA KWA NJIA MOJA  WAKIMBIA MBELE YA MACHO  YANGU KWA NJIA SABA,
MUNGU BARAKA YAKO ZIKAE  JUU YANGU NA JUU YA MKE WANGU,
BARAKA ZIWE ZIIDI JUU YA WATOTO WANGU NA KATIKA FAMILIA YANGU,
MWENYEZI MUNGU  NIFANYE KICHWA SIO MKIA,
NAMI NIWE JUU ZAIDI NA SIO CHINI,
MUNGU NIFUNULIE HAZINA NZURI NAYO NI MBINGU,
KWA KUINYESHEA MVUA NCHI YANGU,
MWENYEZI MUNGU  BARIKI KAZI YOTE YA MIKONO YANGU,
 NAMI NITAKOPESHA WALA SITOKOPA TENA,

SHUSHA BARAKA SASA KWA NJIA YA KRISTO BWANA NA MKOMBOZI WANGU, AMINA.

Dawa za kulevya ni haramu!

Baba Mtakatifu Francisko, Ijumaa tarehe 20 Juni 2014 amekutana na wajumbe waliokuwa wanashiriki kwenye mkutano wa kimataifa kuhusu uthibiti wa dawa za kulevya, tatizo ambalo linaendelea kusababisha majanga makubwa kwa watu wa nyakati hizi.

Auawa kwa kupigwa risasi

MKAZI wa Kijiji cha Masuguru, Kata ya Masagala, wilayani Kishapu, Juma Masalu (25), ameuawa kwa kupigwa risasi baada ya kuingia katika mgodi wa Almasi unaomilikiwa na Wiliamson Diamond. Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Shinyanga, Kamishina Msaidizi Kihenya Kihenya, alisema tukio hilo lilitokea Juni 13, saa 5 usiku wakati Masalu na wenzake 20 walipoingia ndani ya mgodi huo kwa nia ya kuiba mchanga wenye madini ya almasi.
Kamanda Kihenya alisema wakati wakiiba

Wadau wakutana kupinga ubakaji


Angelina Jolie ni mmoja wa wanaharakati maarufu wanaopinga dhuluma za kingono ikiwemo ubakaji
Viongozi wa kimataifa wanakutana jijini London kwa wiki nzima, kwa kongamano la kumaliza dhulma za kimapenzi katika mataifa yanayokabiliwa na mizozo.
Mkutano huo, wa siku nne umeandaliwa

Saratani ya mlango wa kizazi tatizo Tanzania


Rais Jakaya Kikwete, amesema Tanzania inatambulika kuwa ni moja ya nchi zenye kiwango kikubwa cha maradhi ya saratani ya mlango wa kizazi  Afrika ya Mashariki na kwamba inakadiriwa kuwa takriban wanawake 56 katika kila wanawake 100,000, hupata saratani hii.

Kadhalika, inakadiriwa pia kuwa zaidi ya watu 35,000 hupata saratani hiyo kila mwaka na zaidi ya watu 27,000 hupoteza maisha huku ripoti ikionyesha mwaka 2010 peke yake, wanawake 6,000 waligundulika kuwa na saratani ya mlango wa kizazi na  4,000 kati yao walikufa kutokana na maradhi hayo.

Rais Kikwete aliyasema hayo wakati akizungumza

Roho Mtakatifu anafundisha, anakumbusha, anasali na kufanya unabii!

Baba Mtakatifu Francisko katika maadhimisho ya Siku kuu ya Pentekoste, tarehe 8 Juni 2014 kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican wakati wa mahubiri yake anasema kwamba, Yesu aliwaahidia Mitume wake zawadi kutoka kwa Baba, yaani Roho Mtakatifu na ahadi hii inatekelezwa wakati wa Siku kuu ya Pentekoste.

Hili ni tukio endelevu linaojionesha katika maisha na utume wa Kanisa, kwani Roho Mtakatifu analihuisha Kanisa, anawafundisha, anawakumbusha na kuwasaidia waamini kuzungumza.

Papa Francisko anasema, Roho Mtakatifu ni mwalimu wa maisha yandani anayewaonesha waamini dira na njia ya maisha kama alivyofanya wakati wa Kanisa la mwanzo. Roho Mtakatifu ni njia kama alivyo Yesu mwenyewe, kwani anawasaidia waamini kumfuasa Kristo na kutembea katika nyayo zake. Roho Mtakatifu ni mwalimu wa maisha, ujuzi na maarifa katika uwepo na utume wa maisha ya Kikristo.

Roho Mtakatifu anawakumbusha waamini yale ambayo Yesu

Pentekoste

Tafakari imeletwa kwako na Pd Richard Tiganya, C.PP.S.  

Ni siku nyingine tena tunapokutana katika meza ya Neno la Mungu. Leo tunaadhimisha sherehe ya Pentekoste, sherehe ambayo katika kalenda ya litrujia huja siku hamsini baada ya pasaka. RealAudioMP3

Ni sherehe ambayo wakristu humshangilia Kristu mfufuka katika Roho Mtakatifu na kufurahia ukombozi ambao umeletwa na Kristo mwenyewe. Katika sherehe ya Pentekoste fumbo la pasaka hukamilika maana ni katika sikukuu hii Roho Mtakatifu hulishukia Kanisa ili likaendeleze kazi ya Kristu bila woga, likiwa na nguvu za kimungu. Ni sherehe ambayo kwayo Roho Mtakatifu huthibitisha muungano wetu na Mungu. Ujumbe wa Neno la Mungu unalala katika Roho Mtakatifu kuwa sheria mpya na nguvu ya Wakristu, taifa jipya lililoshikamana katika upendo na Mungu.

Katika somo la kwanza toka kitabu cha Matendo

Njoo Roho Mtakatifu!



Kumsadiki Roho Mtakatifu ni kukiri Nafsi ya tatu ya Fumbo la Utatu Mtakatifu, atokaye kwa Baba na Mwana na anayeabudiwa na kutukuzwa pamoja na Baba na Mwana. Huyu ndiye Roho Mtakatifu aliyetumwa mioyoni mwa waamini, ili kupokea uzima mpya wa wana wateule wa Mungu. RealAudioMP3

Katika Fumbo la Utatu Mtakatifu usiogawanyika, Mwana na Roho ni Nafsi tofauti lakini hawatenganiki. Tangu mwanzo hadi mwisho wa nyakati, Baba anapomtuma Mwanaye, anamtuma pia Roho wake anayewaunganisha na Kristo kwa imani ili waamini wakiwa wamefanywa waana waweze kumwita Mungu, Abba, yaani Baba.

Siku hamsini baada ya ufufuko wake nidyo Siku kuu ya Pentekoste, Yesu Kristo aliyetukuzwa mbinguni alimmimina Roho Mtakatifu pasi na kipimo, akamdhihirisha kuwa Nafsi ya Kimungu, hivi kwamba, Fumbo la Utatu Mtakatifu limefunuliwa kikamilifu. Utume wa Kristo na ule wa Roho Mtakatifu vilikuwa utume wa Kanisa, lililopelekwa litangaze na kueneza Fumbo la Umoja wa Utatu Mtakatifu.

Kwa ufupi, Roho Mtakatifu anajenga, anahuisha na kutakasa Kanisa. Roho Mtakatifu anawarudishia Wabatizwa hali ya kufanana na Mungu iliyopotezwa kwa njia ya dhambi na anawafanya waishi ndani ya Kristo uzima uleule wa Fumbo la Utatu Mtakatifu. Anawatuma washuhudie ukweli wa Kristo na kuwapanga katika kazi zao maalum, ili wote wazae tunda la Roho.

Hili ndilo Fumbo ambalo linatarajiwa kuadhimishwa na Baba Mtakatifu Francisko katika Siku kuu ya Pentekoste, Jumapili ijayo kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican kuanzia saa 4:00 asubuhi kwa saa za Ulaya, kadiri ya taarifa iliyotolewa na Monsinyo Guido Marini Mshereheshaji mkuu wa Ibada za Kipapa.

Historia ya Kanisa la Sabato (4)

NDUGU yangu, ninatumaini nimekufikisha mahali pazuri. Hiyo ndiyo historia ya mshazari wa Kanisa la Wasabato. Kifupi haina mashiko na mtiririko wa kimantiki. Hata hivyo baada ya kuzaliwa kimtindo namna hiyo, Kanisa la Wasabato halikubaki moja kifikra na kimtazamo. Ukilichungulia ndani, Kanisa la Wasabato ni Muungano wa Vikundi vitatu vya Waadventisti; Kikundi cha Bw. Hiram Edson, kilichosisitiza zaidi mafundisho ya huduma ya Yesu Patakatifu pa Patakatifu mbinguni, Kikundi cha Bw. Joseph Bates, kilichosisitiza zaidi kufuata Sabato ya Agano la

Mwanamke Aadhibiwa kwa kumtelekeza mume


Roseline anadaiwa kuwatelekeza watoto wake wanaoishi na baba yao
Na Paskal Linda-Kenya.
Mwanamke mmoja nchini Kenya ameamrishwa na mahakama kumlipa mumewe shilingi elfu tatu au dola 35 kama hela za kukidhi mahitaji yake na watoto wake kila mwezi.
Mwanamke huyo kwa jina Roselyn Muyonga, ambaye anatuhumiwa kwa kuwatelekeza mumewe na watoto wake watatu , huenda akafungwa miezi mitano jela au kutozwa faini ya shilingi laki mbili ikiwa atakosa kutekeleza amri ya mahakama.
Mwanamume huyo hufanya kazi za kibarua.

Kila toba ni Pentekoste Mpya!

 Na: Paskal LindaKardinali Mauro Piacenza, mhudumu mkuu wa Toba katika barua yake kwa mapadre waungamishaji anasema kwamba, kila mara Mkristo anapoungama dhambi zake na kupokea msamaha, huruma na upendo wa Mungu kutoka kwenye kiti cha maungamo, kwa Mkristo hii ni Pentekoste Mpya! Siku kuu ya Pentekoste, ili ni fursa kwa waamini kujipatanisha na Mungu pamoja na jirani zao, ili kuweza kumpokea vyema Roho Mtakatifu anayemiminwa mioyoni mwao, tayari kumtolea Mwenyezi Mungu ushuhuda wa maisha adili na matakatifu!

Neema ya Sakramenti ya Upatanisho anasema Kardinali Piacenza ni mang'amuzi mapya ya Pentekoste kwani hapa Roho Mtakatifu anaendelea kulitakasa Kanisa la Kristo kwa njia ya huduma ya maungamo inayotolewa na Padre akiwa ameungana na Yesu Kristo, ili kusikiliza na kupima, kuamua na kutoa ushauri na hatimaye, kuponya dhambi kwa kumwondolea mwamini dhambi zake. Hii ni kazi ya Roho Mtakatifu anayetenda kwa njia ya wachungaji wake wanaojisadaka katika viti vya maungamano.

Mapadre wanakumbushwa kwamba, wamechaguliwa na kuwekwa wakfu kwa ajili ya kuwahudumia watu wa Mungu si kwa mastahili yao wenyewe bali kwa njia ya neema ya Roho Mtakatifu inayowaunganisha kwa dhati kabisa na Kristo mwenyewe, ili kushiriki upendo na kazi yake ya ukombozi. Kwa sababu hii, Padre ni mhudumu wa huruma ya Mungu na daraja kati ya waungamaji na Kristo mwenyewe.

Mapadre wanachangamotishwa na Mama Kanisa kuwa wasikivu kwa Roho Mtakatifu na karama zake zinazoliwezesha Kanisa kujitakasa na kuwatakatifuza watoto wake kwa njia ya Sakramenti ya Upatanisho!

Upendo kwa Mungu na jirani!

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S.
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
 
Baba Mtakatifu Francisko katika utume wake kama Khalifa wa Mtakatifu Petro amegusia mambo msingi katika maisha na utume wa Kanisa kwa kukazia zaidi na zaidi kanuni maadili na utu wema; utu na heshima ya binadamu; tunu msingi za maisha ya ndoa na familia: Yote haya ni kadiri ya Mafundisho ya Kanisa Katoliki na Kweli za Kiinjili na wala hakuna mabadiliko! RealAudioMP3

Baba Mtakatifu Francisko anapozungumzia masuala haya kwa unyenyekevu mkubwa kutokana na uzoefu wake katika shughuli za kichungaji kuna baadhi ya watu wanapata hisia kwamba, pengine anataka kubadilisha mafundisho na msimamo wa Kanisa Katoliki katika masuala haya, lakini ukweli wa mambo ni kwamba, anachofanya ni kuendelea kukazia masuala haya kwa mwelekeo mpya zaidi!

Ametuacha vibaya!

Amepaa mbinguni na ameketi mkono wa kuume wa Mungu:

Siku arobaini baadaye ….. Mt. 1,23 – Mungu yu nasi leo tena tunasikia tamko hilo la Yesu mwenyewe.Maana yake nini? Hivyo tunaadhimisha leo uwepo wa Mungu kati yetu na uwepo wa Mungu kati yetu waoneshwa na kazi za watu wake wanaomtii Roho Mtakatifu.

I. Mdo 1,1-11
II. Efe. 1,17-23
III. Mt. 28,16-20

UTANGULIZI

Sherehe ya kanisa siku 40 baada ya sherehe ya Pasaka - kupaa mbinguni Bwana wetu Yesu Kristo. Mhubiri mmoja asema hakuna awezaye kukaa peke yake mke/mume ahitaji mke/mume mwema, mwalimu ahitaji wanafunzi wa kinyume chake nini?

Hivi pia kwa mkristo leo hii yupo Roho Mtakatifu na

Rais mpya wa Malawi aapishwa rasmi


Peter Muthirika anayeongoza chama cha DPP.
Rais mpya wa Malawi Peter Mutharika ameapishwa rasmi baaada ya kucheleweshwa kwa matokeo ya uchaguzi kufuatia madai ya udanganyifu na wizi wa kura.
Mutharika aliibuka mshindi wa uchaguzi huo baada ya kujipatia zaidi ya asilimia 36 ya kura zilizopigwa.
Rais anayeondoka mamlakani Joyce Banda alikuwa katika nafasi ya tatu.
Banda amewataka wafuasi wake kuheshimu matokeo hayo.
Mahakama kuu ilipinga ombi la kura kuhesabiwa upya baada ya Banda kudai kuwa kumekuwa na udanganyifu mkubwa katika shughuli hiyo.
Peter Mutharika aliwahi kuhudumu kama