Week Hot newz

Mbiu ya Imani: Watawa waliouwawa huko Yemen ni mashuhuda wa upendo!

Watawa wa Mama Theresa wa Calcutta waliouwawa huko Yemen ni mashuhuda wa upendo na wahanga wa utandawazi usiojali wala kuguswa na mahangaiko ya wengine!




Baba Mtakatifu anakaza kusema, hawa ni mashuhuda wa imani kwa nyakati hizi! Ni watu ambao hawawezi kuwa ni sehemu ya habari inayopewa uzito wa juu; kwa baadhi ya vyombo vya habari, hii si habari! Hawa ni watu wanaoyamimina maisha yao kwa ajili ya utume na maisha ya Kanisa. Ni wahanga wa mashambulizi ya kigaidi na kielelezo cha utandawazi usiojali wala kuguswa na mahangaiko ya wengine. Baba Mtakatifu anamwomba Mwenyeheri Mama Theresa wa Calcutta awasindikize watoto wake ambao wamekuwa ni mashuhuda wa upendo kwenye maisha ya uzima wa milele pamoja na kuombea amani na heshima kwa utakatifu wa maisha ya binadamu!

Pope Francis General Audience 2016.02.24

Bodaboda zapigwa marufuku!

Burundi imepiga marufuku bodaboda au pikipiki kuingia katikati mwa mji mkuu Bujumbura katika juhudi za kujaribu kupunguza mashambulio.Pikipiki hutumiwa sana kusafirisha watu na mizigo Bujumbura lakini sasa zimekuwa zikitumiwa kutekeleza mashambulio, meya wa Bujumbura Freddy Mbonimpa anasema.

Mtu mmoja aliuawa Jumatatu wiki hii watu waliokuwa wamepaki pikipiki waliporusha guruneti tatu.
Usalama umeimarishwa mjini humo tangu kutoka kwa mashambulio hayo na polisi wanapekua watu na magari, shirika la habari la AFP linasema.

“Polisi wamegundua kwamba wahalifu hubeba guruneti wakitumia mabegu au vikapu,
” Bw Mbonimpa anasema. Mwandishi wa BBC aliyeko Bujumbura Prime Ndikumagenge anasema marufuku hiyo itaathiri sana watu wanaosafiri kutoka eneo moja hadi jingine mjini.

Huwezi kutoka kusini mwa mji hadi kaskazini bila kupitia katikati mwa mji, anasema.
Machafuko yalizuka nchini Burundi Aprili mwaka jana Rais Pierre Nkurunziza, ambaye amekuwa uongozini tangu 2005, alipotangaza kwamba angewania urais kwa muhula wa tatu.
Watu 400 wamefariki na wengine 240,000 kutorokea nchi jirani tangu wakati huo.

Papa Francisko nchini Mexico

Majadiliano ya kiekumene yamechukua sura mpya kwa papa Francisko na Patriaki Kirill wa Moscow na Russia nzima kukutana.
Majadiliano ya kiekumene yamechukua sura mpya kwa papa Francisko kukutana na Patriaki Kirill wa Moscow na Russia nzima.
Mapambazuko mapya ya majadiliano ya kiekumene!
16/02/2016 14:43Baba Mtakatifu Francisko na Patriaki Kirill wa Moscow na Russia nzima wamekutana na kuzungumza pamoja na kutia sahihi Tamko la shughuli za kichungaji kwa Makanisa haya mawili, ili kuanza kuandika ukurasa mpya wa majadiliano ya kiekumene katika Millenia ya tatu ya Ukristo!

 

 
 Baba Mtakatifu akishiriki chakula cha mchana na familia ya Mungu nchini Mexico.
Baba Mtakatifu Francisko akiwa nchini Mexico, Jumatatu tarehe 15 Februari 2016 ametembelea Kanisa kuu la san Cristòbal de las Casa na kusali humo, ameshiriki chakula cha mchana pamoja na wawakilishi wa Familia ya Mungu nchini Mexico pamoja na kuzungumza na  kusali nao!

 

Baba Mtakatifu Francisko akiwa Mexico amesikiliza shuhuda za Injili ya familia.
Baba Mtakatifu Francisko akiwa nchini Mexico amesikiliza shuhuda wa Injili ya familia.

Mashuhuda wa Injili ya familia!

16/02/2016 10:42Baba Mtakatifu Francisko alipokutana na familia nchini Mexico amesikiliza shuhuda za watu waliotelekezwa na familia zao, lakini wakapata fursa ya kuonja huruma na upendo wa Mungu kwa njia ya Kanisa; amesikiliza mashuhuda waliokumbatia utamaduni wa kifo, leo hii wanashuhudia Injili ya uhai!

 


Baba Mtakatifu Francisko anawahimiza wananchi wa Mexico kujikita katika ushuhuda wa tunu msingi za Injili ya furaha!
Baba Mtakatifu Francisko anawahimiza wananchi wa Mexico kuwa ni mashuhuda wa Injili ya familia.

Iweni mashuhuda wa Injili ya familia na huruma ya Mungu!

16/02/2016 10:21Baba Mtakatifu anawaalika wanafamilia kuwa kweli ni mashuhuda wa Injili ya familia na vyombo vya huruma ya Mungu ili kuweza kupambana na changamoto mbali mbali zinazojitokeza katika maisha na utume wa familia; kwa kushinda upweke na kinzani za maisha!
Baba Mtakatifu Francisko akiadhimisha Ibada ya Misa Takatifu na wenyeji wa Chiapas, nchini Mexico
Baba Mtakatifu Francisko akiadhimisha Ibada ya Misa Takatifu na wenyeji wa Chiapas, nchini Mexico.

Onesheni ujasiri wa kuomba msamaha!

16/02/2016 10:02Baba Mtakatifu Francisko akiwa nchini Mexico anasema, umefika wakati wa kujenga na kudumisha udugu, haki, mshikamano na amani; kwa kutambua kwamba haya ni mambo msingi yanayowaunganisha binadamu kama watoto wateule wa Mungu dhidi ya nyanyaso, dhuluma na ubaguzi!
Maskini wanapaswa kujipanga vyema zaidi ili kupambana na ubaguzi kwa kushikamana ili kudumisha utu wao na kupata mahitaji msingi!
Maskini wanapaswa kujipanga vyema kwa kushikamana kutetea utu na heshima yao kwa kupinga ubaguzi na nyanyaso, ili kukuza utu na heshima yao pamoja na kujipatia mahitaji msingi ya maisha.

Changamoto za utunzaji bora wa mazingira nyumba ya wote!

15/02/2016 10:39Kardinali Peter Turkson, Rais wa Baraza la Kipapa la haki na amani anawapongeza wenyeji wa Mexico kwa kuonesha mwanga angavu katika kulinda na kutunza mazingira nyumba ya wote, sanjari na kuendelea kushikamana ili kupambana na changamoto za maisha ili kudumisha utu wao!

 

Baada ya Askofu mkuu Ivan Jurkovic kukamilisha utume wake nchini Russia ameteuliwa kuwa Mwakilishi wa kudumu wa Vatican UN, Geneva.
Baada ya Askofu mkuu Ivan Jurkovic kukamilisha utume wake kama Balozi wa Vatican nchini Russia, ameteuliwa kuwa mwakilishi wa kudumu wa Vatican kwenye ofisi za UN zilizoko Geneva, Uswiss.

Askofu mkuu Ivan Jurkovic ateuliwa kuwa Mwakilishi wa kudumu UN, Geneva

15/02/2016 10:24Askofu mkuu Ivan Jurkovic ameteuliwa kuwa Mwakilishi wa kudumu wa Vatican kwenye Ofisi za Umoja wa Mataifa zilizoko mjini Geneva ili kuchukua nafasi ya Askofu mkuu Silvano Maria Tomasi ambaye amekuwepo huko tangu mwaka 2003. Aliwahi kuwa Balozi wa Vatican nchini Ethiopia na Eritrea.

 

Baba Mtakatifu Francisko ametembelea Hospitali ya "Federico Gomez" Mexico kushukuru kwa huduma na kuwabariki watoto wagonjwa wa saratani!
Baba Mtakatifu Francisko ametembelea Hospitali ya "Federico Gomez" ili kushukuru kwa huduma makini zinazotolewa kudumisha Injili ya uhai pamoja na kuwaombea watoto wagonjwa katika shida na mhangaiko yao!

Papa Francisko kielelezo cha faraja na matumaini kwa wagonjwa!

15/02/2016 10:07Baba Mtakatifu Francisko, Jumapili tarehe 14 Februari 2016 ametembelea Hospitali ya "Federico Gomez" nchini Mexico ili kumshukuru Mungu kwa huduma inayotelewa kwa ajili ya watoto wagonjwa pamoja na kubariki kazi njema inayofanywa na wazazi pamoja na wahudumu wa sekta ya afya!

Pope Francis' prayer intentions for February 2016

Baba Mtakatifu: Onesheni ujasiri wa kuomba msamaha!



Familia ya Mungu mjini Chiapas, nchini Mexico imempokea Baba Mtakatifu Francisko katika mji wao kwa bashasha na shangwe kubwa iliyokuwa inajionesha katika nyuso za watu, katika midundo na rangi za mavazi yao. Bahari ya watu ilifurika, siku ya Jumatatu tarehe 15 Februari 2016 huko Chiapasa, wakati Baba Mtakatifu alipokwenda mjini humo kuadhimisha Ibada ya Misa takatifu pamoja na wenyeji wa Chiapas, huko San Cristobal, DLC. Ibada hii imeadhimishwa kwa kutumia lugha mahalia, changamoto ya kutamadunisha Injili ili kweli Injili iweze kuingia na kuzama katika maisha, mila na tamaduni za watu!
 Katika mahubiri yake, Baba Mtakatifu anasema, Neno la Mungu linafanya rejea katika maisha ya watu wa Chiapas, ambao kwa miaka mingi walitengwa, wakadhulumiwa na kunyanyaswa na mifumo mbali mbali ya kisiasa. Umefika wakati wa kuchunguza dhamiri na kuomba msamaha kwa makosa yaliyotendeka katika historia, tayari kuanza kuandika ukurasa mpya unaojikita katika haki msingi za binadamu, sanjari na utunzaji bora wa mazingira, nyumba ya wote! Baba Mtakatifu anafafanua kwamba, Waisraeli walipokuwa utumwani Misri walionja mateso na nyanyaso, wakamlilia Mungu naye akawasikiliza, kwa kuwaonesha uso wa huruma kwa njia ya Neno na Sheria zake, ambazo zikawa ni chemchemi ya uhuru, furaha, hekima na mwanga wa maisha kwa watu waliokuwa wanatembea katika giza la maisha. Hata wananchi wa Chiapas anasema Baba Mtakatifu kwa miaka mingi wametembea katika dhuluma na nyanyaso; wakang’olewa hata katika ardhi yao; mambo ambayo yameacha chapa ya kudumu katika nyoyo za watu!
Baba Mtakatifu anakaza kusema, umefika wakati wa kujenga na kudumisha udugu, haki, mshikamano na amani, kwa kutambua kwamba, haya ni mambo msingi yanayowaunganisha wote kama watoto wa Baba yao wa mbinguni, aliyewaletea Kristo Yesu, anayetembea pamoja nao katika hija yao ya maisha. Yesu ni njia, ukweli na uzima anayetaka kuwasaidia waja wake kushinda giza la maisha. Nyanyaso na dhuluma zimesababisha madhara makubwa katika maisha ya watu wengi, lakini bado Mwenyezi Mungu anaonesha huruma na upendo kwa waja wake.
Baba Mtakatifu anaendelea kukemea vikali matumizi mabaya ya rasilimali na utajiri wa dunia ambao ni zawadi kubwa kwa binadamu kwa kudhani kwamba, wao ni wamiliki na kusahau kuwa wamedhaminishwa na Mwenyezi Mungu ili kuitunza na kuiendeleza dunia, iweze kuwa ni mahali pazuri zaidi pa kuishi. Vita inayojikita bado katika mioyo ya binadamu ni matokeo ya madhara ya dhambi yanayojionesha hata katika matumizi mabaya ya ardhi na maji pamoja na kusababisha uchafuzi mkubwa wa mazingira; mambo ambayo yana athati kubwa katika maisha ya watu wengi.
Baba Mtakatifu anaendelea kufafanua kwamba, athari za uchafuzi wa mazingira zinawagusa binadamu wote na kwamba, hii ni kati ya changamoto kubwa inayomwandama mwanadamu katika ulimwengu mamboleo. Wananchi wa Chiapas ni mfano bora wa kuigwa kwa kulinda, kutunza na kudumisha mazingira bora na kwamba, Jumuiya ya Kimataifa inaweza kujifunza mengi kutoka kwao. Mazingira imekuwa ni nyumba ya wote, chanzo cha lishe na Altare ya ushirikiano kati ya watu!
Baba Mtakatifu Francisko anasikitika kusema, wananchi wa Chiapas wakati mwingine hawakueleweka; tunu msingi, tamaduni na mapokeo yao yakadhalilishwa; kwa watu kutaka kukumbatia madaraka, utajiri, fedha huku wakisukumwa na kanuni msingi za soko; wakawekeza katika mambo makubwa, ambayo kwa wakati huu ni chanzo kikuu cha uharibifu wa mazingira. Umefika wakati wa kuchunguza dhamiri na kuthubu kuomba msamaha kutokana na utandawazi usiojali wala kuguswa na mahangaiko ya wengi kwa kuonesha kwamba, hata wao ni muhimu sana katika mchakato wa maendeleoya jamii.

St. Valentine

Short Cuts


Facts
Feastday: February 14
Patron of Love, Young People, Happy Marriages
Death: 269

Click Here for St. Valentine Prayer's
 
Saint Valentine, officially known as Saint Valentine of Rome, is a third-century Roman saint widely celebrated on February 14 and commonly associated with "courtly love."
Although not much of St. Valentine's life is reliably known, and whether or not the stories involve two different saints by the same name is also not officially decided, it is highly agreed that St. Valentine was martyred and then buried on the Via Flaminia to the north of Rome.
In 1969, the Roman Catholic Church removed St. Valentine from the General Roman Calendar, because so little is known about him. However, the church still recognizes him as a saint, listing him in the February 14 spot of Roman Martyrolgy.

Tafakari ya Neno la Mungu: Dominika ya I ya Kwaresima Mwaka C

“Katika Waraka Uso wa huruma, maalum kwa ajili ya kuzindua Maadhimisho ya Mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya huruma ya Mungu niliwaomba kwamba ‘Kwaresima ya Mwaka huu tuiishi kwa uzito zaidi kama muda mahsusi kwa kuadhimisha na kuonja huruma ya Mungu. Ni kurasa ngapi za Maandiko Matakatifu, zinaweza kutafakariwa katika majuma ya Kwaresima kwa lengo la kutusaidia kuugundua tena uso wa huruma wa Baba!”

Papa Francisko achonga na wanahabari!

Padre Federico Lombardi, msemaji mkuu wa Vatican, wakati wa hija ya Baba Mtakatifu Francisko nchini Cuba na Mexico, Ijumaa tarehe 12 Februari 2016, kwa niaba ya waandishi wa habari 76 walioko kwenye msafara wa Baba Mtakatifu, amemtakia heri na mafanikio mema katika hija hii ya kihistoria.

Tafakari ya Neno la Mungu, Jumapili ya IV ya Kipindi cha Mwaka C wa Kanisa


Tafakari ya Neno la Mungu Jumapili ya IV ya Mwaka C wa Kanisa. - OSS_ROM
28/01/2016 14:25
“Leo hii maneno haya yametimia masikioni mwenu”. Kifungu hiki cha maneno ndicho kinafungua Injili ya Dominika hii ya 4 ya mwaka C wa Kanisa. Kusudi tupate kuelewa vema hatuna budi kurejea katika Injili ya Dominika iliyopita tuliposikia Kristo akiwa katika Sinagogi katika kijiji chake cha Nazareti na alisoma sehemu ya kitabu cha Nabii Isaya ambacho kilikuwa ni maneno ya matumaini kwa mmoja ambaye alikuwa anatafuta auheni katika maisha. Kristo leo anawapatia hawa ndugu zake na pia anatupatia sisi habari njema. Anajifunua kwa watu wake wa Nazareti na kwa njia hiyo anajifunua kwa wanadamu kuwa ujio wake ndiyo utimilifu wa uaguzi huo wa nabii Isaya. Ujio wake hapa ulimwenguni ni mwanzo mpya kwa maisha ya mwanadamu; ukurasa mpya umefunguliwa ambao unamuweka mwanadamu katika hali njema tena.
 
Katika lugha adhimu ya Kiswahili upo msemo usemao: “Fadhila mfadhilie mbuzi mwanadamu ana maudhi”. Ujumbe huu wa furaha unapokelewa isivyotegemewa. Fadhila hii ya Mungu kwa mwanadamu inapata mwitikio hasi: “wakajaa ghadhabu wote waliokuwa katika sinagogi walipoyasikia hayo”. Wanashindwa kuipokea huruma ya Mungu inayofunuliwa kwao kwa sababu tu ya unasaba wa mjumbe wa Mungu. Wanashindwa kulipokea Neno na kuanza kumshambulia mtoa neno. Hii ni ajabu kabisa kwani hata kama utafanikiwa kumwangamiza anayekupatia ujumbe wowote ule kamwe hautaweza kuifuta kauli yake aliyoitoa, yaani ukweli alioutangaza.

Papa "Wambea hawana bunge na wala umbea si mtaji wangetajirika wengi"

Baba Mtakatifu Francisko anawataka watawa kuwa ni mashuhuda wa kinabii, watu wanajenga utamaduni wa ujirani mwema na watu wenye matumaini kwa Mwenyezi Mungu. - OSS_ROM
02/02/2016 07:39
Maadhimisho ya kufunga Mwaka wa Watawa Duniani, Jumatatu tarehe Mos Februari 2016 yalichukua sura mpya pale Baba Mtakatifu Francisko alipokabidhi hotuba yake kuhusu wosia ambao amependa kuwakabidhi watawa wakati huu Mama Kanisa anapofunga rasmi maadhimisho ya Mwaka wa Watawa Duniani kwa kuwataka wayakite maisha yao katika mambo makuu matatu: Unabii, Ujirani na Matumaini. Baba Mtakatifu akaamua kutoa katekesi ya kina kwa kuzungumza na watawa moja kwa moja, ili kuangalia ukweli wa maisha na utume wa watawa ndani ya Kanisa.

Vijana wa kizazi kipya wafundwe elimu ya watu kukutana!


Baba Mtakatifu Francisko anawataka wadau mbali mbali wa sekta ya Elimu Katoliki kuhakikisha kwamba, wanawajengea vijana wa kizazi kipya msingi wa elimu utakaowawezesha kukutana na wenzao, kusaidiana na kushirikiana kwa dhati pasi na makunyanzi. - OSS_ROM
Kanisa halina budi kuwasaidia vijana kujenga na kudumisha utamaduni wa watu kukutana, kusaidiana, kuheshimiana na kuthaminiana kwani wote wameumbwa kwa sura na mfano wa Mungu. Hapa binadamu anapaswa kupewa kipaumbele cha kwanza katika sera na mikakati ya elimu makini badala ya kugubikwa na woga pamoja na wasi wasi usiokuwa na mvuto wala mashiko. Hii ni sehemu ya ujumbe kutoka kwa Baba Mtakatifu Francisko kwa njia ya video aliowatumia washiriki wa Kongamano la Ishirini na Nne la Elimu Katoliki Amerika ya Kusini, lililoadhimishwa huko San Paolo del Brasile, hivi karibuni.
Baba Mtakatifu anawataka wadau mbali mbali wa elimu kuhakikisha kwamba, binadamu anapewa kipaumbele cha kwanza pamoja na kuwafunda vijana katika medani mbali mbali za maisha, ili waweze kushiriki kikamilifu katika mchakato wa maboresho ya maisha yao. Vijana waelimishwe namna ya kufikiri na kutenda vyema katika maisha yao. Haitoshi kuwapatia vijana nadharia ya mambo mengi, bila kugusa undani wa maisha yao. Vijana wafundishwe kutambua mema na kuyatafuta katika maisha yao ya kila siku.
Baba Mtakatifu anatambua na kukiri matatizo pamoja na changamoto ambazo wadau mbali mbali wanakabiliana nazo katika sekta ya elimu; changamoto ambazo zinapaswa kuvaliwa njuga na wahusika, ili kweli elimu inayotolewa iweze kuwa bora zaidi, ili kuwasaidia vijana wa kizazi kipya kupambana kikamilifu na mazingira yao, tayari kushiriki katika mchakato wa ujenzi wa dunia inayosimikwa katika haki, amani, umoja na udugu.
Baba Mtakatifu anasema, ili kuweza kufikia lengo hili, kuna haja kwa jamii kujenga na kudumisha utamaduni wa vijana wa kizazi kipya kukutana kati yao, ili waweze kujisikia kuwa ni wamoja; tayari kushirikiana ili kufanya kazi kwa pamoja bila kujali: imani, kabila au mahali anapotoka mtu: hapa utambulisho ni utu na heshima ya binadamu. Kwa njia hii, mchakato wa elimu utawasaidia vijana kukutana na hatimaye, kuzaa matunda yanayokusudiwa na wengi.
Baba Mtakatifu Francisko anakaza kusema, mfumo mpya wa shule ujulikanao kama “Scholas occurrentes” unaendelea kushika kasi kwa kujikita katika sana ana michezo; maeneo muhimu sana yanayowakutanisha vijana wa kizazi kipya. Michezo inawasaidia vijana kupata majiundo makini ya kufanya kazi kwa pamoja kwa kutegemeana. Sanaa inawafunda vijana kujenga na kudumisha majadiliano ya kina. Haya ni maeneo ambayo yanapaswa kufanyiwa kazi, ili kweli sekta ya elimu iweze kuzaa matunda yanayokusudiwa.
Baba Mtakatifu anawataka wadau wa Katoliki kufuata mfano wa Yesu Kristo aliyekuwa ni Mwalimu na Bwana; Mwalimu aliyefaulu kufafanua na kumwilisha Sheria katika uhalisia wa maisha ya watu. Ili waamini waweze kuzama zaidi katika Injili, wanahamasishwa kutafakari, kujisomea na kumwilisha Heri za Mlimani ambazo kimsingi ni muhtasari wa Mafundisho makuu ya Yesu kwa wafuasi wake. Matendo ya huruma ni kigezo ambacho Kristo atakitumia wakati atakapokuja kuwahukumu wazima na wafu na wala Ufalme wake hautakuwa na mwisho! Maadhimisho ya Mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya huruma ya Mungu, iwe ni fursa ya kumwilisha matendo ya huruma katika maisha ya watu, kielelezo cha imani tendaji.

Wakristo ni uzao mteule, ukuhani wa kifalme na taifa la Mungu!




Tamko la pamoja kati ya Kanisa Katoliki la Kanisa la Kiinjili la Kiluteri kuhusu kuhesababiwa haki ni msingi wa majadiliano ya kiekumene kuhusu: Kanisa, Sakramenti na Utume wa Kanisa. - OSS_ROM

Hija ya kiekumene ni utambulisho muhimu sana miongoni mwa Wakristo, unaowasukuma kutoa ushuhuda wao imani yao kwa Kristo na Kanisa lake, msingi wa umoja wa Wakristo. Ni maneno ya Baba Mtakatifu Francisko aliyoyatoa Jumatatu tarehe 18 Januari 2016 wakati alipokutana na kuzungumza na waamini wa Kanisa la Kiinjili la Kiluteri kutoka Finland ambao kwa sasa wako mjini Roma kwa ajili ya hija ya kiekumene na kama sehemu ya maadhimisho ya Siku kuu ya kumbu kumbu ya Mtakatifu Enric.

Huruma ni jina na utambulisho wa Mungu!


Huruma ni jina na utambulisho wa Mungu anasema Baba Mtakatifu Francisko. - AFP

Huruma ndilo jina na utambulisho wa Mwenyezi Mungu, hivi ndivyo anavyosema Baba Mtakatifu Francisko katika mahojiano maalum na Andrea Tornielli, mwandishi wa habari za gazeti la “La Stampa” na mhariri mkuu wa tovuti ya “Vatican insider” katika kitabu ambacho kimezinduliwa na Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican, “Jina la Mungu ni huruma”. Kitabu hiki kimegawanyika katika sura tisa ambazo ni majibu ya maswali 40 aliyoulizwa Baba Mtakatifu Francisko kama sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya Mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya huruma ya Mungu, uliozinduliwa hapo tarehe 8 Desemba 2015.
Baba Mtakatifu Francisko katika mahojiano haya anafanya rejea katika Maandiko Matakatifu, Mafundisho ya Mababa wa Kanisa pamoja na watangulizi wake, yaani Papa mstaafu Benedikto XVI, Mtakatifu Yohane Paulo II, Mtakatifu Yohane XXIII na Mwenyeheri Paulo VI. Kitabu hiki kimechapishwa katika lugha tano na nakala ya kwanza ikawasilishwa kwa Baba Mtakatifu Francisko, hivi karibuni. Kitabu hiki ni matunda ya mahojiano ya kina na majibu muafaka yaliyotolewa na Baba Mtakatifu Francisko huku akiwahamasisha waamini kutambua udhaifu wao, tayari kukimbilia huruma na upendo wa Mungu.

Tafakari ya Neno la Mungu, Sherehe ya Bikira Maria Mama wa Mungu

Bikira Maria Mama wa Mungu na Kanisa. - RV
Na Paskal Linda.
Mpendwa, unayeitegea sikio Radio Vatican, leo Mama Kanisa anasherehekea sherehe ya Mama wa Mungu ambayo huja daima kila tarehe mosi ya mwezi Januari. Ni sherehe ya amani kwa maana Mama Maria ni Mama wa amani. Amemzaa Mkombozi mfalme wa amani na hivi Mama Kanisa anaona ni vema tukasali tukimwomba Mungu kwa njia ya Mama huyu kwa ajili ya amani ya ulimwengu. Sherehe hii ya kuombea amani duniani iliwekwa rasmi na Papa Paulo VI kunako mwaka 1968. Kwa namna ya pekee kabisa, Kanisa linaadhimisha Sherehe hii katika Mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya huruma ya Mungu. Kanisa linamkumbuka Bikira Maria kama Tabernakulo ya kwanza ya huruma na upendo wa Mungu na Sanduku la Agano kati ya Mungu na binadamu.

Salaam Mama Mtakatifu wa Mungu uliyemzaa mfalme mwenye kutawala mbingu na dunia daima na milele. Hii ndiyo salaam yetu kwa Mama mpendelevu Mama asiye na doa, katika sherehe hii tukufu tunapofungua mwaka mpya.

Zawadi ya Noeli kwa Mwaka 2015: Huruma, amani, furaha na mapendo!


Bikira Maria ni sanduku la: Agano jipya, huruma, msamaha na mapendo ya Mungu!

NA PASKAL LINDA



Kadiri ya mila za Waafrika mgeni akutembeleapo hubeba zawadi. Kwa kawaida zawadi hiyo inakuwa chakula kama vile unga katika sanduku liitwalo jamanda, linafungwa nguo nzuri na kubebwa kichwani na mwanamke, kisha mgongoni hubeba kuku kama mtoto mchanga. Afikapo ugenini, mama mwenye nyumba huzipokea zawadi kwa furaha na kumkaribisha mgeni nyumbani. Noel ni kipindi cha kutembeleana, kupeana zawadi na kufurahiana.
Mama Maria baada ya kuambiwa na Malaika Gabrieli kuwa ana baraka, (mja mzito), akaondoka mara moja kwenda kumtembelea ndugu yake Elizabeti aliyekuwa na baraka ya Yohane mbatizaji. Ndivyo tunavyosali katika fumbo la pili la rozari ya furaha: “Uliyekuchukua ulipokwenda kumtazama Elizabeth.” Aliwasili huko, Maria akamwamkia Elizabeth na kuendelea na mazungumzo. Lakini mazungumzo ya akina mama hawa ni tofauti. Hawa wanaongea lugha ya utaalamu wa hali ya juu wakinukuu Agano la kale kama vile unasikiliza mhadhala wa Wataalamu wa Biblia. Kwa hiyo, ili kuupata ujumbe wa mazungumzo ya akina mama wa leo, yakubidi ukae mkao wa nidhamu na kuwasikiliza kwa nidhamu, vinginevyo utatoka kapa.

Huduma kwa waathirika wa dawa za kulevya ijikite katika kukinga na kuponya!


Matumizi haramu ya dawa za kulevya ni janga kwa vijana wengi wa kizazi kipya! Jumuiya ijitahidi kuwa na mikakati ya kuzuia na kuwaganga waliotumbukia huko! -

Kardinali Pietro Parolin, kama sehemu ya maadhimisho ya Mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya huruma ya Mungu, Jumanne, tarehe 22 Desemba 2015 ameadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwa waathirika wa dawa za kulevya pamoja na familia; kundi linalohudumiwa kwenye kituo cha mshikamano cha Don Mario Picchi, kilichoko mjini Roma. Katika mahubiri yake, Kardinali Parolin amekazia umuhimu wa kuzuia na kuwapatia tiba wale walioathirika kutokana na matumizi haramu ya dawa za kulevya; watu ambao idadi yao inazidi kuongezeka maradufu kutokana na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii.

Nani wafisadi zaidi Afrika?


Na Paskal Linda

Ni mara ya kwanza wafanyibiashara wametajwa kuwa mafisadi wakubwa Barani. Shirika hili limeongeza kwamba utumizi mbaya wa mamlaka unasababisha ongezeko la umasikini, na kuwanyima raia mahitaji muhimu.
Watu wengi ambao ni masikini wamejipata mara kadhaa wakilazimika kulipa hongo ikilinganishwa na matajiri, inasema "Transparency International".
Nchi ya Liberia imetajwa kama inayoongoza kwa visa vya ufisadi Afrika. Inafuatwa na Cameroon, Nigeria na Sierra leone.Afrika mashariki Uganda inaongoza kwa visa vya ufisadi, ikifuatwa na Kenya. Kusini mwa Afrika Zimbabwe na Zambia zinaongoza katika nchi zenye visa vingi vya ufisadi.
Botswana, Mauritius na Cape Verde, ndiyo mataifa pekee ya Afrika ambapo visa vya ufisadi ni vya chini zaidi ikiwa ni asili mia mbili pekee.
Wafanyibiashara wakubwa wametakwa kuwa miongoni mwa watu wafisadi zaidi sawa na maafisa wa polisi Barani Afrika. Hii ni kwa mujibu ya kura ya maoni iliyofanywa na shirika la kuchunguza ufisadi duniani "Transparency International".
Wafanyibiashara wakubwa wametakwa kuwa miongoni mwa watu wafisadi zaidi sawa na maafisa wa polisi Barani Afrika. Hii ni kwa mujibu ya kura ya maoni iliyofanywa na shirika la kuchunguza ufisadi duniani "Transparency International".
Ni mara ya kwanza wafanyibiashara wametajwa kuwa mafisadi wakubwa Barani. Shirika hili limeongeza kwamba utumizi mbaya wa mamlaka unasababisha ongezeko la umasikini, na kuwanyima raia mahitaji muhimu.
Watu wengi ambao ni masikini wamejipata mara kadhaa wakilazimika kulipa hongo ikilinganishwa na matajiri, inasema "Transparency International".
Image caption Raia wengi wa Kenya wamelalamikia visa vya ufisadi serikalini
Nchi ya Liberia imetajwa kama inayoongoza kwa visa vya ufisadi Afrika. Inafuatwa na Cameroon, Nigeria na Sierra leone.
Afrika mashariki Uganda inaongoza kwa visa vya ufisadi, ikifuatwa na Kenya. Kusini mwa Afrika Zimbabwe na Zambia zinaongoza katika nchi zenye visa vingi vya ufisadi.
Botswana, Mauritius na Cape Verde, ndiyo mataifa pekee ya Afrika ambapo visa vya ufisadi ni vya chini zaidi ikiwa ni asili mia mbili pekee.

St. Bibiana

Short Cuts
Image of St. Bibiana

Facts

Feastday: December 2

St. Bibiana, Virgin and Martyr (Feast day - December 2nd) Other than the name, nothing is known for certain about this saint. However, we have the following account from a later tradition.
In the year 363, Julian the Apostate made Apronianus Governor of Rome. St. Bibiana suffered in the persecution started by him. She was the daughter of Christians, Flavian, a Roman knight, and Dafrosa, his wife. Flavian was tortured and sent into exile, where he died of his wounds. Dafrosa was beheaded, and their two daughters, Bibiana and Demetria, were stripped of their possessions and left to suffer poverty. However, they remained in their house, spending their time in fasting and prayer.
Apronianus, seeing that hunger and want had no effect upon them, summoned them. Demetria, after confessing her Faith, fell dead at the feet of the tyrant. St. Bibiana was reserved for greater sufferings. She was placed in the hands of a wicked woman called Rufina, who in vain endeavored to seduce her. She used blows as well as persuasion, but the Christian virgin remained faithful.
Enraged at the constancy of this saintly virgin, Apronianus ordered her to be tied to a pillar and beaten with scourges, laden with lead plummets, until she expired. The saint endured the torments with joy, and died under the blows inflicted by the hands of the executioner.

Papa: Hata katika umaskini wao, Waafrika daima ni watu wa furaha! Wamenikuna!

Hata katika umaskini wao, waafrika bado ni watu wenye furaha! - OSS_ROM

Baba Mtakatifu Francisko amerejea mjini Vatican baada ya kuhitimisha hija yake ya kitume Barani Afrika alikotembelea Kenya, Uganda na Jamhuri ya Watu wa Afrika ya Kati kuanzia tarehe 25 hadi 30 Novemba 2015. Huko amepata nafasi ya kujionea na kusikiliza kilio cha Familia ya Mungu kuhusiana na umaskini, ukosefu wa haki msingi na mahitaji muhimu ya binadamu. Ameguswa na kilio cha vijana wanaotaka saratani ya rushwa na vitendo vya kigaidi, uharibifu wa mazingira ipewe tiba muafaka; mambo yote haya yanahatarisha utu na heshima ya binadamu.
Baba Mtakatifu akiwa njiani amepata fursa ya kujibu baadhi ya maswali yaliyoulizwa na waandishi wa habari waliokuwa kwenye msafara wake. Anasema, pale ambapo sera za uchumi na maendeleo zinajikita katika ubinafsi, utajiri na mali, hapo utu na heshima ya binadamu viko rehani. Inasikitisha kuona kwamba, kuna watu wachache sana wanaomiliki utajiri wa dunia wakati ambapo kuna kundi kubwa la watu bado linaendelea kuogelea katika dimbwi la umaskini na magonjwa.
Baba Mtakatifu anasema, amesikitishwa sana na mahangaiko ya wananchi  wa kitongoji cha Kangemi, Kenya; ameguswa na mateso ya watoto waliolazwa kwenye Hospitali ya Watoto Bangui. Amejionea jinsi watoto wanavyoteseka kutokana na utapiamlo mkubwa, kwa kukosa dawa na vifaa tiba. Yote haya ni kwa sababu watu wanapenda kuabudu fedha na mali kuliko utu na heshima ya binadamu. Magonjwa, umaskini na maafa yataendelea kuwaandama wanadamu ikiwa kama binadamu mwenyewe hataweza kufanya toba na kumwongokea Mungu. Matajiri wawe na ujasiri wa kugawana rasilimali ya dunia na maskini, ili waweze wao pia kufurahia Injili ya maisha!
Baba Mtakatifu anakiri kwamba, ameguswa kwa namna ya pekee na ukarimu, furaha na maisha ya Familia ya Mungu Barani Afrika hata katika umaskini wao, bado wanaweza kufurahia maisha. Wameonesha ukarimu wa ajabu kwa kujitokeza kwa wingi kumpokea na kumsikiliza. Kenya inaonekana kuwa na maendeleo; Uganda bado inajikita katika mashuhuda wa imani; huu ndio utambulisho wao unaowapatia ujasiri wa kushuhudia imani inayomwilishwa katika matendo! Katika Jamhuri ya Watu wa Afrika ya Kati, Baba Mtakatifu anakaza kusema, wao wana kiu ya amani, upatanisho na msamaha wa kweli; udugu, umoja na mshikamano wa kitaifa kwa kutambua kwamba wao ni ndugu wamoja! Waamini wanapaswa kuwa wajenzi wa haki, amani na maridhiano kati ya watu na wala si wachochezi wa kinzani na misigano mambo ambayo yanasigana na imani wanayoiungama. Serikali ya mpito Jamhuri ya Watu wa Afrika ya Kati isaidie kuwapatia wananchi: haki, amani, msamaha na upatanisho wa kitaifa.
Bara la Afrika lina utajiri na raslimali nyingi; lina tunu na tamaduni zinazopaswa kuendelezwa. Kwa bahati mbaya Bara la Afrika linaonekana na wengi kuwa ni uwanja wa fujo pasi na usalama. Baba Mtakatifu anakaza kusema, Bara la Afrika limekuwa kama kichwa cha mwendawazimu, watu wengi wanalinyonya kiasi kwamba limekuwa ni shahidi wa unyonyaji pasi na huruma. Anasema analipenda Bara la Afrika na kwamba, kuna haja ya kushikamana ili kuliendeleza Bara la Afrika badala ya kuendelea kunyanyaswa na wenye nguvu wachache duniani!
Baba Mtakatifu anawataka waandishi wa habari kutekeleza dhamana na wajibu wao kwa kuzingatia kanuni, maadili na sheria kwani hakuna uhuru pasi na mipaka hata katika mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi ambao umeenea sehemu mbali mbali  za dunia hata mjini Vatican. Vyombo vya habari viwe na ujasiri wa kufunua maovu na vyombo vya sheria vitekeleze wajibu wake barabara.Waandishi wa habari waseme ukweli pasi na kuuvuruga kwa ajili ya mafao yao binafsi; waoneshe weledi katika kazi zao kwa kujikita katika ukweli pamoja na kuheshimu sifa ya mtu! Waandishi wa habari wawe na ujasiri wa kuomba msamaha pale wanapokosea na kukiuka kanuni maadili za kazi. 
Katika mapambano dhidi ya vitendo vya kigaidi na misimamo mikali ya kidini, viongozi wa kidini wanapaswa kutekeleza dhamana na wito wao kwa kutambua kwamba, wao ni vyombo na wajenzi wa: umoja, haki, amani,upatanisho na maridhiano. Misimamo mikali ya kidini ni saratani ambayo iko katika dini zote na inakwenda kinyume kabisa cha mafundisho msingi ya kidini. Hapa kuna watu wanatumia misimamo mikali ya kidini kwa ajili ya mafao ya binafsi, ili kujipatia fedha na utajiri wa haraka haraka.
Baba Mtakatifu Francisko anakiri kwamba, kumekuwepo na tatizo la kumshirikisha Monsinyo Vallejo Balda pamoja na Francesca Immaculata Chaouqui katika Tume ya Marekebisho ya masuala ya uchumi na fedha Vatican, ingawa baada ya kumaliza kazi zao waliondoka na kwamba, watuhumiwa hawa hawakumnyima usingizi hata kidogo kwani kile kilichochapishwa kwenye vitabu kinaonesha kazi ya mageuzi iliyofanywa. Rushwa anakaza kusema Baba Mtakatifu ni adui wa haki. Mapambano dhidi ya rushwa mjini Vatican ni mchakato ulioanzishwa na Kardinali Joseph Ratzinger wakati alipotoa tafakari ya Njia ya Msalaba, siku chache kabla ya kifo cha Papa Yohane Paulo II, akachaguliwa na Makardinali kuwa Khalifa wa Mtakatifu Petro ili kuendeleza mchakato wa mageuzi.
Kumbe, wizi wa nyaraka za siri kutoka Vatican ni tendo la jinai na kwamba, Baba Mtakatifu angependa kesi hii iwe imekamilika na kutolewa hukumu kabla ya kuanza maadhimisho ya Mwaka Mtakatifu wa Jubilei kuu ya huruma ya Mungu, hapo tarehe 8 Desemba 2015, pengine jambo hili halitawezekana anasikitika kusema Baba Mtakatifu Francisko na kwamba kwa kushirikiana na Makardinali wataendelea kufanya mageuzi kadiri ya maelekezo yaliyotolewa na Makardinali katika mikutano yao kabla ya uchaguzi wa Khalifa wa Mtakatifu Petro kunako mwaka 2013.
Kuhusu Ugonjwa wa Ukimwi ambao bado unaendelea kusababisha vifo vingi miongoni mwa vijana wa kizazi kipya, Baba Mtakatifu anakaza kusema, Kanisa litaendelea kuhimiza kanuni maadili na utu wema; kwa kusimama kidete kutangaza na kushuhudia Injili ya uhai dhidi ya utamaduni wa kifo. Matumizi ya kondomu si dawa ya kuzuia matatizo na majanga yanayoliandama Bara la Afrika. Kuna ukosefu wa haki msingi za binadamu; uharibifu mkubwa wa mazingira; baa la njaa na utapiamlo; ukosefu wa maji safi na salama; bado kuna biashara kubwa ya silaha, unyonyaji na udhalilishaji wa binadamu; watu hawana makazi bora na salama. Matatizo na changamoto hizi zikipewa ufumbuzi muafaka hata Ukimwi utatoweka.
Baba Mtakatifu anasema aliwaahidia Mapatriaki wa Armenia kushiriki katika maadhimisho ya Jubilei ya miaka 101 ya mauaji ya kimbari yaliyotokea nchini Armenia. Lakini ikumbukwe kwamba, vita ni kiwanda kinachozalisha silaha na utajiri kwa watu wachache, hata katika nchi zile ambazo uchumi wake unachechemea, bado utakuta wananunua silaha za mapambano! Vita ni dhambi dhidi ya ubinadamu na madhara yake ni makubwa licha ya vifo na maafa; vita inasababisha pia biashara haramu ya binadamu, udhalilishaji wa utu na heshima ya binadamu bila kusahau unyonyaji. Kuna haja kwa Jumuiya ya Kimataifa kusimama kidete ili kuhakikisha kwamba, vita inasitishwa ili amani iweze kutawala katika akili na mioyo ya watu. Mwenyezi Mungu ndiye asili ya amani changamoto kwa watu wote kuwa ni vyombo na wajenzi wa amani.
Baba Mtakatifu Francisko akizungumzia kuhusu mazingira anakaza kusema, viongozi wa Jumuiya ya Kimataifa wanaoshiriki katiki katika mkutano wa athari za mabadiliko ya tabianchi, Cop21 huko Paris, Ufaransa wanao wajibu mkubwa kuhakikisha kwamba kunakuwepo na udhibiti wa athari za mabadiliko ya tabianchi vinginevyo, dunia itaendelea kushuhudia maafa makubwa kwa watu na mali zao. Baba Mtakatifu anasema, ana imani na matumaini kwa viongozi wa Jumuiya ya Kimataifa kwamba, wataweza kutoa majibu muafaka kuhusiana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
Dini ya Kiislam ina tunu msingi za maisha ya kiroho zinazoweza kutumika katika mchakato wa majadiliano ya kidini katika ujenzi wa udugu na urafiki; maisha ya kiroho yanayojika katika mambo msingi badala ya kushabikia misimamo mikali ya kidini ambayo inapatikana katika dini zote. Hii ni changamoto kwa waamini kutubu, kuongoka na kuomba msamaha, ili dunia iweze kuwa ni mahali pazuri zaidi pa kuishi.
Baba Mtakatifu anasema katika umri wake, safari ndefu ni taabu na shida anatarajia kwenda nchini Mexico ili kutoa heshima yake kwa Bikira Maria pamoja na kutembelea baadhi ya maeneo ambayo hayajawahi kutembelewa na Mapapa. Kunako mwaka 2017 tayari amekwisha kupata mwaliko wa kutembelea baadhi ya nchi za Amerika ya Kusini. Mwishoni, Baba Mtakatifu amewashukuru waandishi wa habari wote waliokuwa kwenye msafara wake Barani Afrika kwa kazi kubwa waliyoifanya ili kuwahabarisha watu. Amewashukuru kwa maswali yao na kwamba, ameyajibu kadiri anavyofahamu pale ambapo haja jibu amewaambia wazi wazi na wala si sehemu ya utamaduni wake kuficha mambo!