Week Hot newz

Papa "Wambea hawana bunge na wala umbea si mtaji wangetajirika wengi"

Baba Mtakatifu Francisko anawataka watawa kuwa ni mashuhuda wa kinabii, watu wanajenga utamaduni wa ujirani mwema na watu wenye matumaini kwa Mwenyezi Mungu. - OSS_ROM
02/02/2016 07:39
Maadhimisho ya kufunga Mwaka wa Watawa Duniani, Jumatatu tarehe Mos Februari 2016 yalichukua sura mpya pale Baba Mtakatifu Francisko alipokabidhi hotuba yake kuhusu wosia ambao amependa kuwakabidhi watawa wakati huu Mama Kanisa anapofunga rasmi maadhimisho ya Mwaka wa Watawa Duniani kwa kuwataka wayakite maisha yao katika mambo makuu matatu: Unabii, Ujirani na Matumaini. Baba Mtakatifu akaamua kutoa katekesi ya kina kwa kuzungumza na watawa moja kwa moja, ili kuangalia ukweli wa maisha na utume wa watawa ndani ya Kanisa.

Vijana wa kizazi kipya wafundwe elimu ya watu kukutana!


Baba Mtakatifu Francisko anawataka wadau mbali mbali wa sekta ya Elimu Katoliki kuhakikisha kwamba, wanawajengea vijana wa kizazi kipya msingi wa elimu utakaowawezesha kukutana na wenzao, kusaidiana na kushirikiana kwa dhati pasi na makunyanzi. - OSS_ROM
Kanisa halina budi kuwasaidia vijana kujenga na kudumisha utamaduni wa watu kukutana, kusaidiana, kuheshimiana na kuthaminiana kwani wote wameumbwa kwa sura na mfano wa Mungu. Hapa binadamu anapaswa kupewa kipaumbele cha kwanza katika sera na mikakati ya elimu makini badala ya kugubikwa na woga pamoja na wasi wasi usiokuwa na mvuto wala mashiko. Hii ni sehemu ya ujumbe kutoka kwa Baba Mtakatifu Francisko kwa njia ya video aliowatumia washiriki wa Kongamano la Ishirini na Nne la Elimu Katoliki Amerika ya Kusini, lililoadhimishwa huko San Paolo del Brasile, hivi karibuni.
Baba Mtakatifu anawataka wadau mbali mbali wa elimu kuhakikisha kwamba, binadamu anapewa kipaumbele cha kwanza pamoja na kuwafunda vijana katika medani mbali mbali za maisha, ili waweze kushiriki kikamilifu katika mchakato wa maboresho ya maisha yao. Vijana waelimishwe namna ya kufikiri na kutenda vyema katika maisha yao. Haitoshi kuwapatia vijana nadharia ya mambo mengi, bila kugusa undani wa maisha yao. Vijana wafundishwe kutambua mema na kuyatafuta katika maisha yao ya kila siku.
Baba Mtakatifu anatambua na kukiri matatizo pamoja na changamoto ambazo wadau mbali mbali wanakabiliana nazo katika sekta ya elimu; changamoto ambazo zinapaswa kuvaliwa njuga na wahusika, ili kweli elimu inayotolewa iweze kuwa bora zaidi, ili kuwasaidia vijana wa kizazi kipya kupambana kikamilifu na mazingira yao, tayari kushiriki katika mchakato wa ujenzi wa dunia inayosimikwa katika haki, amani, umoja na udugu.
Baba Mtakatifu anasema, ili kuweza kufikia lengo hili, kuna haja kwa jamii kujenga na kudumisha utamaduni wa vijana wa kizazi kipya kukutana kati yao, ili waweze kujisikia kuwa ni wamoja; tayari kushirikiana ili kufanya kazi kwa pamoja bila kujali: imani, kabila au mahali anapotoka mtu: hapa utambulisho ni utu na heshima ya binadamu. Kwa njia hii, mchakato wa elimu utawasaidia vijana kukutana na hatimaye, kuzaa matunda yanayokusudiwa na wengi.
Baba Mtakatifu Francisko anakaza kusema, mfumo mpya wa shule ujulikanao kama “Scholas occurrentes” unaendelea kushika kasi kwa kujikita katika sana ana michezo; maeneo muhimu sana yanayowakutanisha vijana wa kizazi kipya. Michezo inawasaidia vijana kupata majiundo makini ya kufanya kazi kwa pamoja kwa kutegemeana. Sanaa inawafunda vijana kujenga na kudumisha majadiliano ya kina. Haya ni maeneo ambayo yanapaswa kufanyiwa kazi, ili kweli sekta ya elimu iweze kuzaa matunda yanayokusudiwa.
Baba Mtakatifu anawataka wadau wa Katoliki kufuata mfano wa Yesu Kristo aliyekuwa ni Mwalimu na Bwana; Mwalimu aliyefaulu kufafanua na kumwilisha Sheria katika uhalisia wa maisha ya watu. Ili waamini waweze kuzama zaidi katika Injili, wanahamasishwa kutafakari, kujisomea na kumwilisha Heri za Mlimani ambazo kimsingi ni muhtasari wa Mafundisho makuu ya Yesu kwa wafuasi wake. Matendo ya huruma ni kigezo ambacho Kristo atakitumia wakati atakapokuja kuwahukumu wazima na wafu na wala Ufalme wake hautakuwa na mwisho! Maadhimisho ya Mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya huruma ya Mungu, iwe ni fursa ya kumwilisha matendo ya huruma katika maisha ya watu, kielelezo cha imani tendaji.

Wakristo ni uzao mteule, ukuhani wa kifalme na taifa la Mungu!




Tamko la pamoja kati ya Kanisa Katoliki la Kanisa la Kiinjili la Kiluteri kuhusu kuhesababiwa haki ni msingi wa majadiliano ya kiekumene kuhusu: Kanisa, Sakramenti na Utume wa Kanisa. - OSS_ROM

Hija ya kiekumene ni utambulisho muhimu sana miongoni mwa Wakristo, unaowasukuma kutoa ushuhuda wao imani yao kwa Kristo na Kanisa lake, msingi wa umoja wa Wakristo. Ni maneno ya Baba Mtakatifu Francisko aliyoyatoa Jumatatu tarehe 18 Januari 2016 wakati alipokutana na kuzungumza na waamini wa Kanisa la Kiinjili la Kiluteri kutoka Finland ambao kwa sasa wako mjini Roma kwa ajili ya hija ya kiekumene na kama sehemu ya maadhimisho ya Siku kuu ya kumbu kumbu ya Mtakatifu Enric.

Huruma ni jina na utambulisho wa Mungu!


Huruma ni jina na utambulisho wa Mungu anasema Baba Mtakatifu Francisko. - AFP

Huruma ndilo jina na utambulisho wa Mwenyezi Mungu, hivi ndivyo anavyosema Baba Mtakatifu Francisko katika mahojiano maalum na Andrea Tornielli, mwandishi wa habari za gazeti la “La Stampa” na mhariri mkuu wa tovuti ya “Vatican insider” katika kitabu ambacho kimezinduliwa na Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican, “Jina la Mungu ni huruma”. Kitabu hiki kimegawanyika katika sura tisa ambazo ni majibu ya maswali 40 aliyoulizwa Baba Mtakatifu Francisko kama sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya Mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya huruma ya Mungu, uliozinduliwa hapo tarehe 8 Desemba 2015.
Baba Mtakatifu Francisko katika mahojiano haya anafanya rejea katika Maandiko Matakatifu, Mafundisho ya Mababa wa Kanisa pamoja na watangulizi wake, yaani Papa mstaafu Benedikto XVI, Mtakatifu Yohane Paulo II, Mtakatifu Yohane XXIII na Mwenyeheri Paulo VI. Kitabu hiki kimechapishwa katika lugha tano na nakala ya kwanza ikawasilishwa kwa Baba Mtakatifu Francisko, hivi karibuni. Kitabu hiki ni matunda ya mahojiano ya kina na majibu muafaka yaliyotolewa na Baba Mtakatifu Francisko huku akiwahamasisha waamini kutambua udhaifu wao, tayari kukimbilia huruma na upendo wa Mungu.

Tafakari ya Neno la Mungu, Sherehe ya Bikira Maria Mama wa Mungu

Bikira Maria Mama wa Mungu na Kanisa. - RV
Na Paskal Linda.
Mpendwa, unayeitegea sikio Radio Vatican, leo Mama Kanisa anasherehekea sherehe ya Mama wa Mungu ambayo huja daima kila tarehe mosi ya mwezi Januari. Ni sherehe ya amani kwa maana Mama Maria ni Mama wa amani. Amemzaa Mkombozi mfalme wa amani na hivi Mama Kanisa anaona ni vema tukasali tukimwomba Mungu kwa njia ya Mama huyu kwa ajili ya amani ya ulimwengu. Sherehe hii ya kuombea amani duniani iliwekwa rasmi na Papa Paulo VI kunako mwaka 1968. Kwa namna ya pekee kabisa, Kanisa linaadhimisha Sherehe hii katika Mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya huruma ya Mungu. Kanisa linamkumbuka Bikira Maria kama Tabernakulo ya kwanza ya huruma na upendo wa Mungu na Sanduku la Agano kati ya Mungu na binadamu.

Salaam Mama Mtakatifu wa Mungu uliyemzaa mfalme mwenye kutawala mbingu na dunia daima na milele. Hii ndiyo salaam yetu kwa Mama mpendelevu Mama asiye na doa, katika sherehe hii tukufu tunapofungua mwaka mpya.

Zawadi ya Noeli kwa Mwaka 2015: Huruma, amani, furaha na mapendo!


Bikira Maria ni sanduku la: Agano jipya, huruma, msamaha na mapendo ya Mungu!

NA PASKAL LINDA



Kadiri ya mila za Waafrika mgeni akutembeleapo hubeba zawadi. Kwa kawaida zawadi hiyo inakuwa chakula kama vile unga katika sanduku liitwalo jamanda, linafungwa nguo nzuri na kubebwa kichwani na mwanamke, kisha mgongoni hubeba kuku kama mtoto mchanga. Afikapo ugenini, mama mwenye nyumba huzipokea zawadi kwa furaha na kumkaribisha mgeni nyumbani. Noel ni kipindi cha kutembeleana, kupeana zawadi na kufurahiana.
Mama Maria baada ya kuambiwa na Malaika Gabrieli kuwa ana baraka, (mja mzito), akaondoka mara moja kwenda kumtembelea ndugu yake Elizabeti aliyekuwa na baraka ya Yohane mbatizaji. Ndivyo tunavyosali katika fumbo la pili la rozari ya furaha: “Uliyekuchukua ulipokwenda kumtazama Elizabeth.” Aliwasili huko, Maria akamwamkia Elizabeth na kuendelea na mazungumzo. Lakini mazungumzo ya akina mama hawa ni tofauti. Hawa wanaongea lugha ya utaalamu wa hali ya juu wakinukuu Agano la kale kama vile unasikiliza mhadhala wa Wataalamu wa Biblia. Kwa hiyo, ili kuupata ujumbe wa mazungumzo ya akina mama wa leo, yakubidi ukae mkao wa nidhamu na kuwasikiliza kwa nidhamu, vinginevyo utatoka kapa.

Huduma kwa waathirika wa dawa za kulevya ijikite katika kukinga na kuponya!


Matumizi haramu ya dawa za kulevya ni janga kwa vijana wengi wa kizazi kipya! Jumuiya ijitahidi kuwa na mikakati ya kuzuia na kuwaganga waliotumbukia huko! -

Kardinali Pietro Parolin, kama sehemu ya maadhimisho ya Mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya huruma ya Mungu, Jumanne, tarehe 22 Desemba 2015 ameadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwa waathirika wa dawa za kulevya pamoja na familia; kundi linalohudumiwa kwenye kituo cha mshikamano cha Don Mario Picchi, kilichoko mjini Roma. Katika mahubiri yake, Kardinali Parolin amekazia umuhimu wa kuzuia na kuwapatia tiba wale walioathirika kutokana na matumizi haramu ya dawa za kulevya; watu ambao idadi yao inazidi kuongezeka maradufu kutokana na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii.

Nani wafisadi zaidi Afrika?


Na Paskal Linda

Ni mara ya kwanza wafanyibiashara wametajwa kuwa mafisadi wakubwa Barani. Shirika hili limeongeza kwamba utumizi mbaya wa mamlaka unasababisha ongezeko la umasikini, na kuwanyima raia mahitaji muhimu.
Watu wengi ambao ni masikini wamejipata mara kadhaa wakilazimika kulipa hongo ikilinganishwa na matajiri, inasema "Transparency International".
Nchi ya Liberia imetajwa kama inayoongoza kwa visa vya ufisadi Afrika. Inafuatwa na Cameroon, Nigeria na Sierra leone.Afrika mashariki Uganda inaongoza kwa visa vya ufisadi, ikifuatwa na Kenya. Kusini mwa Afrika Zimbabwe na Zambia zinaongoza katika nchi zenye visa vingi vya ufisadi.
Botswana, Mauritius na Cape Verde, ndiyo mataifa pekee ya Afrika ambapo visa vya ufisadi ni vya chini zaidi ikiwa ni asili mia mbili pekee.
Wafanyibiashara wakubwa wametakwa kuwa miongoni mwa watu wafisadi zaidi sawa na maafisa wa polisi Barani Afrika. Hii ni kwa mujibu ya kura ya maoni iliyofanywa na shirika la kuchunguza ufisadi duniani "Transparency International".
Wafanyibiashara wakubwa wametakwa kuwa miongoni mwa watu wafisadi zaidi sawa na maafisa wa polisi Barani Afrika. Hii ni kwa mujibu ya kura ya maoni iliyofanywa na shirika la kuchunguza ufisadi duniani "Transparency International".
Ni mara ya kwanza wafanyibiashara wametajwa kuwa mafisadi wakubwa Barani. Shirika hili limeongeza kwamba utumizi mbaya wa mamlaka unasababisha ongezeko la umasikini, na kuwanyima raia mahitaji muhimu.
Watu wengi ambao ni masikini wamejipata mara kadhaa wakilazimika kulipa hongo ikilinganishwa na matajiri, inasema "Transparency International".
Image caption Raia wengi wa Kenya wamelalamikia visa vya ufisadi serikalini
Nchi ya Liberia imetajwa kama inayoongoza kwa visa vya ufisadi Afrika. Inafuatwa na Cameroon, Nigeria na Sierra leone.
Afrika mashariki Uganda inaongoza kwa visa vya ufisadi, ikifuatwa na Kenya. Kusini mwa Afrika Zimbabwe na Zambia zinaongoza katika nchi zenye visa vingi vya ufisadi.
Botswana, Mauritius na Cape Verde, ndiyo mataifa pekee ya Afrika ambapo visa vya ufisadi ni vya chini zaidi ikiwa ni asili mia mbili pekee.

St. Bibiana

Short Cuts
Image of St. Bibiana

Facts

Feastday: December 2

St. Bibiana, Virgin and Martyr (Feast day - December 2nd) Other than the name, nothing is known for certain about this saint. However, we have the following account from a later tradition.
In the year 363, Julian the Apostate made Apronianus Governor of Rome. St. Bibiana suffered in the persecution started by him. She was the daughter of Christians, Flavian, a Roman knight, and Dafrosa, his wife. Flavian was tortured and sent into exile, where he died of his wounds. Dafrosa was beheaded, and their two daughters, Bibiana and Demetria, were stripped of their possessions and left to suffer poverty. However, they remained in their house, spending their time in fasting and prayer.
Apronianus, seeing that hunger and want had no effect upon them, summoned them. Demetria, after confessing her Faith, fell dead at the feet of the tyrant. St. Bibiana was reserved for greater sufferings. She was placed in the hands of a wicked woman called Rufina, who in vain endeavored to seduce her. She used blows as well as persuasion, but the Christian virgin remained faithful.
Enraged at the constancy of this saintly virgin, Apronianus ordered her to be tied to a pillar and beaten with scourges, laden with lead plummets, until she expired. The saint endured the torments with joy, and died under the blows inflicted by the hands of the executioner.

Papa: Hata katika umaskini wao, Waafrika daima ni watu wa furaha! Wamenikuna!

Hata katika umaskini wao, waafrika bado ni watu wenye furaha! - OSS_ROM

Baba Mtakatifu Francisko amerejea mjini Vatican baada ya kuhitimisha hija yake ya kitume Barani Afrika alikotembelea Kenya, Uganda na Jamhuri ya Watu wa Afrika ya Kati kuanzia tarehe 25 hadi 30 Novemba 2015. Huko amepata nafasi ya kujionea na kusikiliza kilio cha Familia ya Mungu kuhusiana na umaskini, ukosefu wa haki msingi na mahitaji muhimu ya binadamu. Ameguswa na kilio cha vijana wanaotaka saratani ya rushwa na vitendo vya kigaidi, uharibifu wa mazingira ipewe tiba muafaka; mambo yote haya yanahatarisha utu na heshima ya binadamu.
Baba Mtakatifu akiwa njiani amepata fursa ya kujibu baadhi ya maswali yaliyoulizwa na waandishi wa habari waliokuwa kwenye msafara wake. Anasema, pale ambapo sera za uchumi na maendeleo zinajikita katika ubinafsi, utajiri na mali, hapo utu na heshima ya binadamu viko rehani. Inasikitisha kuona kwamba, kuna watu wachache sana wanaomiliki utajiri wa dunia wakati ambapo kuna kundi kubwa la watu bado linaendelea kuogelea katika dimbwi la umaskini na magonjwa.
Baba Mtakatifu anasema, amesikitishwa sana na mahangaiko ya wananchi  wa kitongoji cha Kangemi, Kenya; ameguswa na mateso ya watoto waliolazwa kwenye Hospitali ya Watoto Bangui. Amejionea jinsi watoto wanavyoteseka kutokana na utapiamlo mkubwa, kwa kukosa dawa na vifaa tiba. Yote haya ni kwa sababu watu wanapenda kuabudu fedha na mali kuliko utu na heshima ya binadamu. Magonjwa, umaskini na maafa yataendelea kuwaandama wanadamu ikiwa kama binadamu mwenyewe hataweza kufanya toba na kumwongokea Mungu. Matajiri wawe na ujasiri wa kugawana rasilimali ya dunia na maskini, ili waweze wao pia kufurahia Injili ya maisha!
Baba Mtakatifu anakiri kwamba, ameguswa kwa namna ya pekee na ukarimu, furaha na maisha ya Familia ya Mungu Barani Afrika hata katika umaskini wao, bado wanaweza kufurahia maisha. Wameonesha ukarimu wa ajabu kwa kujitokeza kwa wingi kumpokea na kumsikiliza. Kenya inaonekana kuwa na maendeleo; Uganda bado inajikita katika mashuhuda wa imani; huu ndio utambulisho wao unaowapatia ujasiri wa kushuhudia imani inayomwilishwa katika matendo! Katika Jamhuri ya Watu wa Afrika ya Kati, Baba Mtakatifu anakaza kusema, wao wana kiu ya amani, upatanisho na msamaha wa kweli; udugu, umoja na mshikamano wa kitaifa kwa kutambua kwamba wao ni ndugu wamoja! Waamini wanapaswa kuwa wajenzi wa haki, amani na maridhiano kati ya watu na wala si wachochezi wa kinzani na misigano mambo ambayo yanasigana na imani wanayoiungama. Serikali ya mpito Jamhuri ya Watu wa Afrika ya Kati isaidie kuwapatia wananchi: haki, amani, msamaha na upatanisho wa kitaifa.
Bara la Afrika lina utajiri na raslimali nyingi; lina tunu na tamaduni zinazopaswa kuendelezwa. Kwa bahati mbaya Bara la Afrika linaonekana na wengi kuwa ni uwanja wa fujo pasi na usalama. Baba Mtakatifu anakaza kusema, Bara la Afrika limekuwa kama kichwa cha mwendawazimu, watu wengi wanalinyonya kiasi kwamba limekuwa ni shahidi wa unyonyaji pasi na huruma. Anasema analipenda Bara la Afrika na kwamba, kuna haja ya kushikamana ili kuliendeleza Bara la Afrika badala ya kuendelea kunyanyaswa na wenye nguvu wachache duniani!
Baba Mtakatifu anawataka waandishi wa habari kutekeleza dhamana na wajibu wao kwa kuzingatia kanuni, maadili na sheria kwani hakuna uhuru pasi na mipaka hata katika mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi ambao umeenea sehemu mbali mbali  za dunia hata mjini Vatican. Vyombo vya habari viwe na ujasiri wa kufunua maovu na vyombo vya sheria vitekeleze wajibu wake barabara.Waandishi wa habari waseme ukweli pasi na kuuvuruga kwa ajili ya mafao yao binafsi; waoneshe weledi katika kazi zao kwa kujikita katika ukweli pamoja na kuheshimu sifa ya mtu! Waandishi wa habari wawe na ujasiri wa kuomba msamaha pale wanapokosea na kukiuka kanuni maadili za kazi. 
Katika mapambano dhidi ya vitendo vya kigaidi na misimamo mikali ya kidini, viongozi wa kidini wanapaswa kutekeleza dhamana na wito wao kwa kutambua kwamba, wao ni vyombo na wajenzi wa: umoja, haki, amani,upatanisho na maridhiano. Misimamo mikali ya kidini ni saratani ambayo iko katika dini zote na inakwenda kinyume kabisa cha mafundisho msingi ya kidini. Hapa kuna watu wanatumia misimamo mikali ya kidini kwa ajili ya mafao ya binafsi, ili kujipatia fedha na utajiri wa haraka haraka.
Baba Mtakatifu Francisko anakiri kwamba, kumekuwepo na tatizo la kumshirikisha Monsinyo Vallejo Balda pamoja na Francesca Immaculata Chaouqui katika Tume ya Marekebisho ya masuala ya uchumi na fedha Vatican, ingawa baada ya kumaliza kazi zao waliondoka na kwamba, watuhumiwa hawa hawakumnyima usingizi hata kidogo kwani kile kilichochapishwa kwenye vitabu kinaonesha kazi ya mageuzi iliyofanywa. Rushwa anakaza kusema Baba Mtakatifu ni adui wa haki. Mapambano dhidi ya rushwa mjini Vatican ni mchakato ulioanzishwa na Kardinali Joseph Ratzinger wakati alipotoa tafakari ya Njia ya Msalaba, siku chache kabla ya kifo cha Papa Yohane Paulo II, akachaguliwa na Makardinali kuwa Khalifa wa Mtakatifu Petro ili kuendeleza mchakato wa mageuzi.
Kumbe, wizi wa nyaraka za siri kutoka Vatican ni tendo la jinai na kwamba, Baba Mtakatifu angependa kesi hii iwe imekamilika na kutolewa hukumu kabla ya kuanza maadhimisho ya Mwaka Mtakatifu wa Jubilei kuu ya huruma ya Mungu, hapo tarehe 8 Desemba 2015, pengine jambo hili halitawezekana anasikitika kusema Baba Mtakatifu Francisko na kwamba kwa kushirikiana na Makardinali wataendelea kufanya mageuzi kadiri ya maelekezo yaliyotolewa na Makardinali katika mikutano yao kabla ya uchaguzi wa Khalifa wa Mtakatifu Petro kunako mwaka 2013.
Kuhusu Ugonjwa wa Ukimwi ambao bado unaendelea kusababisha vifo vingi miongoni mwa vijana wa kizazi kipya, Baba Mtakatifu anakaza kusema, Kanisa litaendelea kuhimiza kanuni maadili na utu wema; kwa kusimama kidete kutangaza na kushuhudia Injili ya uhai dhidi ya utamaduni wa kifo. Matumizi ya kondomu si dawa ya kuzuia matatizo na majanga yanayoliandama Bara la Afrika. Kuna ukosefu wa haki msingi za binadamu; uharibifu mkubwa wa mazingira; baa la njaa na utapiamlo; ukosefu wa maji safi na salama; bado kuna biashara kubwa ya silaha, unyonyaji na udhalilishaji wa binadamu; watu hawana makazi bora na salama. Matatizo na changamoto hizi zikipewa ufumbuzi muafaka hata Ukimwi utatoweka.
Baba Mtakatifu anasema aliwaahidia Mapatriaki wa Armenia kushiriki katika maadhimisho ya Jubilei ya miaka 101 ya mauaji ya kimbari yaliyotokea nchini Armenia. Lakini ikumbukwe kwamba, vita ni kiwanda kinachozalisha silaha na utajiri kwa watu wachache, hata katika nchi zile ambazo uchumi wake unachechemea, bado utakuta wananunua silaha za mapambano! Vita ni dhambi dhidi ya ubinadamu na madhara yake ni makubwa licha ya vifo na maafa; vita inasababisha pia biashara haramu ya binadamu, udhalilishaji wa utu na heshima ya binadamu bila kusahau unyonyaji. Kuna haja kwa Jumuiya ya Kimataifa kusimama kidete ili kuhakikisha kwamba, vita inasitishwa ili amani iweze kutawala katika akili na mioyo ya watu. Mwenyezi Mungu ndiye asili ya amani changamoto kwa watu wote kuwa ni vyombo na wajenzi wa amani.
Baba Mtakatifu Francisko akizungumzia kuhusu mazingira anakaza kusema, viongozi wa Jumuiya ya Kimataifa wanaoshiriki katiki katika mkutano wa athari za mabadiliko ya tabianchi, Cop21 huko Paris, Ufaransa wanao wajibu mkubwa kuhakikisha kwamba kunakuwepo na udhibiti wa athari za mabadiliko ya tabianchi vinginevyo, dunia itaendelea kushuhudia maafa makubwa kwa watu na mali zao. Baba Mtakatifu anasema, ana imani na matumaini kwa viongozi wa Jumuiya ya Kimataifa kwamba, wataweza kutoa majibu muafaka kuhusiana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
Dini ya Kiislam ina tunu msingi za maisha ya kiroho zinazoweza kutumika katika mchakato wa majadiliano ya kidini katika ujenzi wa udugu na urafiki; maisha ya kiroho yanayojika katika mambo msingi badala ya kushabikia misimamo mikali ya kidini ambayo inapatikana katika dini zote. Hii ni changamoto kwa waamini kutubu, kuongoka na kuomba msamaha, ili dunia iweze kuwa ni mahali pazuri zaidi pa kuishi.
Baba Mtakatifu anasema katika umri wake, safari ndefu ni taabu na shida anatarajia kwenda nchini Mexico ili kutoa heshima yake kwa Bikira Maria pamoja na kutembelea baadhi ya maeneo ambayo hayajawahi kutembelewa na Mapapa. Kunako mwaka 2017 tayari amekwisha kupata mwaliko wa kutembelea baadhi ya nchi za Amerika ya Kusini. Mwishoni, Baba Mtakatifu amewashukuru waandishi wa habari wote waliokuwa kwenye msafara wake Barani Afrika kwa kazi kubwa waliyoifanya ili kuwahabarisha watu. Amewashukuru kwa maswali yao na kwamba, ameyajibu kadiri anavyofahamu pale ambapo haja jibu amewaambia wazi wazi na wala si sehemu ya utamaduni wake kuficha mambo!

Hija ya Baba Mtakatifu Francisko Barani Afrika inaendelea kama ilivyopangwa!

Kardinali Pietro Parolin Katibu mkuu wa Vatican katika mahojiano maalum na Gazeti la Avvenire linalomilikiwa na Baraza la Maaskofu Katoliki Italia anasema, Jumuiya ya Kimataifa pamoja na wapenda amani wote wameshtushwa na mashambulizi ya kigaidi yaliyojitokeza nchini Ufaransa na kusababisha maafa makubwa kwa watu na mali zao. Hakuna mtu au taifa ambalo linaweza kujihakikishia usalama wake kwa asilimia mia moja, jambo la msingi ni watu kuwa waangalifu zaidi na kamwe wasimezwe na woga na hofu zisizo na mvuto wala mashiko!
Ziara ya Baba Mtakatifu Francisko Barani Afrika kuanzia tarehe 25- 30 Novemba 2015 kwa kutembelea Kenya, Uganda na Jamhuri ya Watu wa Afrika ya Kati inatarajiwa kutekelezwa kama ilivyopangwa na kwamba, kwa sasa hakuna mabadiliko yoyote. Kuna changamoto ya ulinzi na usalama Afrika ya Kati, lakini Baba Mtakatifu ameipatia kipaumbele cha kwanza kwani anataka kuwaimarisha ndugu zake katika imani, mapendo na matumaini, tayari kujikita katika majadiliano na ujenzi wa madaraja ya watu kukutana na kusaidiana.
Kuhusu hali ya ulinzi na usalama mjini Vatican anasema, wasi wasi na hofu ipo, lakini mambo haya yanapaswa kukabiliwa kwa ujasiri pasi na kukata wala kukatishwa tamaa, jambo ambalo linaendelea kuoneshwa na Ufaransa pamoja na mataifa mengine. Lengo la magaidi ni kupandikiza mbegu ya hofu na wasi wasi miongoni mwa watu. Jumuiya ya Kimataifa inapaswa kuwa na ujasiri na mbinu mpya za kupambana na vitendo vya kigaidi.
Kardinali Pietro Parolin anasema, safari ya kikazi iliyokuwa imepangwa na Rais Hassan Rohan wa Iran ili kutembelea Vatican ilifutwa kutokana na sababu za ulinzi na usalama na kwamba, malango ya Vatican yako wazi, anaweza kuja Vatican wakati atakapoona kwamba, inafaa zaidi. Vatican inapenda kuonesha mshikamano na majadiliano na nchi ya Iran kwa ajili ya mafao ya wengi.
Jumuiya ya Kimataifa anasema Kardinali Parolin inaweza kupambana na vitendo vya kigaidi kwa kushirikiana kwa dhati na kwamba, kila serikali inawajibu wa kulinda amani na usalama wa raia wake sanjari na kuhakikisha kwamba, inatumia njia muafaka ili kutekeleza lengo hili msingi na muhimu katika mchakato wa maendeleo na ustawi wa jamii. Kuna haja ya kuendeleza mchakato wa majadiliano kati ya watu, ili kukuza na kudumisha misingi ya haki, amani na maridhiano; mambo ambayo yanaweza kuchukua muda mrefu kutekelezwa, lakini hatima yake ni amani, utulivu na upatanisho.
Ni wajibu wa Jumuiya ya Kimataifa kufikia maamuzi msingi katika mapambano dhidi ya vitendo vya kigaidi, kwa kuzingatia sheria za kimataifa, haki msingi za binadamu kwa kuendelea kushirikiana pamoja na kudumisha majadiliano kati ya watu, ili kweli maamuzi yanayofikiwa yaweze kutekelezwa na watu wengi zaidi. Viongozi wa kidini wanayo dhamana mahususi katika kusaidia majiundo ya dhamiri za watu ili kusimama kidete kulinda, kutetea na kushuhudia haki, amani na maridhiano ya kweli.
Kardinali Parolin anakaza kusema, maadhimisho ya Mwaka Mtakatifu wa Jubilei kuu ya huruma ya Mungu yaliyotangazwa na Baba Mtakatifu Francisko yatazinduliwa rasmi hapo tarehe 8 Desemba 2015 yataendelea kama yalivyopangwa na wala hakuna sababu ya msingi ya kutaka kufuta wala kuhailishwa kwa maadhimisho haya. Hiki ni kipindi cha kuendelea kuhimiza umuhimu wa majadiliano, haki, amani na upatanisho. Maadhimisho ya Jubilei ya huruma ya Mungu iwe ni fursa ya kujikita katika majadiliano ya kidini kama anavyokazia Baba Mtakatifu Francisko katika Waraka wake wa kichungaji juu ya maadhimisho ya Mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya huruma ya Mungu, “Misericordiae vultus” Uso wa huruma.
Mwaka Mtakatifu iwe ni fursa muhimu ya kuwaunganisha waamini wa dini mbali mbali ili kwa pamoja waweze kuondokana na nyanyaso, ubaguzi na vurugu zinazosababishwa na waamini wenye misimamo mikali ya kidini. Dini zote hizi zinaonesha utajiri mkubwa katika dhana ya huruma ya Mungu kwa mwanadamu, katika maadhimisho ya Mwaka Mtakatifu wa Jubilei yahuruma ya Mungu waamini wa dini hizi wanaweza kukutana kama sehemu ya majadiliano ya kidini!
Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S.

Spika Job Ndugai alivyopokea bahasha yenye jina la Waziri Mkuu mpya

Kenya na Afrika kwa ujumla wajiandaa kumpokea Papa Francisko




 Baraza la Maaskofu Katoliki Kenya kwa kushirikiana na Serikali linaendelea kuwahamasisha wananchi wa Kenya na Afrika kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kumpokea na kusali pamoja na Baba Mtakatifu Francisko wakati wa hija yake nchini Kenya kuanzia tarehe 25 hadi tarehe 27 Novemba 2015.

Vatican na Zambia waadhimisha Jubilei ya miaka 50 ya mahusiano ya kidiplomasia


Zambia na Vatican zinaadhimisha Jubilei ya miaka 50 ya uhusiano wa kidiplomasia. - ANSA
17/11/2015 08:19
Askofu mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu mkuu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican kuanzia tarehe 7 hadi tarehe 12 Novemba 2015 amekuwa na ziara ya kikazi nchini Zambia kama sehemu ya maadhimisho ya Jubilei ya miaka 50 ya Uhuru wa Zambia sanjari na Miaka 50 ya uhusiano wa Kidiplomasia kati ya Vatican na Zambia. Mahusiano haya yalianzishwa na Mwenyeheri Paulo VI kunako tarehe 27 Oktoba 1965 katika Waraka wake wa kitume “Africae gentes”.
Akiwa nchini Zambia, Askofu mkuu Gallagher amepata nafasi ya kukutana na kuzungumza na viongozi wa Kanisa, Serikali ya Zambia chini ya uongozi wa Rais Edgar Chagwa Lungu pamoja na Mabalozi na wawakilishi wa Jumuiya ya Kimataifa nchini Zambia. Askofu mkuu Gallagher amebahatika kuadhimisha Ibada ya Misa Takatifu katika Makanisa kadhaa kwa kukazia umuhimu wa Zambia kuendelea kuwa ni udongo mzuri kwa ajili ya kupandikiza Habari Njema ya Wokovu. Akiadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwa Majandokasisi wa Seminari kuu ya Mtakatifu Dominiko, Askofu mkuu Gallagher amewataka Waseminari hao kufanya tafakari ya kina kuhusu maisha na wito wao, daima wakilenga juu zaidi kwa kuonesha upendo na uaminifu.
Akizungumza na Rais Edgar Chagwa Lungu, wakati wa kumbu kumbu ya Jubilei ya Miaka 50 ya mahusiano ya kidiplomasia kati ya Zambia na Vatican, Askofu mkuu Galagher amepongeza mahusiano mazuri ya kidiplomasia kati ya Vatican na Zambia pamoja na mchango mkubwa unaotolewa na Kanisa katika ustawi na maendeleo ya wananchi wote wa Zambia. Kanisa kwa namna ya pekee, limekuwa mstari wa mbele katika huduma kwa maskini na wote wanaosukumizwa pembezoni  mwa jamii. Mahusiano ya kidiplomasia kati ya nchi hizi mbili yanalenga kwa namna ya pekee kudumisha na kuimarisha huduma kwa familia ya binadamu, kwa kujikita katika mchakato wa maendeleo endelevu, haki na amani. Serikali ya Zambia kwa namna ya pekee, inalipongeza Kanisa Katoliki kwa  mchango wake katika maendeleo ya wananchi wengi wa Zambia, lakini zaidi katika sekta ya elimu na afya.
Askofu mkuu Gallagher, amepata pia nafasi ya kutembelea nchini Malawi, huku akiongozana na Askofu mkuu Julio Murat, Balozi wa Vatican nchini Zambia na Malawi, ambako amepokelewa na viongozi wa Kanisa na Serikali ya Malawi. Viongozi hawa katika mazungumzo yao wamegusia kwa namna ya pekee, mambo msingi katika mchakato wa maendeleo endelevu ya wananchi wa Malawi, ambao kwa sasa wanakabiliwa na changamoto nyingi, lakini kwa namna ya pekee baa la njaa na umaskini.
Askofu mkuu Tarcisius Zizaye, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Zambia, amemshukuru kwa namna ya pekee kabisa Baba Mtakatifu Francisko kwa kuijali Familia ya Mungu nchini Malawi katika shida na mahangaiko yake; wakati wa raha na machungu. Kwa upande wake, Askofu mkuu Richard Paul Gallagher amewasilisha salam za Baba Mtakatifu Francisko anaendelea kuonesha moyo wake wa upendo na sala kwa wale wote walioathirika kutokana na mafuriko pamoja na ukame wa kutisha nchini Malawi. Askofu mkuu Gallagher katika Ibada ya Misa Takatifu, akiwa Malawi, amewataka waamini kuwa ni mashuhuda wa mwanga wa Injili ya Kristo, kwa kuonesha mshikamano na huduma kwa maskini na wagonjwa, hasa wale wanaoteseka kutokana na ukimwi. Maaskofu wa Malawi wamemshirikisha Askofu mkuu Gallagher maisha na utume wa Kanisa nchini Malawi pamoja na changamoto wanazoendelea kukabiliana nazo.
Askofu mkuu Gallagher akiwa nchini Malawi amekutana na kuzungumza na Rais Peter Mutharika wa Malawi aliyekuwa ameambatana na viongozi wa Serikali pamoja na Kanisa. Kwa muda wa miaka arobaini na tisa, Malawi imekuwa na uhusiano wa kidiplomasia na Vatican. Katika kipindi cha miaka yote hii, Kanisa limekuwa mdau wa pekee kabisa katika ustawi na maendeleo ya wananchi wa Malawi: kiroho na kimwili. Kanisa limesaidia kudumisha mchakato wa utawala bora na demokrasia nchini Malawi.
Rais Mutharika amelishukuru kwa namna ya pekee kabisa Kanisa Katoliki kwa msaada mkubwa lililotoa kwa wananchi wa Malawi walipokumbwa na mafuriko pamoja na ukame wa kutisha. Askofu mkuu Gallagher ametumia nafasi hii kuwasilisha pia salam na matashi mema kutoka kwa Baba Mtakatifu Francisko kwa wananchi wa Malawi. Kabla ya kuondoka kutoka Malawi, Askofu mkuu Gallagher alipata nafasi ya kuadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwa Watawa wa ndani wa Mtakatifu Clara kwa kuwataka kuwa kweli ni mashuhuda amini wa maisha ya kuwekwa wakfu, kwa kufuata mfano wa karama na moyo wa Mtakatifu Clara wa Assisi. Askofu mkuu Paul Richard Gallagher tayari amerejea mjini Vatican na anaendelea “kudunda mzigo kama kawa”.

Magufuli atua Dodoma na jina la Waziri Mkuu!

RAIS John Magufuli amewasili mkoani Dodoma kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe kuongoza Tanzania akiwa ametumia njia ya barabara huku akiwa na siri moyoni ya nani atakuwa Waziri Mkuu wake. Njia aliyotumia kufika Dodoma imewashangaza wengi kutokana na ukweli kwamba marais waliotangulia wamekuwa wakitumia usafiri wa ndege. Baada ya kuwasili Ikulu Ndogo ya Rais iliyopo Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma akitokea jijini Dar es Salaam, alipokewa na viongozi mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Serikali.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kijiji cha Chamwino Ikulu, Joseph Seganje, wananchi wamefarijika kuona Rais huyo akiishi kwenye Ikulu hiyo kama alivyokuwa ameahidi. “Tayari tumempokea Rais wetu na wananchi wana furaha isiyo na kifani,” alisema Seganje.
Wakizungumza mapema wiki iliyopita, baadhi ya wakazi wa Chamwino Ikulu walisema itakuwa ni faraja kubwa kwa Rais kuishi kijijini hapo. Alice Chidong’oi alisema Dk Magufuli ni kiongozi anayeonesha nia ya dhati ya kuwatumikia watu wake kwa kujali zaidi wanyonge kama ilivyokuwa kwa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.
“Tunaamini akiishi hapa atakuwa sehemu ya jamii ya Wana Chamwino na hilo litasaidia hata kuboreshwa kwa huduma za jamii ikiwemo maji,” alisema Chidong’oi. Alisema hiyo itakuwa fursa nzuri kwa wakazi wa eneo hilo kufanya biashara, kwani uwepo wake ndani ya wilaya hiyo utaongeza idadi ya wageni.
Mkazi mwingine, Stanley Richard, alisema vijana wa Chamwino wanapenda kazi na Dk Magufuli akiwa hapo itakuwa ni kazi tu. “Ni mtu ambaye anapenda kazi na sisi vijana tunapenda kufanya kazi, tutampa ushirikiano mkubwa katika kipindi chote atakachokuwa madarakani,” alisema.
Alisema alifurahi alipochaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwani alijua nchi imepata kiongozi ambaye yuko tayari kuwaletea wananchi wake mabadiliko. Tayari Serikali mkoani hapa imepiga marufuku kufanyika kwa mikutano ya hadhara na maandamano wakati wa vikao vya Bunge vikiendelea.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Chiku Galawa, alisema amri hiyo ya kuzuia mikutano ya hadhara na maandamano ya vyama vya siasa bado inaendelea ili kuweka utulivu muda wote wa vikao vya Bunge.
Kwa mujibu wa ratiba ya vikao vya Bunge, kesho Alhamisi, Bunge litapokea na kuthibitisha kwa kupiga kura jina la Waziri Mkuu wa 11 wa Tanzania ambalo Dk Magufuli atakuwa ameliwasilisha kwa Spika Job Ndugai.
Kwa hiyo, Dk Magufuli atakuwa ametua mjini hapa akiwa na siri yake moyoni ya nani atakuwa Waziri Mkuu wake kwa miaka ya mwanzo ya utawala wake inayokoma mwaka 2020.
Mbali ya kutoa jina la Waziri Mkuu, Dk Magufuli anatarajia kulihutubia Bunge, Ijumaa alasiri baada ya kuwa amemwapisha Waziri Mkuu asubuhi. Hotuba yake itakuwa dira ya utawala wake kwa miaka mitano ijayo.

Batarokota live na Bahari FM!

Pichani juu msanii wa nyimbo za asili ya Kitanzania Batarokota akiwa katika Hoteli ya Misana aliyofikia jijini Mwanza..

 MSANII wa nyimbo za asili ya Kitanzania Batarokota siku ya jumatatu ijayo saa 11:30 jioni anatarajia kuongea kwa njia ya simu live kutoka Mwanza katika kipindi cha Africa Sana kinachorushwa na radio Bahari FM kutoka Zanzibari. Msanii Batarokota atakuwa na maojiano na mwandishi wa Bahari FM Joan Donisya Thimas maharufu saut ya Black Sugar ndani ya mawimbi ya 97.3 Bahari FM. Jumatatu hiyo Batarokota ataongea moja kwa moja kutoka Jijini Mwanza aliko kwa sasa kwa maandalizi ya sikuu za mwishoni mwa mwaka 2015 kaa mkao wa kula kupata habari za Batarokota na ujio wa mwaka 2016.

Pambano Taifa Stars, Algeria kesho gumzo

PAMBANO la kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia nchini Urusi mwaka 2018 kati ya timu ya soka ya Tanzania `Taifa Stars’ dhidi ya Algeria, linalotarajiwa kupigwa kesho Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, limekuwa gumzo miongoni mwa mashabiki wa soka ndani na nje ya nchi. Aidha, idadi kubwa ya mashabiki katika `vijiwe’ vya soka, wameonesha dhamira ya dhati ya kutaka kuiunga mkono Stars. Ujio wa Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wa Stars wanaochezea klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na pia taarifa za Rais, Dk John Magufuli kuwa atajitokeza kuishangilia timu ya taifa ya Tanzania `Mwanzo Mwisho’, kwa pamoja vimechangia kuongeza hamasa ya mchezo huo.
Samatta na Ulimwengu wametoka kuweka historia ya kuwa wa wanasoka wa kwanza wa Tanzania kutwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya klabu yao kufanya hivyo mwishoni mwa wiki, huku Samatta akiongeza taji jingine la ufungaji bora.
Aidha, kwa Magufuli, hilo litakuwa pambano lake la kwanza kushuhudia akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tangu alipoapishwa kuchukua nafasi ya Rais Jakaya Kikwete, mwanamichezo aliyeondoka madarakani baada ya kumaliza muda wake wa uongozi kwa mujibu wa Katiba ya nchi.
Tayari waamuzi wa mchezo huo kutoka nchini Mali, Keita Mahamadou, Diarra Bala, Niare Drissa Kamory na mwamuzi wa akiba Coulibaly Harouna wameshawasili nchini tangu jana asubuhi, huku mtathimini wa waamuzi Attama Ibrahim Boureima kutoka nchini Niger naye akiwa tayari nchini tangu juzi usiku.

Daily Reading for Sunday, November 8th, 2015

Reading 1, First Kings 17:10-16 10 So he went off to Sidon. And when he reached the city gate, there was a widow gathering sticks. Addressing her he said, 'Please bring a little water in a pitcher for me to drink.'
11 She was on her way to fetch it when he called after her. 'Please', he said, 'bring me a scrap of bread in your hand.'
12 'As Yahweh your God lives,' she replied, 'I have no baked bread, but only a handful of meal in a jar and a little oil in a jug; I am just gathering a stick or two to go and prepare this for myself and my son to eat, and then we shall die.'
13 But Elijah said to her, 'Do not be afraid, go and do as you have said; but first make a little scone of it for me and bring it to me, and then make some for yourself and for your son.
14 For Yahweh, God of Israel, says this: Jar of meal shall not be spent, jug of oil shall not be emptied, before the day when Yahweh sends rain on the face of the earth.'
15 The woman went and did as Elijah told her and they ate the food, she, himself and her son.
16 The jar of meal was not spent nor the jug of oil emptied, just as Yahweh had foretold through Elijah.

Responsorial Psalm, Psalms 146:7, 8-9, 9-10

7 gives justice to the oppressed, gives food to the hungry; Yahweh sets prisoners free.
8 Yahweh gives sight to the blind, lifts up those who are bowed down.
9 Yahweh protects the stranger, he sustains the orphan and the widow. Yahweh loves the upright,but he frustrates the wicked.
10 Yahweh reigns for ever, your God, Zion, from age to age.

Gospel, Mark 12:38-44

38 In his teaching he said, 'Beware of the scribes who like to walk about in long robes, to be greeted respectfully in the market squares,
39 to take the front seats in the synagogues and the places of honour at banquets;
40 these are the men who devour the property of widows and for show offer long prayers. The more severe will be the sentence they receive.'
41 He sat down opposite the treasury and watched the people putting money into the treasury, and many of the rich put in a great deal.
42 A poor widow came and put in two small coins, the equivalent of a penny.
43 Then he called his disciples and said to them, 'In truth I tell you, this poor widow has put more in than all who have contributed to the treasury;
44 for they have all put in money they could spare, but she in her poverty has put in everything she possessed, all she had to live on.'

Reading 2, Hebrews 9:24-28

24 It is not as though Christ had entered a man-made sanctuary which was merely a model of the real one; he entered heaven itself, so that he now appears in the presence of God on our behalf.
25 And he does not have to offer himself again and again, as the high priest goes into the sanctuary year after year with the blood that is not his own,
26 or else he would have had to suffer over and over again since the world began. As it is, he has made his appearance once and for all, at the end of the last age, to do away with sin by sacrificing himself.
27 Since human beings die only once, after which comes judgement,
28 so Christ too, having offered himself only once to bear the sin of many, will manifest himself a second time, sin being no more, to those who are waiting for him, to bring them salvation.

St. Leonard

Short Cuts
Image of St. Leonard

Facts

Feastday: November 6
Patron of political prisoners, imprisoned people, prisoners of war, and captives, women in labour, as well as horses
Death: 559


According to unreliable sources, he was a Frank courtier who was converted by St. Remigius, refused the offer of a See from his godfather, King Clovis I, and became a monk at Micy. He lived as a hermit at Limoges and was rewarded by the king with all the land he could ride around on a donkey in a day for his prayers, which were believed to have brought the Queen through a difficult delivery safely. He founded Noblac monastery on the land so granted him, and it grew into the town of Saint-Leonard. He remained there evangelizing the surrounding area until his death. He is invoked by women in labor and by prisoners of war because of the legend that Clovis promised to release every captive Leonard visited. His feast day is November 6.

Tafakari ya Neno la Mungu, Jumapili ya 32 ya Kipindi cha Mwaka B wa Kanisa


Tafakari ya Neno la Mungu Jumapili ya 32 ya Mwaka B wa Kanisa. - EPA
 
Mpendwa msikilizaji wa Radio Vatican, ninakuleteeni tafakari Neno la Mungu lililo taa na mwanga wa maisha yetu. Tayari tuko ukingoni mwa mwaka wa Kanisa, ni Dominika ya 32 ya mwaka B wa Kanisa. Mama Kanisa ametuwekea Neno likitualika kujitoa na kujiaminisha katika Bwana bila kujibakiza, tukiwa na matumaini na kwa namna hiyo tutajaliwa yale yote mema yatokayo kwa Mungu. Ujumbe huu tunaupata kwa mifano hai ya wajane wawili wanaokubali mpango wa Mungu na kutoa kile chote walichokuwanacho, kinyume na matajiri. Matokeo ya tendo lao jema wanakirimiwa baraka tele katika maisha yao.
Katika Somo la kwanza tunamwona Nabii Eliya akimkimbia mfalme Ahab ambaye alitaka kumwangamiza. Nabii anapokimbia anakutana na mama mjane ambaye yuko katika taabu ya njaa! Nabii akitambua taabu ya mama huyu lakini pia akiwa na tumaini katika Bwana, anamwomba maji na kipande cha mkate. Mama huyu alikuwa na unga kidogo kiasi cha kutosheleza siku moja kwa ajili yake na mwanaye, na baada ya hapo kadiri ya mjane huyo basi wangekufa! Lakini kwa sababu ya tumaini kuu na akisikiliza sala ya msisitizo ya Nabii Eliya anakubali kutoa kila kitu. Kwa ufadhili huu alioufanya kwa Nabii wa Mungu, mjane huyu anapata chakula cha kutosheleza maisha yake mpaka njaa itakapoisha katika nchi ile.
Mpendwa mwana wa Mungu, ukarimu na tumaini la mjane huyu ndio unaozaa matunda mema. Matunda haya ni baraka na amani itokayo kwa Mungu. Ni alama ya kwamba Mungu huwajali walio maskini ambao wanamkimbilia na kumtumaini daima katika maisha yao. Mungu huwajali wale wote ambao wanakubali kushirikisha vipaji vyao na kugawana mali zao na wengine walio wahitaji. Jaribu kuwa mkarimu kwa Mungu utaona matunda yake!
Ewe ndugu msikilizaji, bado tunaendelea na sehemu ya barua kwa Waebrania ambayo leo yatufundisha kwa msisitizo, tofauti iliyopo kati ya Kuhani mkuu wa kweli yaani Yesu Kristo na makuhani wengine. Yesu Kristu anatolea sadaka yake si katika madhabahu yaliyotengenezwa kwa mawe bali ukuhani wake ni wa madhabahu ya mbinguni ambayo hayakujengwa kwa mikono ya wanadamu. Kuhani Mkuu Yesu Kristo hutolea sadaka mara moja na hutosheleza maisha yote kwa kuondoa dhambi na kutakasa mioyo ya watu, tofauti na sadaka za makuhani wa Agano la Kale ambazo hazikumaliza shughuli ya kuwatakasa watu, kumbe iliwapasa kurudia kila mwaka! Basi mwaliko kwetu ni kumfuasa Bwana kwa kushiriki sadaka ya Misa kwa ajili ya wokovu wetu.
Katika Injili, Mtakatifu Marko akinukuu mafundisho ya Bwana anakazia kujitoa bila kujibakiza kama mama mjane aliyetoa sadaka senti mbili ambazo ilikuwa ndiyo hazina yake! Anatoa yote bila kuogopa kwa maana analo tumaini katika Bwana ambaye ni mgawaji wa mapaji yote. Mjane huyu ni kinyume na watu wengine ambao hutoa ziada na si mali hasa inayotoka katika mioyo yao! Mpendwa yafaa kujitazama moyoni wapi ulipo katika makundi haya mawili! Kama uko katika kundi la mjane basi unayo heri ya milele na uishikilie kwa furaha maana ni zawadi toka kwa Bwana.
Basi mpendwa ndugu unayetafakari nami, jaribu kujikuza katika sala ukiomba fadhila ya ukarimu katika maisha yako. Kula, ishi, cheka na zungumza na wengine kwa furaha daima.

Tumsifu Yesu Kristo. Tafakari hii imeletwa kwako na Pd Richard Tiganya C.PP.S.

'Viongozi wateule shughulikieni vifo vya wazazi, watoto'


Wazazi waliotoka kujifungua wakiwa na watoto wao.

Tatizo la vifo vya wajawazito na watoto wachanga linasababisha majonzi makubwa kwa jamii lakini pia linaleta  ongezeko la watoto waliodumaa, wagonjwa, watoto wa mitaani kupunguza  nguvu kazi ya taifa.
 
Ili taifa lisonge mbele kimaendeleo halina budi kuimarisha huduma za afya kwa wananchi , ili kupunguza vifo vya wajawazito, wazazi na watoto wachanga kwa lengo   la  kuepusha matatizo hayo.
 
Takwimu za Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii za mwaka 2014 zinaonyesha kwamba Tanzania ni nchi ya saba duniani kwa idadi kubwa ya vifo vitokanavyo na uzazi, ikikadiriwa kuwa  wajawazito karibu 7,900  hufa kila mwaka, huku wastani wa watoto wachanga 40,000 wakipoteza maisha kila mwaka kabla ya kutimiza mwezi mmoja baada ya kuzaliwa.
 
Kama vile haitoshi inakadiriwa kwamba watoto 100,000 hufa kila mwaka kabla ya kufikisha umri wa miaka mitano.Kadhalika wengine 50,000 huzaliwa wakiwa wafu kutokana na sababu mbalimbali ambazo iwapo jitihada za makusudi zingechukuliwa mapema, zaidi ya asilimia 45 ya vifo hivyo visingezuiliwa.
 
Pia asilimia 44 ya wasichana wanaofikisha umri wa miaka 19 nchini wanapata ujauzito, haijalishi wapo shuleni au nje ya masomo.
 
Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 asilimia 54 ya Watanzania ni watu walio chini ya miaka 20 na hii inatafsirika kuwa takribani miaka 15 hadi 20 ijayo idadi kubwa ya vijana wataingia katika umri wa uzalishaji mali na kuwa nguzo ya kiuchumi.
 
Kutokana na hali hiyo makala hii inawapa changamoto wateule wa nafasi za urais na ubunge kuweka wazi namna watakavyo lishughulikie tatizo kubwa la vifo vya wajawazito na watoto wachanga.
 
Ukweli ni kwamba viongozi hawa wanakwenda kufunga mkataba kati yao na raia kwa miaka mitano ijayo hivyo kazi yao ni kutafuta ufumbuzi wa kumaliza tatizo hili.
 
Waliochaguliwa wafahamu kuwa afya ya mama ni muhimu kama ilivyo ya mtoto wajue kuwa tangu mwanzo suala hili halijapewa kipaumbele cha kutosha kutokana na kutokuwapo mfumo bora wa kutoa huduma kikamilifu.
 
Ni vyema sasa wabunge na mawaziri watakaounda serikali ya awamu ya tano wakatueleza kwa kina namna gani watakavyosimamia na kuhakikisha uzazi salama wa mpango unavyosimamiwa ili kuhakisha kuwa adha ya kufa wakati wa kujifungua inamalizika ama kuondoka.
 
Aidha viongozi waieleze jamii vipaumbele vyao kwenye afya ya mama na mtoto ikiwa ni pamoja na kuishauri serikali kuona suala hilo kuwa na umuhimu wa kipekee na kulipa kipaumbele zaidi ikilinganishwa na masuala mengine.
 
Tafiti mbalimbali zilizofanywa na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali ya DSW, Marie Stopes Tanzania, Pathfinder International, Chama cha Maelezi Bora (Umati) na HDT zinabainisha kuwa tatizo la uzazi wa mpango ni kubwa.
 
Tafiti za mashirika hayo zinaonyesha kuwa mimba zisizotarajiwa husababisha uwezekano mkubwa wa vifo vya mama na mtoto kwa asilimia tisa ya vifo vinavyotokea nchini.
 
Angalizo linatolewa kuwa kiwango hicho kinaweza kuongezeka zaidi iwapo hatua za makusudi hazitatolewa katika jamii kwa hiyo ni suala ambalo wabunge wanatakiwa kulitizama na kulipa umuhimu wa kipekee.
 
Uzazi wa mpango ni mkakati muhimu wa kuwasaidia wanawake kupanga muda wa kutosha kati ya kizazi kimoja na kingine, kuzuia mimba katika umri mdogo na kuepuka mimba zisizotarajiwa.
 
Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani, (WHO) gharama za kuzuia ujauzito ni za chini zaidi kuliko za matibabu yanapotokea wakati wa kujifungua.
 
Kwa hiyo uzazi wa mpango unazipa familia au mtu binafsi uwezo wa kuchagua ukubwa wa familia ambayo anaimudu, kuwekeza katika elimu na makuzi ya kila mtoto na kubaki na fedha za ziada hatua inayoweza kuchangia kukuza uchumi wa taifa. 
 
Daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake Moke Magoma, anasema kuna uwezekano mkubwa wa Tanzania kupiga hatua za haraka kimaendeleo iwapo jamii itapata uelewa wa kutosha kuhusu uzazi wa mpango.
 
“Ni muhimu sana kuwepo kwa huduma za afya ya mjamzito na mtoto mchanga, ambayo katika uhalisia wake inajidhihirisha kwa kila aliye hai sasa amepatikana kupitia mama yake kuwa mjamzito” anasema Dk. Magoma.
 
“Uzazi wa mpango ni muhumu kwa kuwa wanaweza kudhibiti na kupanga idadi ya watoto, kuendeleza na kutunza familia kitaaluma, lishe na wakati huo wakafanya kazi wanazozitaka na kushiriki katika maamuzi ya kiuchumi na kisiasa”
Daktari Magoma anasema uzazi wa mpango ni njia bora zaidi katika afya ya mama na mtoto na kwamba mbinu za kitaalamu za uzazi wa mpango hazina madhara kama baadhi ya watu wanazovumisha na kuwatia hofu wananchi.
 
Naye Dk. Msiima Mushumba,kutoka shirika la Marie Stopes Tanzania,anasema jamii inapaswa kutambua kuwa kuzaa watoto wengi bila mpangilio ni kuhatarisha maisha ya mama, watoto na kudumaza uchumi wa taifa.
 
Anasema kwa wastani familia inapaswa kuzaa watoto wasiozidi watano na kwamba kuanzia mimba ya sita na kuendelea huitwa mimba hatarishi ambapo anaitaka jamii kufuata njia za uzazi wa mpango.
 
Kadhalika anabainisha kuwa wananchi ambao hawakusoma wanazaa zaidi kuliko waliosoma kwa kuwa wengi wao hutambua umuhimu wa kuzaa kwa mpango kuliko ambao hawakusoma.
 
Dk. Mushumba, anasema jitihada za makusudi zinahitajika kupitia serikali, mashirika yasiyokuwa ya kiserikali na jamii kwa ujumla kuhakikisha huduma za uzazi wa mpango zinawafikia wanawake wote nchini.

Magufuli aduwaza Wizara ya Fedha


RAIS John Magufuli, aliyeanza kazi juzi kwa kumteua Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju, baada ya kumuapisha jana amefanya ziara ya kushtukiza katika ofisi za Wizara ya Fedha, Hazina.
Tofauti na ziara za viongozi wengine wakiwemo mawaziri waliowahi kuongoza ofisi hiyo, ambao huingia katika vyumba vya mikutano au ofisi za viongozi, Dk Magufuli yeye alianza kuingia katika ofisi za watumishi wa kawaida.
Dk Magufuli aligeuka kivutio kwa wananchi, pale alipotoka katika lango kuu la Ikulu Dar es Salaam kwa miguu kwenda wizarani hapo kupitia njia ambayo imekuwa ikitumiwa zaidi na wananchi.
Wizara hiyo mbali na kuwa karibu na Ikulu, lakini imezungukwa na ofisi nyingi, ikiwemo Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na Ofisi Ndogo ya Bunge na mara kwa mara nje kuna kawaida ya kuwa na wananchi na magari mengi yenye madereva wa maofisa wanaofika wizarani hapo na wengine katika ofisi nyingine kwa shughuli mbalimbali.
Baada ya kuingia katika ofisi hizo, Dk Magufuli alianza kufungua milango ya ofisi za watumishi hao na kuwasalimia aliowakuta na kuhoji pale alipokuta meza haina mtendaji.
Katika hatua hiyo, Dk Magufuli alishangazwa kukuta meza sita kati ya nane katika moja ya ofisi hizo, hazina watumishi akalazimika kuuliza majina ya watumishi husika na alipoambiwa walikuwepo, akahoji walikokwenda akajibiwa walikwenda kunywa chai. Huku akionekana kutoridhishwa na majibu hayo, Dk Magufuli alitikisa kichwa huku akisema “wameenda kunywa chai eee!” na kuondoka ofisini hapo kwenda kwenye ofisi za viongozi wa wizara hiyo.
Alipoingia ndani, alifanya kikao cha muda mfupi na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dk Servacius Likwelile pamoja na makamishna wa fedha na alipotoka taarifa za wizara hiyo zilieleza kuwa Dk Magufuli ameagiza watumishi wa Wizara hiyo inayosimamia Mamlaka ya Mapato (TRA), kuhakikisha wanaongeza kasi ya ukusanyaji mapato, na akaelekeza hasa kwa wafanyabiashara wakubwa.
Mbinu aliyotumia Dk Magufuli, ni ya kitawala ambapo viongozi husimamia wizara kwa kufanya ziara za ghafla, au kutembelea maeneo ya watumishi bila kutoa taarifa, tena bila kufuata utaratibu wowote. Lengo lake mara nyingi ni kujulia hali ya watumishi na matunda yake ni kuongeza ari ya kufanya kazi, kuhimiza na kusisitiza malengo ya taasisi.
*Kuapishwa kwa Masaju
Awali kabla ya kufanya ziara hiyo, Dk Magufuli alimuapisha Masaju kuendelea kushikilia nafasi hiyo, ambapo Mwanasheria Mkuu huyo aliahidi kuendelea kusimamia kesi mbalimbali dhidi ya Serikali ili kuokoa fedha za umma.
Uapisho huo ulifanyika Ikulu na kuhudhuriwa na watu mbalimbali akiwemo Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, Jaji Mkuu Othman Chande, Spika wa Bunge, Anna Makinda na Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Ernest Mangu.
Masaju alisema ni tumaini lake kuwa wananchi wataendelea kutii sheria za nchi, ili kudumisha amani na mshikamano kama ilivyokuwa wakati wote huku Serikali ikiendelea kuimarisha utii wa sheria.
“Serikali shughuli yake ya msingi ni kusimamia utekelezaji wa sheria na yenyewe ina jukumu la kusimamia amani. Nashauri ushirikiano uliotolewa wakati wa Uchaguzi Mkuu uendelee kudumishwa,” alisema Masaju.
Masaju alisema Serikali inaokoa fedha nyingi za umma kwa kushinda kesi dhidi yake na kwamba inajitahidi kuendesha kesi zake kwa weledi, huku akitoa mfano wa mashauri 34 ya kesi za uchaguzi ya kupinga matokeo zilizofunguliwa mwaka 2010, ambazo Serikali ilizishinda zote.
Alishukuru kupatikana kwa Serikali mpya kwa amani na kwa kuzingatia maelekezo ya sheria na kuomba hali hiyo iendelee ili shughuli mbalimbali ziendelee hasa zile za kujenga uchumi na za kijamii. Alitaka amani ya nchi ipewe kipaumbele na kuonya kuwa ikivurugika hakuna kazi itakayofanyika na kusisitiza amani ndiyo itakayodumisha uchumi wa nchi.

Prayer to St. Dymphna - Perseverance

St. Charles Borromeo

Short Cuts
Image of St. Charles Borromeo

Facts

Feastday: November 4
Patron of learning and the arts.
Death: 1584

Charles was the son of Count Gilbert Borromeo and Margaret Medici, sister of Pope Pius IV. He was born at the family castle of Arona on Lake Maggiore, Italy on October 2. He received the clerical tonsure when he was twelve and was sent to the Benedictine abbey of SS. Gratian and Felinus at Arona for his education.
In 1559 his uncle was elected Pope Pius IV and the following year, named him his Secretary of State and created him a cardinal and administrator of the see of Milan. He served as Pius' legate on numerous diplomatic missions and in 1562, was instrumental in having Pius reconvene the Council of Trent, which had been suspended in 1552. Charles played a leading role in guiding and in fashioning the decrees of the third and last group of sessions. He refused the headship of the Borromeo family on the death of Count Frederick Borromeo, was ordained a priest in 1563, and was consecrated bishop of Milan the same year. Before being allowed to take possession of his see, he oversaw the catechism, missal, and breviary called for by the Council of Trent. When he finally did arrive at Trent (which had been without a resident bishop for eighty years) in 1556, he instituted radical reforms despite great opposition, with such effectiveness that it became a model see. He put into effect, measures to improve the morals and manners of the clergy and laity, raised the effectiveness of the diocesan operation, established seminaries for the education of the clergy, founded a Confraternity of Christian Doctrine for the religious instruction of children and encouraged the Jesuits in his see. He increased the systems to the poor and the needy, was most generous in his help to the English college at Douai, and during his bishopric held eleven diocesan synods and six provincial councils. He founded a society of secular priests, Oblates of St. Ambrose (now Oblates of St. Charles) in 1578, and was active in preaching, resisting the inroads of protestantism, and bringing back lapsed Catholics to the Church. He encountered opposition from many sources in his efforts to reform people and institutions.
He died at Milan on the night of November 3-4, and was canonized in 1610. He was one of the towering figures of the Catholic Reformation, a patron of learning and the arts, and though he achieved a position of great power, he used it with humility, personal sanctity, and unselfishness to reform the Church, of the evils and abuses so prevalent among the clergy and the nobles of the times. His feast day is November 4th.

Siku ya kuwaombea Marehemu wote!


Na Paskal Linda 

Ninakualika katika tafakari yetu tukiwakumbuka marehemu wote. Kila mwaka tarehe 2 Novemba na zaidi sana mwezi Novemba ni siku na wakati ambao Mama Kanisa anatualika kwa ajili ya kuwaombea marehemu walioko toharani. Kwa kawaida siku zote mama Kanisa anasali kwa ajili ya marehemu mmoja mmoja au kikundi lakini leo anasali kwa ajili ya Kanisa zima la wateswa lililoko toharani. Huo ndio utajiri wa Kanisa linapogawa mastahili ya Msalaba wa Kristu kwa wahitaji walioko safarini kuelekea mbinguni.

Picha juu ni Mwandishi wa habari Paskal Linda wa www.batarokota.blogspot.com

Siku ya Marehemu wote!

Mwanafalsafa John Mbiti alisema “Niko kwa sababu tuko na kwa vile tuko, kwa hiyo niko ” Sentesi hii yanitafakarisha na kunisaidia kuhisi uwapo wa mwingine pembeni mwangu aliye mhitaji na hivi yaonesha hitaji la jumuiya. Katika siku ya leo Kanisa lahisi uwapo wa wahitaji ndio marehemu wote, ndio waliolala toharani wakitakaswa ili waingie mbinguni. Kanisa lahisi na kutekeleza ule muunganiko uliopo kati ya marehemu (kanisa la wateswa), watakatifu wa mbinguni (kanisa la washindi) na kanisa la wapiganaji ndio sisi na hivi kwa pamoja ni kanisa moja familia ya Mungu.
Fundisho tulilolisikia juu ya muunganiko wa kanisa shindi, kanisa la wateswa na kanisa la mahujaji linawekwa mbele yetu na Papa Paulo VI akisema “sisi twasadiki ushirika wa waamini wote wa Kristo, wa wale walio bado safarini duniani, wa wale waliokufa ambao wanapata utakaso, wa wale wenye heri ya mbingu, wote pamoja hufanya Kanisa moja tu. Nasi twasadiki kwamba katika umoja huu, mapendo ya huruma ya Mungu na ya watakatifu wake yasikiliza daima sala zetu” (KKK 962) Ndiyo kusema kuwaombea marehemu ni sehemu ya imani yetu, ni upendo kwa jirani tukiitikia injili ya Bwana ya kumsaidia aliye katika taabu, aliyemhitaji.
Kuwaombea marehemu ni kielelezo kimojawapo cha imani yetu katika ufufuko, kwa maana kama hatusadiki yakuwa Kristu alikufa na kufufuka imani yetu ni bure. Ni kutokana na msingi huo twaamini kwamba wale waliolala usingizi katika Yesu Kristo mfufuka, parapanda ya Mungu ikilia watafufuliwa kwanza nasi tuliosalia tutanyakuliwa kwa kuwafuata wao.
Kuwaombea marehemu ni jambo la thamani na la imani ambalo si la leo bali limekuwepo katika safari ya wokovu. Tunasoma daima katika kitabu cha pili cha Wamakabayo kuwa Yuda kiongozi wa Wayahudi alichanga fedha kwa kila mtu jumla drakma mbili elfu, akazipeleka Yerusalemu kutoa sadaka ya dhambi. Kwa kufanya hivi alitenda vema na kwa haki kwa kuwa aliukumbuka ufufuo wa wafu. Alifanya hili kwa sababu ya imani na kama asingekuwa na imani kuwa wafu watafufuliwa ingekuwa upumbavu na kazi bure kuwaombea marehemu. (Rej. 2Wak. 12: 43-45).
Basi ndugu yangu mpendwa ninakualika katika msingi uleule wa imani katika ufufuko, kusali daima sala hii “raha ya milele uwape Ee Bwana na mwanga wa milele uwaangazie wapumzike kwa amani, amina”. Ni Sala ya kujenga urafiki na marehemu walioko toharani na hatimaye watakatifu wa mbinguni. Ni sala ambayo yatukumbusha wapendwa wetu ambao wengine tuliwafahamu kwa karibu na hivi yatudai wajibu wa kuomba huruma ya Mungu kwa ajili yao pasipo kukoma.
Mama Kanisa ametuwekea Misa tatu kwa ajili ya marehemu wote ili kwa njia hiyo marehemu wapate msaada wa masitahili ya Kristo kwa njia sadaka yake ya msalabani. Anataka asiwepo hata mmoja atakayekosa huruma na msaada wa Mungu. Katika Misa hizi tatu injili zagusa Heri Nane njia ya utakatifu na habari ya ufufuko wa wafu lililotumaini letu na imani yetu tunaposafiri kuelekea ukamilifu yaani uzima wa milele ambao huja baada ya kifo. Tunasali na kutumaini kuwa, kwa kifo maisha hayaondolewi ila hugeuzwa na kuwa maisha mapya, maisha makamilifu.
Basi mpendwa mwanatafakari, leo ni wakati wa kusali na kuwatembelea waliolala kule makaburini ili muunganiko katika sala ukamilishwe katika upendo unaoonekana katika maisha ya watu. Yafaa pia kufunga kidogo kwa ajili ya wapendwa wetu ili kuisimika sala yetu katika majitoleo ya Kristo mteswa na hatimaye uibuke na ushindi wa Kristu mfufuka. Kumbukeni pia kujiombea wewe mwenyewe kwa maana kwakukumbusha kujitayarisha kwa ajili ya safari ya kugeuzwa na kuingia maisha mapya, maisha ya mbinguni.