Week Hot newz

Padri atahadharisha ndoa za jinsia moja, uzazi wa mpango


Geita
Imeelezwa kuwa kuna hatari ya familia kwa nchi zinazoendelea ikiwamo Tanzania kufikia ukomo wa ustawi na furaha na pamoja na kujenga taifa lisilo na uhai wa nguvu kazi na lenye maadili kutokana na ndoa za jinsia moja zinazoshika kasi katika mataifa ya Ulaya na Amerika.

Padri wa Kanisa Katoliki nchini amesema kuwapo kwa mazingira hayo matokeo yake ni watu kukoma kuzaa watoto na kukosa familia.

Familia ina dhamana kubwa kwa Kanisa na Jamii, ingawa inakabiliwa na changamoto nyingi!



Maadhimisho ya Siku kuu ya Familia Takatifu ya Yesu, Maria na Yosefu ni kielelezo cha upendo mkuu ambao Mwenyezi Mungu amemwonesha mwanadamu kwa kutaka Mwanaye wa Pekee, Yesu Kristo azaliwe katika familia ya binadamu, akiwa na Baba na Mama kama binadamu mwingine yoyote yule!

Liturujia ya Neno la Mungu inaonesha jinsi ambavyo Familia Takatifu ilivyoteseka hadi kukimbilia uhamishoni Misri ili kuokoa maisha ya Mtoto Yesu

Sherehe ya Familia Takatifu ya Yesu, Maria na Yosefu



Mpendwa mwana wa Mungu, leo tunasherehekea na kushangilia sherehe ya familia Takatifu. Masiha amezaliwa ndani ya familia hii. Ndani ya familia hii kuna majukumu ya kutekeleza ili Mwana wa Mungu akae mahali stahili na kwa namna hiyo atufundisha namna ya kutenda na kuishi kwenye familia zetu.

Somo la kwanza toka kitabu cha Hekima ya Yoshua bin Sira linaweka mbele yetu fahari na heri ya kuwaheshimu wazazi na kuwatunza katika uzee wao. Heri ambazo ziko wazi kadiri ya somo hili ni kuwa na uzao, na si uzao tu bali kufurahia uzao huo. Kuwa na maisha marefu na uzee wa kusifika. Kwa kuwatunza wazazi na kuwapa heshima stahili mmoja afanya malipizi ya dhambi zake. Kwa hakika somo hili lasisitiza na kuweka mkazo juu ya amri ya nne ya Mungu. Waheshimu baba na mama upate miaka mingi na heri duniani

Viongozi wa serikali waombewa msamaha kwa Mungu

28th December 2013

Waumini wa huduma ya Mtakatifu Prince Mission yenye Makao Makuu yake Sinza jijini Dar es Salaam, wameomba msamaha wa Mungu kwa baadhi ya viongozi  wa umma kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni kuusaliti umma wanaoungoza.

Hatua hiyo inatokana na matumizi ya misahafu wanapokula viapo vya kuutumikia umma, kisha kutotimiza azma hiyo badala yake kujinufaisha binafsi na ‘kuwaangamiza’ raia wanaowachagua.

Papa mstaafu Benedikto XVI apata chakula cha mchana na Baba Mtakatifu Francisko



Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI, Ijumaa, tarehe 27 Desemba 2013 amemtembelea Papa Francisko na kupata chakula cha pamoja kwenye Hosteli ya Mtakatifu Martha iliyoko mjini Vatican.

Francis prepares to celebrate first Christmas as Pope


Pope Francis marks his first Christmas as leader of the world's Roman Catholics on Tuesday and Wednesday, with crowds of pilgrims expected to attend the annual celebrations in the Vatican.


"Like the Virgin Mary, the Church this week is expecting a birth," the pope said on Monday in the homily at one of his daily masses in the Vatican residence, where he has been staying since his election in March.
"Is there space for the Lord or is there space only for parties, shopping and making noise?" he asked.
The Christmas festivities begin with the unveiling on St Peter's Square of a traditional Nativity scene named in honour of Latin America's first ever pontiff at 1530 GMT.
The 77-year-old Francis is expected to watch the ceremony from the window of the Apostolic Palace overlooking the square and light a candle for peace.
Then from 2030 GMT the Argentine will celebrate the solemn Christmas Vigil mass in St Peter's Basilica.
On Wednesday, Francis delivers the "Urbi et Orbi" ("To the City and the World") blessing at 1130 GMT on St Peter's Square -- where he first appeared after his momentous election by fellow cardinals on March 13.
Popes often use their "Urbi et Orbi" blessings to announce specific prayers, for instance, for the victims of conflicts or for global economic justice.

Papa Francis atetea wanyonge wa vita


Papa Francis akipungia mkono waumini Vatikani
Katika hotuba yake ya mwanzo ya Krismasi, Papa Francis amezungumza mjini Rome juu ya maeneo ya vita duniani.
Alitoa wito kwa pande zote zilizohusika na vita vya Syria ziruhusu msaada kufika kwa wanyonge.
Alisema:
"Maisha mengi yamevunjika katika vita vya Syria na kuchochea chuki na kulipiza kisasi.

"Hakuna Krismas bila Mama... Bikira Maria"

Padre Faustin Kamugisha katika Kitabu chake cha "Hakuna Krismas bila Mama... Bikira Maria" anasema baraka zitasimama ikiwa kama Jamii itamsahau mama. Mama ni nambari moja na wala hana mpinzani. Hivi ndivyo ilivyokuwa kwa Bikira Maria Mama wa Mkombozi, siku moja Mama mmoja alipaza sauti akamwambia Yesu, "heri tumbo lililokuchukua na maziwa uliyonyonya"

Hizi ni sifa kwa Bikira Maria Mama wa Mungu, anayestahili kuheshimiwa hasa wakati huu, tunapoadhimisha Siku kuu ya Noeli. Mwenyeheri Yohane Paulo wa pili aliwahi kusema kwamba, wanawake ni walimu wa amani. Hawa ni wale wanaosimama kidete kupinga nyanyaso na kutoheshimiwa; ni watu wanaokumbatia Injili ya Uhai. Bikira Maria Mama wa Yesu, amepewa sifa ya kuitwa Malkia wa amani. Hii ni kutokana na ukweli kwamba, alitunza zawadi ya Uhai, changamoto kwa wanawake wote kusimama kidete ili kulinda na kutetea Injili ya Uhai.

Mama Theresa wa Calcutta aliwahi kusema kwamba, wavurugaji wa amani leo hii ni wale wanaokumbatia utamaduni wa kifo unaokumbatia sera za utoaji mimba na kutowajali wanyonge na watu wasiokuwa na mtetezi. Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa ajili ya Siku ya Kuombea Amani kwa Mwaka 2014 anasema, Fumbo la Msalaba linawawajibisha binadamu kutaabikiana na kusumbukiana katika maisha kwani udugu unazima vita na madhara yake; udugu unaponya na kuganga mapungufu ya binadamu.

Kipindi cha Noeli kiwasukume wanawake kutolea ushuhuda wa sifa njema za kimama, kwa kuiga mfano wa Bikira Maria. Umama ni kazi nzito kama ambavyo aliwahi kusema Mwenyeheri Yohane Paulo wa Pili; kwani hawa ni wadau wakuu wa matunzo na makuzi kwa watoto wao: kiroho na kimwili. Mwanamke anayetunza watoto wake nyumbani kwa imani na mapendo makuu anafanya kazi halisi na yenye thamani kubwa katika Jamii. Wanawake wawe mstari wa mbele kutangaza Injili ya Uhai kwa njia ya ushuhuda wa maisha yao; na kwa kutimiza nyajibu zao kwa Familia na Jamii na Jamii pia ioneshe hali na moyo wa kuwajali na kuwasaidia wanawake.

Bikira Maria awe ni mfano wa tunza bora ya kimama kwa watoto kama alivyofanya kwa Mtoto Yesu, tangu alipozaliwa hadi pale aliposimama chini ya Msalaba akamwona Mwanaye akihitimisha kazi ya Ukombozi. Bikira Maria ni mwanamke wa imani na mfano bora wa kuigwa. Kwa kumwangalia Bikira Maria, mwamini anaweza kujifunza tena kujiachilia mikononi mwa Mwenyezi Mungu; ni Mama wa Matumaini hata pale ambapo hakuna tena cheche za matumaini.

Kwa kumwangalia Bikira Maria, waamini wajifunze kumpenda Mtoto Yesu na kwa njia hii, Bikira Maria anakuwa kweli ni Mama wa Mungu na Kanisa. Hongera Bikira Maria kwa kutuzalia Mtoto mwanaume, mwenye Ufalme na uku
u mabegani mwake!

Tafakari ya Neno la Mungu, Siku kuu ya Noeli, 2013

Mpendwa mwanatafakari, kwanza ninakutakieni heri na baraka tele za kuzaliwa Mwana wa Mungu.
Leo ni Krismas, ni Noeli, ni neema ya Mungu iliyofunuliwa kwa ulimwengu mzima. Kwa hakika ile ahadi ya Mungu aliyoitoa tangu zamani sasa imefunuliwa na hivi tunafurahi na kushangilia tukiimba utukufu kwa Mungu juu na amani duniani kwa watu wenye mapenzi mema. Mtoto Emanueli aliye na uweza wa kifalme mabegani mwake, Mungu pamoja nasi amezaliwa kwa ajili yetu. Kanisa duniani kote linaimba “pangoni Batlehemu amezaliwa Mtoto Yesu, twendeni sote tukamwone na kumpa zawadi”

MERRY CHRISTMAS – HERI KWA NOELI!


Kristmas ni Birthday ya mmoja katika UTATU aliyetumwa kufanya kazi kwenye sayari hii inayoitwa dunia. Hebu tujaribu kupiga twasira. Siku moja, huko mbinguni kulikuwa na mkutano wa Halmashauri kuu ya Utatu Mtakatifu.

Ajenda kuu ya mkutano ilihusu kuizungumzia sayari dunia. Hasa kutokana na mabadiliko makuu yaliyokuwa yanajitokeza hapa na pale baada ya uumbaji. Ikabidi

Ombi la Papa Francisko kwa niaba ya familia zisizo na nyumbani.



Baba Mtakatifu Francisko , Jumapili iliyopita, baada ya sala ya Malaika wa Bwana, alitoa ombi kwa watu wote, binafsi, Taasisi, Makampuni na mamlaka, kujali mahangaiko na mateso ya watu wasiokuwa na makazi maalum yaani wasiokuwa na nyumbani. Papa aliotoa ombi hili kwa niaba ya familia zisizo na makazi , mbele ya mahujaji na wageni waliokuwa wamekusanyika katika uwanja wa kanisa kuu la Mtakatifu Petro,Vatican.

Taarifa inabaini Papa alitoa wito huo kwa kuhamasishwa na

Maisha Mchanganyiko: Nani kama Mama!



Zikiwa zimebaki siku tatu, kuadhimisha tukio la Mama Bikira Maria kutuzalia Mtoto Yesu , Emannuel, Mkombozi wa Dunia, inafaa kwa wakati huu kumtafakari Mwanamke, mama mzazi, hadhi yake, wajibu wake na Kanisa lasema nini juu mwanamke mama mzazi.
Ni wazi kipindi cha Krismas, ni wakati wa hekaheka nyingi za katika jamii , na familia pia. Nyuso nyingi huonekana kuwa na furaha, na pia ndani ya familia, huonekana mshikamano zaidi, ambamo licha ya hamu ya kusubiri ibada ya kusisimua ya

Tafakari ya Neno la Mungu, Jumapili ya IV ya Kipindi cha Majilio



Hatuna budi kumshukuru Mungu kwa kutujalia tena siku nzuri kama hii na hasa tunapoijongea meza ya Neno lake. 

Ni Dominika ya IV ya Kipindi cha Majilio, tukikaribia kuzaliwa kwa Mwana wa Mungu, Mfalme wa amani, Mtoto Emanueli. Katika somo la kwanza tunapata kusikia kuwa Mungu atatoa ishara na hapa ndipo kuna mzizi na kiini cha masomo ya Dominika hii. Basi ishara yenyewe ni Mtoto Emanueli yaani Mungu pamoja nasi.

Mpendwa msikilizaji wa Neno la Mungu, katika somo la kwanza

West Ham yapeleka majanga Spurs.



West Ham wakipambana na Tottenham
Mabao mawili katika dakika 10 za mwisho yaliipa ushindi West Ham dhidi ya Tottenham na kuiwezesha kuingia nusu fainali ya kombe la Capital One ambapo itapambana na Manchester City. Tottenham walifungua mlango katika nusu ya pili wakati Emmanuel Adebayor alipofunga bao lake la kwanza tangu mwezi wa Mei.
Westham walisawazisha kupitia kwa Matt Jarvis na zikiwa zimesalia dakika tano mchezo huo kumalizika, Modibo

Mkalimani wa mazishi ya Mandela awa chizi


Thamsanqa Jantjie, mkalimani wa lugha ya ishara
Mkalimani wa lugha ya ishara katika siku ya mazishi ya kitaifa, ya aliyekuwa rais wa kwanza mzalendo wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, amelazwa katika hospitali ya magonjwa ya ya akili.
Mkalimani huyo anashutumiwa kutoa ishara ambazo hazikuendana na kile kilichokuwa kikiongelewa.
Thamsanqa Jantjie "anaweza kuwa na matatizo", amekaririwa mke wake Siziwe akisema hayo.
Wataalam wa lugha ya ishara wamemshutumu kwa

Noeli ni Siku kuu ya imani



Na Paskal Linda,Vatican.
19/12/2013
Baba Mtakatifu Francisko, Jumatano tarehe 18 Desemba 2013 amefanya mazungumzo na Papa mstaafu Benedikto XVI, ili kutakiana kheri na matashi mema kwa ajili ya Siku kuu ya Noeli na Mwaka Mpya wa 2014. Baba Mtakatifu amekumbusha kwamba,

Chelsea yachapwa na Sunderland


Sunderland imesonga mbele hatua ya nusu fainali ya michuano ya ya Kombe la Capital One baada ya kuichapa Chelsea mabao 2-1.
Chelsea ilimiliki mchezo huo kwa muda mrefu katika dakika zote 90, huku Chelsea ikipata goli kutokana na mchezaji wa Sunderland, Lee Cattermole kujifunga mwenyewe.
Chelsea walionekana kufuzu kucheza hatua ya nusu fainali hadi dakika za mwisho za mchezo,

Noeli iwe ni siku kuu ya imani na matumaini; mapendo na amani

Baba Mtakatifu Francisko katika Katekesi yake, Jumatano, tarehe 18 Desemba 2013, amewakumbusha waamini kwamba, siku hizi za mwisho mwisho za Kipindi cha Majilio ni mwaliko kwa waamini kujiandaa kiroho ili kumpokea Yesu anayezaliwa tena katika maisha yao.

Baba Mtakatifu anasema, Noeli ni Siku kuu ya furaha na matumaini kwa Mwenyezi Mungu ambaye ameamua kuja na kuishi kati ya watu wake kwa njia ya Mwanaye wa

Mzee Nelson Mandela alikuwa pia shujaa wa Tanzania

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa Baba wa Demokrasia ya Afrika Kusini, Mzee Nelson Mandela alikuwa pia kiongozi wa Tanzania, shujaa wa Watanzania na Baba wa wananchi wa Tanzania kama alivyokuwa kwa wananchi wa Afrika Kusini.

Aidha, Rais Kikwete amesema kuwa Tanzania na Afrika Kusini zina uhusiano wa kindugu na wa karibu sana kwa sababu ya kazi kubwa iliyofanywa na waanzilishi wa mataifa hayo mawili, Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na Mzee Mandela.

Maisha ya Mandela Afrika ya Kusini wanaikumbuka sana Tanzania

Wananchi wa Afrika ya Kusini wanaikumbuka sana Tanzania kutokana na mchango wake katika harakati za ukombozi kusini mwa Afrika, jambo ambalo limejenga urafiki na undugu wa dhati kati ya Afrika ya Kusini na Tanzania.

Tanzania chini ya uongozi wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ilikuwa mstari wa mbele katika mapambono dhidi ya ukoloni na utawala wa ubaguzi wa rangi Afrika ya Kusini kwa kuamini kwamba, binadamu wote ni sawa na Afrika ni moja.

Yesu Kristo ndiye kiini na chemchemi ya furaha ya kweli!

Baba Mtakatifu Francisko katika tafakari yake kwa Jumapili ya tatu ya Kipindi cha Majilio, anawaalika waamini na watu wote wenye mapenzi mema kufurahi kwani Noeli i karibu na kwamba, Kanisa linatumwa kutangaza Habari Njema ya Wokovu, hii ndiyo Injili. Kanisa si kimbilio la watu wenye nyuso za kukunjamana bali ni nyumba ya furaha! Kwa wale wenye majonzi wanaonja furaha ya kweli ndani ya Kanisa.

Furaha hii inatokana na utambuzi kwamba, mtu anapendwa

Chiefs banking on Madiba magic




Kaizer Chiefs will entertain the University of Pretoria at the FNB Stadium in an Absa Premiership match on Monday evening, kick-off at 8:30pm.
Chiefs racked up a third straight league victory when they beat Free State Stars 2-0 away from home in late November.
The Soweto giants are unbeaten at home this season, with four wins and two draws from six matches.
The Amakhosi are placed second on the Absa Premiership log with 21 points from 11 matches.
If they win their game against Tuks and log leaders Mamelodi Sundowns lose their derby match against SuperSport United on the same day, Chiefs will assume first place on the standings.

Mama Maria Nyerere,Kikwete wafunika mazishi ya Mandela


16th December 2013
Rais Jakaya Kikwete, akizungumza katika mazishi ya aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini, hayati Neson Mandela, yaliyofanyika katika kijiji cha Qunu nchini humo jana.
Rais Jakaya Kikwete na mjane wa Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere, jana walifunika kwenye ibada maalumu ya kumuaga aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, iliyofanyika kijijini kwake Qunu, Mashariki mwa Cape.

Tukio hilo lilitokea baada ya Rais Kikwete kupewa fursa ya kuzungumza kwenye ibada hiyo ambayo ilianza mapema

EMMANUEL ANORLD OKWI ATUA YANGA!!

Klabu ya Yanga SC imefanikiwa kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa kimataifa kutoka nchini Uganda Emmanuel Arnold Okwi ambaye alikua akiichezea klabu ya SC Villa ya Uganda.

Yanga SC imempata mshambuliaji huyo msumbufu kwa mabeki wengi kwa mkataba wa miaka miwili na nusu ambapo kwa sasa ataitumika klabu yake mpya ya watoto wa jangwani mpaka mwishoni mwa msimu wa 2015/2016.

Dirisha dogo la usajili nchini Tanzania limefungwa leo usiku Disemba 15, 2013 saa 6 usiku ambapo mabingwa wa kihistoria klabu ya Yanga wamekalilisha taratibu zote za usajili ikiwa ni pamoja na kupata hati ya uhamisho wa kimataifa maarufu kama ITC.

Usajili wa Emmanuel Okwi unaifanya timu ya Yanga kufikisha idadi ya wachezaji watano wa kimataifa wakiwemo mganda mwenzake Hamis Kiiza, Haruna Niyonzima, Mbuyu Twite na Didier Kavumbagu.

Uongozi wa Yanga unawaomba wanachama, wapenzi na washabiki kuwapa ushirikiano wachezaji wote wa zamani na wapya waliosajiliwa katika dirisha dogo la usajili.

Wachezaji wengine waliosajiliwa hivi karibuni katika kuimarisha kikosi cha Yanga ni mlinda mlango Juma Kaseja ambaye alikuwa mchezaji huru na Hassan Dilunga aliyesajiliwa kutoka timu ya Ruvu Shooting.

Baraka Kizuguto

Afisa Habari – Young Africans SC

Disemba 15, 2013.
Photo: BREEEEEEAKING NEEEEEEWWS!!!!

SASA NI RASMIIIIIIIIIIIIIIIIII!!  EMMANUEL ANORLD OKWI ATUA YANGA!!
>> Kweli mwenye pesa sio mwenzako!!
>> Hiini habari kwa mujibu wa Afisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto

Klabu ya Yanga SC imefanikiwa kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa kimataifa kutoka nhcini Uganda Emmanuel Arnold Okwi ambaye alikua akiichezea klabu ya SC Villa ya Uganda.
 
Yanga SC imempata mshambuliaji huyo msumbufu kwa mabeki wengi kwa mkataba wa miaka miwili na nusu ambapo kwa sasa ataitumika klabu yake mpya ya watoto wa jangwani mpaka mwishoni mwa msimu wa 2015/2016.
 
Dirisha dogo la usajili nchini Tanzania limefungwa leo usiku  Disemba 15, 2013 saa 6 usiku ambapo mabingwa wa kihistoria  klabu ya Yanga wamekalilisha taratibu zote za usajili ikiwa ni pamoja na kupata hati ya uhamisho wa kimataifa maarufu kama ITC.
 
Usajili wa Emmanuel Okwi unaifanya timu ya Yanga kufikisha idadi ya wachezaji  watano wa kimataifa wakiwemo mganda mwenzake Hamis Kiiza, Haruna Niyonzima, Mbuyu Twite na Didier Kavumbagu.
 
Uongozi wa Yanga unawaomba wanachama, wapenzi na washabiki kuwapa ushirikiano wachezaji wote wa zamani na wapya waliosajiliwa katika dirisha dogo la usajili.
 
Wachezaji wengine waliosajiliwa hivi karibuni katika kuimarisha kikosi cha Yanga ni mlinda mlango Juma Kaseja ambaye alikuwa mchezaji huru na Hassan Dilunga aliyesajiliwa kutoka timu ya Ruvu Shooting.
 
Baraka Kizuguto
 
 Afisa Habari – Young Africans SC
 
Disemba 15, 2013.

Papa Francisko mtu mashuhuri kwa Mwaka 2013

Baba Mtakatifu Francisko ameteuliwa na Gazeti maarufu la TIME kuwa ni mtu mashuhuri kwa Mwaka 2013. Akizungumzia uteuzi huu, Padre Federico Lombardi, msemaji mkuu wa Vatican anabainisha kwamba, Vatican kwa ujumla hakushangazwa na uteuzi huu, kwani kuna vielelezo makini vinavyoonesha mguso na mashiko tangu Baba Mtakatifu Francisko achaguliwe kuliongoza Kanisa Katoliki kama Khalifa wa Mtakatifu Petro.

Nelson Mandela amezikwa kimila



Hayati Mandela alikuwa kipenzi cha dunia nzima
Rais wa kwanza mzalendo wa Afrika Kusini Hayati Nelson Mandela amezikwa katika kijiji cha Qunu mkoa wa Cape Mashariki nchini Afrika Kusini.
Mjane wa Mandela Graca Machel pamoja na Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma walikuwepo katika hafla ya mazishi iliyohudhuriwa na jamaa za karibu wa familia ya Mandela pamoja na viongozi wengine wakuu.
Takriban watu 4,500 ikiwemo wageni wa kimataifa walihudhuria mazishi hayo ambayo yalikuwa ya mchanganyiko wa tamaduni za kale na mambo ya

Safari ya Mandela yaishia Kijiji cha Qunu!


Mandela daima alisema anataka kuzikwa nyumbani alikozaliwa Qunu
Kijiji cha Qunu ambako atazikwa Hayati Nelson Mandela, kinaomboleza kifo cha shujaa aliyetoka katika kijiji hicho Nelson Mandela.
Mazingira hapa ni ya kipekee, mchanganyiko wa nyumba za kisasa na za kitamduni ambazo mfano wake ni mizinga ya Nyuki.

Udugu ni silaha dhidi ya umaskini, rushwa na ufisadi;

Udugu ni msingi na njia ya amani; ndiyo kauli mbiu inayoongoza Maadhimisho ya Siku ya 47 ya Kuombea Amani Duniani, itakayofanyika tarehe Mosi, Januari 2014 sanjari na Maadhimisho ya Siku kuu ya Bikira Maria Mama wa Mungu. Huu ni ujumbe unaochota utajiri wake kutoka katika Maandiko Matakatifu pamoja na mang'amuzi ya mshikamano wa kidugu kati ya watu.

Tafakari ya Neno la Mungu, Jumapili ya tatu ya Kipindi cha Majilio

Tafakari masomo Dominika, ninafurahi tena kuwa nawe katika safari yetu ya Majilio tukijiandaa kwa ajili ya ujio wa Mwana wa Mungu. Ni wakati huu tunapoimba kwa furaha Masiha wetu njoo, ukatuokoe.
Tuko sasa Dominika ya tatu ya Kipindi cha Majilio ambapo Neno la Mungu linatualika kutambua kwa njia ya imani alama zinazomtambulisha Masiha. Tunapata kutafakari katika Injili juu ya wasiwasi wa Yohane Mbatizaji juu ya Masiha, kiasi kwamba anatuma wafuasi wake tokea gerezani wakamwulize Bwana wakisema, eti wewe ndiye Masiha tuliyemtarajia au tumngojee mwingine?
Yohane Mbatizaji anaingiwa na wasiwasi kwa sababu aliweka matumaini yake katika alama zisizo za kweli! Kwetu sisi yaweza tokea na inatokea mara kadhaa kutumaini katika bwana asiye mwenyewe! Kumbe leo mwaliko ni huo, yaani kuwa makini ili tusianguke katika mtego kama huo!
Mpendwa msikilizaji, alama ambazo zilisadikika na Yohane Mbatizaji na wafuasi wake ni kuwa Masiha ajaye atakuwa hakimu mkali atakayewapatiliza mbali wadhambi. Kinyume chake Masiha hafanyi hilo isipokuwa upendo kwao akitafuta kuwaokoa katika taabu yao hiyo. Mpendwa msikilizaji, kazi na wajibu wetu mkuu, ni kutambua wakati huo tukijiuliza daima, ni alama zipi zinazomtambulisha Masiha ambaye tunaimba kwa furaha tukisema uje kutuokoa!
Ndiyo kusema, alama za kweli tunazipata katika Somo la kwanza toka kitabu cha Nabii Isaya 35:1-6,10 akisema ndipo vipofu na viziwi watakapoona na kusikia, mwenye kupooza atarukaruka tena na bubu kuimba kwa furaha. Mara moja toka katika alama hizi tunagundua kuwa Masiha anakuja kwa ajili ya kuwaondoa walio katika taabu na kuwaweka huru. Taabu kwa kawaida ni tokeo la dhambi, yawezekana dhambi ya mtu binafsi lakini hasa dhambi kwa ujumla.
Mpendwa msikilizaji, katika hili tunaalikwa kuingia katika safari ya toba na uaminifu kwa Injili kama tusomavyo katika Injili ya Marko. 1:15. Katika toba na kuishi Injili tunafikia kwa namna ya pekee kabisa hatua ya kutambua alama zinazomtambulisha Masiha.
Jukumu la kuishi alama hizi linatuweka katika mazingira ya furaha na linatuonesha waziwazi kwamba utawala wa Masiha unaanza kukolea katika maisha yetu.
Mpendwa mwana wa Mungu, inawezekana ikajitokeza kukawa na kuchelewa katika utekelezaji, yaani kuishi toba na hivi tukaweza kukata tamaa, basi Mtume Yakobo anatutia moyo na tumaini akisema, kuweni na subira mpaka Bwana atakapokuja. Katika subira tunataka polepole kutenganisha uovu na ubaya ulio katika jumuiya na katika mtu awaye yote katika ubinafsi wake.
Katika subira Mtume Yakobo anatuonya daima kuachana na tabia ya kuhukumiana maana hakimu mwaminifu ni mmoja yaani Mfalme Masiha. Mtume Yakobo anatuonya katika subira kutambua kuwa safari ya wokovu lazima itazamwe kama mkulima anavyongojea mvua za masika na za vuli.
Mpendwa msikilizaji, kipindi cha Majilio ni kipindi cha neema, ni kipindi cha kupanda ili kujipatia mavuno hapo baadaye, na kwa hakika mavuno ni furaha ya moyo inayokamilishwa katika Yesu Kristu mfufuka ambaye atatufufua siku ya mwisho na kukaa naye katika kiti cha enzi pamoja na Baba mbinguni.
Nikikutakia majilio njema napenda kusema fikiria zaidi kuwalisha maskini na kuwahudumia wagonjwa katika jumuiya yako na jitahidi kuwa adui wa dhambi kila siku ya maisha yako. Mpendwa, hiyo ndiyo namna ya kuishi Majilio ya mwaka huu. Nakukumbusha tena hapo jirani kwako kuna mtoto ambaye amekosa ada ya shule msaidie na mfundishe namna ya kuitumia na zawadi yako kwa hakika ni mbinguni. Tumsifu Yesu Kristo na Bikira Maria.

Tafakari hii imeletwa kwako na Padre Richard Tiganya, C.PP.S.

Teacher handed 3 life sentences for rape

Colonel Jay Naicker said Nkosingiphile Hlekwayo, 50, raped the 11-year-old girl on three occasions in 2009. The court sentenced him on Wednesday.
 

A KwaZulu-Natal school teacher has been handed three life sentences by the Empangeni Regional Court for the rape of an 11-year-old pupil, police said on Friday.
Colonel Jay Naicker said Nkosingiphile Hlekwayo, 50, raped the 11-year-old girl on three occasions in 2009. The court sentenced him on Wednesday.
"The victim reported the matter to her parents and a case was opened at the Empangeni police station," he said.
"The Empangeni family, child protection and sexual offences unit took over the investigation that led to the arrest of the accused on the same day that the offence was reported."
He said Hlekwayo's family allegedly approached the girl's family and promised to pay them or give them cattle if they withdrew the case.
"The victim's parents refused to do so and they... allegedly received death threats. The victim was taken to a place of safety until the case was finalised."
Provincial police commissioner, Lt-Gen Mmamonnye Ngobeni welcomed the sentence and expressed her confidence in the judicial system.

Robin van Persie hatachezea Manchester United kipindi hiki

Robin van Persie 




Robin van Persie hatachezea Manchester United kipindi hiki cha mechi nyingi baada ya kupata jeraha la paja ambalo litamuweka nje mwezi mmoja, meneja David Moyes alisema Ijumaa.
"Robin Van Persie atakuwa nje mwezi mmoja. Alipata jeraha kwenye paja akipiga kona ambayo ilizaa goli (dhidi ya Shakhtar Donetsk on Tuesday)," Moyes aliambia kikao cha wanahabari kabla ya mechi yao ya Jumapili Aston Villa.
Mholanzi huyo, ambaye amefunga mabao saba katika mechi 11 za Ligi ya Premia msimu huu, alirejea baada ya kuuguza jeraha la mtoki wikendi iliyopita wakati wa

Arsenal ya lala kwa Man City 6-3

a
Man City
Manchester City, wametoa ujumbe mkali kwa mahasimu wao kwenye ligi ya Premier Arsenal baada ya kuwacharaza mabao sita kwa matatu.
Upande wa Manuel Pellegrini uliwacharaza Arsenal na kuziba pengo la pointi tatu.
Arsenal walilalamika wakitaka kupewa penalty moja ingawa kwa kweli Man City walikuwa wamejiandaa vilivyo dhidi ya Arsenal, huu ulikuwa kama upepo kwao.

Safari ya Mandela mwisho Kijiji cha Qunu


Jeneza la Mandela
Mwili wa hayati Nelson Mandela umepelekwa katika mkoa wa Eastern Cape kwa safari ya mwisho kabla ya kuzikwa siku ya Jumapili kijijini Qunu.
Idadi kubwa ya watu walifurika barabara angalau kumtupia jicho shujaa wao na kutoa heshima zao za mwisho.
Mandela aliyefariki tarehe 5/12/2013 atafanyiwa maziko ya kitaifa siku ya Jumapili tarehe 15/12/2013,

Jumuiya ya Kimataifa inaomboleza Kifo cha Tata Madiba!

Viongozi wa Jumuiya ya Kimataifa pamoja na wananchi wa Afrika ya Kusini wameanza kutoa heshima zao za mwisho kwa Tata Madiba kwa sala kutoka kwa viongozi mbali mbali wa kidini nchini Afrika ya Kusini. Mvua iliyokuwa inanyeesha imewazuia wananchi wa kawaida kufika uwanjani ili kutoa heshima zao za mwisho kwa Mzee Nelson Mandela, lakini mvua ni kielelezo cha baraka kwa makabila mengi Barani Afrika.

Siku ya pili heshima mwili wa Mandela


Jeneza lenye mwili wa Hayati Nelson Mandela
Waombolezaji nchini Afrika Kusini wanaingia siku ya pili katika zoezi la kutoa heshima za mwisho kwenye mwili wa Rais wa kwanza mweusi nchini Afrika Kusini Hayati Nelson Mandela.
Maelfu ya watu wamejipanga kwenye mistari wakisubiri kutoa heshima zao za mwisho kwenye mwili huo uliolazwa katika ikulu kwenye jengo la Muungano mjini Pretoria.

Madiba, kwa heri! Umekuwa ni daraja la upatanisho!


Mwili wa Marehemu Nelson Mandela, Siku ya Jumatano tarehe 11 Desemba 2013 umewasili mjini Pretoria ambako utakaa kwa muda wa siku tatu, ili kutoa nafasi kwa wananchi wa Afrika ya Kusini kutoka heshima zao za mwisho. Magari ya Polisi yaliusindikiza Mwili wa Tata Madiba kutoka kwenye Hospitali ya Kijeshi.

Wezi wavunja nyumba ya Askofu Tutu!


Desmond Tutu
Wezi wamevunja na kuingia nyumbani kwa Askofu mstaafu Desmond Tutu
Polisi wamesema wizi huo ulifanyika wakati bwana Tutu akiwa katika ibada ya Nelson Mandela Mjini Johannesberg.
Inaarifiwa Tutu aliibiwa vitu vyake wakati akiwa anahudhuria ibada maalum ya kumuaga Hayati Nelson Mandela siku ya Jumanne.
Aidha wameelezea kuwa uvamizi ulifanyika nyumbani kwake mjini Cape Town Ahamisi jioni baada ya kutoa hotuba katika ibada ya Mandela siku hiyo.
Ibada hiyo ilifanyika katika uwanja wa FNB mtaani Soweto.
Wizi na uvamizi wa nyumba za watu ni jambo la kawaida nchini Afrika Kusini ambako visa vya uhalifu viko juu sana.

Heshima za mwisho kwa mwili wa Mandela


Mwili wa Mandela ukisindikizwa na polisi Afrika Kusini
Viongozi mbali mbali pamoja na raia wa Afrika Kusini wanaendelea kutoa heshma za mwisho kwenye mwili wa aliyekuwa rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini Marehemu Nelson Mandela ambao umelazwa kwenye ikulu ya Afrika Kusini mji Mkuu wa Pretoria, ambapo utalala hapo kwa siku tatu.
Mwili ulichukuliwa katika msafara kutoka chumba cha maiti cha hosptali hadi kwenye jengo la Muungano.
Msafara wenye jeneza la Marehemu uliondoka mjini katika Hosptali ya jeshi muda mfupi siku ya jumatano. Jeneza lilibebwa kwenye gari maalum na kufunikwa bendera ya Afrika Kusini.
Wananchi walijipanga kando kando ya barabara lilipopitishwa jeneza kama ishara ya kutoa heshma za mwisho kwa mwili wa marehemu.
Msafara ulipita katika mitaa huku baadhi ya raia wakikimbia pembeni kwenye mstari wa askari wa

Kili Stars yafa, lakini kiwango


Picha kushoto ni Mshambuliaji wa Tanzania Bara, Mbwana Samata akiwatoka mabeki wa Kenya, Joackins Atudo (kulia) na Aboud Omar kwenye Uwanja wa Nyayo jana. Kili Stars ililala 1-0.

Licha ya timu ya Taifa ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) kumiliki mpira kwa dakika zote 90, imeshindwa kutinga fainali ya michuano ya Kombe la Chalenji baada ya jana kukubali kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Kenya (Harambee Stars).

Drogba, Eboue salute to Madiba sparks row

ANKARA - Turkey's sports minister lashed out on Monday at moves by the football authorities to punish two top Ivorian club players for paying homage to Nelson Mandela.
 
Emmanuel Eboue

Didier Drogba and Emmanuel Eboue have been threatened with disciplinary action by the Turkish Football Federation for violating a ban on wearing political slogans on T-shirts, triggering outrage on Twitter.
Turkish Sports Minister Suat Kilic called on the federation to review its decision against the two star players with Istanbul giants Galatasaray.
"I don't find it a healthy choice in terms of Turkey's image abroad and the two footballers' [freedom of] expression," he said.
Drogba removed his club shirt after a match at the weekend against SB Elazigspor to reveal a T-shirt that read "Thank You Madiba", using Mandela's clan name.
Teammate Eboue also honoured the South African anti-apartheid hero who died on Thursday with a T-shirt that said "Rest in Peace Nelson Mandela".

Obama scripts world farewell


"It is hard to eulogise any man... How much harder to do so for a giant of history, who moved a nation toward justice, and in the process moved billions around the world," Obama began, in a speech that placed Mandela in the pantheon of Mahatma Gandhi and Martin Luther King.


US President Barack Obama summed up the awed respect Nelson Mandela inspired around the world at a rain-drenched memorial in Soweto on Tuesday that hinted at the tension straining South African politics after his death last week.
"It is hard to eulogise any man... How much harder to do so for a giant of history, who moved a nation toward justice, and in the process moved billions around the world," Obama began, in a speech that placed Mandela in the pantheon of Mahatma Gandhi and Martin Luther King.

Mlango wa Bwana daima ni wazi na kutupatia tumaini



Hatupaswi kuhofia ukombozi wa Bwana , badala yake , ni kujiweka tayari kwa ajili ya ujio wake. Ni kuufungua mlango wa moyo na kumpokea kwa matumaini. Papa alieleza katika homilia yake wakati wa Ibada ya Misa, mapema asubuhi Jumanne, katika Kanisa dogo la Mtaktifu Marta hapa Vatican.

Papa alitafakari maneno ya somo la kwanza, kutoka Kitabu cha Nabii Isaya, ambamo Nabii Isaya anasema, "farijikeni enyi watu wangu, Bwana, yu karibu na watu wake, kuwatuliza ,na kuwapa amani". Papa ameeleza kazi hii ya kufariji, ina uwezo wa kubadili yote. Bwana, kweli ana uwezo wa kuviumba vyote upya .

Mama Maria Nyerere amsimulia Mandela





Maria Nyerere pichani ambaye ni mke wa aliyekuwa rais wa kwanza nchini Tanzania Mwalimu Nyerere, amesema Nelson Mandela ataendelea kukumbukwa kwa moyo wake wa kusamehe na kumtaja kwamba alikuwa ni zawadi ya dunia katika kuleta upendo na maridhiano.
Uhusiano kati ya familia ya Mwalimu Nyerere na ile ya Mzee Nelson Mandela umekuwa ni wa karibu kiasi kwamba familia yake inajiandaa kwenda kuhudhuria katika mazishi yatakayofanyika tarehe 15 mwezi huu.