Baba Mtakatifu Francisko anawaambia watumiaji wa mitandao ya kijamii kwamba, Ufalme wa mbinguni ni kwa ajili ya watu wanaojiaminisha kwenye upendo wa Mungu na wala si katika mambo ya kidunia.
Katika kilele cha Mwaka wa Imani, Baba Mtakatifu anatarajiwa, Jumamosi jioni kuongoza Ibada ya kuwapokea Wakatekumeni kama kielelezo cha kuvuka Mlango wa Imani, tayari kumpokea Kristo katika hija ya maisha yao ya Kikristo. Ibada hii inatarajiwa kuhudhuriwa na wakatekumeni kutoka sehemu mbali mbali za dunia kama kielelezo cha Ukatoliki wa Kanisa la Kiulimwengu.
Jumapili asubuhi, kwa mara ya kwanza waamini watapata fursa ya kutolea heshima kwa masalia yanayosadikiwa kuwa ni ya Mtakatifu Petro, Mwamba wa Imani, aliyeyamimina maisha yake kwa ajili ya Kristo na Kanisa lake. Ilikuwa ni Mwaka 1971, Papa Paulo VI alipopewa masalia haya yanayohifadhiwa kwenye Kikanisa cha Papa na kila mwaka ifikapo tarehe 29 Juni, Siku kuu ya Watakatifu Petro na Paulo miamba wa imani masalia haya hupelekwa kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican.
Katika Sherehe ya Kristo Mfalme wa Dunia, Baba Mtakatifu Francisko anatarajiwa kuongoza Ibada ya Misa Takatifu kama kilele cha kufunga Mwaka wa Imani, Ibada inayotarajiwa kuanza saa 4:30 kwa saa za Ulaya. Katika Ibada hii, Baba Mtakatifu atawagawia baadhi ya waamini Waraka wake wa kichungaji baada ya Maadhimisho ya Mwaka wa Imani unaojulikana kama "Furaha ya Injili" "Evangelii Gaudium", itakayozinduliwa rasmi, Jumatatu ijayo hapa mjini Vatican.
Week Hot newz
-
Prayer in Time of Anger Lord Jesus, there is anger in my heart and I cannot root it out. I know that I should calm down and offer the hu...
-
Dear Lord! Fill our parents with Thy choicest blessings; enrich their souls with Thy holy grace; grant that they may faithfully and cons...
-
na Paskal Linda-Dar es salaam SHULE ya Msingi St. Joseph iliyopo Mbezi Beach, Dar es Salaam, kwa kushirikiana na wazazi wa wanafunzi wa...
-
Baba Mtakatifu Francisko anawataka wadau mbali mbali wa s...
-
The Prayer Thank You God! Dear Loving and Compassionate God, Giver of all gifts, we pray especially today for the mercy and love You give...
-
A Prayer for Grandparents. Jesus our Savior As your grandson. I know that every period Of our lives Has its responsibiliti...
-
Guardian Angel Prayer #2 (This is an old Guardian Angel Prayer) O Holy Angel, attendant of my wretched soul and of mine afflicted li...
-
Canticle of Brother Sun and Sister Moon of St. Francis of Assisi Most High, all-powerful, all-good Lord, All praise is Yours, all glory,...
-
Family Blessing at a Gathering Father in Heaven, We praise You for giving us Your Son To be our Saviour and Lord. Bless us all as we g...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni