Week Hot newz

MERRY CHRISTMAS – HERI KWA NOELI!


Kristmas ni Birthday ya mmoja katika UTATU aliyetumwa kufanya kazi kwenye sayari hii inayoitwa dunia. Hebu tujaribu kupiga twasira. Siku moja, huko mbinguni kulikuwa na mkutano wa Halmashauri kuu ya Utatu Mtakatifu.

Ajenda kuu ya mkutano ilihusu kuizungumzia sayari dunia. Hasa kutokana na mabadiliko makuu yaliyokuwa yanajitokeza hapa na pale baada ya uumbaji. Ikabidi

Ombi la Papa Francisko kwa niaba ya familia zisizo na nyumbani.



Baba Mtakatifu Francisko , Jumapili iliyopita, baada ya sala ya Malaika wa Bwana, alitoa ombi kwa watu wote, binafsi, Taasisi, Makampuni na mamlaka, kujali mahangaiko na mateso ya watu wasiokuwa na makazi maalum yaani wasiokuwa na nyumbani. Papa aliotoa ombi hili kwa niaba ya familia zisizo na makazi , mbele ya mahujaji na wageni waliokuwa wamekusanyika katika uwanja wa kanisa kuu la Mtakatifu Petro,Vatican.

Taarifa inabaini Papa alitoa wito huo kwa kuhamasishwa na

Maisha Mchanganyiko: Nani kama Mama!



Zikiwa zimebaki siku tatu, kuadhimisha tukio la Mama Bikira Maria kutuzalia Mtoto Yesu , Emannuel, Mkombozi wa Dunia, inafaa kwa wakati huu kumtafakari Mwanamke, mama mzazi, hadhi yake, wajibu wake na Kanisa lasema nini juu mwanamke mama mzazi.
Ni wazi kipindi cha Krismas, ni wakati wa hekaheka nyingi za katika jamii , na familia pia. Nyuso nyingi huonekana kuwa na furaha, na pia ndani ya familia, huonekana mshikamano zaidi, ambamo licha ya hamu ya kusubiri ibada ya kusisimua ya

Tafakari ya Neno la Mungu, Jumapili ya IV ya Kipindi cha Majilio



Hatuna budi kumshukuru Mungu kwa kutujalia tena siku nzuri kama hii na hasa tunapoijongea meza ya Neno lake. 

Ni Dominika ya IV ya Kipindi cha Majilio, tukikaribia kuzaliwa kwa Mwana wa Mungu, Mfalme wa amani, Mtoto Emanueli. Katika somo la kwanza tunapata kusikia kuwa Mungu atatoa ishara na hapa ndipo kuna mzizi na kiini cha masomo ya Dominika hii. Basi ishara yenyewe ni Mtoto Emanueli yaani Mungu pamoja nasi.

Mpendwa msikilizaji wa Neno la Mungu, katika somo la kwanza

West Ham yapeleka majanga Spurs.



West Ham wakipambana na Tottenham
Mabao mawili katika dakika 10 za mwisho yaliipa ushindi West Ham dhidi ya Tottenham na kuiwezesha kuingia nusu fainali ya kombe la Capital One ambapo itapambana na Manchester City. Tottenham walifungua mlango katika nusu ya pili wakati Emmanuel Adebayor alipofunga bao lake la kwanza tangu mwezi wa Mei.
Westham walisawazisha kupitia kwa Matt Jarvis na zikiwa zimesalia dakika tano mchezo huo kumalizika, Modibo

Mkalimani wa mazishi ya Mandela awa chizi


Thamsanqa Jantjie, mkalimani wa lugha ya ishara
Mkalimani wa lugha ya ishara katika siku ya mazishi ya kitaifa, ya aliyekuwa rais wa kwanza mzalendo wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, amelazwa katika hospitali ya magonjwa ya ya akili.
Mkalimani huyo anashutumiwa kutoa ishara ambazo hazikuendana na kile kilichokuwa kikiongelewa.
Thamsanqa Jantjie "anaweza kuwa na matatizo", amekaririwa mke wake Siziwe akisema hayo.
Wataalam wa lugha ya ishara wamemshutumu kwa

Noeli ni Siku kuu ya imani



Na Paskal Linda,Vatican.
19/12/2013
Baba Mtakatifu Francisko, Jumatano tarehe 18 Desemba 2013 amefanya mazungumzo na Papa mstaafu Benedikto XVI, ili kutakiana kheri na matashi mema kwa ajili ya Siku kuu ya Noeli na Mwaka Mpya wa 2014. Baba Mtakatifu amekumbusha kwamba,

Chelsea yachapwa na Sunderland


Sunderland imesonga mbele hatua ya nusu fainali ya michuano ya ya Kombe la Capital One baada ya kuichapa Chelsea mabao 2-1.
Chelsea ilimiliki mchezo huo kwa muda mrefu katika dakika zote 90, huku Chelsea ikipata goli kutokana na mchezaji wa Sunderland, Lee Cattermole kujifunga mwenyewe.
Chelsea walionekana kufuzu kucheza hatua ya nusu fainali hadi dakika za mwisho za mchezo,

Noeli iwe ni siku kuu ya imani na matumaini; mapendo na amani

Baba Mtakatifu Francisko katika Katekesi yake, Jumatano, tarehe 18 Desemba 2013, amewakumbusha waamini kwamba, siku hizi za mwisho mwisho za Kipindi cha Majilio ni mwaliko kwa waamini kujiandaa kiroho ili kumpokea Yesu anayezaliwa tena katika maisha yao.

Baba Mtakatifu anasema, Noeli ni Siku kuu ya furaha na matumaini kwa Mwenyezi Mungu ambaye ameamua kuja na kuishi kati ya watu wake kwa njia ya Mwanaye wa

Mzee Nelson Mandela alikuwa pia shujaa wa Tanzania

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa Baba wa Demokrasia ya Afrika Kusini, Mzee Nelson Mandela alikuwa pia kiongozi wa Tanzania, shujaa wa Watanzania na Baba wa wananchi wa Tanzania kama alivyokuwa kwa wananchi wa Afrika Kusini.

Aidha, Rais Kikwete amesema kuwa Tanzania na Afrika Kusini zina uhusiano wa kindugu na wa karibu sana kwa sababu ya kazi kubwa iliyofanywa na waanzilishi wa mataifa hayo mawili, Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na Mzee Mandela.

Maisha ya Mandela Afrika ya Kusini wanaikumbuka sana Tanzania

Wananchi wa Afrika ya Kusini wanaikumbuka sana Tanzania kutokana na mchango wake katika harakati za ukombozi kusini mwa Afrika, jambo ambalo limejenga urafiki na undugu wa dhati kati ya Afrika ya Kusini na Tanzania.

Tanzania chini ya uongozi wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ilikuwa mstari wa mbele katika mapambono dhidi ya ukoloni na utawala wa ubaguzi wa rangi Afrika ya Kusini kwa kuamini kwamba, binadamu wote ni sawa na Afrika ni moja.

Yesu Kristo ndiye kiini na chemchemi ya furaha ya kweli!

Baba Mtakatifu Francisko katika tafakari yake kwa Jumapili ya tatu ya Kipindi cha Majilio, anawaalika waamini na watu wote wenye mapenzi mema kufurahi kwani Noeli i karibu na kwamba, Kanisa linatumwa kutangaza Habari Njema ya Wokovu, hii ndiyo Injili. Kanisa si kimbilio la watu wenye nyuso za kukunjamana bali ni nyumba ya furaha! Kwa wale wenye majonzi wanaonja furaha ya kweli ndani ya Kanisa.

Furaha hii inatokana na utambuzi kwamba, mtu anapendwa

Chiefs banking on Madiba magic




Kaizer Chiefs will entertain the University of Pretoria at the FNB Stadium in an Absa Premiership match on Monday evening, kick-off at 8:30pm.
Chiefs racked up a third straight league victory when they beat Free State Stars 2-0 away from home in late November.
The Soweto giants are unbeaten at home this season, with four wins and two draws from six matches.
The Amakhosi are placed second on the Absa Premiership log with 21 points from 11 matches.
If they win their game against Tuks and log leaders Mamelodi Sundowns lose their derby match against SuperSport United on the same day, Chiefs will assume first place on the standings.

Mama Maria Nyerere,Kikwete wafunika mazishi ya Mandela


16th December 2013
Rais Jakaya Kikwete, akizungumza katika mazishi ya aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini, hayati Neson Mandela, yaliyofanyika katika kijiji cha Qunu nchini humo jana.
Rais Jakaya Kikwete na mjane wa Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere, jana walifunika kwenye ibada maalumu ya kumuaga aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, iliyofanyika kijijini kwake Qunu, Mashariki mwa Cape.

Tukio hilo lilitokea baada ya Rais Kikwete kupewa fursa ya kuzungumza kwenye ibada hiyo ambayo ilianza mapema

EMMANUEL ANORLD OKWI ATUA YANGA!!

Klabu ya Yanga SC imefanikiwa kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa kimataifa kutoka nchini Uganda Emmanuel Arnold Okwi ambaye alikua akiichezea klabu ya SC Villa ya Uganda.

Yanga SC imempata mshambuliaji huyo msumbufu kwa mabeki wengi kwa mkataba wa miaka miwili na nusu ambapo kwa sasa ataitumika klabu yake mpya ya watoto wa jangwani mpaka mwishoni mwa msimu wa 2015/2016.

Dirisha dogo la usajili nchini Tanzania limefungwa leo usiku Disemba 15, 2013 saa 6 usiku ambapo mabingwa wa kihistoria klabu ya Yanga wamekalilisha taratibu zote za usajili ikiwa ni pamoja na kupata hati ya uhamisho wa kimataifa maarufu kama ITC.

Usajili wa Emmanuel Okwi unaifanya timu ya Yanga kufikisha idadi ya wachezaji watano wa kimataifa wakiwemo mganda mwenzake Hamis Kiiza, Haruna Niyonzima, Mbuyu Twite na Didier Kavumbagu.

Uongozi wa Yanga unawaomba wanachama, wapenzi na washabiki kuwapa ushirikiano wachezaji wote wa zamani na wapya waliosajiliwa katika dirisha dogo la usajili.

Wachezaji wengine waliosajiliwa hivi karibuni katika kuimarisha kikosi cha Yanga ni mlinda mlango Juma Kaseja ambaye alikuwa mchezaji huru na Hassan Dilunga aliyesajiliwa kutoka timu ya Ruvu Shooting.

Baraka Kizuguto

Afisa Habari – Young Africans SC

Disemba 15, 2013.
Photo: BREEEEEEAKING NEEEEEEWWS!!!!

SASA NI RASMIIIIIIIIIIIIIIIIII!!  EMMANUEL ANORLD OKWI ATUA YANGA!!
>> Kweli mwenye pesa sio mwenzako!!
>> Hiini habari kwa mujibu wa Afisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto

Klabu ya Yanga SC imefanikiwa kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa kimataifa kutoka nhcini Uganda Emmanuel Arnold Okwi ambaye alikua akiichezea klabu ya SC Villa ya Uganda.
 
Yanga SC imempata mshambuliaji huyo msumbufu kwa mabeki wengi kwa mkataba wa miaka miwili na nusu ambapo kwa sasa ataitumika klabu yake mpya ya watoto wa jangwani mpaka mwishoni mwa msimu wa 2015/2016.
 
Dirisha dogo la usajili nchini Tanzania limefungwa leo usiku  Disemba 15, 2013 saa 6 usiku ambapo mabingwa wa kihistoria  klabu ya Yanga wamekalilisha taratibu zote za usajili ikiwa ni pamoja na kupata hati ya uhamisho wa kimataifa maarufu kama ITC.
 
Usajili wa Emmanuel Okwi unaifanya timu ya Yanga kufikisha idadi ya wachezaji  watano wa kimataifa wakiwemo mganda mwenzake Hamis Kiiza, Haruna Niyonzima, Mbuyu Twite na Didier Kavumbagu.
 
Uongozi wa Yanga unawaomba wanachama, wapenzi na washabiki kuwapa ushirikiano wachezaji wote wa zamani na wapya waliosajiliwa katika dirisha dogo la usajili.
 
Wachezaji wengine waliosajiliwa hivi karibuni katika kuimarisha kikosi cha Yanga ni mlinda mlango Juma Kaseja ambaye alikuwa mchezaji huru na Hassan Dilunga aliyesajiliwa kutoka timu ya Ruvu Shooting.
 
Baraka Kizuguto
 
 Afisa Habari – Young Africans SC
 
Disemba 15, 2013.

Papa Francisko mtu mashuhuri kwa Mwaka 2013

Baba Mtakatifu Francisko ameteuliwa na Gazeti maarufu la TIME kuwa ni mtu mashuhuri kwa Mwaka 2013. Akizungumzia uteuzi huu, Padre Federico Lombardi, msemaji mkuu wa Vatican anabainisha kwamba, Vatican kwa ujumla hakushangazwa na uteuzi huu, kwani kuna vielelezo makini vinavyoonesha mguso na mashiko tangu Baba Mtakatifu Francisko achaguliwe kuliongoza Kanisa Katoliki kama Khalifa wa Mtakatifu Petro.

Nelson Mandela amezikwa kimila



Hayati Mandela alikuwa kipenzi cha dunia nzima
Rais wa kwanza mzalendo wa Afrika Kusini Hayati Nelson Mandela amezikwa katika kijiji cha Qunu mkoa wa Cape Mashariki nchini Afrika Kusini.
Mjane wa Mandela Graca Machel pamoja na Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma walikuwepo katika hafla ya mazishi iliyohudhuriwa na jamaa za karibu wa familia ya Mandela pamoja na viongozi wengine wakuu.
Takriban watu 4,500 ikiwemo wageni wa kimataifa walihudhuria mazishi hayo ambayo yalikuwa ya mchanganyiko wa tamaduni za kale na mambo ya

Safari ya Mandela yaishia Kijiji cha Qunu!


Mandela daima alisema anataka kuzikwa nyumbani alikozaliwa Qunu
Kijiji cha Qunu ambako atazikwa Hayati Nelson Mandela, kinaomboleza kifo cha shujaa aliyetoka katika kijiji hicho Nelson Mandela.
Mazingira hapa ni ya kipekee, mchanganyiko wa nyumba za kisasa na za kitamduni ambazo mfano wake ni mizinga ya Nyuki.

Udugu ni silaha dhidi ya umaskini, rushwa na ufisadi;

Udugu ni msingi na njia ya amani; ndiyo kauli mbiu inayoongoza Maadhimisho ya Siku ya 47 ya Kuombea Amani Duniani, itakayofanyika tarehe Mosi, Januari 2014 sanjari na Maadhimisho ya Siku kuu ya Bikira Maria Mama wa Mungu. Huu ni ujumbe unaochota utajiri wake kutoka katika Maandiko Matakatifu pamoja na mang'amuzi ya mshikamano wa kidugu kati ya watu.

Tafakari ya Neno la Mungu, Jumapili ya tatu ya Kipindi cha Majilio

Tafakari masomo Dominika, ninafurahi tena kuwa nawe katika safari yetu ya Majilio tukijiandaa kwa ajili ya ujio wa Mwana wa Mungu. Ni wakati huu tunapoimba kwa furaha Masiha wetu njoo, ukatuokoe.
Tuko sasa Dominika ya tatu ya Kipindi cha Majilio ambapo Neno la Mungu linatualika kutambua kwa njia ya imani alama zinazomtambulisha Masiha. Tunapata kutafakari katika Injili juu ya wasiwasi wa Yohane Mbatizaji juu ya Masiha, kiasi kwamba anatuma wafuasi wake tokea gerezani wakamwulize Bwana wakisema, eti wewe ndiye Masiha tuliyemtarajia au tumngojee mwingine?
Yohane Mbatizaji anaingiwa na wasiwasi kwa sababu aliweka matumaini yake katika alama zisizo za kweli! Kwetu sisi yaweza tokea na inatokea mara kadhaa kutumaini katika bwana asiye mwenyewe! Kumbe leo mwaliko ni huo, yaani kuwa makini ili tusianguke katika mtego kama huo!
Mpendwa msikilizaji, alama ambazo zilisadikika na Yohane Mbatizaji na wafuasi wake ni kuwa Masiha ajaye atakuwa hakimu mkali atakayewapatiliza mbali wadhambi. Kinyume chake Masiha hafanyi hilo isipokuwa upendo kwao akitafuta kuwaokoa katika taabu yao hiyo. Mpendwa msikilizaji, kazi na wajibu wetu mkuu, ni kutambua wakati huo tukijiuliza daima, ni alama zipi zinazomtambulisha Masiha ambaye tunaimba kwa furaha tukisema uje kutuokoa!
Ndiyo kusema, alama za kweli tunazipata katika Somo la kwanza toka kitabu cha Nabii Isaya 35:1-6,10 akisema ndipo vipofu na viziwi watakapoona na kusikia, mwenye kupooza atarukaruka tena na bubu kuimba kwa furaha. Mara moja toka katika alama hizi tunagundua kuwa Masiha anakuja kwa ajili ya kuwaondoa walio katika taabu na kuwaweka huru. Taabu kwa kawaida ni tokeo la dhambi, yawezekana dhambi ya mtu binafsi lakini hasa dhambi kwa ujumla.
Mpendwa msikilizaji, katika hili tunaalikwa kuingia katika safari ya toba na uaminifu kwa Injili kama tusomavyo katika Injili ya Marko. 1:15. Katika toba na kuishi Injili tunafikia kwa namna ya pekee kabisa hatua ya kutambua alama zinazomtambulisha Masiha.
Jukumu la kuishi alama hizi linatuweka katika mazingira ya furaha na linatuonesha waziwazi kwamba utawala wa Masiha unaanza kukolea katika maisha yetu.
Mpendwa mwana wa Mungu, inawezekana ikajitokeza kukawa na kuchelewa katika utekelezaji, yaani kuishi toba na hivi tukaweza kukata tamaa, basi Mtume Yakobo anatutia moyo na tumaini akisema, kuweni na subira mpaka Bwana atakapokuja. Katika subira tunataka polepole kutenganisha uovu na ubaya ulio katika jumuiya na katika mtu awaye yote katika ubinafsi wake.
Katika subira Mtume Yakobo anatuonya daima kuachana na tabia ya kuhukumiana maana hakimu mwaminifu ni mmoja yaani Mfalme Masiha. Mtume Yakobo anatuonya katika subira kutambua kuwa safari ya wokovu lazima itazamwe kama mkulima anavyongojea mvua za masika na za vuli.
Mpendwa msikilizaji, kipindi cha Majilio ni kipindi cha neema, ni kipindi cha kupanda ili kujipatia mavuno hapo baadaye, na kwa hakika mavuno ni furaha ya moyo inayokamilishwa katika Yesu Kristu mfufuka ambaye atatufufua siku ya mwisho na kukaa naye katika kiti cha enzi pamoja na Baba mbinguni.
Nikikutakia majilio njema napenda kusema fikiria zaidi kuwalisha maskini na kuwahudumia wagonjwa katika jumuiya yako na jitahidi kuwa adui wa dhambi kila siku ya maisha yako. Mpendwa, hiyo ndiyo namna ya kuishi Majilio ya mwaka huu. Nakukumbusha tena hapo jirani kwako kuna mtoto ambaye amekosa ada ya shule msaidie na mfundishe namna ya kuitumia na zawadi yako kwa hakika ni mbinguni. Tumsifu Yesu Kristo na Bikira Maria.

Tafakari hii imeletwa kwako na Padre Richard Tiganya, C.PP.S.

Teacher handed 3 life sentences for rape

Colonel Jay Naicker said Nkosingiphile Hlekwayo, 50, raped the 11-year-old girl on three occasions in 2009. The court sentenced him on Wednesday.
 

A KwaZulu-Natal school teacher has been handed three life sentences by the Empangeni Regional Court for the rape of an 11-year-old pupil, police said on Friday.
Colonel Jay Naicker said Nkosingiphile Hlekwayo, 50, raped the 11-year-old girl on three occasions in 2009. The court sentenced him on Wednesday.
"The victim reported the matter to her parents and a case was opened at the Empangeni police station," he said.
"The Empangeni family, child protection and sexual offences unit took over the investigation that led to the arrest of the accused on the same day that the offence was reported."
He said Hlekwayo's family allegedly approached the girl's family and promised to pay them or give them cattle if they withdrew the case.
"The victim's parents refused to do so and they... allegedly received death threats. The victim was taken to a place of safety until the case was finalised."
Provincial police commissioner, Lt-Gen Mmamonnye Ngobeni welcomed the sentence and expressed her confidence in the judicial system.

Robin van Persie hatachezea Manchester United kipindi hiki

Robin van Persie 




Robin van Persie hatachezea Manchester United kipindi hiki cha mechi nyingi baada ya kupata jeraha la paja ambalo litamuweka nje mwezi mmoja, meneja David Moyes alisema Ijumaa.
"Robin Van Persie atakuwa nje mwezi mmoja. Alipata jeraha kwenye paja akipiga kona ambayo ilizaa goli (dhidi ya Shakhtar Donetsk on Tuesday)," Moyes aliambia kikao cha wanahabari kabla ya mechi yao ya Jumapili Aston Villa.
Mholanzi huyo, ambaye amefunga mabao saba katika mechi 11 za Ligi ya Premia msimu huu, alirejea baada ya kuuguza jeraha la mtoki wikendi iliyopita wakati wa

Arsenal ya lala kwa Man City 6-3

a
Man City
Manchester City, wametoa ujumbe mkali kwa mahasimu wao kwenye ligi ya Premier Arsenal baada ya kuwacharaza mabao sita kwa matatu.
Upande wa Manuel Pellegrini uliwacharaza Arsenal na kuziba pengo la pointi tatu.
Arsenal walilalamika wakitaka kupewa penalty moja ingawa kwa kweli Man City walikuwa wamejiandaa vilivyo dhidi ya Arsenal, huu ulikuwa kama upepo kwao.

Safari ya Mandela mwisho Kijiji cha Qunu


Jeneza la Mandela
Mwili wa hayati Nelson Mandela umepelekwa katika mkoa wa Eastern Cape kwa safari ya mwisho kabla ya kuzikwa siku ya Jumapili kijijini Qunu.
Idadi kubwa ya watu walifurika barabara angalau kumtupia jicho shujaa wao na kutoa heshima zao za mwisho.
Mandela aliyefariki tarehe 5/12/2013 atafanyiwa maziko ya kitaifa siku ya Jumapili tarehe 15/12/2013,

Jumuiya ya Kimataifa inaomboleza Kifo cha Tata Madiba!

Viongozi wa Jumuiya ya Kimataifa pamoja na wananchi wa Afrika ya Kusini wameanza kutoa heshima zao za mwisho kwa Tata Madiba kwa sala kutoka kwa viongozi mbali mbali wa kidini nchini Afrika ya Kusini. Mvua iliyokuwa inanyeesha imewazuia wananchi wa kawaida kufika uwanjani ili kutoa heshima zao za mwisho kwa Mzee Nelson Mandela, lakini mvua ni kielelezo cha baraka kwa makabila mengi Barani Afrika.

Siku ya pili heshima mwili wa Mandela


Jeneza lenye mwili wa Hayati Nelson Mandela
Waombolezaji nchini Afrika Kusini wanaingia siku ya pili katika zoezi la kutoa heshima za mwisho kwenye mwili wa Rais wa kwanza mweusi nchini Afrika Kusini Hayati Nelson Mandela.
Maelfu ya watu wamejipanga kwenye mistari wakisubiri kutoa heshima zao za mwisho kwenye mwili huo uliolazwa katika ikulu kwenye jengo la Muungano mjini Pretoria.

Madiba, kwa heri! Umekuwa ni daraja la upatanisho!


Mwili wa Marehemu Nelson Mandela, Siku ya Jumatano tarehe 11 Desemba 2013 umewasili mjini Pretoria ambako utakaa kwa muda wa siku tatu, ili kutoa nafasi kwa wananchi wa Afrika ya Kusini kutoka heshima zao za mwisho. Magari ya Polisi yaliusindikiza Mwili wa Tata Madiba kutoka kwenye Hospitali ya Kijeshi.

Wezi wavunja nyumba ya Askofu Tutu!


Desmond Tutu
Wezi wamevunja na kuingia nyumbani kwa Askofu mstaafu Desmond Tutu
Polisi wamesema wizi huo ulifanyika wakati bwana Tutu akiwa katika ibada ya Nelson Mandela Mjini Johannesberg.
Inaarifiwa Tutu aliibiwa vitu vyake wakati akiwa anahudhuria ibada maalum ya kumuaga Hayati Nelson Mandela siku ya Jumanne.
Aidha wameelezea kuwa uvamizi ulifanyika nyumbani kwake mjini Cape Town Ahamisi jioni baada ya kutoa hotuba katika ibada ya Mandela siku hiyo.
Ibada hiyo ilifanyika katika uwanja wa FNB mtaani Soweto.
Wizi na uvamizi wa nyumba za watu ni jambo la kawaida nchini Afrika Kusini ambako visa vya uhalifu viko juu sana.

Heshima za mwisho kwa mwili wa Mandela


Mwili wa Mandela ukisindikizwa na polisi Afrika Kusini
Viongozi mbali mbali pamoja na raia wa Afrika Kusini wanaendelea kutoa heshma za mwisho kwenye mwili wa aliyekuwa rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini Marehemu Nelson Mandela ambao umelazwa kwenye ikulu ya Afrika Kusini mji Mkuu wa Pretoria, ambapo utalala hapo kwa siku tatu.
Mwili ulichukuliwa katika msafara kutoka chumba cha maiti cha hosptali hadi kwenye jengo la Muungano.
Msafara wenye jeneza la Marehemu uliondoka mjini katika Hosptali ya jeshi muda mfupi siku ya jumatano. Jeneza lilibebwa kwenye gari maalum na kufunikwa bendera ya Afrika Kusini.
Wananchi walijipanga kando kando ya barabara lilipopitishwa jeneza kama ishara ya kutoa heshma za mwisho kwa mwili wa marehemu.
Msafara ulipita katika mitaa huku baadhi ya raia wakikimbia pembeni kwenye mstari wa askari wa

Kili Stars yafa, lakini kiwango


Picha kushoto ni Mshambuliaji wa Tanzania Bara, Mbwana Samata akiwatoka mabeki wa Kenya, Joackins Atudo (kulia) na Aboud Omar kwenye Uwanja wa Nyayo jana. Kili Stars ililala 1-0.

Licha ya timu ya Taifa ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) kumiliki mpira kwa dakika zote 90, imeshindwa kutinga fainali ya michuano ya Kombe la Chalenji baada ya jana kukubali kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Kenya (Harambee Stars).

Drogba, Eboue salute to Madiba sparks row

ANKARA - Turkey's sports minister lashed out on Monday at moves by the football authorities to punish two top Ivorian club players for paying homage to Nelson Mandela.
 
Emmanuel Eboue

Didier Drogba and Emmanuel Eboue have been threatened with disciplinary action by the Turkish Football Federation for violating a ban on wearing political slogans on T-shirts, triggering outrage on Twitter.
Turkish Sports Minister Suat Kilic called on the federation to review its decision against the two star players with Istanbul giants Galatasaray.
"I don't find it a healthy choice in terms of Turkey's image abroad and the two footballers' [freedom of] expression," he said.
Drogba removed his club shirt after a match at the weekend against SB Elazigspor to reveal a T-shirt that read "Thank You Madiba", using Mandela's clan name.
Teammate Eboue also honoured the South African anti-apartheid hero who died on Thursday with a T-shirt that said "Rest in Peace Nelson Mandela".

Obama scripts world farewell


"It is hard to eulogise any man... How much harder to do so for a giant of history, who moved a nation toward justice, and in the process moved billions around the world," Obama began, in a speech that placed Mandela in the pantheon of Mahatma Gandhi and Martin Luther King.


US President Barack Obama summed up the awed respect Nelson Mandela inspired around the world at a rain-drenched memorial in Soweto on Tuesday that hinted at the tension straining South African politics after his death last week.
"It is hard to eulogise any man... How much harder to do so for a giant of history, who moved a nation toward justice, and in the process moved billions around the world," Obama began, in a speech that placed Mandela in the pantheon of Mahatma Gandhi and Martin Luther King.

Mlango wa Bwana daima ni wazi na kutupatia tumaini



Hatupaswi kuhofia ukombozi wa Bwana , badala yake , ni kujiweka tayari kwa ajili ya ujio wake. Ni kuufungua mlango wa moyo na kumpokea kwa matumaini. Papa alieleza katika homilia yake wakati wa Ibada ya Misa, mapema asubuhi Jumanne, katika Kanisa dogo la Mtaktifu Marta hapa Vatican.

Papa alitafakari maneno ya somo la kwanza, kutoka Kitabu cha Nabii Isaya, ambamo Nabii Isaya anasema, "farijikeni enyi watu wangu, Bwana, yu karibu na watu wake, kuwatuliza ,na kuwapa amani". Papa ameeleza kazi hii ya kufariji, ina uwezo wa kubadili yote. Bwana, kweli ana uwezo wa kuviumba vyote upya .

Mama Maria Nyerere amsimulia Mandela





Maria Nyerere pichani ambaye ni mke wa aliyekuwa rais wa kwanza nchini Tanzania Mwalimu Nyerere, amesema Nelson Mandela ataendelea kukumbukwa kwa moyo wake wa kusamehe na kumtaja kwamba alikuwa ni zawadi ya dunia katika kuleta upendo na maridhiano.
Uhusiano kati ya familia ya Mwalimu Nyerere na ile ya Mzee Nelson Mandela umekuwa ni wa karibu kiasi kwamba familia yake inajiandaa kwenda kuhudhuria katika mazishi yatakayofanyika tarehe 15 mwezi huu.

Mandela the secret weapon in 1995 final


For South Africans, winning the 1995 Rugby World Cup final marked the emergence of the "Rainbow Nation" -- for New Zealanders, it was the day Nelson Mandela single-handedly outpsyched the mighty All Blacks.

 
Former President Nelson Mandela congratulates South African rugby team'

The Jonah Lomu-inspired New Zealanders were red-hot favourites going into the decider, breezing through the group stages and humiliating England in the semi-finals.
In contrast, the Springboks scraped through on the back of an unconvincing 19-15 semi-final win over France, raising fears they would be blown away in the final at Johannesburg's Ellis Park.
Then Mandela, in one of the most audacious political gambles of his career, appeared before the mostly white crowd of 62,000 wearing a Springbok jersey to shake the players' hands before kick-off.

FIFA World Cup History

South Africa 2010
Winner: Spain
Runners-Up: Netherlands
Third: Germany
Fourth: Uruguay
adidas Golden Ball: Diego FORLAN (URU)
adidas Golden Boot: Thomas MUELLER (GER)
Best Young Player Award: Thomas MUELLER (GER)
adidas Golden Glove: Iker CASILLAS (ESP)
FIFA Fair Play award: Spain

Mwandishi wa BBC amkumbuka Mandela


Mandela aliwagusa watu wengi duniani
Nelson Mandela alijiondoa kutoka maisha ya umma mwaka 2004. Mwandishi wa BBC Richard Hamilton alikuwa mwandishi wa BBC mjini Cape Town wakati huo na anatuletea kumbukumbu zake kuhusu rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini:
"Bwana Mandela, unawezaje kuwa katika hali hii nzuri ya mwili? Aliuliza ripota msichana wa tv, ambaye aligongana jicho na Bwana Mandela.
Tulikuwa katika eneo la gereza la Kisiwa cha Robben ambako Nelson Mandela alitumikia miaka kumi na nane kati ya ishirini na saba aliyofungwa jela.

Struggle giants die within 10 years of each other


In the 1940s Tambo, Sisulu, Mandela and other young intellectuals of the time regularly visited the house of then ANC president Dr AB Xuma. It was there that they came up with a plan to revive the ANC and make it more accessible to ordinary people. In 1944 the three men helped form the ANC Youth League.


Three giants of the struggle -- Oliver Tambo, Walter Sisulu, and former president Nelson Mandela -- died within 10 years of each other.
The first to die was former African National Congress president Oliver Tambo in 1993.
Tambo and Mandela met when they were studying at the University of Fort Hare in the Eastern Cape.
In the 1940s Tambo, Sisulu, Mandela and other young intellectuals of the time regularly visited the house of then ANC president Dr AB Xuma. It was there that they came up with a plan to revive the ANC and make it more accessible to ordinary people. In 1944 the three men helped form the ANC Youth League.
Tambo spent over 30 years in exile. He become acting ANC president in 1967 following the death of Chief Albert Luthuli and in 1985 he was re-elected president of the party.
The same year Tambo returned from exile he was elected ANC chairman. He died on April 24, 1993 at the age of 75 due to complications after a stroke.
During his speech at Tambo's funeral Mandela said: "Here lies before you the body of a man who is tied to me by an umbilical cord which cannot be broken."
In 2003 former ANC secretary general and deputy president of the ANC Walter Sisulu died.
Sisulu, who was born in 1912, the year the ANC was founded, died at his Johannesburg home in the arms of his wife Albertina, herself a legend in her own lifetime.
In a tribute to Sisulu Mandela said: "Xhamela is no more. May he live forever! His absence has carved a void. A part of me is gone."
Mandela's impassioned statement at the time spoke of a 62-year-old friendship.
"Our paths first intersected in 1941. During the past 62 years our lives have been intertwined. We shared the joy of living, and the pain," he said.
"In a sense I feel cheated by Walter. If there be another life beyond this physical world I would have loved to be there first so that I could welcome him. Life has determined otherwise."
On Thursday, 10 years after his old friend's death, Mandela died at the age of 95. He will be buried in his hometown of Qunu in the Eastern Cape next Sunday.

Msiba wa Mandela kuwabeba Tanzanite leo?


the TanzaniteMKUU wa msafara wa timu ya taifa ya wanawake ya Afrika Kusini chini ya miaka 20, Peter Manchonyane, ameelezea wasiwasi wa kikosi chake kuathiriwa na msiba wa Rais wa zamani wa nchi yake, Nelson Mandela, katika mechi ya leo dhidi ya Tanzania ‘Tanzanite’.
Bara la Afrika na dunia kwa jumla, inaomboleza msiba wa Mandela, aliyefariki juzi usiku, saa chache baada ya kikosi cha vijana cha nchi hiyo kutua nchini kwa mechi ya mchujo kuwania kufuzu fainali za dunia kwa wanawake chini ya umri huo, zitakazochezwa nchini Canada mwakani.
Manchonyane alisema kuwa kikosi chake kinachojulikana kwa jina la ‘Basetsana’, kimekumbwa na simanzi miongoni mwa wachezaji na viongozi, baada ya kifo cha Mandela na kwamba anahisi kitaathiri harakati zao leo.
Pamoja na hofu hiyo, kiongozi huyo alisisitiza kuwa lengo lililowaleta ni kupigana kusaka ushindi, ili kujiwekea mazingira mazuri kuelekea mechi ijayo kuwania tiketi ya kufuzu raundi ya tatu na ya mwisho ya mchujo huo wa fainali za mwakani huko Canada.
“Tumeshtushwa na kifo cha Mzee Mandela, kambi imejaa simanzi. Licha ya kutarajia ugumu kucheza tukiwa katika hali hiyo, lakini tunaamini tutashinda changamoto hiyo na kuibuka na ushindi ili kuondoa presha katika mechi ya marudiano nyumbani,” alisema Manchonyane.
Kwa upande wake kocha wa Tanzanite, Rogasian Kaijage, alisema, kauli ya kiongozi huyo ni ‘danganya toto’ iliyobeba mantiki ya kuwahadaa na kuvimbisha kichwa na kwamba ameligundua hilo na kikosi chake kitacheza kwa tahadhari dhidi ya Basetsana.
Alisema, anakitambua kikosi cha Basetsana ni kizuri, imara na bora, hivyo kazi ya nyota wake itakuwa kupigania matokeo mazuri nyumbani kama ilivyokuwa dhidi ya Msumbiji na wala hawatobweteka kwa alichokiongea kiongozi huyo.

“Basetsana kama jina lao lilivyo ni wasichana wadogo, ambao ni vigumu kushikwa na simanzi kubwa juu ya msiba wa kiongozi ambaye wakati anatawala wengine walikuwa wadogo, wengine hawajazaliwa. Watoto mara nyingi hawaguswi sana na vifo,” alifafanua Kaijage.
Aliongeza kuwa, nia yao kama timu ni kupigania matokeo mazuri na kuwataka Watanzania kumiminika kwa wingi kuwasapoti mabinti hao, ili kuwapa nguvu ya kushinda na kujiweka pazuri kuelekea raundi ya tatu ya michuano hiyo.
Kwa upande wake nahodha wa Tanzanite, Fatuma Issa, alisema, morali katika kikosi chake iko juu na kwamba, Watanzania wanapaswa kujitokeza kwa wingi Uwanja wa Taifa ili kuwashangilia kuwaongezea nguvu na Mungu akipenda wataibuka na ushindi.
Viingilio katika mechi ya leo itakayopigwa kuanzia saa 10:00 alasiri, vitakuwa ni sh 1,000, sh 2000, sh 5,000 na sh 10,000, ambako tiketi zitauzwa uwanjani hapo leo.

Papa Francisko aomboleza kifo cha Mzee Madiba!



Baba Mtakatifu Francisko ametuma salam za rambirambi kwa Rais Jacob Zuma wa Afrika ya kusini na wananchi wa Afrika ya Kusini kwa ujumla wao kutokana na kifo cha Mzee Nelson Mandela. Anaiombea roho ya Mzee Mandela iweze kupata huruma ya Mungu pamoja na kuendelea kuwaimarisha wote walioguswa na msiba huu mzito!

Baba Mtakatifu Francisko anasema, Mzee Nelson Mandela alisimama kidete kulinda na kutetea utu na heshima ya raia wake; akajenga na kuimarisha umoja wa wananchi wa Afrika ya Kusini pasi na vita, wakitembea katika njia ya upatanisho na ukweli. 



Ni matumaini ya Baba Mtakatifu kwamba, mchango wa Mzee Mandela utakuwa ni changamoto kwa wananchi wa Afrika ya Kusini kusimama kidete kulinda haki na mafao ya wengi; wanasiasa wakiwa mstari wa mbele. Baba Mtakatifu anawapatia wananchi wote wa Afrika ya Kusini baraka zake za kitume, wakati huu wa maombolezo ya kitaifa!

Ni kisasi leo Kili Stars vs Cranes


Kili na CranesKIKOSI cha timu ya taifa ya Tanzania bara ‘Kilimanjaro Stars’, kinatarajiwa kushuka dimbani leo kuwakabili Uganda ‘The Cranes’ katika mechi ngumu ya robo fainali ya michuano ya Chalenji iliyoanza kutimua vumbi Novemba 27.
Mechi kati ya Stars na Cranes ambao ndio mabingwa watetezi, inafananishwa na fainali kutokana na upinzani wa timu hizo. Itachezwa saa 8:00 mchana kisha kufuatiwa na mchezo mwingine wa hatua hiyo saa 10:00 jioni kati ya wenyeji Kenya ‘Harambee Stars’ na Rwanda.
Akizungumzia mchezo huo, Kocha Mkuu wa Stars, Kim Poulsen, alisema ana imani ya kufanya vema kutokana na ubora wa kikosi chake, hasa baada ya kuwasili kwa nyota wa kimataifa, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu.
Poulsen alisema siku mbili tangu walipotoka kucheza na Burundi, amehakikisha anarekebisha matatizo aliyoyaona katika mchezo huo, hasa safu ya ulinzi ambayo ilionekana kulegalega.
Naye kipa wa Stars, Ivo Mapunda, alisema hakuna timu ambayo wanaihofia katika michuano hiyo, bali cha muhimu ni dakika 90 za uwanjani ndizo zitaamua nani anasonga mbele na nani anafungasha virago.
Alisema ana imani kubwa ya kufanya vema katika mchezo wa leo, huku akiwataka wachezaji wenzake kutulia na kucheza mpira, kwani kuwafunga Uganda kuko pale pale ila cha muhimu Watanzania ni dua zao.
“Unajua hakuna mtu aliyetegemea kama tutafika hapa tulipo sasa, hivyo basi kwanini mbele tushindwe? Uganda ni timu ya kawaida tu kama timu nyingine, nina imani tutashinda,” alisema Mapunda.
Naye Kocha wa Uganda, Milutin Micho aliyewahi kuifundisha Yanga, alisema anauhofia mchezo wa leo, baada ya kuwaona Samatta na Ulimwengu wakiwemo katika kikosi cha Kili Stars.
Micho alisema lolote linaweza kutokea katika mchezo huo, cha muhimu ni kusubiri dakika 90 za mwamuzi uwanjani ila Tanzania ni timu nzuri.
“Mechi hiyo itakuwa ngumu, kwa kuwa nimefuatilia mechi za Tanzania, ni wazuri, lakini vijana wangu pia watapambana ili kuhakikisha wanashinda,” alisema Micho.

Nelson Mandela kuzikwa Desemba 15 siku ya Jumapili


Nelson Rolihlahla MandelaSIKU moja baada ya kifo cha  Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, Mzee Nelson Mandela (95), mazishi yake yanatarajiwa kufanyika wiki moja kuanzia sasa, Desemba 15, siku ya Jumapili.
Mazishi hayo ya kihistoria na ya aina yake, yatafanyika katika kijiji chake cha Qunu, mahala alipopachagua mwenyewe kabla ya kifo chake.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, Mzee Madiba atazikwa katika eneo hilo la Mashariki ya Cape kwa heshima zote.
Zuma alisema mazishi ya kitaifa, ikiwamo utoaji wa heshima za mwisho, yatafanyika jijini Pretoria ambapo baadaye mwili wake utasafirishwa kwenda Mkoa wa Cape Mashariki hadi katika Kijiji cha Qunu ambako ndiko  Mzee Madiba alipozaliwa na kukulia.
Aidha, taarifa hiyo ilieleza kuwa  Mzee Madiba  atazikwa kwa sherehe maalumu za kimila karibu na makaburi ya watoto wake watatu.
Kutokana na msiba huo ulioikumba dunia, wakuu wa nchi mbalimbali duniani, akiwemo Rais wa Marekani, Barack Obama, Oprah Winfrey na Hillary Clinton wanatarajiwa kuhudhuria mazishi hayo mbali ya viongozi wengine kutuma salamu za rambirambi kwa Rais Zuma na kwa familia ya Mzee Madiba.
Viongozi duniani wanena
Miongoni mwa marais waliotuma salamu za rambirambi kwa Rais Zuma na kwa mjane  wa Mzee Madiba, Graca Machel, wanafamilia wote na wananchi wote wa Afrika Kusini ni pamoja na Jakaya Kikwete wa Tanzania ambaye pia ametangaza siku tatu za maombolezo kuanzia jana hadi Desemba 8  na kuagiza bendera kupepea nusu mlingoti kwa siku hizo.
Katibu Mkuu wa  Umoja wa Mataifa,  Ban Kin Moon alisema Mandela alikuwa kielelezo cha  Umoja wa Mataifa  kwani alikuwa mtu wa heshima na mtetezi wa haki za binadamu,  aliyepinga ubaguzi wa rangi na mpigania usawa.
“Kwa niaba ya Umoja wa Mataifa, natoa rambirambi zangu kwa watu wa Afrika Kusini na hasa kwa familia ya Nelson Mandela na wapendwa,” alisema.
Aidha, Moon alieleza kuwa inashangaza, kuona Mandela alitoka kizuizini bila uadui baada ya kifungo cha miaka 27, ambapo nia yake ilikuwa kujenga nchi yake katika misingi bora kwa kutumia akili.
Salamu za Rais Kikwete kwa Zuma
Rais Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Rais Zuma, wanafamilia na wananchi wote wa Afrika Kusini kutokana na kifo cha Mzee Mandela.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mwandishi wa habari wa rais msaidizi, Ikulu Premi Kibanga, Rais Kikwete ametangaza siku tatu za maombolezo kuanzia jana Desemba 6 hadi 8 mwaka huu.
Aidha, Rais Kikwete alisema kuwa katika siku hizo bendera zote zitapepea nusu mlingoti.
Rais Kikwete alisema kuwa msiba huo ni wa bara zima la Afrika na dunia.
“Afrika Kusini, Afrika na dunia kwa ujumla imepoteza mtu mashuhuri na shujaa mkubwa wa karne ya 20 na 21. Tunaelewa machungu waliyonayo wananchi wa Afrika Kusini kwa kupoteza kiongozi shupavu, jasiri, mwanamapinduzi na mstahamilivu,” alisema.
Rais Kikwete alimuelezea Mzee Mandela kuwa ni  kielelezo cha aina yake kwa wanadamu kwa moyo wake wa kusamehe, huruma na upendo uliomuwezesha  kuwaunganisha wananchi wa Afrika Kusini kuwa taifa moja baada ya kipindi kirefu cha mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi.
“Mandela ni mfano bora kwa wanadamu, wa jinsi binadamu muungwana anavyopaswa kuwa. Ni wajibu wa wana Afrika Kusini, Afrika na dunia kwa jumla kuiga mfano wake, hasa moyo wake wa uzalendo, kujitolea hata maisha yake kwa ajili yake na wananchi wenzake.”
Alisema ni muhimu kumuombea kwa Mwenyezi Mungu ailaze roho yake  mahali pema peponi.
Kwa upande wake Mkuu wa Idhaa za Kiafrika katika DW, Claus Stäcker alisema kuwa vyombo vya habari na wanasiasa duniani kote wanaendelea kushindana katika kuonyesha heshima zao kwa Mandela, ambaye yeye mwenyewe hakupenda kuchukuliwa kama Mungu.
Stäcker alisema Mandela hakuwa mtakatifu, hata ingawa hivyo ndivyo vyombo vya habari vinavyomwelezea. Kila kichwa cha habari kinamfanya aonekane kama mtu aliyefanya maajabu na hasa kuonekana kama kuiabudu sanamu.
“Mandela mwenyewe hakupenda kuabudiwa. Alikuwa akikubali tu shingo upande barabara, shule na taasisi kuitwa jina lake, kuruhusu sanamu za shaba na majumba ya makumbusho ya Mandela kujengwa, mtindo ambao bila shaka utaendelea kukua,” alibainisha  Stäcker.
Jijini Dar es Salaam, vilio, simanzi na majonzi  vilitawala katika Ofisi za Ubalozi wa Afrika Kusini uliopo nchini baada ya raia wa mataifa mbalimbali wakiwemo Waafrika Kusini wanaoishi nchini, kufika kwa ajili ya kutoa pole kutokana na kifo cha Mzee Mandela.
Raia hao ambao wengi ni wa kigeni walifika katika ubalozi huo kuanzia majira ya saa moja asubuhi, huku wakibeba mashada ya maua na kuyaweka katika picha kubwa ya Mandela iliyowekwa mbele ya ofisi za kuingilia za ubalozi huo.
Raia wa Canada anayeishi hapa nchini aliyejitambulisha kwa jina moja la Jeff, alisema ameguswa na kifo hicho kutokana na Mzee Mandela kuwa mfano bora kwa jamii hasa katika harakati zake za kupinga ubaguzi wa rangi.
“Nimeamua kuambatana na familia yangu kuja kutoa pole kwa kifo hicho kimetugusa sana kwani tumekuwa tukimuangalia Mandela kama mfano wa kuigwa kwa dunia nzima,” alisema.
Akizungumzia kifo hicho, Balozi wa Afrika Kusini nchini, Thanduyise Henry Chiliza alisema ni huzuni kubwa na majuto kuwajulisha kuwa rais wa zamani na nembo ya kitaifa, Nelson Rolihlahla Mandela, amefariki dunia juzi Desemba 5, mwaka huu, majira ya saa 2:50 usiku akiwa na umri wa miaka 95.
“Ingawa sisi tulijua kwamba siku hii itakuja, lakini hakuna kitu kinachoweza kupunguza hisia zetu na hasara kubwa tuliyopata na ya kudumu kwa kumpoteza kiongozi huyo,” alisema.
Alisema kutokana na msiba huo bendera ya taifa hilo itapepea nusu mlingoti hadi mazishi ya Mzee Mandela yatakapofanyika.
“Kitabu cha maombolezo kimefunguliwa katika ubalozi wetu plot 1338/9, barabara ya Mwaya, Masaki, Dar es Salaam kuanzia Jumatatu hadi Alhamisi saa 3:30 hadi saa 9:30 na Ijumaa saa 3:30 hadi saa 6:30 mchana kasoro siku za sikukuu,” alisema.
Chiliza alisema Serikali ya Afrika Kusini inaendelea na mipango ya mazishi na Waafrika Kusini kila pembe ya dunia watajulishwa suala hilo.
Maisha ya Mandela
Mandela alikuwa mtu aliyezaliwa kuwa kiongozi.
Kama rafiki yake waliyefungwa naye pamoja, Ahmed Kathrada, alivyosema hivi karibuni, Mandela alizaliwa katika familia ya kifalme na ilikuwa kawaida kwake kuwa alizaliwa kuwa kiongozi.
Mandela alijibeba vyema sana alipokuwa kiongozi wa chama cha ANC na kwamba hakuna hata nusu ya imani yake iliwahi kumuondoka miaka yote 27 aliyokuwa gerezani.
Ingawa Mandela alijitaja mwenyewe kuwa kama sehemu tu ya uongozi wa ANC, hapakuwa na shaka kuwa alikuwa kiongozi mkuu wa chama hicho kwa kizazi chake wakati huo nchini Afrika Kusini.
Kwa dunia nzima Mandela alikuwa ishara ya mambo mengi, sio kiongozi tu, lakini mfano wa viongozi ambao dunia inastahili kuwa nao enzi hizo.
Wengi wanamfahamu Mandela kwa kuwa na moyo mwepesi wa kusamehe na wengi wanamkumbuka hivyo kwani baadhi walimshangaa sana miaka ya tisini, aliposema kuwa hana chuki na mtu na kuwa amewasamehe waliomtendea ubaya na hata kumfunga.
Alizaliwa mwaka 1918, katika Rolihlahla Dalibhunga, na kulelewa katika Kijiji cha Mvezo Mashariki mwa Mkoa wa Cape.
Alikuwa na ndugu zake 13 katika familia iliyokuwa na uhusiano wa karibu na familia ya kifalme ya Thembu.
Mandela alienziwa na wengi kwa sababu ya vita aliyopigana dhidi ya utawala wa wazungu.
Baba yake alifariki Mandela akiwa na miaka tisa. Alimtaja baba yake kama mtu mkali mwenye kutaka watu kufuata maadili mema.
Lakini alimsifu sana baba yake kwa kumsisitizia kuwa na maadili mema kwani yeye ndiye alimfanya kuwa mtu mwema maishani.
Ilikua muhimu kwake kupata elimu. Na hivyo akasomea katika shule ya kimethodisti na kisha mwaka 1939 akaenda katika Chuo Kikuu cha Fort Hare.
MAISHA YAKE KWA UFUPI
1943: Alijiunga na chama cha ANC.
1956: Alifunguliwa kesi ya uhaini, lakini baada ya miaka minne ikatupiliwa mbali.
1962: Alikamatwa na kushitakiwa kwa kosa la uchochezi na kufungwa jela miaka mitano.
1964: Alishitakiwa kwa kosa la kuhujumu serikali na kufungwa maisha jela.
1990: Aliachiliwa kutoka gerezani.
1993: Alishinda tuzo ya Amani ya Nobel.
1994: Alichaguliwa kuwa rais wa kwanza mweusi Afrika Kusini.
1999: Aling’atuka madarakani.
2001: Aligundulika kuwa na saratani ya tezi kibofu.
2004: Alistaafu.
2005: Alitangaza kuwa mwanawe alifariki kwa maradhi ya ukimwi.

Kifo cha Mandela:Dunia waomboleza


Nelson Mandela kuzikwa tarehe 15 Desemba
Raia wa Afrika Kusini wako kwenye maombolezo kwa siku ya pili hii leo wakiwa kwenye mkesha kwa usiku nzima kwa ajili ya kuomboleza mpendwa wao Kiongozi wa zamani wa taifa hilo Nelson Mandela, aliyeaga dunia siku ya Alhamisi akiwa na umri wa miaka 95.
Watu wamekuwa wakikumbuka mema yake , wakicheza na kuimba Mbele ya makazi yake ya zamani mjini Soweto.
Katika mkutano na Waandishi wa habari , Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma aliainisha matukio ya juma zima kwa ajili ya maombolezo ambapo ametangaza kuwa siku ya jumapili siku maalum ya maombi na ibada maalum.
Siku ya Jumanne, itakuwa ni siku ya shughuli maalum za maombolezo ya kitaifa ambapo shughuli hizo zitafanyika katika uwanja wenye uwezo wa kukusanya watu 95,000 ulio nje kidogo ya mji wa Johannesburg.
Raia wa Afrika kusini wakiwa kwenye maombolezo
Mwili wa Mandela utalala Ikulu ya nchi hiyo jijini Pretoria kuanzia siku ya jumatano mpaka siku ya ijumaa.
Mazishi ya Mandela yatafayika jumapili ijayo tarehe 15 kijijini kwake alikokulia,Qunu.
Mandela alitumikia kifungo cha miaka 27 kabla ya kuwa rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini.
Serikali yake iliondoa utawala wa kibaguzi wa watu weupe ambao ulikuwa na sera za kuwagawa watu wenye asili ya weupe na weusi.
Raia wa Afrika Kusini nchi nzima wamekuwa wakisali, wakiimba nyimbo za kupinga ubaguzi wa rangi na kuwasha mishumaa, wakikumbuka maisha ya Kiongozi wao na namna alivyo wavuta kwa mtindo wa maisha yake.