Jengeni
matumaini kwa Bwana, hata katika hali ngumu, Papa amehimiza wakati wa
Ibada ya Misa ya asubuhi Jumatatu hii katika Kanisa dogo la Mtakatifu
Marta mjini Vatican. Papa alisisitiza kwamba Wakristo wameitwa kufanya
maamuzi thabiti , kama yanavyo fundisha maisha ya mashahidi wa dini wa
kila wakati. Hata leo, alibainisha, kuna wake kwa waume wanao teseka kwa
sababu ya imani yao kwa Kristu. Na hivyo wao ni mfano kwetu wa kuiga,
kwa ajili ya kupata nguvu za kujikabidhi kwa Bwana bila kujibakiza.
Papa
aliendelea kufundisha kwamba, kumchagua Kristu, hakuna ukomo. Alieleza
hilo akingalisha katika somo la Kitabu cha Nabii Daniel, na Injili :
ambamo vijana Wayahudi watumwa katika mahakama ya Nebukadreza na mjane
aliyekwenda katika hekalu kumwabudu Bwana. Katika kesi zote, Papa
anaona, hapakuwa na ukomo wa hali. Mjane katika hali ya umaskini na
vijana katika hali ya utumwa, wote walijikabidhi kwa Bwana . Mjane
aliweka vyote alivyokuwa navyo katika hazina ya Hekalu, ambapo kwa
vijana walibaki aminifu kwa Bwana, hata katika hatari ya maisha.
Papa
aliendelea kusema, katika hali za wote, mjane na vijana – hawakujali
hatari za maisha zilizokuwa mbele yao. Walimchagua Bwana kwa moyo moja,
bila wasiwasi na bila upungufu. Kwao Bwana alikuwa ni juu ya yote juu.
Walitambua Bwana wao ni Mungu na kwake walijikabidhi wenyewe. Na hii
hawakufanya kwa sababu za kujitafutia sifa bandia , lakini walifanya
hivyo kwa kutambua kwamba, Bwana ndiye mkuu wa yote. Walijua kwamba
Bwana ni mwaminifu. Na ndivyo tunavyotakiwa nasi pia kufanya.
Ni
kumtegemea Bwana kwa uaminifu na imani kwamba daima yupo, kwa sababu
Bwana hawezi kubadilika kubadilika na kujikana mwenyewe. Imani hii
katika Bwana Papa Francisko aliongeza, huongoza katika maamuzi thabiti
ya kumchagua Yeye kuwa ndiye Bwana wa Yote, Yeye ni mwaminifu, katika
katika mambo yote madogo , makubwa na hata magumu.
Papa alieleza
na kuitazama historia ya kanisa kwamba, historia yake inaonyesha
wanaume, wanawake, wazee, vijana, waliofanya uchaguzi huu, kama tunavyo
sikia katika vyombo vya mawasiliano au kusoma katika magazeti juu ya
maisha ya mateso yanayokabili hata leo hii, Wakristo katika maeneo
mbalimbali duniani.
Wakristu hao wanaoishi nasi katika wakati
huu, ni mfano hai kwetu, wenye kutuhimiza pia sisi, kuiweka hazina
yetu ndani ya kanisa, ili kwamba, ambamo Bwana yumo ndani mwake.
Ushuhuda wa Wakristu hawa wateswa, unashuhudia neema ya ujasiri wa
kusonga mbele katika maisha ya Kikristo , katika hali ya kawaida ,
maisha magumu na hata katika mazingira hatarishi . Ni kuwa na Maamuzi
thabiti kwa Bwana.
Week Hot newz
-
Tafakari ya Neno la Mungu Jumapili ya IV ya Mwaka C wa Kanisa. - OSS_ROM 28/01/2016 14:25 Mitandao ya kijamii: “...
-
Rubani msaidizi, Andreas Lubitz, aliangusha makusudi ndege hiyo kwenye milima ya Alps. Wachunguz...
-
Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI, Ijumaa, tarehe 27 Desemba 2013 amemtembelea Papa Francisko na kupata chakula cha pamoja...
-
Watawa wa Mama Theresa wa Calcutta waliouwawa huko Yemen ni mashuhuda wa upendo na wahanga wa utandawazi usiojali wala kuguswa na maha...
-
Yesu amekuja ulimwenguni ili kuufunua, kuutangaza na kuus...
-
Daily Reading for Tuesday, March 22nd, 2016 Reading 1, Isaiah 49:1-6 1 Coasts and islands, listen ...
-
Watu 6 wamejeruhiwa katika mlipuko uliotokea katika uwanja wa ndege ulioko mjini Beledweyne nchini Somalia.
-
By Paskal Linda (Batarokota Network ) Feast Day October 22 With St. John Paul II feast day just around the corner, T...
-
Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya maadhimisho ya Ib...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni