Wakizungumza kwa nyakati tofauti juzi na jana, wadau hao wameelezea
kufurahia kufikiwa na tamasha hilo la kimataifa ambalo litapambwa na
waimbaji wa ndani na nje ya Tanzania.
Kwa upande wake, Matata Ndizi, kati ya wadau wakubwa wa muziki wa
Injili, alisema angependa kumuona muimbaji Edson Mwasabwite katika
tamasha hilo.
“Kwanza tunashukuru kutuletea tamasha hilo mkoani Morogoro, lakini
kati ya waimbaji ambao tungependa kuwaona ni Edson Mwasabwite,” alisema
Matata.
Alisema amekuwa akibarikiwa sana anapomsikiliza mwimbaji huyo anayetamba na albamu yake ya ‘Ni Kwa Neema.’
“Mbali ya ukali wa kibao chake, Mwasabwite ni mwimbaji mpya, hivyo
wengi wangependa kumuona ‘live’ siku hiyo ya tamasha,” alisema.
Mwasabwite, mzaliwa wa Mbeya amekuwa aking’ara na albamu hiyo yenye
nyimbo nyingine saba, ambazo ni ‘Tarajia’, ‘Mujiza’, ‘Asante Yesu’,
‘Usiwe Mbali Nami’, ‘Bwana Yesu’, ‘Atanifuta Machozi’, ‘Milele
Usifiwe’ na ‘Mungu Wetu Anaweza’.
Mwingine aliyempendekeza Mwasabwite ni Innocent Kobelo wa Mafisa
mkoani humo, ambaye amekiri kuwa amekuwa akivutiwa naye hivyo angefurahi
kumwona ‘live’
.
Waandaaji wa Tamasha la Krismasi, wamebainisha kuwa wamepania
kulifanya liwe la aina yake tofauti na mengineyo kwa kualika waimbaji
maarufu ndani ya nje ya nchi, ambako tayari wamemtangaza Upendo Nkone
kuwemo katika tamasha hilo litakaloanza kukata utepe Desemba 25 jijini
Dar es Salaam.
Week Hot newz
-
SIKU moja baada ya kifo cha Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, Mzee Nelson Mandela (95), mazishi yake yanatarajiwa kufanyika wiki m...
-
Baba Mtakatifu Francisko katika tafakari yake kwa Jumapili ya tatu ya Kipindi cha Majilio, anawaalika waamini na watu wote wenye mapenzi ...
-
Na Paskal Linda,Vatican. 19/12/2013 Baba Mtakatifu Francisko, Jumatano tarehe 18 Desemba 2013 amefanya mazungumzo na Papa ms...
-
Mpendwa mwana wa Mungu, leo tunasherehekea na kushangilia sherehe ya familia Takatifu. Masiha amezaliwa ndani ya familia hii....
-
Ndege iliyokuwa imetekwa Rubani msaidizi wa ndege ya abiria ya shir...
-
Na Dina Ismail, Dar es Salaam MSANII wa muziki wa asili nchini, Pascal linda maarufu kama Batarokota amewaomba mashabiki wa muziki nc...


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni