Week Hot newz

Uhaba wa dawa unavyowatesa wagonjwa wa saratani


Mtu aliyeathirika na saratani ya kinywaKUNA changamoto nyingi ambazo wagonjwa wa saratani wanakutana nazo hasa kwa wanawake ambao wana saratani ya titi.
Changamoto hizo zimesababisha wagonjwa hao kukata tamaa ya kuendelea na matibabu na kuamua kukatisha dozi na kurudi majumbani mwao.
Hali hiyo hutokea baada ya kuchoka kuhangaika kutafuta fedha za kumudu gharama za dawa huku wakizidi kunyanyasika wakiwa ugenini kwa kuja hospitali ya Ocean Road (ORCI) ambayo inashughulikia tiba na uchunguzi wa ugonjwa huo.
Changamoto kubwa ambayo waathirika wengi wanaomba kusaidiwa ni pamoja na upatikanaji wa dawa aina ya Chemotherapy ambayo hupewa kama tiba katika hospitali hiyo.
Akizungumza hivi karibuni wakati wa uzinduzi wa Chama cha Matumaini ya Mwanamke, mmoja wa wagonjwa hao, Bihuda Shaiza, anasema huwa wanaambiwa dawa hizo ni bure lakini wanapoziulizia mara nyingi huambiwa zimeisha hivyo hulazimika kununua kwenye maduka ya nje ambako huuzwa ghali.
“Nimelipia dozi hiyo mzunguko wa kwanza kwa shida sana kwa gharama ya Sh 200,000 baada ya kuambiwa dawa hiyo haipatikani hospitalini, hapa nilipo sijui dozi ya pili na ya tatu nitaipata vipi,”anasema Shaiza.

Batarokota: Tusimsimange Chid Benz mitandaoni

MKURUGENZI wa Batarokota Daily Gospel Newz pia msanii wa nyimbo za bongo fleva nchini Tanzania, Paskal Linda ‘Batarokota ’, amewataka wadau wa muziki, wasanii na Watanzania kwa ujumla kuacha kumsimanga msanii, Chid Benz ambaye ameathirika na matumizi ya dawa za kulevya kwa kuwa ni mambo yanayoweza kumtokea mtu yeyote.

Batarokota alisema kwa sasa msanii huyo yupo mikono salama chini yake akiwa chini ya uangalizi wa kituo cha Life And Hope Rehabilitation Organization, kilichopo Ukuni huko Bagamoyo akipambana kuachana na matumizi ya dawa za kulevya.

Batarokota alisema yeye kama mdau wa muziki wa Bongo Fleva na  anasaidia wasanii wengi ili wapate mafanikio kupitia muziki na kwenye matatizo pia anawasaidia.
“Nimechukua jukumu la kumsaidia Chid Benz, naomba Watanzania tumuombee aweze kupona na si kumchafua kupitia mitandao,” alieleza Batarokota.

Busu la Papa Francis lamponya uvimbe mtoto


2EB7459800000578-0-image-a-78_1448248918588PHILADELPHIA, Marekani

KIONGOZI wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis, anasadikiwa kufanya muujiza baada ya kumbusu mtoto mwenye umri wa mwaka mmoja aliyekuwa akisumbuliwa na maradhi ya uvimbe kwenye ubongo.
Muujiza huo unadaiwa kufanywa na Papa, wakati wa ziara yake katika Jimbo la Philadelphia, nchini Marekani, Septemba mwaka jana 2015.
Vyombo vya habari nchini Marekani tayari vimefanya mahojiano na wazazi wa mtoto huyo anayeitwa Gianna Masciantonio na kukiri baada ya Papa kumbusu mtoto huyo uvimbe huo umepotea.
Uvimbe wa Gianna ilisemekana hauwezi kutibika, hasa baada ya kufanyiwa operesheni nane na hata kupewa matibabu mengi  ya mionzi (chemotherapy),  akiwa na umri wa miezi 15 tu  katika hospitali ya watoto ya Philadelphia.
Tayari madaktari walikwishatoa ripoti yao kwamba hataweza kupona na zaidi wakimpa miezi kadhaa tu ya kuishi.

JINSI WALIVYOMFIKIA PAPA

Wazazi wa mtoto huyo, Joey Masciantonio na Kristen waliarifiwa juu ya ujio wa Papa katika jimbo wanaloishi la Philadelphia na rafiki yao ambaye ni wakala wa FBI, Donny Asper.
Wakala huyo wa FBI alikuwa amepewa jukumu la kuimarisha ulinzi akiwa na maofisa wenzake zaidi ya 100 katika ziara hiyo ya Papa.
Inaelezwa wakala huyo wa FBI aliwaelekeza wazazi hao kufika haraka iwezekanavyo karibu na eneo la kihistoria la James S. Byrne, ambako Papa alikuwa akitarajiwa kupita baada ya kuhutubia katika ukumbi wa Uhuru.
Joey na familia yake walifika katika eneo hilo na baba huyo wa mtoto anasema alimnyanyua juu Gianna ili maofisa wa Polisi na mawakala wa FBI waweze kumuona kama alivyoelekezwa na  Asper.
Pamoja na kwamba mama wa mtoto huyo, Kristen, alikuwa akitamani binti yake huyo kukutana na Papa, lakini wakala huyo wa FBI ndiye aliyehakikisha Joey, mkewe pamoja na watoto wao wawili wanafanikiwa kupita mbele kumuona kiongozi huyo wa kiroho ambaye alimbusu Gianna kichwani na kisha kumshika kama ishara ya kumbariki.

WANACHOSEMA WAZAZI
Kwa mujibu wa mahojiano yaliyofanyika wiki iliyopita kati ya kituo cha NBC-News na wazazi wa mtoto huyo ambao wote ni waumini wa Kanisa Katoliki, uvimbe uliokuwa ukimsumbua ni kama umekwisha kabisa.
Baba wa mtoto huyo, Joey anasema: “Ni kama alikuwa akisubiri kifo…mimi ni baba ambaye nilikuwa sitaki kumuona Papa.”
Joey anaelezea tukio la binti yake, Gianna kukutana na Papa ni kama muujiza ambao hakutarajia ungetokea.
Joey ameliambia Daily News kwamba alikuwa na wasiwasi mkubwa juu ya mfumo wa kinga wa binti yake, ambao tayari ulikuwa umedhoofika kwa matibabu ya mionzi na  kwa sababu hiyo alipinga binti yake kwenda kwenye mkusanyiko wa watu, hatua ambayo ingesababisha  hali yake kutetereka zaidi.
Lakini anasema madaktari ndio waliomtia moyo kwenda kumuona Papa.
Kwa mujibu wa mtandao wa PhillyVoice.com, uvimbe huo ulitokana na seli za damu kushambulia shina la ubongo wiki chache tu baada ya kuzaliwa.
Ugonjwa huo unadaiwa kuathiri kila mwaka watoto chini ya watano nchini Marekani.

Nyota wa muziki Malawi afariki dunia



Grace-ChingaNYASA, MALAWI

MSANII wa muziki wa injili nchini Malawi, Grace Chinga, amefariki dunia juzi kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya kichwa.
Rafiki wa karibu wa familia ya marehemu Grace, Pasta Chris Suya, akiongea na blogu hii kwa njia ya simu juzi  la nchini humo kwamba, mwanamuziki huyo alikimbizwa hospitalini baada ya kulalamikia maumivu makali ya kichwa.

“Tulipokea simu kwamba alikuwa anasumbuliwa na maumivu makali ya kichwa na tukakimbia hadi kwake kwa mwendo wa saa moja, baada ya kufika tulimpeleka hospitali ya Queens Elizabeth lakini alifariki dunia,” alisema Suya.
Katika akaunti ya facebook ya marehemu Grace, siku chache zilizopita alitangaza kwamba anatarajia kuachia albamu yake mpya hivi karibuni lakini ndoto hizo zimezimika.

Daily Reading for Tuesday, March 22nd, 2016 HD



Reading 1, Isaiah 49:1-6

1 Coasts and islands, listen to me, pay attention, distant peoples. Yahweh called me when I was in the womb, before my birth he had pronounced my name.
2 He made my mouth like a sharp sword, he hid me in the shadow of his hand. He made me into a sharpened arrow and concealed me in his quiver.
3 He said to me, 'Israel, you are my servant, through whom I shall manifest my glory.'
4 But I said, 'My toil has been futile, I have exhausted myself for nothing, to no purpose.' Yet all the while my cause was with Yahweh and my reward with my God.
5 And now Yahweh has spoken, who formed me in the womb to be his servant, to bring Jacob back to him and to re-unite Israel to him;-I shall be honoured in Yahweh's eyes, and my God has been my strength.-
6 He said, 'It is not enough for you to be my servant, to restore the tribes of Jacob and bring back the survivors of Israel; I shall make you a light to the nations so that my salvation may reach the remotest parts of earth.'

Responsorial Psalm, Psalms 71:1-2, 3-4, 5-6, 15, 17

1 In you, Yahweh, I take refuge, I shall never be put to shame.
2 In your saving justice rescue me, deliver me, listen to me and save me.
3 Be a sheltering rock for me, always accessible; you have determined to save me, for you are my rock, my fortress.
4 My God, rescue me from the clutches of the wicked, from the grasp of the rogue and the ruthless.
5 For you are my hope, Lord, my trust, Yahweh, since boyhood.
6 On you I have relied since my birth, since my mother's womb you have been my portion, the constant theme of my praise.
15 My lips shall proclaim your saving justice, your saving power all day long.
17 God, you have taught me from boyhood, and I am still proclaiming your marvels.

Gospel, John 13:21-33, 36-38

21 Having said this, Jesus was deeply disturbed and declared, 'In all truth I tell you, one of you is going to betray me.'
22 The disciples looked at each other, wondering whom he meant.
23 The disciple Jesus loved was reclining next to Jesus;
24 Simon Peter signed to him and said, 'Ask who it is he means,'
25 so leaning back close to Jesus' chest he said, 'Who is it, Lord?'
26 Jesus answered, 'It is the one to whom I give the piece of bread that I dip in the dish.' And when he had dipped the piece of bread he gave it to Judas son of Simon Iscariot.
27 At that instant, after Judas had taken the bread, Satan entered him. Jesus then said, 'What you are going to do, do quickly.'
28 None of the others at table understood why he said this.
29 Since Judas had charge of the common fund, some of them thought Jesus was telling him, 'Buy what we need for the festival,' or telling him to give something to the poor.
30 As soon as Judas had taken the piece of bread he went out. It was night.
31 When he had gone, Jesus said: Now has the Son of man been glorified, and in him God has been glorified.
32 If God has been glorified in him, God will in turn glorify him in himself, and will glorify him very soon.
33 Little children, I shall be with you only a little longer. You will look for me, and, as I told the Jews, where I am going, you cannot come.
36 Simon Peter said, 'Lord, where are you going?' Jesus replied, 'Now you cannot follow me where I am going, but later you shall follow me.'
37 Peter said to him, 'Why can I not follow you now? I will lay down my life for you.'
38 'Lay down your life for me?' answered Jesus. 'In all truth I tell you, before the cock crows you will have disowned me three times.'

Matendo ya huruma na toba ya kweli!


Mwilisheni matendo ya huruma: kiroho na kimwili katika maisha yenu ya kila siku! - RV
Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania katika ujumbe wake wa Kwaresima kwa Mwaka 2016 linatafakari kwa kina na mapana kuhusu huruma ya Mungu; ufunuo wa huruma ya Mungu kwa mwanadamu; Kanisa na huruma ya Mungu. Leo katika Makala ya Hazina Yetu, Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican inaendelea kukushirikisha kuhusu matendo ya huruma: kiroho na kimwili; umuhimu wa toba ya kweli, Bikira Maria Mwenyehuruma na hatimaye, hitimisho la Ujumbe wa Kwaresima kutoka kwa Maaskofu Katoliki Tanzania.
 
Matendo ya huruma
“Iweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma”. Kristo Bwana wetu anatufundisha na kututaka kuwatendea wanadamu wote kwa mapendo na huruma. “Kama Baba yenu”. Hiki ndicho kipimo. Mungu ndiye kipimo cha upendo na huruma ambao wanadamu wanaalikwa kuudhihirisha katika maisha yako. Tunapowatendea wenzetu matendo ya huruma tunamtendea Kristo mwenyewe anayetueleza uwepo wake kwao. “Kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitenda mimi (Rej. Mt 25:40). Mapendo na huruma yakikristo si ya vionjo bali ya hitaji. Mungu anatupenda sisi si kwa sababu tunavutia, bali tunavutia kwa sababu anatupenda na kutuhurumia daima (Rej. Kum 6:5, Law 19:8). Hivi tunapopendana kuhurumia jirani zetu, tunawafanya wavutie na kupendeza na tunaufanya uumbaji uvikwe kwa sura yake ya uhalisia wa awali inayovutia.
Mapendo kwa jirani yana msingi wake katika kumpenda Mungu. Ndiyo maana Yesu anasisitiza kuwa, kumpenda Mungu kuende sambamba na kumpenda jirani (Rej. Mt 22:39). Jirani ni mtu yeyote, mhitaji. Mfano wa Msamaria mwema unasisitiza fundisho hilo (Rej. Lk 10:25-37). Na sheria yote na manabii inategemea amri hiyo ya Mapendo (Rej. Mt 22:40). Kumpenda Mungu ina maana pia kupenda vyote vinavyopendwa na Mungu. “Kwahiyo, huruma kwa masikini na wagonjwa, vilevile matendo ya huruma ya ujima, yenye lengo la kupunguza kila aina ya dhiki za wanadamu, yanaheshimiwa na Kanisa kwa namna ya pekee… Utendaji wa huruma leo waweza kuwaelekea watu wote kabisa na mahitaji yao, na lazima uwe wa namna hiyo. Kila mahali wapo watu wenye kukosa chakula, na kinywaji, mavazi, makao, madawa, kazi na elimu, na vifaa vinavyohitajika ili kuweza kuishi maisha yaliyo kweli ya kiutu. Wapo wanaohangaika katika dhiki au kwa sababu ya kukosa afya, wanaoteseka mbali na makwao au walio kifungoni, na hapo mapendo ya Kikristo lazima yawatafute na kuwapata, kuwaliwaza kwa uangalizi mkarimu na kuwainua kwa kuwapatia msaada.” 
Tunapenda basi kuwakumbusha tena mafundisho ya Kanisa letu juu yamatendo ya huruma ya mwili na ya roho. Mapokeo ya Kanisa letu yanatufundisha juu ya matendo saba ya mwili, ambayo Kanisa limechota toka Maandiko Matakatifu (Rej. Mt 25:36; Tobit 1:17).
(i) Kuwalisha wenye njaa
(ii) Kuwanywesha wenye kiu
(iii) Kuwavika wasio na nguo
(iv) Kuwakaribisha wasio na makazi
(v) Kuwatembelea wagonjwa
(vi) Kuwatembelea wafungwa
(vii) Kuwazika wafu.
Tukifanya hivyo, huruma ya Mungu itakuwa wazi kwetu na kwao. “Katika parokia zetu, jumuiya zetu, vyama vyetu vya Kitume na vikundi, katika maana kwamba popote alipo Mkristo; kila mmoja apate chemchemi ya huruma.” Kusoma, kutafakari na kusikiliza Neno la Mungu ni msaada mkubwa katika kutembea kwenye njia ya huruma. Pamoja na matendo hayo ya huruma ya mwili mapokeo ya Kanisa yanatufundisha pia kutenda matendo ya huruma ya roho yanayotupeleka kuwajibika katika:
(i) Kuwashauri wenye mashaka
(ii) Kuwafundisha wasiojua
(iii) Kuwafariji wenye huzuni
(iv) Kuonya wakosefu
(v) Kusamehe makosa
(vi) Kuvumilia wasumbufu
(vii) Kuombea wazima na wafu
Jamii yetu inajumuisha watu wenye uwezo mkubwa na wenye uwezo mdogo. Wengine ni wazee, watoto, wagonjwa na walemavu, n.k. Tunawahimiza walio na uwezo kuwasaidia wasio na uwezo. Haya ni makundi ya watu wanaotuzunguka kila siku na huu ni uhalisia wa maisha. Tujifunze kumwona Yesu katika wahitaji hawa na tutambue kuwa kila tunapowahudumia tunakuwa tunaliboresha hekalu la Roho Mtakatifu. Tukitumie kipindi cha Kwaresima mwaka huu kama fursa ya kujikumbusha mapokeo haya ya Kanisa na kiwe kipindi cha kuadhimisha na kung’amua huruma ya Mungu. Tukiyatenda matendo haya ya huruma tutakuwa tunadhihirisha huruma na upendo wa Mungu unaoendelezwa katika maisha yetu ya kila siku kupitia ukarimu wa kikristo. Huruma na upendo huenda pamoja.
Toba ya kweli
Mungu wetu ni mwingi wa huruma na mtakatifu. Ingawa anachukia dhambi, hamchukii mkosefu. Anatupokea kila tunaporudi kwake na kutubu. Tunawahimiza kuikimbilia Sakramenti ya Kitubio ili kila mkosefu anayetubu ajipatanishe na Mungu na Kanisa. Sakramenti ya Kitubio inatuwezesha kuugusa utukufu wa huruma ya Mungu. Toba ya kweli inatudai kujirekebisha na kubadilika, kuacha dhambi na kuepuka nafasi ya dhambi. Ili kupokelewa katika ufalme wa Mungu, mwanadamu ni lazima ageuke na kuachana na njia zake mbaya na kushikamana na tangazo la Yesu la ufalme wa Mungu. Hivyo toba ni dai la kwanza la Yesu kwa wale wanaotaka kushiriki katika utawala wa Mungu (Rej. Mt 21:28 – 32).
Toba ni nafasi ya kubadili hali na misimamo yetu mibovu; kama vile dhuluma, uonevu kwa wanyonge, mauaji na rushwa inayopoteza matumaini ya wanyonge. Tusikilize sauti za wanyonge na maisha yao, kwa haki na upendo. Tujue kuwa dhambi zetu hata zile nyepesi zinatuletea shida. Dhambi nyepesi zinadhoofi sha mapendo na kuzuia maendeleo ya kiroho katika zoezi la fadhila na maisha mema.Tuziungame nazo hizo pia! Tendo la upendo wenye huruma linakuwa na huruma kweli kweli, pale tunapojiridhisha na kujiaminisha kwamba wakati tunalitenda, vilevile, tunapokea huruma kutoka kwa watu wale tunaowatendea. Kama sifa hii ya kutoa na kupokea haipo,matendo yetu yatakuwa hayajastahili kuitwa matendo ya huruma; wala ule wongofu ambao Kristo alituonyesha kwa maneno na maisha yake, hata kufa msalabani, utakuwa haujakamilika; wala tutakuwa hatujashiriki katika chanzo cha ajabu cha upendo wenye huruma ambao yeye alitufunulia.”
SURA YA NNE: BIKIRA MARIA MAMA MWENYEHURUMA
Mapokeo ya Kanisa letu yanatupatia sala ya “Salamu Malkia”inatutafakarisha huruma ya Mungu kwa kumuangalia Mama yetu Bikira Maria, aliye tulizo katika mahangaiko yetu. Yeye aliepushwa na kila doa la dhambi; alikuwa wa kwanza kati ya wote na kwa namna ya pekee alifaidi ushindi ulioletwa na Kristo juu ya dhambi: alikingiwa kila doa la dhambi ya asili, na katika maisha yake yote ya hapa duniani, kwa neema ya pekee ya Mungu, hakutenda dhambi yoyote. Mama huyu alitumia vizuri uhuru wake akakubali kuwa Mama wa Mwana pekee wa Mungu, Yesu Kristo Bwana wetu. Kwa maisha yake amemwimbia Mungu sifa daima. Anatukumbusha pia kuwa huruma ya Mungu kwetu sisi wanadamu “hudumu kizazi hata kizazi” (Lk 1:50).
Mama Maria ameshiriki mpango wa ukombozi kwa kutustahilia uzima mpya wa Roho zetu. Maana “Bwana mwenyewe amekuja kumkomboa binadamu na kumtia nguvu akimwumba upya ndani yake na kumfukuza mkuu wa ulimwengu huu, aliyekuwa amemfunga katika utumwa wa dhambi.” Tunawahimizeni nyote kwa maombezi ya mama Bikira Maria kujibidisha kutenda mema ili kujijengea fadhila na kujipatia majina yenye sifa njema katika maisha. Tumuombe mama Bikira
Maria mwenye huruma awe msaada na mwombezi wetu katika juhudi zetu. Tujue kuwa Mama Bikira Maria ni mfano wetu wa namna ya kuwa mfuasi mwaminifu wa Kristo. Tuombe msaada wa maombezi ya Mama Bikira Maria ili tuweze kuwa wafuasi waaminifu wa kuonesha huruma ya Mungu kwa watu wote. Mtakatifu Bernardo anatuasa kumkimbilia Mama huyu akisema; “Ikiwa tunahofu kuikimbilia huruma ya Baba, tumgeukie Yesu Kristo aliyetwaa mwili wetu na Kaka yetu Mwenye Huruma. Na ikiwa kwa Yesu tunahofi a ukuu wa enzi ya Umungu wake, tunaweza kumkimbilia Maria Mama yetu na mtetezi wetu mwenye huruma, awasikilizae wanae kama Baba amsikilizavyo Mwana.”
HITIMISHO
Wapendwa Taifa la Mungu, kipindi cha Kwaresima ni cha kuitayarisha mioyo yetu kwa toba, kufunga, kusali, kutoa sadaka, na kutenda matendo mema ili kujiandaa kukumbuka Fumbo la Pasaka: yaani, mateso, kifo, na ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo.Tukumbuke pia kwa kushiriki msalaba wake, na kwa neema yake tutashirikishwa pia utukufu wa ufufuko wake. Ni kipindi cha kutafakari zaidi zawadi ya fumbo la ukombozi wetu na namna tunavyoshiriki upendo wa Kristo katika suala zima la ukombozi, kwa mjibu wa ubatizo wetu. Tuombe neema ili tujivike fadhila ya unyenyekevu tuweze kutenda vema na kiaminifu katika utumishi wetu. Yafaa tumwombe Mungu atujalie fadhila ya unyenyekevu ambayo inatusaidia kujitambua kuwa tu wadhambi na tukishajitambua hivyo yatupasa tufanye toba mara.Tunahitaji msaada wa Kristo aliye Bwana wetu mwenye huruma tukimkimbilia atusaidie. Tukaze nia ya kuishi kama watumishi wenye huruma.
Na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania.

Video: Hadithi ya Yesu Kristo

Daily Reading for Friday, March 18th, 2016



Reading 1, Jeremiah 20:10-13

10 I heard so many disparaging me, 'Terror on every side! Denounce him! Let us denounce him!' All those who were on good terms with me watched for my downfall, 'Perhaps he will be seduced into error. Then we shall get the better of him and take our revenge!'
11 But Yahweh is at my side like a mighty hero; my opponents will stumble, vanquished, confounded by their failure; everlasting, unforgettable disgrace will be theirs.
12 Yahweh Sabaoth, you who test the upright, observer of motives and thoughts, I shall see your vengeance on them, for I have revealed my cause to you.
13 Sing to Yahweh, praise Yahweh, for he has delivered the soul of one in need from the clutches of evil doers.

Responsorial Psalm, Psalms 18:2-3, 3-4, 5-6, 7

2 Yahweh is my rock and my fortress, my deliverer is my God. I take refuge in him, my rock, my shield, my saving strength, my stronghold, my place of refuge.
3 I call to Yahweh who is worthy of praise, and I am saved from my foes.
4 With Death's breakers closing in on me, Belial's torrents ready to swallow me,
5 Sheol's snares every side of me, Death's traps lying ahead of me,
6 I called to Yahweh in my anguish, I cried for help to my God; from his Temple he heard my voice, my cry came to his ears.
7 Then the earth quaked and rocked, the mountains' foundations shuddered, they quaked at his blazing anger.

Gospel, John 10:31-42

31 The Jews fetched stones to stone him,
32 so Jesus said to them, 'I have shown you many good works from my Father; for which of these are you stoning me?'
33 The Jews answered him, 'We are stoning you, not for doing a good work, but for blasphemy; though you are only a man, you claim to be God.'
34 Jesus answered: Is it not written in your Law: I said, you are gods?
35 So it uses the word 'gods' of those people to whom the word of God was addressed -- and scripture cannot be set aside.
36 Yet to someone whom the Father has consecrated and sent into the world you say, 'You are blaspheming' because I said, 'I am Son of God.'
37 If I am not doing my Father's work, there is no need to believe me;
38 but if I am doing it, then even if you refuse to believe in me, at least believe in the work I do; then you will know for certain that the Father is in me and I am in the Father.
39 They again wanted to arrest him then, but he eluded their clutches.
40 He went back again to the far side of the Jordan to the district where John had been baptising at first and he stayed there.
41 Many people who came to him said, 'John gave no signs, but all he said about this man was true';
42 and many of them believed in him.

A Prayer For My Family




O dear Jesus,
I humbly implore You to grant Your special graces to our
family.
May our home be the shrine of peace, purity, love, labor
and faith.
I beg You, dear Jesus, to protect and bless all of us,
absent and present, living
and dead.

O Mary,
loving Mother of Jesus,
and our Mother,
pray to Jesus for our family,
for all the families of the world,
to guard the cradle of the newborn,
the schools of the young and their vocations.

Blessed Saint Joseph,
holy guardian of Jesus and Mary,
assist us by your prayers
in all the necessities of life.
Ask of Jesus that special grace
which He granted to you,
to watch over our home
at the pillow of the sick and the dying,
so that with Mary and with you,
heaven may find our family unbroken
in the Sacred Heart of Jesus.

Amen.

Batarokota historia yake kwa ufupi!



Nyimbo hapo juu ni ya kisukuma iliyopitwa na Mama Nyamoko akiwa na Msanii Batarokota.

Mwazirishi wa blogu hii ni Paskal Linda  Mgundu maharufu  Batarokota Pichani kushoto alizaliwa 1974 Kijiji cha Kigamboni katika Hospitali Teule ya Kigamboni Mkoa wa Temeke jijini Dar es salaam. 

Batarokota kabila ni Msukuma kutoka kijiji cha Nyashigwe kilomita 35 kutoka jijini Mwanza kaskazini mwa nchi ya Tanzania.
Batarokota ni mtoto wa kwanza katika familia ya Baba na Mama Beatus Linda iliyopo Nyamhongolo kijijini katika jiji la  Mwanza, yenye watoto saba (7)  kwa majina ni Happy Linda ambae ni marehemu aliyefariki tarehe 9/Mai/2007 maeneo ya Mbagala jijini Dar es salaam(rest in peace sister Happy Linda), Naomi linda, Zakaria Linda (dj zhari),Yohana linda (y brain), Monical linda na Norbert Linda.
Batarokota ana mke na watoto wanne na alifunga ndoa Jumamosi ya tarehe 5/Machi/2011 katika kanisa Katoriki la Mtakatifu Partic la mjini Morogoro,Batarokota alifunga ndoa na Sara Abed Linda.Na kabla ya ndoa alifanikiwa kupata watoto wawili na wawili baada ya kufunga ndoa.
Watoto wanne wa Batarokota wakwanza alizaa na mchumba wake wa kwanza Saula Athony Kapama ambae kwa sasa ni marehemu aliyefariki tarehe 9/Agosti/2005 Sumve Matare kwa ajali ya Treni ya abiria iliyokuwa ikienda Dar essalaam, Saula Kapama alimwachia Batarokota mtoto mmoja jina Ng`wibis Linda ambae alizaliwa Agosti 2000 katika Dispensary ya St Michael  mtoto wa pili wa Batarokota ni Shija Paskal ambae alizaliwa Desemba 2006 katika Hospital ya Bugando jijini Mwanza, Batarokota alizaa mtoto na rafiki wake wa kike Ruti Fidel Kanuti na Mtoto wa tatu wa Batarokota ni mtoto wa kike Makrina Juliana ambae alizawa Novemba/ 2011 mjini Morogoro katika Hospital ya Morogoro amezaa na mke wake Sarah Dile Linda na wanne ni Telezia wa Yesu aliye zaliwa Desemba,2013

. 
ELIMU
Batarokota amesoma shule ya msingi Igoma, nakumaliza shule 1990 na alifanikiwa kuendelea na masomo ya sekondari 1991 katika shule ya sekondari Buswelu na kufanikiwa kumaliza mwaka 1994, baada kidato cha tano na sita Mweli Sekondari  1997.

Na mwaka 2010 Batarokota akufanikiwa kujiunga na  chuo cha Powercomputer kilichopo jijini Mwanza- Tanzania na kuahitimu masomo kutengeneza computer, tovuti, blogu, grafics, Logo design, video editing and production baada ya kumaliza masomo ya computer Batarokota aliendelea na masomo ya Computer Nchini - Kenya katika chuo cha Moi na kumaliza masomo ya Diploma miaka 3, 2013.

Na picha chini Batarokota akiwa ofisini kwake anakofanyia shunguli za design na kutengeneza matangazo.

BATAROKOTA  AMEFANYA SHOW MAENEO MENGI

Mwaka Novemba/1994 Batarokota alifanya show ya kuwaanga kidato cha nne katika shule ya Buswelu Sekondari na Mgeni rasmi alikuwa Hayati Paulo Bomani.Mwaka.

 Julai/1996 Batarokota alialikwa katika show ya kusaka mrembo wa Kigamboni Miss Kigamboni katika ukumbi wa CCM kivukoni .Katika show alikuwa wamealikwa wasanii Fune with Sanse kiongozi wao J- Mtambo na kundi lake la POSOJU.

Mwaka Agosti/1998 ,Batarokota alikalibishwa na kundi lake la G tha Dunia katika ukumbi wa Liberty Hall jijini Mwanza, siku hiyo walikuwa wanazindua singo ya wimbo wao 'upendo kwa mama' wasanii walio alikwa ni Mr 2, Dr KB, BWV, Makamanda wa Gola, Daz P, na wengine wengi.

Mwaka, 2004 Batarokota akiwa na kungi la G THA Dunia alialikwa pamoja na wasaniii H- Baba, J- Mo, Mr Paulo, Solo Thang, Vick Kamata na BWV. katika kufanya show kubwa iliyo fanyika katika uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini Tabora show hii iliandaliwa na Zizou Entertnment.

Mwaka2004 , 25,Desemba. Batarokota alialikwa yeye pamoja na msanii wa nyimbo za kiasili Mama Nyamoko (Suzana Nyamoko), kwenye show ya kuwaburudisha watu wa Geita siku ya kristimasi katika ukumbi wa Lake View Hotel .

Mwaka 2013,Machi, Batarokota amefanya show aliyo alikwa jijini Nairobi katika ukumbi wa Brokriny uliopo Gethorai 44 onyesho hili lilifadhiriwa na Princess Studio. 


MAISHA  
Kipaji cha Batarokota kilianza kuonekana toka akiwa shule ya msingi Igoma mwaka 1987, Akiwa shuleni alikuwa akicheaza ngoma za asilia kwenye kundi la shule na alikuwa akifundishwa na Mwalimu Matongo ambae nimarehemu na Mwalimu Mayuyu ambae kwa sasa ni mwana kwaya wa Mtakatifu Bakita katika kanisa la Romani Katoriki Igoma.

Wanafunzi ambao Batarokota anakumbuka walio kuwa wanacheza wote ngoma ni Tasi Kosinatantine, Paskal Makaka, Peter Makuke,Frimat Lyimo na wengine wengi.

Tarehe 9/Januari/1998, Batarokota alianziha kundi la mziki wa kurap jijini Mwanza kwa jina G THA Dunia, kundi hili G Tha Dunia lilikuwa ni moto wa kuotea mbali ambalo lilitikisha kanda ya Ziwa na lilikuwa likiundwa na Paskal linda a.k.a Batarokota, Juma Hassani a.k.a Big D na Danny Ngollo a.k.a Ngollo 2. Kundi hili lilifanikiwa kurekodi albamu nchini Kenya ambayo ilikuwa ikiitwa '' ONE DAY'' ambayo ilirekodiwa Agosti/1998 mjini Nairobi, Kenya katika studio ya SYNC SOUND STUDIO chini ya Producer Mahamud Omari a.k.a Mr M O .Album hii ya ''One Day'' ilikuwa imajazwa na nyimbo kumi ambazo ni 'one day' jina la albam, 'upendo kwa mama', 'kiama','ogopa 666' , 'nimzuri tu', 'baby shake', 'wenyewe kwa wenyewe', 'watoto kwanza' , 'total balaa' na 'majonzi'. 

Baada ya kukaa nalo kundi hilo Batarokota aliondoka na kuachana na kundi hili 2004 na kwenda Dermank kwa ajili ya kufundisha ngoma Wadenish.Tarehe15/,februari/2006 Batarokota alirejea kutoka Dermank na kuanzihsa kundi jipya liitwalo Watu wa Gola liliko jijini Mwanza, alianzisha kundi hili akiwa na Juma Hassani a.k.a Big D, Kundi hili Watu wa Gola walifanikiwa kurekodi nyimbo mbili 'Tumerudi' na 'vichwa vya kale' nyimbo hizi zimerekodiwa katika studio ya M.O. Record iliyopo Pasiasi jijini Mwanza chini ya mtayarishaji Q the Don na Dj Zari. 


TUZO  KATIKA SANAA
 Mwaka 2001 tarehe 4/Machi msanii Batarokota akiwa na kundi lake la G THA Dunia,Kundi hili walifanikiwa kupata zawadi ya cheti cha ushindi wa best single rap katika wimbo wa -upendo kwa mama- cheti hicho kilitolewa na Gloryhood Music Award ya jijini Mwanza .

Mwaka 2004,Octoba 22-23, Batarokota alifanikiwakupta cheti cha kuudhulia na kushiriki Music Crossroads Tanzania Workshops jijini Mwanza.

Mwaka 2014 msanii Batarokota alifanikiwa kuingia kwenye tuzo za Kilimanjaro Tanzania Music Award 2014 (KTMA 2014) kama nominiss katika kategori ya Wimbo bora wenye Vionjo vya Asili ya Kitanzania na wimbo wa kisukuma uitwao `Kwejaga Nyangisha` 


NYIMBO MPYA AKIWA NJE YA KUNDI 
 Batarokota kwa sasa ana nyimbo saba ambazo amesha kamilliza kwa ajili ya maandalizi ya albamu yake mpya atakayo zindua hivi karibuni yenye nyimbo  sita ambazo ziko tiyari ni 

` hongera mama` na  `amani` nyimbo hizi zimerekodiwa Mwaka 2003 Januari katika studio Mushroom Studio jijini Nairobi Kenya chini ya mtayarishaji Teddy Karanda Harrison na Dj Zari.

Nyimbo vingine ni `Sukurubu` ambayo imerekodiwa Multimedia Studio jijini Mwanza mtayarishaji Alon Mikomangwa wasanii walioshiriki kwenye nyimbo hii ni Ceni na Castro kutoka DRC, Kongo na nyimbo nyingineni `sauti ya haki` na `kwejaga Nyangisha` zimerekodiwa Januari,2012 studio ya Sky Studio iliyopo Kihonda Morogoro watayarishaji Orecy Owden na Julius Chares.

Nyimbo nyingine ni ya kisukuma ihitwayo `irombo rise`iliyo rekodiwa 6/Decemba/2012 katika studio za Sunlight Records Mazimbu road -Kihonda Morogoro mtayarishaji King Maroh.

KUINGIA KATIKA SIASA 
Msanii Batarokota ameingia rasimi katika siasa tarehe
18/08/2015 katika chama cha ATC-Wazalendo na kupata kadi namba 223643 alikabidhiwa kadi na Afisa wa Chama mkoani Morogoro Mjini-Tanzania

China na Marekani zaafiki vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini



Leo Rais wa Marekani Barack Obama ameidhinisha vikwazo vipya dhidi ya Korea Kaskazini baada ya taifa hilo kufanyia majaribio silaha za nyuklia na makombora hivi majuzi.
Msemaji wa ikulu ya White House amesema Marekani na jamii ya kimataifa hawatavumilia “shughuli haramu za nyuklia” zinazotekelezwa na Korea Kaskazini.
Awali, ikulu ya White House iliishutumu Korea Kaskazini ikisema inawatumia raia wa Marekani kama rahani katika juhudi za kuendeleza ajenda yake ya kisiasa.

Bw Otto Warmbier, mwenye umri wa miaka 21, alikiri kuiba bango la kisiasa katika hoteli alimokuwa akikaa pamoja na kundi jingine la watalii mjini Pyongyang.
Marekani imeitaka Korea Kaskazini kumwachilia huru mwanafunzi huyo mara moja.

Pope Francis' prayer intentions for March 2016

Jesus triumphant entry into Jerusalem [Palm Sunday]


By Adelaide Mena (CNA/EWTN News)
3/16/2016 (15 hours ago)
Catholic Online (www.catholic.org)
The feast commemorates Jesus' triumphant entry into Jerusalem the week before his passion.
With Palm Sunday right around the corner, Catholics across the globe will soon be handed leaves as they walk into church. Some might fold them into elaborate little crosses. Kids will poke each other with them. But it's safe to say most won't know where they came from. 
Washington D.C., (CNA/EWTN News) - The feast commemorates Jesus' triumphant entry into Jerusalem the week before his passion and crucifixion. The Gospels attest that as Jesus entered the city, crowds lay down palm branches and cloaks as he rode into Jerusalem on a donkey.

For centuries, Christians have commemorated the feast day that begins Holy Week by waving branches of either palm or another local tree, as well as with liturgical processions and other celebrations.

In the U.S. alone, nearly 18,000 Catholic parishes will celebrate Palm Sunday by blessing and distributing palm branches to the faithful. That makes millions of palm leaves each year - and that doesn't include all of the Protestant churches that observe the tradition.

Where do all those palms come from? While many Catholics know the final destination of their palms - they are burned to become ashes for next year's Ash Wednesday - the origin of the leafy branches is less well known.

The journey from tree to church begins with the harvesters around the world who cut and prepare the leaves for their role in worship. The work needed to provide palms for Palm Sunday is so immense that it actually constitutes a full-time year-round job for some harvesters.

Thomas Sowell is one such palm harvester from Florida who has been helping to supply parishes with fresh palm leaves for more than five decades. Sowell began harvesting wild palm leaves from trees as a child to earn extra money in the springtime. Over the past several decades, he has grown his business into a palm supplier that ships the leafy branches to all 50 states and Canada.

Despite the growth in his business, Sowell says he tries to maintain his focus on the purpose behind it all.

"We try to do the best job that we can," he told CNA. "Every bag that we send out to churches, every individual bag has been examined, cleaned - we go to extreme measures to make sure that everything we do for these churches is done in the honor of Jesus Christ."

While there are more than 2,600 different species of palm that grow across the world, palm plants cannot survive outside of tropical and subtropical climates. Historically, parishes that could not source palm locally would instead substitute branches of another local tree such as olive or willow, although modern churches also have the option of sourcing palm fronds from other regions of the world.

In the United States and Canada, most parishes seek out suppliers who deliver fresh palms shortly before Palm Sunday, said Fr. Michael J. Flynn, Secretariat of Divine Worship for the U.S. Conference of Catholic Bishops.

Many of these parishes contact church goods suppliers such as Peter Munley of Falls Church, Virginia, who helps provide parishes year-round with supplies like candles and sacramental wine, along with palms for Holy Week.

Munley told CNA that in preparation for Palm Sunday, he works to deliver palms from their source to different parishes that place orders around the country. In addition to Florida, palms are sourced from Texas, California and elsewhere in the Southern United States, he said.

While nearly all of the palms Munley sells are individually pre-cut, church goods suppliers also helps to source decorative palms for altar centerpieces and larger palm fronds as well. Dealers also work to ensure that palms get burnt and ground into ashes for Ash Wednesday, for parishes that cannot burn the palms for ashes themselves.

Daily Reading for Thursday, March 17th, 2016 HD




Reading 1, Genesis 17:3-9
3 And Abram bowed to the ground. God spoke to him as follows,
4 'For my part, this is my covenant with you: you will become the father of many nations.
5 And you are no longer to be called Abram; your name is to be Abraham, for I am making you father of many nations.
6 I shall make you exceedingly fertile. I shall make you into nations, and your issue will be kings.
7 And I shall maintain my covenant between myself and you, and your descendants after you, generation after generation, as a covenant in perpetuity, to be your God and the God of your descendants after you.
8 And to you and to your descendants after you, I shall give the country where you are now immigrants, the entire land of Canaan, to own in perpetuity. And I shall be their God.'
9 God further said to Abraham, 'You for your part must keep my covenant, you and your descendants after you, generation after generation.

Responsorial Psalm, Psalms 105:4-5, 6-7, 8-9

4 Seek Yahweh and his strength, tirelessly seek his presence!
5 Remember the marvels he has done, his wonders, the judgements he has spoken.
6 Stock of Abraham, his servant, children of Jacob whom he chose!
7 He is Yahweh our God, his judgements touch the whole world.
8 He remembers his covenant for ever, the promise he laid down for a thousand generations,
9 which he concluded with Abraham, the oath he swore to Isaac.

Gospel, John 8:51-59

51 In all truth I tell you, whoever keeps my word will never see death.
52 The Jews said, 'Now we know that you are possessed. Abraham is dead, and the prophets are dead, and yet you say, "Whoever keeps my word will never know the taste of death."
53 Are you greater than our father Abraham, who is dead? The prophets are dead too. Who are you claiming to be?'
54 Jesus answered: If I were to seek my own glory my glory would be worth nothing; in fact, my glory is conferred by the Father, by the one of whom you say, 'He is our God,'
55 although you do not know him. But I know him, and if I were to say, 'I do not know him,' I should be a liar, as you yourselves are. But I do know him, and I keep his word.
56 Your father Abraham rejoiced to think that he would see my Day; he saw it and was glad.
57 The Jews then said, 'You are not fifty yet, and you have seen Abraham!'
58 Jesus replied: In all truth I tell you, before Abraham ever was, I am.
59 At this they picked up stones to throw at him; but Jesus hid himself and left the Temple.

Ziara Ya Rais Magufuli Arusha

Magufuli aapisha wakuu wa Mikoa, awaonya


RAIS Dk John Pombe Magufuli amewaapisha wakuu wa mikoa aliowateua hivi karibuni na kuwapa maagizo mazito. Rais amewaambia wakafanye kazi ya kutatua kero za wananchi na sio kwenda kufanya siasa.
Katika hotuba yake fupi kwao, Rais amewapa wakurugenzi wa halmashauri siku 15 wawatoe katika Orodha ya Malipo ya Mshahara (Pay Roll) wafanyakazi hewa wote katika halmashauri zote nchini.
Ameonya kuwa halmashauri yoyote baada ya muda huo itakayokuwa na mfanyakazi hewa, mkurugenzi wake atakuwa amejifuta kazi mwenyewe.
Vilevile Rais amewaagiza mawaziri wokati wowote kuwaeleza watendaji wao wawaondoe wafanyakazi hewa wote ndani ya kipindi hicho cha siku 15 na kubainisha kuwa watakaoshindwa kutekeleza agizo hilo watafukuzwa kazi kwani sheria ni msumeno.
Rais ameeleza matumaini yake kuwa kupitia kwa wakuu hao wa mikoa, kero nyingi zitamalizwa na wananchi watakuwa huru katika nchi yao. Baadhi ya kero ambazo Rais amezigusia ni migogoro ya wafugaji na wakulima, ukosefu wa usalama barabarani hadi mabasi kusindikizwa na polisi pamoja na tatizo la njaa.

Jua lanaswa na mwezi Indonesia

Raia Indonesia wameshuhudia jua likizibwa kikamilifu na mwezi.

wiki hii siku ya tarehe 9 Marchi 216 Indonesia ndio nchi pekee iliyoshuhudia tukio hilo kote duniani.
Hoteli zilizopo katika maeneo mazuri ya kushuhudiwa jua likinaswa zilijaa miezi kadhaa iliopita na katika baadhi ya maeneo ilibidi maafisa watafute nafasi za ziada kwa watalii waliokuwa kwenye maboti.
Katika kisiwa cha Belitung mamia ya wageni na watalii wa nchni walikusanyika katika fukwe za bahari kabla ya alfajiri. Wakati jua lilipoanza kunaswa na mwezi walishangilia na baadaye kunyamaza kimya kwa mshangao.
Wengi wamelielezea tukio hilo kama 'tukio la miujiza'. Kwa wengi Indonesia, tukio hilo linashirikishwa sana na dini na watu huomba, sherehe za kitamaduni na ngoma zimeandaliwa katika sehemu kubwa la eneo hilo.
Wanasayansi pia wamkuwepo hususan katika eneo la Maba katika visiwa vya Maluku ambako tukio hilo limeshuhudiwa kwa dakika tatu, ambao ni muda mrefu kuwahi kushuhudiwa jua likinaswa na mwezi.

Korea Kaskazini kufanyia majaribio nyuklia!


Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un ametangaza kwamba taifa hilo litafanyia majaribio silaha za nyuklia na makombora ya masafa marefu karibuni.

Amesema majaribio hayo yataimarisha uwezo wa taifa hilo kutekeleza mashambulio ya nyuklia, vyombo vya habari vya serikali nchini humo vimeripoti.

Putin aagiza jeshi lake kuondoka Syria

Urusi ni mshirika wa karibu sana wa rais wa Syria Bashar al-Assad.
Rais wa Urusi Vladimir Putin ametoa amri kwa wanajeshi walioko Syria kurejea nyumbani mara moja kwa sababu tayari wametekeleza asilimia kubwa ya malengo yao.Akizungumza katika ikulu ya Kremlin Putin, alisema

TAARIFA ZA HIVI PUNDE;RAIS MAGUFULI ATANGAZA WAKUU WA MKOA WAPYA!



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa wakuu wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara, ambapo kati yao 13 ni wapya, 7 wamebakizwa katika vituo vyao vya kazi, 5 wamehamishwa vituo vya kazi na 1 amepangiwa Mkoa Mpya wa Songwe.