TAASISI ya Bilal Muslim Mission of Tanzania imewashauri Watanzania
kujitolea damu salama ili kuokoa maisha ya wengi wanaohitaji damu
hospitalini.
Ombi hilo limetolewa juzi na Mwenyekiti wa taasisi hiyo, Sibtain
Meghji, alipozungumza wakati wa utoaji damu salama, tukio
lililofadhiliwa na taasisi hiyo jijini Mwanza.
Meghji alisema utoaji damu salama unatakiwa kufanywa na kila mtu
mwenye sifa ili kuisaidia jamii iliyopo hospitalini ikihitaji huduma
hiyo muhimu.
“Sote tunajua kwamba damu ni kiungo muhimu kwa mwili wa mwanadamu…
kwa hiyo mimi naomba sana Watanzania wote tujenge hulka ya kujitolea
damu mara kwa mara kwa ajili ya ndugu zetu,” alisema Meghji.
Alisema kila mwaka taasisi hiyo ya Bilal Muslim Mission of Tanzania
kwa kushirikiana na waumini wote wa madhehebu ya Shia, wanachangia
damu, ambapo jana ilitarajiwa kupata zaidi ya watu 400.
Kwa upande wake, Ofisa Uhamasishaji wa Mpango wa Damu Salama Kanda ya
Ziwa, Vincent Muhada, alisema zaidi ya chupa 40,000 za damu salama
zinahitajika katika hospitali mbalimbali za mikoa ya Kanda ya Ziwa.
Alisema mahitaji halisi ya damu salama kwa mikoa ya Kanda ya Ziwa ni
chupa 70,000 lakini hadi sasa chupa 25,000 hadi 30,000 zimeshapatikana,
hivyo kusababisha upungufu wa chupa 40,000.
Week Hot newz
-
Tafakari ya Neno la Mungu Jumapili ya IV ya Mwaka C wa Kanisa. - OSS_ROM 28/01/2016 14:25 Mitandao ya kijamii: “...
-
Rubani msaidizi, Andreas Lubitz, aliangusha makusudi ndege hiyo kwenye milima ya Alps. Wachunguz...
-
Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI, Ijumaa, tarehe 27 Desemba 2013 amemtembelea Papa Francisko na kupata chakula cha pamoja...
-
Watawa wa Mama Theresa wa Calcutta waliouwawa huko Yemen ni mashuhuda wa upendo na wahanga wa utandawazi usiojali wala kuguswa na maha...
-
Yesu amekuja ulimwenguni ili kuufunua, kuutangaza na kuus...
-
Daily Reading for Tuesday, March 22nd, 2016 Reading 1, Isaiah 49:1-6 1 Coasts and islands, listen ...
-
Watu 6 wamejeruhiwa katika mlipuko uliotokea katika uwanja wa ndege ulioko mjini Beledweyne nchini Somalia.
-
By Paskal Linda (Batarokota Network ) Feast Day October 22 With St. John Paul II feast day just around the corner, T...
-
Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya maadhimisho ya Ib...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni