Week Hot newz
-
Tafakari ya Neno la Mungu Jumapili ya IV ya Mwaka C wa Kanisa. - OSS_ROM 28/01/2016 14:25 Mitandao ya kijamii: “...
-
Rubani msaidizi, Andreas Lubitz, aliangusha makusudi ndege hiyo kwenye milima ya Alps. Wachunguz...
-
Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI, Ijumaa, tarehe 27 Desemba 2013 amemtembelea Papa Francisko na kupata chakula cha pamoja...
-
Watawa wa Mama Theresa wa Calcutta waliouwawa huko Yemen ni mashuhuda wa upendo na wahanga wa utandawazi usiojali wala kuguswa na maha...
-
Yesu amekuja ulimwenguni ili kuufunua, kuutangaza na kuus...
-
Daily Reading for Tuesday, March 22nd, 2016 Reading 1, Isaiah 49:1-6 1 Coasts and islands, listen ...
-
Watu 6 wamejeruhiwa katika mlipuko uliotokea katika uwanja wa ndege ulioko mjini Beledweyne nchini Somalia.
-
By Paskal Linda (Batarokota Network ) Feast Day October 22 With St. John Paul II feast day just around the corner, T...
-
Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya maadhimisho ya Ib...
Vatican: Papa Francis hayuko hatarini
MAKAO Makuu ya Kanisa Katoliki Duniani, yamekanusha vikali uvumi ulioenea kwamba Baba Mtakatifu, Francis, yuko hatarini kwa kuwa kundi la kimafia linamuwinda kumfanyia uhalifu kwa kile kilichoelezwa kuhusu uamuzi wake wa kufanya mageuzi katika kanisa hilo.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari wa Vatican, Frederico Kardinali Lombard, alikiambia kituo cha habari cha ABC kwamba hakuna sababu za wazi zinazoweza kuwafanya kuwa na wasiwasi.
“Tuna utulivu wa kutosha, hakuna haja ya kuanza kuwekeana mashaka,” alisema.
Habari zilizonukuliwa hivi karibuni zilimtaja Nicola Gratteri anayeheshimika nchini Italia kwa msimamo wake kinyume na kundi hilo la Mafia akisema kuwa uamuzi wa Baba Mtakatifu kutaka kulifanyia marekebisho kanisa ulilikasirisha kundi hilo la kijasusi.
“Siwezi kusema kama Mafia wanaweza kufanya kitendo hiki, tunawajua kuwa ni watu hatari,” aliongeza Lombard.
Gratteri alilianyia uchunguzi wa kutosha kundi hilo lenye nguvu duniani lenye makazi yake Calabria, Kusini mwa Italia katika sehemu inayoitwa Ndrangheta.
Aliyaongea hayo kwenye kipindi cha televisheni alipokuwa anazindua kitabu chake cha maji matakatifu, kinachohusu Kanisa Katoliki na vikwazo linavyopata katika eneo hilo la Ndrangheta.
Grateri ananukuliwa akisema kuwa uamuzi wa Papa utaangusha nguvu ya kibiashara iliyoko katika mamlaka za Vatican ikiwemo Benki ya Vatican iliyokuwa inafanya biashara zilizolaumiwa kama ni za kiukoo kati ya makleri wa eneo hilo.
Ingawa kwa kiasi kikubwa mauaji yaliyokuwa yanapangwa na Mafia yamepungua kwa kiasi kikubwa tangu miaka ya 1990, matendo ya kihalifu bado yanafanywa na vikundi vinavyojihusisha na ukahaba na watumiaji wa dawa za kulevya, hayo ndio makundi hatari kwa ukuaji wa uchumi wa Italia.
Koo kubwa zinazopatikana Italia kwa sasa zinahusisha, Wasisili wa Cosa Nostra, Wakamora wanaotoka mji wa Napoli, na Kalabrian maarufu kama Ndrangheta, ambao unasadikiwa kuwa wenye nguvu katika matendo ya kihalifu, hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Umoja wa Mataifa.
Tayari Baba Mtakatifu ameshatangaza kufanya mabadiliko makubwa katika kanisa, akitaka kanisa la kimaskini kwa ajili ya maskini, na ndani ya wiki hii ameshazungumza mara mbili katika misa zake za asubuhi akikemea vitendo vya rushwa na fedha chafu.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni