Wakizungumza kwa nyakati tofauti juzi na jana, wadau hao wameelezea
kufurahia kufikiwa na tamasha hilo la kimataifa ambalo litapambwa na
waimbaji wa ndani na nje ya Tanzania.
Kwa upande wake, Matata Ndizi, kati ya wadau wakubwa wa muziki wa
Injili, alisema angependa kumuona muimbaji Edson Mwasabwite katika
tamasha hilo.
“Kwanza tunashukuru kutuletea tamasha hilo mkoani Morogoro, lakini
kati ya waimbaji ambao tungependa kuwaona ni Edson Mwasabwite,” alisema
Matata.
Alisema amekuwa akibarikiwa sana anapomsikiliza mwimbaji huyo anayetamba na albamu yake ya ‘Ni Kwa Neema.’
“Mbali ya ukali wa kibao chake, Mwasabwite ni mwimbaji mpya, hivyo
wengi wangependa kumuona ‘live’ siku hiyo ya tamasha,” alisema.
Mwasabwite, mzaliwa wa Mbeya amekuwa aking’ara na albamu hiyo yenye
nyimbo nyingine saba, ambazo ni ‘Tarajia’, ‘Mujiza’, ‘Asante Yesu’,
‘Usiwe Mbali Nami’, ‘Bwana Yesu’, ‘Atanifuta Machozi’, ‘Milele
Usifiwe’ na ‘Mungu Wetu Anaweza’.
Mwingine aliyempendekeza Mwasabwite ni Innocent Kobelo wa Mafisa
mkoani humo, ambaye amekiri kuwa amekuwa akivutiwa naye hivyo angefurahi
kumwona ‘live’
.
Waandaaji wa Tamasha la Krismasi, wamebainisha kuwa wamepania
kulifanya liwe la aina yake tofauti na mengineyo kwa kualika waimbaji
maarufu ndani ya nje ya nchi, ambako tayari wamemtangaza Upendo Nkone
kuwemo katika tamasha hilo litakaloanza kukata utepe Desemba 25 jijini
Dar es Salaam.
Week Hot newz
-
Tunaendelea kama kawaida katika kipindi chetu, tafakari masomo Dominika, na leo tunatafakari masomo Dominika ya 33 ya mwaka C wa Kanisa...
-
Teach me, Lord Jesus, to be generous: to serve You as You deserve; to give, not counting the cost; to fight, not heeding the wound...
-
Uchunguzi wa mwili wa Askofu Józef Wesolowski, umekamilika na matokeo kwamba amekufa kifo cha kawaida. Kuf...
-
Baraza la Kipapa la Elimu Katoliki limezindua tovuti yake inayotoa habari muhimu kuhusu mchango wa Kanisa Katoliki katika sekta ya elimu ...
-
Reading 1, Romans 6:19-23 19 I am putting it in human terms because...
-
NA OSCAR ASSENGA, TANGA-Tanzania.Gazeti Mtanzania. KATIBU wa Chama cha Watu Wenye Albino Mkoa wa Tanga (TAS), Mah...
-
Mpendwa mwana wa Mungu, tuko tena pamoja katika ile habari ya furaha ndiyo kushirikishana mapendo ya Mungu kwa njia ya meza y...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni