Week Hot newz

Moro wazitaka neema Tamasha la Krismasi

Wakizungumza kwa nyakati tofauti juzi na jana, wadau hao wameelezea kufurahia kufikiwa na tamasha hilo la kimataifa ambalo litapambwa na waimbaji wa ndani na nje ya Tanzania.
Kwa upande wake, Matata Ndizi, kati ya wadau wakubwa wa muziki wa Injili, alisema angependa kumuona muimbaji Edson Mwasabwite katika tamasha hilo.

“Kwanza tunashukuru kutuletea tamasha hilo mkoani Morogoro, lakini kati ya waimbaji ambao tungependa kuwaona ni Edson Mwasabwite,” alisema Matata.
Alisema amekuwa akibarikiwa sana anapomsikiliza mwimbaji huyo anayetamba na albamu yake ya ‘Ni Kwa Neema.’
“Mbali ya ukali wa kibao chake, Mwasabwite ni mwimbaji mpya, hivyo wengi wangependa kumuona ‘live’ siku hiyo ya tamasha,” alisema.
Mwasabwite, mzaliwa wa Mbeya amekuwa aking’ara na albamu hiyo yenye nyimbo nyingine saba, ambazo ni ‘Tarajia’, ‘Mujiza’, ‘Asante Yesu’, ‘Usiwe Mbali Nami’,  ‘Bwana Yesu’, ‘Atanifuta Machozi’, ‘Milele Usifiwe’ na ‘Mungu Wetu Anaweza’.
Mwingine aliyempendekeza Mwasabwite ni Innocent Kobelo wa Mafisa mkoani humo, ambaye amekiri kuwa amekuwa akivutiwa naye hivyo angefurahi kumwona ‘live’
.
Waandaaji wa Tamasha la Krismasi, wamebainisha kuwa wamepania kulifanya liwe la aina yake tofauti na mengineyo kwa kualika waimbaji maarufu ndani ya nje ya nchi, ambako tayari wamemtangaza Upendo Nkone kuwemo katika tamasha hilo litakaloanza kukata utepe Desemba 25 jijini Dar es Salaam.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni