Watawa wa Mama Theresa wa Calcutta
waliouwawa huko Yemen ni mashuhuda wa upendo na wahanga wa utandawazi
usiojali wala kuguswa na mahangaiko ya wengine!
Baba Mtakatifu anakaza kusema, hawa ni mashuhuda wa imani kwa nyakati hizi! Ni watu ambao hawawezi kuwa ni sehemu ya habari inayopewa uzito wa juu; kwa baadhi ya vyombo vya habari, hii si habari! Hawa ni watu wanaoyamimina maisha yao kwa ajili ya utume na maisha ya Kanisa. Ni wahanga wa mashambulizi ya kigaidi na kielelezo cha utandawazi usiojali wala kuguswa na mahangaiko ya wengine. Baba Mtakatifu anamwomba Mwenyeheri Mama Theresa wa Calcutta awasindikize watoto wake ambao wamekuwa ni mashuhuda wa upendo kwenye maisha ya uzima wa milele pamoja na kuombea amani na heshima kwa utakatifu wa maisha ya binadamu!