Baba Mtakatifu Francisko kwa kuguswa na mahangaiko ya wananchi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, anawaalika watumiaji wa mitandao ya kijamii, kumuunga mkono katika kusali kwa ajili ya kuombea amani na utulivu huko Jamhuri ya Watu wa Afrika ya Kati na Sudan ya Kusini.
Week Hot newz
-
Tafakari ya Neno la Mungu Jumapili ya IV ya Mwaka C wa Kanisa. - OSS_ROM 28/01/2016 14:25 Mitandao ya kijamii: “...
-
Rubani msaidizi, Andreas Lubitz, aliangusha makusudi ndege hiyo kwenye milima ya Alps. Wachunguz...
-
Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI, Ijumaa, tarehe 27 Desemba 2013 amemtembelea Papa Francisko na kupata chakula cha pamoja...
-
Watawa wa Mama Theresa wa Calcutta waliouwawa huko Yemen ni mashuhuda wa upendo na wahanga wa utandawazi usiojali wala kuguswa na maha...
-
Daily Reading for Tuesday, March 22nd, 2016 Reading 1, Isaiah 49:1-6 1 Coasts and islands, listen ...
-
Watu 6 wamejeruhiwa katika mlipuko uliotokea katika uwanja wa ndege ulioko mjini Beledweyne nchini Somalia.
-
By Paskal Linda (Batarokota Network ) Feast Day October 22 With St. John Paul II feast day just around the corner, T...
-
Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya maadhimisho ya Ib...
-
Interested In Learning More About The Catholic Church? Welcome! This page explains the process by which one can - through their l...
Ombeeni amani Barani Afrika!
Baba Mtakatifu Francisko kwa kuguswa na mahangaiko ya wananchi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, anawaalika watumiaji wa mitandao ya kijamii, kumuunga mkono katika kusali kwa ajili ya kuombea amani na utulivu huko Jamhuri ya Watu wa Afrika ya Kati na Sudan ya Kusini.
Rais wa Cyprus akutana na Papa!
Viongozi hawa wawili wamejadili pamoja na mambo mengine kuhusu uhusiano kati ya Cyprus na Vatican; mchango mkubwa unaotolewa na Kanisa Katoliki nchini humo pamoja na umuhimu wa kuendelea kusimama kidete kulinda na kutetea uhuru wa kidini. Kwa pamoja wameonesha matumaini makubwa baada ya kuanza tena majadiliano ya kisiasa yanayopania kupata ufumbuzi wa kudumu kutokana na hali ngumu inayoendelea nchini Cyprus kwa sasa.
Baba Mtakatifu na mgeni wake wameangalia pia kinzani, migogoro na vita huko Mashariki ya Kati ambayo imesababisha maafa makubwa kwa watu na mali zao. Ni matumaini ya viongozi hawa kwamba, Jumuiya za Kikristo huko Mashariki ya kati zitachangia katika ustawi na maendeleo ya Ukanda huu.
10 Top Churches in Norfolk
![]() There were over 1,000 medieval churches built in Norfolk and 659 still remain, this is the greatest concentration in the world. Not only are these beautiful internationally important buildings, but they contain hundreds of medieval works of art and craftsmanship. The simple and easily built round towers of early times gave way to the rich and spacious buildings in the prosperous Middle Ages, many noted for their beautiful rood screens, decorated roofs and bench carvings. The decline in the population of Norfolk left many churches isolated from their villages, but their towers still dominate the Norfolk landscape. Each of these wonderful buildings, offers a great place to escape our busy lives and experience peace and tranquility. Make sure you get to visit some of these magnificent medieval churches during your stay in Norfolk. |
|||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||
![]() |
10 Top Churches in Norfolk |
|
|||||
|
|||||
|
|||||
|
|||||
|
|||||
|
|||||
|
|||||
|
|||||
|
|||||
|
Tafakari ya neno la Mungu, Jumapili ya VI ya Kipindi cha Mwaka A wa Kanisa
Ninakuleteeni
tena ujumbe wa Neno la Mungu katika Dominika ya VI ya kipindi cha mwaka
A. Neno la Mungu latukumbusha kuwa Kristu Mwana wa Mungu hakuja
kutangua Torati bali kuikamilisha. Kristo ni sheria mpya na hivi analeta
ukamilifu wa sheria ya Mungu. Katika Somo la kwanza toka kitabu cha
Yoshua bin Sira, Mungu anatangaza uhuru kamili kwa mwanadamu.
Anamtaka mwanadamu aamue mwenyewe kumchagua Mungu au kumchagua shetani! Anatumia alama za moto na maji, uzima au mauti akitaka mtu aone katika uhuru wake mwenyewe wajibu wa kuchagua jema au baya. Kwa hakika ni alama yakwamba mwanadamu alizaliwa akiwa huru na hivi matendo yote ya nje hayawi ya kutenda tu bali mwanadamu anawajibika kuchagua kwa kuwa anao uwezo huo. Kama anataka maisha ya kiroho basi atachagua amri za Mungu, kama anataka kifo cha kiroho basi atachagua rushwa na vionjo vya mwili!
Katika somo la II mtume Paulo anaendelea kuwasisitizia Wakorinto juu ya hekima ya Mungu yakuwa ni siri ambayo haikufunuliwa kwa watawala wa dunia bali ilifunuliwa kwa Mitume. Kwa kuthibitisha hilo anasema kama wangalipewa hekima hiyo wasingalimtundika msalabani Mwana wa Mungu. Ndiyo kusema hekima waliyonayo wakristu si hekima ya kawaida ya kidunia bali hekima ya kimungu. Ni hekima ambayo inakuja kwetu kwa njia ya mpango wa Mungu ulio wa milele. Siri ya hekima hii ni kwamba wanaijua wale waliokomaa katika imani na tumaini la kweli katika Kristo Yesu.
Katika somo la Injili , Mwinjili Matayo akinukuu maneno ya Bwana anasema sikuja kuondoa hata yodi moja wala nukta moja bali kuifanya sheria ya Mungu iweze kueleweka vizuri zaidi katikati ya watu. Nimekuja kuifanya sheria iwe kwa ajili ya watu wa Mungu yaani kuwajengea uhuru kamili.
Mpendwa msikilizaji, Bwana anao uwezo wa kutafsiri sheria katika mtazamo wa mapendo kwa watu. Ona jinsi anavyowapenda wanadamu na hata akathubutu hata kuivunja Sabato. Anachotafuta kwa uhakika ni kuipa sheria uwezo wa ndani unaozaa mapendo kwa mwanadamu. Sheria iliyokuwa kavu anaipa nyama na hivi inaweza kutafunwa kwa urahisi!
Anakazia pia maana na namna ya kutafsiri sheria, akitaka tusiishie katika kile kilichoandikwa katika mwonekano wa kawaida, mfano usiue, kwa namna ya kutambua kuua kama ile hali ya kuondoa maisha kimwili, bali tutazame ndani na kugundua kuwa hata wale walio na lugha chafu, hasira, chuki wanashiriki katika mauaji ya wenzao.
Anatoa mfano wa kunawa hata viwiko ulio utamaduni wa Wayahudi kabla ya kwenda Hekaluni kwa ajili ya kutolea sadaka, hili kwake halina maana kama mmoja haangalii moyo wake. Matendo haya ya kilitrujia hayatoshi kama hayaambatani na toba ya ndani na upatanisho na wenzetu. Bwana akisonga mbele na mafundisho yake anakazia amri ya ndoa yakwamba kadiri ya mpango wa Mungu ndoa haitenganishwi. Ndiyo kusema katika mantiki ya ndoa ya kudumu, yafaa kukazia maisha ya unyenyekevu ili kuweza kuhimili vitimbwi nyemelezi dhidi ya familia. Hii haina maana yakwamba wale walioanguka katika utengano wadharauliwe katika jumuiya bali waombewe daima kwa ajili ya mabadiliko yao ya ndani.
Mpendwa mwanatafakari, Bwana anazidi kufunua namna ambavyo mkristu anapaswa afanye anapojikuta mbele ya kutoa ahadi na kiapo. Anawaalika wakristu daima wawe ni watu wa kusema ukweli daima. Maneno yao yawe ya unyoofu, wasiishi undumilakuwili yaani katika mazingira fulani ndiyo na katika mazingira tofauti siyo kwa jambo lilelile. Hii ni sumu kwa familia na jumuiya kwa ujumla, ni sumu wa serkali na utawala wa nchi.
Basi mpendwa jaribu kufuata hatua kwa hatua mafundisho ya Bwana kwa ajili ya kukua kiroho katika tumaini la kweli litakalokupa uzima wa milele. Nikutakie furaha na matumaini katika kushika mausia ya Bwana ambayo ndiyo sasa dira kamilifu na itupayo uhuru kamili wa wana wa Mungu.
Tumsifu Yesu Kristo.
Tafakari hii imeletwa kwako na Padre Richard Tiganya, C.PP.S
Anamtaka mwanadamu aamue mwenyewe kumchagua Mungu au kumchagua shetani! Anatumia alama za moto na maji, uzima au mauti akitaka mtu aone katika uhuru wake mwenyewe wajibu wa kuchagua jema au baya. Kwa hakika ni alama yakwamba mwanadamu alizaliwa akiwa huru na hivi matendo yote ya nje hayawi ya kutenda tu bali mwanadamu anawajibika kuchagua kwa kuwa anao uwezo huo. Kama anataka maisha ya kiroho basi atachagua amri za Mungu, kama anataka kifo cha kiroho basi atachagua rushwa na vionjo vya mwili!
Katika somo la II mtume Paulo anaendelea kuwasisitizia Wakorinto juu ya hekima ya Mungu yakuwa ni siri ambayo haikufunuliwa kwa watawala wa dunia bali ilifunuliwa kwa Mitume. Kwa kuthibitisha hilo anasema kama wangalipewa hekima hiyo wasingalimtundika msalabani Mwana wa Mungu. Ndiyo kusema hekima waliyonayo wakristu si hekima ya kawaida ya kidunia bali hekima ya kimungu. Ni hekima ambayo inakuja kwetu kwa njia ya mpango wa Mungu ulio wa milele. Siri ya hekima hii ni kwamba wanaijua wale waliokomaa katika imani na tumaini la kweli katika Kristo Yesu.
Katika somo la Injili , Mwinjili Matayo akinukuu maneno ya Bwana anasema sikuja kuondoa hata yodi moja wala nukta moja bali kuifanya sheria ya Mungu iweze kueleweka vizuri zaidi katikati ya watu. Nimekuja kuifanya sheria iwe kwa ajili ya watu wa Mungu yaani kuwajengea uhuru kamili.
Mpendwa msikilizaji, Bwana anao uwezo wa kutafsiri sheria katika mtazamo wa mapendo kwa watu. Ona jinsi anavyowapenda wanadamu na hata akathubutu hata kuivunja Sabato. Anachotafuta kwa uhakika ni kuipa sheria uwezo wa ndani unaozaa mapendo kwa mwanadamu. Sheria iliyokuwa kavu anaipa nyama na hivi inaweza kutafunwa kwa urahisi!
Anakazia pia maana na namna ya kutafsiri sheria, akitaka tusiishie katika kile kilichoandikwa katika mwonekano wa kawaida, mfano usiue, kwa namna ya kutambua kuua kama ile hali ya kuondoa maisha kimwili, bali tutazame ndani na kugundua kuwa hata wale walio na lugha chafu, hasira, chuki wanashiriki katika mauaji ya wenzao.
Anatoa mfano wa kunawa hata viwiko ulio utamaduni wa Wayahudi kabla ya kwenda Hekaluni kwa ajili ya kutolea sadaka, hili kwake halina maana kama mmoja haangalii moyo wake. Matendo haya ya kilitrujia hayatoshi kama hayaambatani na toba ya ndani na upatanisho na wenzetu. Bwana akisonga mbele na mafundisho yake anakazia amri ya ndoa yakwamba kadiri ya mpango wa Mungu ndoa haitenganishwi. Ndiyo kusema katika mantiki ya ndoa ya kudumu, yafaa kukazia maisha ya unyenyekevu ili kuweza kuhimili vitimbwi nyemelezi dhidi ya familia. Hii haina maana yakwamba wale walioanguka katika utengano wadharauliwe katika jumuiya bali waombewe daima kwa ajili ya mabadiliko yao ya ndani.
Mpendwa mwanatafakari, Bwana anazidi kufunua namna ambavyo mkristu anapaswa afanye anapojikuta mbele ya kutoa ahadi na kiapo. Anawaalika wakristu daima wawe ni watu wa kusema ukweli daima. Maneno yao yawe ya unyoofu, wasiishi undumilakuwili yaani katika mazingira fulani ndiyo na katika mazingira tofauti siyo kwa jambo lilelile. Hii ni sumu kwa familia na jumuiya kwa ujumla, ni sumu wa serkali na utawala wa nchi.
Basi mpendwa jaribu kufuata hatua kwa hatua mafundisho ya Bwana kwa ajili ya kukua kiroho katika tumaini la kweli litakalokupa uzima wa milele. Nikutakie furaha na matumaini katika kushika mausia ya Bwana ambayo ndiyo sasa dira kamilifu na itupayo uhuru kamili wa wana wa Mungu.
Tumsifu Yesu Kristo.
Tafakari hii imeletwa kwako na Padre Richard Tiganya, C.PP.S
Majibu ya Papa Francisko kwa wanandoa watarajiwa!
Baba Mtakatifu anasema, upendo wa maisha ya ndoa ni wa kudumu hadi pale kifo kitakapowatenganisha kwani haya ni mahusiano kati ya Bwana na Bibi, yanayokuwa na kukomaa hatua kwa hatua, kwa kutambua kwamba, hii ni zawadi kubwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Huu ni upendo unaowashirikisha wanandoa kazi ya uumbaji na kamwe si upendo mpito usioguswa na mahangaiko ya mwenzi wake. Upendo huu hauna budi kurutubishwa kwa kukutana na Yesu kwa njia ya: Sala, Sakramenti za Kanisa, Neno la Mungu na Matendo ya huruma.
Ubora wa ndoa unajikita katika udumifu wake, changamoto kubwa kwa wanandoa Wakristo. Pale wanandoa wanapohisi kwamba, wamepungukiwa na divai ya upendo na udumifu wasisite kumshirikisha Kristo katika upendo wao wa kila siku; ili wapendane na kutakiana mema.
Baba Mtakatifu anawaambia wanandoa watarajiwa kwamba, kuishi kwa pamoja ni sanaa na hija inayohitaji uvumilivu, inapendeza na kushangaza; ni safari inayojikita katika maneno: tafadhali, asante na samahani. Huu ni urithi ambao wanandoa wanapaswa kuwarithisha watoto wao. Ikumbukwe kwamba, unyenyekevu ni fadhila inaondoa chuki na kujenga upendo.
Si rahisi sana watu kujenga utamaduni wa kushuruku, lakini wanandoa wajenga na kuimarisha utamaduni wa kushuruku kwani mwenzi wako ni zawadi kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Kukosa na kukoseana ni ubinadamu, kusamehe na kusahau ni kuanza hija ya utakatifu wa maisha. Wanandoa wajifunze kutambua mapungufu yao ya kibinadamu na kuwa tayari kukiri makosa yao, tayari kuanza tena upya. Wajenge utamaduni wa kusikilizana kwa makini, ili kujenga na kuimarisha familia ya Kikristo.
Baba Mtakatifu anasema hakuna Familia inayoweza kujidai kwamba ni kamilifu na takatifu; wala hakuna Bwana au Bibi ambaye ni mkamilifu, kila mtu ana fadhila na kasoro na mapungufu yake, changamoto ya kujenga utamaduni wa kuomba na kutoa msamaha kila siku na kwa njia hii Ndoa zinaweza kudumu daima.
Maadhimisho ya Sakramenti ya Ndoa Kanisani yazingatie umuhimu wa Sakramenti ya Ndoa na kiasi bila kumezwa mno na malimwengu. Watambue uwepo wa Yesu Kristo anayeendelea kufanya miujiza kwa wanandoa kama alivyofanya takribani miaka elfu mbili iliyopita kwenye Arusi ya Kana. Kila kitu kiwe na kiasi na kielelezo cha furaha ya ndani na baraka kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Wanandoa wawashirikishe jirani zao ile furaha na kumbu kumbu ya maisha yao ya ndoa.
Haya ndiyo yaliyojiri katika Maadhimisho ya Siku ya Wapendanao Duniani kwa Mwaka 2014, tukio ambalo litakumbukwa na wanandoa hawa watarajiwa katika hija ya maisha yao ya ndoa na familia. Mji wa Roma, umefurika umati wa vijana na wasichana wanaotembea huku wameshikana mikono na maua ya waridi mikononi mwao alama ya upendo!
Friday, February 14, 2014 HISTORIA FUPI YA SIKU YA WAPENDANAO
Sikukuu ya wapendanao inasherekewa kila ifikapo tarehe 14 mwezi wa pili kila mwaka.
Watu wengi wanaosherekea siku hii kwa Nchi za Afrika Mashariki ni vijana walio kati ya miaka 18 hadi 35.
Historia ya sikukuu hii inaanzia miaka mingi jijini, Roma, Italia ikiwa inahusishwa na mtakatifu Valentine au Valentinus aliyekuwa
akiishi jijini humo katika karne hiyo. Wakati wa maisha ya mtakatifu
Valentine Roma ilikuwa ikitawaliwa na Kaisari, Claudius II, ambaye
alipata hisia wakati huo kuwa askari mkakamavu na bora zaidi ni yule
asiyekuwa na mke wala familia.
Claudius alilifanyia kazi wazo lake na
aliamua kupiga marufuku ndoa zote kwa askari wa nchi hiyo, jambo ambalo
halikukubaliwa na mtakatifu, Valentinus. Hivyo Valentinus alichukua
jukumu la kukaidi amri ile na kuendelea kuwafungisha ndoa kwa siri
maaskari waliokuwa wakitaka kufungishwa ndoa.
Haikuchukua
muda mrefu, taarifa zilimfikia mfalme, Claudius na alipopata habari
hizo aliamuru kukamatwa na kufungwa gerezani na kisha Valentinus aliuawa
kwa amri ya Kaisari. Kuna taarifa zinadai kuwa kabla ya kuuawa kwa
Valentine wakati huo akiwa amefungwa, mtakatifu Valentine aliandika
barua ya salamu kwa binti aliyekuwa amekwenda kumsalimia gerezani. Na
mwisho wa barua kulisomeka maneno yaliyoandikwa ‘From your Valentine’.
Tangu hapo Valentine akawa anakumbukwa kama mtetezi wa wapendanao na siku hii ikawa inaadhimishwa duniani kote.
Baada ya kufariki kwa mtakatifu huyo ndipo wananchi wengi duniani wakaamua kuadhimisha siku hii kama sherehe ya kumkumbuka Mtakatifu Valentinus.
Baraza la Kipapa tarehe 18 hadi 20 Februari 2014 litaadhimisha Kongamano la Kimataifa
Kongamano hili litawashirikisha wadau kutoka sehemu mbali mbali za dunia na utakuwa ni muda muafaka kwa ajili ya kusali, kutafakari, kuabudu na kuadhimisha Mafumbo ya Kanisa. Ni kipindi cha kuonjeshana uzoefu na mang'amuzi ya Liturujia ya Kanisa, tayari kutwika hadi kilindini kwa ajili ya
Sheikh Hassan Bashir amwagiwa tindikali!
IMAMU wa Msikiti wa Sawiyatu Qadiria, Hassan Bashir (33) amejeruhiwa vibaya usoni na sehemu ya bega la kushoto baada ya kumwagiwa kimiminika kinachodhaniwa kuwa ni tindikali.
Akizungumza na akiwa kwenye wodi ya wagonjwa katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru anakopatiwa matibabu, imamu huyo alisema tukio hilo lilitokea juzi majira ya kati ya saa 3:30 na saa 4:00 usiku karibu na Msikiti wa Tindiga, uliopo eneo la Unga Ltd.
Alisema ana maumivu makali sehemu ya uso pamoja na bega la upande wa kushoto.
Sheikh huyo ambaye alikuwa akizungumza kwa shida kutokana na maumivu makali, alisema alikumbwa na mkasa huo muda mfupi baada ya kumaliza mazungumzo na babu yake ambaye pia ni Mwenyekiti wa Msikiti, Ismail Olomi na Mwenyekiti wa Ujenzi, Abdalah Kaduma, juu ya maandalizi ya Maulid yanayotazamiwa kufanyika msikitini hapo.
“Tulipomaliza kuzungumza mimi nikawa
Maaskofu KKKT Karagwe wacharuka Mchungaji Kanyiginya, kunyimwa dhamana

Mchungaji huyo ambaye jana alipandishwa kizimbani kwa kosa la kumpiga mfanyabiashara, Joseph Gareba, alinyimwa dhamana baada ya Mwendesha Mashitaka, Meja Juma Litafa, kuzikataa barua za wadhamini hadi azifanyie uhakiki.
Akizungumza na gazeti hili kutoka Karagwe jana, Askofu mstaafu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe, Bagonza, alisema mchungaji Jackson alikuwa kwenye mkutano na viongozi wote wa kanisa hilo kwa ajili ya kufanya mafungo.
Alisema akiwa katika kituo cha mafungo, alipata wito wa polisi wa kumtaka afike mahakamani juzi kwa ajili ya kujibu kesi iliyofunguliwa kwa siri ya
Sunday Gospel Feb 16 2014

Listen:


Gospel Mt 5:20-22A,27-28,33-34, 37
Jesus said to his disciples:
“I tell you, unless your righteousness surpasses
that of the scribes and Pharisees,
you will not enter the kingdom of heaven.
“You have heard that it was said to your ancestors,
You shall not kill; and whoever kills will be liable to judgment.
But I say to you,
whoever is angry with brother
will be liable to judgment.
“You have heard that it was said, You shall not commit adultery.
But I say to you,
everyone who looks at a woman with lust
has already committed adultery with her in his heart.
“Again you have heard that it was said to your ancestors,
Do not take a false oath,
but make good to the Lord all that you vow.
But I say to you, do not swear at all.
Let your ‘Yes’ mean ‘Yes,’ and your ‘No’ mean ‘No.’
Anything more is from the evil one.”
Text from page http://en.radiovaticana.va/news/2014/02/13/sunday_gospel_feb_16_2014/en1-772758
of the Vatican Radio website
Miaka 83 tangu kuanzishwa kwa Radio Vatican

Watangazaji wanawake kutoka Radio Vatican wamekuwa mstari wa mbele kwa kuwa ni sauti ya wanawake wasiokuwa na sauti kutoka sehemu mbali mbali za dunia. Radio Vatican katika mtandao wake imeandaa programe mbali mbali zinazoonesha mchango wa Radio Vatican katika kuwawezesha wanawake Barani Afrika, Asia na Amerika.
Hizi ni programme zinazoonesha ujasiri wa wanawake katika kukabiliana na changamoto mbali mbali za maisha: katika masuala ya maendeleo endelevu, haki na amani duniani. Ukitaka kufaidi zaidi unaweza kutembelea katika tovuti rasmi ya Radio Vatican kwa anuani ifuatayo: www.radiovaticana.va
Unaweza pia kuwashirikisha jirani zako.
Mwaka Mmoja watimia Baba Mtakatifu Benedikto 16, alipotangaza rasmi kung'atuka
Maneno haya yakaushangaza ulimwengu. Kwa Kanisa hili likawa ni tukio la kinabii, ili kutoa nafasi kwa Mama Kanisa kuendelea kufanya mageuzi ya kina katika maisha na utume wake, Mwenyezi Mungu akipewa kipaumbele cha kwanza; waamini wakijikita kutangaza Habari Njema ya Wokovu katika ulimwengu wa utandawazi na maendeleo ya sayansi na teknolojia.
Akachaguliwa Baba Mtakatifu Francisko ambaye ameamua kuendeleza mageuzi yaliyokuwa yameanzishwa na Papa mstaafu Benedikto wa kumi na sita katika maisha na utume wa Kanisa kwa kukazia uaminifu kwa Kristo na Kanisa lake, bila kumezwa na malimwengu, mambo ambayo yamelisababishia Kanisa kujikuta linaandamwa na kashfa mbali mbali. Maaskofu mahalia wamepewa dhamana ya kuhakikisha kwamba, wanatekeleza utume wao wa kufundisha, kuongoza na kuwatakatifuza watu wa Mungu kwa ujasiri na moyo mkuu.
Kuna waamini ambao bado wana madonda makubwa katika mioyo yao, jambo la msingi kwa Kanisa ni kujikita katika mchakato wa uponyaji na upatanisho, ili Kanisa liweze kusonga mbele kwa ari kubwa zaidi katika azma yake ya kuwatangazia watu Injili ya Furaha.
Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto wa kumi na sita, aliona kashfa ya matumizi haramu ya fedha iliyokuwa inalinyemelea Kanisa kwa kutumia migongo ya wajanja wachache ndani ya Kanisa. Vatican ikatunga na kuridhia sheria inayopiga vita utakatishaji wa fedha haramu inayoweza kutumika kugharimia vitendo vya kigaidi. Papa Francisko anaendelea kukazia umuhimu na dhamana ya wanawake katika maisha na utume wa Kanisa.
Kanisa linamshukuru na kumpongeza Papa mstaafu Benedikto wa kumi na sita, kwa ujasiri na uamuzi wake wa busara wa kung'atuka kutoka madarakani, ili aweze kupata nafasi kubwa zaidi ya kusali na kutafakari.

Papa mstaafu Benedikto XVI kwa sasa ana utume wa sala na tafakari; uamuzi wake ni ushuhuda wa kinabii!
Mradi wa miaka 5 kwa ajili ya huduma kwa waathirika wa ugonjwa wa Ukimwi wazinduliwa nchini Tanzania
Mfuko wa Msamaria mwema, unaosimamiwa na Baraza la Kipapa la huduma za kichungaji kwa wafanyakazi katika sekta ya afya kwa kushirikiana na Idara ya afya ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania na Kampuni ya Gilead Sciences kutoka Marekani, wamekubaliana kimsingi kusaidia juhudi za kupambana na ugonjwa wa Ukimwi mkoani Shinyanga, kwa kusaidia juhudi za kupima virusi vya Ukimwi kwa wananchi 120, 000 pamoja na kuwapatia dawa za kurefusha maisha wale watakaokuwa wameathirika.
Makubaliano hayo yamefikiwa Jijini Dar es Salaam, tarehe 11 Februari 2014 katika Maadhimisho ya Siku ya 22 ya Wagonjwa Duniani. Huu ni mradi wa miaka mitano kwa ajili ya kupima virusi vya Ukimwi na kutoa dawa za kurefusha maisha. Ni mradi unaozingatia taaluma, maadili, usafi pamoja na mafunzo kwa walengwa watakaofaidika na mradi huu, kwa kutoa kipaumbele cha kwanza kwa watoto yatima.
Mradi huu utaendelea kuongeza nguvu katika kuwahudumia wagonjwa wa Ukimwi, juhudi zinazofanywa na Jimbo Katoliki la Shinyanga katika Vituo vya Afya vya: Ngokolo, Bugisi, Buhangija na Mija. Mradi utatoa ufadhili kwa ajili ya mafunzo ya hali ya juu kwa wahudumu wa sekta ya afya, ili kuweza kutekeleza wajibu wao barabara pamoja na kuendelea kujikita katika mapambano dhidi ya Virusi vya Ukimwi na maambukizi kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto.
Wananchi watakaogundulika kuwa na maambukizi ya Ukimwi watapewa dawa za kurefusha maisha anasema Askofu mkuu Zygmunt Zimowski, Rais wa Baraza la Kipapa la huduma za kichungaji kwa wafanyakazi katika sekta ya afya. Mradi unapania pamoja na mambo mengine, kudhibiti maambukizi ya virusi kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto, kama sehemu ya huduma makini inayotolewa na Kanisa katika kumhudumia mtu mzima: kiroho na kimwili, kama sehemu ya mwendelezo wa agizo la Kristo katika kuwahudumia wagonjwa.
Askofu mkuu Zygmunt Zimowski, amemkumbuka kwa namna ya pekee, Marehemu Askofu Aloysius Balina wa Jimbo Katoliki Shinyanga, aliyefariki dunia mwezi Novemba 2012. Aliamini kuhusu mafanikio ya mradi huu katika kuwahudumia watanzania waliokuwa wameathirika kwa ugonjwa wa Ukimwi. Ni mradi wa pekee, unaojumuisha Mfuko wa Msamaria Mwema, Baraza la Kipapa la huduma za kichungaji kwa wafanyakazi katika sekta ya afya pamoja na Kampuni ya Gilead.
Lengo li kuhakikisha kwamba, Kanisa Katoliki linashiriki kikamilifu katika mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Ukimwi ambao umekuwa ni chanzo cha vifo na upotevu wa nguvu kazi nchini Tanzania.
Maadhimisho ya Siku ya Wagonjwa Duniani, yalianzishwa kunako mwaka 1992 na Mwenyeheri Yohane Paulo wa Pili, ambaye hapo tarehe 27 Aprili 2014 anatarajiwa kutangazwa kuwa Mtakatifu. Siku ya Wagonjwa Duniani inalenga pamoja na mambo mengine kuhakikisha kwamba, wagonjwa wanapata huduma bora pamoja na kuishirikisha Familia ya Mungu katika huduma kwa wagonjwa, kwani wagonjwa bado wanayo nafasi ya pekee katika maisha na utume wa Kanisa.
Kanisa linawahamasisha watu wa kujitolea, ili waweze kuwashirikisha jirani zao upendo, kwa kuwaonjesha upendo. Kanisa linapania pia kutoa majiundo makini ya kitaaluma na kimaadili kwa wahudumu wa sekta ya afya.
Umejiandaaje na Valentine’s day?
URAFIKI na Mahusiano ndio jina la safu hii mpenzi msomaji. Ni matumaini yangu umzima na unaendelea vema kukabiliana na shughuli mbambali za ujenzi wa taifa hili.
Nami bila hajizi nakukaribisha katika safu hii ili twende sambamba katika kuzungumzia suala la Siku ya Wapendanao (Valentine’s day), ambayo sherehe yake ni Ijumaa ya wiki ijayo – Februari 14.
Kwa kawaida huwa kuna sherehe nyingi na wengine kuwatumia zawadi wahusika kama familia na marafiki, na mojawapo ni hii Siku ya Wapendanao.
Hakuna binadamu yeyote duniani anayeishi duniani bila kukwaruzana na mtu yeyote, iwe rafiki au ndugu.
Hivyo hakuna kitu cha kukufanya uwe na wasiwasi juu ya siku hiyo kwamba utafanya nini kwa uwapendao au umpendae.
Unaweza kuifanya Siku ya Wapendanao iwe nzuri kwako. Kabla ya kufanya chochote; kwa maana kwamba ikiwa bado siku kadhaa hadi ifikie siku hiyo, tembelea maduka ya kadi na utazame aina mbalimbali za kadi.
Njia hii haitokufanya usahau kupata kadi nzuri na pia itakuepusha kukurupuka na kununua kadi ambayo haina mvuto wa kipekee.
Bila shaka wazo kubwa zaidi la zawadi ambalo huwepo miongoni mwa watu wengi ni maua.
Zawadi hizi pia huweza kutumiwa hata kwa walioajiriwa, yaani kwa wafanyakazi wa taasisi au kampuni fulani.
Hata hivyo, watu pia huwa wanasherehekea Siku ya Wapendanao kwa kuja na mitazamo tofauti na kutafakari ni zawadi gani inafaa kumtumia mtu.
Unaweza kuonyesha ukaribu na urafiki kwa wafanyakazi wenzako kwa kununua maua na kuwapa zawadi lengo likiwa ni kuonyesha upendo.
Lakini kwa wapenzi mbali na kupeana zawadi za maua yanayoonyesha upendo, pia wanaweza kutoka ‘out’ kwa ajili ya kwenda sehemu kubadilisha mawazo na kufanya siku hiyo iwe nzuri kwao.
Kama umepanga Siku ya Wapendanao ibaki kuwa kumbukumbu kwa ninyi wapendanao (wapenzi), usisahau kuhusisha zawadi zitokazo kwa sonara, kwani hakika ni chaguo zuri.
Kwa mfano unaweza kununua kimojawapo kati ya vitu vinavyopatikana sonara kwa lengo la kuboresha upendo wenu.
Epuka kuwa na kisirani pamoja na kumkera umpendae au uwapendao kwani kwa hakika utakuwa umeifanya siku hiyo kuwa mbaya kwako.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)