Week Hot newz

Daily Reading for Thursday, March 17th, 2016 HD




Reading 1, Genesis 17:3-9
3 And Abram bowed to the ground. God spoke to him as follows,
4 'For my part, this is my covenant with you: you will become the father of many nations.
5 And you are no longer to be called Abram; your name is to be Abraham, for I am making you father of many nations.
6 I shall make you exceedingly fertile. I shall make you into nations, and your issue will be kings.
7 And I shall maintain my covenant between myself and you, and your descendants after you, generation after generation, as a covenant in perpetuity, to be your God and the God of your descendants after you.
8 And to you and to your descendants after you, I shall give the country where you are now immigrants, the entire land of Canaan, to own in perpetuity. And I shall be their God.'
9 God further said to Abraham, 'You for your part must keep my covenant, you and your descendants after you, generation after generation.

Responsorial Psalm, Psalms 105:4-5, 6-7, 8-9

4 Seek Yahweh and his strength, tirelessly seek his presence!
5 Remember the marvels he has done, his wonders, the judgements he has spoken.
6 Stock of Abraham, his servant, children of Jacob whom he chose!
7 He is Yahweh our God, his judgements touch the whole world.
8 He remembers his covenant for ever, the promise he laid down for a thousand generations,
9 which he concluded with Abraham, the oath he swore to Isaac.

Gospel, John 8:51-59

51 In all truth I tell you, whoever keeps my word will never see death.
52 The Jews said, 'Now we know that you are possessed. Abraham is dead, and the prophets are dead, and yet you say, "Whoever keeps my word will never know the taste of death."
53 Are you greater than our father Abraham, who is dead? The prophets are dead too. Who are you claiming to be?'
54 Jesus answered: If I were to seek my own glory my glory would be worth nothing; in fact, my glory is conferred by the Father, by the one of whom you say, 'He is our God,'
55 although you do not know him. But I know him, and if I were to say, 'I do not know him,' I should be a liar, as you yourselves are. But I do know him, and I keep his word.
56 Your father Abraham rejoiced to think that he would see my Day; he saw it and was glad.
57 The Jews then said, 'You are not fifty yet, and you have seen Abraham!'
58 Jesus replied: In all truth I tell you, before Abraham ever was, I am.
59 At this they picked up stones to throw at him; but Jesus hid himself and left the Temple.

Ziara Ya Rais Magufuli Arusha

Magufuli aapisha wakuu wa Mikoa, awaonya


RAIS Dk John Pombe Magufuli amewaapisha wakuu wa mikoa aliowateua hivi karibuni na kuwapa maagizo mazito. Rais amewaambia wakafanye kazi ya kutatua kero za wananchi na sio kwenda kufanya siasa.
Katika hotuba yake fupi kwao, Rais amewapa wakurugenzi wa halmashauri siku 15 wawatoe katika Orodha ya Malipo ya Mshahara (Pay Roll) wafanyakazi hewa wote katika halmashauri zote nchini.
Ameonya kuwa halmashauri yoyote baada ya muda huo itakayokuwa na mfanyakazi hewa, mkurugenzi wake atakuwa amejifuta kazi mwenyewe.
Vilevile Rais amewaagiza mawaziri wokati wowote kuwaeleza watendaji wao wawaondoe wafanyakazi hewa wote ndani ya kipindi hicho cha siku 15 na kubainisha kuwa watakaoshindwa kutekeleza agizo hilo watafukuzwa kazi kwani sheria ni msumeno.
Rais ameeleza matumaini yake kuwa kupitia kwa wakuu hao wa mikoa, kero nyingi zitamalizwa na wananchi watakuwa huru katika nchi yao. Baadhi ya kero ambazo Rais amezigusia ni migogoro ya wafugaji na wakulima, ukosefu wa usalama barabarani hadi mabasi kusindikizwa na polisi pamoja na tatizo la njaa.

Jua lanaswa na mwezi Indonesia

Raia Indonesia wameshuhudia jua likizibwa kikamilifu na mwezi.

wiki hii siku ya tarehe 9 Marchi 216 Indonesia ndio nchi pekee iliyoshuhudia tukio hilo kote duniani.
Hoteli zilizopo katika maeneo mazuri ya kushuhudiwa jua likinaswa zilijaa miezi kadhaa iliopita na katika baadhi ya maeneo ilibidi maafisa watafute nafasi za ziada kwa watalii waliokuwa kwenye maboti.
Katika kisiwa cha Belitung mamia ya wageni na watalii wa nchni walikusanyika katika fukwe za bahari kabla ya alfajiri. Wakati jua lilipoanza kunaswa na mwezi walishangilia na baadaye kunyamaza kimya kwa mshangao.
Wengi wamelielezea tukio hilo kama 'tukio la miujiza'. Kwa wengi Indonesia, tukio hilo linashirikishwa sana na dini na watu huomba, sherehe za kitamaduni na ngoma zimeandaliwa katika sehemu kubwa la eneo hilo.
Wanasayansi pia wamkuwepo hususan katika eneo la Maba katika visiwa vya Maluku ambako tukio hilo limeshuhudiwa kwa dakika tatu, ambao ni muda mrefu kuwahi kushuhudiwa jua likinaswa na mwezi.

Korea Kaskazini kufanyia majaribio nyuklia!


Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un ametangaza kwamba taifa hilo litafanyia majaribio silaha za nyuklia na makombora ya masafa marefu karibuni.

Amesema majaribio hayo yataimarisha uwezo wa taifa hilo kutekeleza mashambulio ya nyuklia, vyombo vya habari vya serikali nchini humo vimeripoti.

Putin aagiza jeshi lake kuondoka Syria

Urusi ni mshirika wa karibu sana wa rais wa Syria Bashar al-Assad.
Rais wa Urusi Vladimir Putin ametoa amri kwa wanajeshi walioko Syria kurejea nyumbani mara moja kwa sababu tayari wametekeleza asilimia kubwa ya malengo yao.Akizungumza katika ikulu ya Kremlin Putin, alisema

TAARIFA ZA HIVI PUNDE;RAIS MAGUFULI ATANGAZA WAKUU WA MKOA WAPYA!



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa wakuu wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara, ambapo kati yao 13 ni wapya, 7 wamebakizwa katika vituo vyao vya kazi, 5 wamehamishwa vituo vya kazi na 1 amepangiwa Mkoa Mpya wa Songwe.

Huruma ya Mungu inamwilishwa katika huduma ya upendo!


Huruma ya Mungu inamwilishwa katika huduma ya mapendo: kiroho na kimwili!
Siku ile iliyotangulia kuteswa kwake, Yesu aliwaosha mitume wake miguu, jambo ambalo halikumfurahisha Mtakatifu Petro kiasi cha kukataa kuoshwa miguu na Yesu. Lakini Yesu akamfafanulia maana yake, akiwataka wafuasi wake kujikita katika huduma ya upendo, kama kielelezo makini cha ushuhuda wa imani inayomwilishwa katika matendo! Yesu ni kielelezo cha hali ya juu kabisa cha

Germanwings: Madaktari watoe siri za marubani

  Rubani msaidizi, Andreas Lubitz, aliangusha makusudi ndege hiyo kwenye milima ya Alps.

Wachunguzi kutoka Ufaransa, wamependekeza sheria kali inayozuia madaktari kufichua siri za marubani wagonjwa iondolewe.Wanasema iwapo sheria hiyo isingelikuwepo , ajali iliyosababishwa na rubani mwenza aliyekuwa amezongwa na mawazo isingelitokea.

Braeking News: Al shaabab walimezima shambulizi la kuvizia la Marekani leo

Wenyeji wa eneo hilo wanasema waliamshwa na milio ya risasi na ndege za kivita zikitua na kuondoka

 Wapiganaji wa kundi la wanamgambo la Al shaabab walimezima shambulizi la kuvizia lililotekelezwa na makomando wa jeshi la Marekani usiku wa kuamkia leo.
Kwa mujibu wa Afisa mmoja wa ngazi ya juu jeshini ambaye hakutaka jina lake litajwe anasema kuwa shambulizi hilo lililotekelezwa na vikosi vya usalama la Marekani kwa ushirikiano na majeshi ya Somalia yalifanikishwa kwa kuruka kwa ndege za helikopta kwa kambi ya wapiganaji hao iliyoko Awdhegle, takriban kilomita 50 Kusini mwa Somalia.

Michezo: Samata kuiongoza Taifa Stars AFCON

Nahodha ni Mbwana Samatta (KRC Genk), 
 
Kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa ametangaza kikosi cha wa wachezaji 25 kwa ajili ya mchezo wa kuwania kufuzu kwa fainali za mataifa ya Afrika (AFCON) dhidi ya Chad.
Mechi hiyo imeratibiwa kusakatwa tarehe 23 Machi mjini Djamena.

Dunia" Atungwa mimba ya pacha na wanaume wawili!

Mke huyo wa mtu amejipata pabaya baada ya kugunduliwa kuwa alifanya mapenzi na mwaname wa kando aliyemdunga mimba 

 Mapacha wa kipekee wamezaliwa nchini Vietnam.najua unajiuliza mapacha si kawaida tu ?
La hasha .
Mapacha hawa imegunduliwa kuwa walitungwa na baba wawili tofauti !
Amini usiamini !

Aliyenyanyasa kingono mayatima Kenya afungwa

M!mishenari mmoja wa zamani kutoka nchini Marekani amehukumiwa miaka 40 jela kwa kuwanyanyasa kingono watoto mayatima katika nyumba moja nchini Kenya.Matthew Lane Durham mwenye umri wa miaka 21,alitekeleza ''kitendo hicho kiovu kwa watoto wasioweza kujitetea'',mahakama ya Marekani ilisema.

Sanders amshinda Clinton, Trump abwagwa

 Bw Sanders alishinda Kansas na Nebraska

Bernie Sanders amemshinda Hillary Clinton katika mchujo wa chama cha Democratic uliofanyika katika jimbo la Maine.
Baada ya 91% ya kura kuhesabiwa, seneta huyo wa Vermont ana 64%, huku Clinton akiwa na 36%.
Katika chama cha Republican, Marco Rubio ameshinda kwa urahisi mchujo katika eneo la Puerto Rico, na kumbwaga bilionea Donald Trump.

Breaking newz: Bomu la laptop lalipuka Somalia

Watu 6 wamejeruhiwa katika mlipuko uliotokea katika uwanja wa ndege ulioko mjini Beledweyne nchini Somalia.

Mbiu ya Imani: Watawa waliouwawa huko Yemen ni mashuhuda wa upendo!

Watawa wa Mama Theresa wa Calcutta waliouwawa huko Yemen ni mashuhuda wa upendo na wahanga wa utandawazi usiojali wala kuguswa na mahangaiko ya wengine!




Baba Mtakatifu anakaza kusema, hawa ni mashuhuda wa imani kwa nyakati hizi! Ni watu ambao hawawezi kuwa ni sehemu ya habari inayopewa uzito wa juu; kwa baadhi ya vyombo vya habari, hii si habari! Hawa ni watu wanaoyamimina maisha yao kwa ajili ya utume na maisha ya Kanisa. Ni wahanga wa mashambulizi ya kigaidi na kielelezo cha utandawazi usiojali wala kuguswa na mahangaiko ya wengine. Baba Mtakatifu anamwomba Mwenyeheri Mama Theresa wa Calcutta awasindikize watoto wake ambao wamekuwa ni mashuhuda wa upendo kwenye maisha ya uzima wa milele pamoja na kuombea amani na heshima kwa utakatifu wa maisha ya binadamu!

Pope Francis General Audience 2016.02.24

Bodaboda zapigwa marufuku!

Burundi imepiga marufuku bodaboda au pikipiki kuingia katikati mwa mji mkuu Bujumbura katika juhudi za kujaribu kupunguza mashambulio.Pikipiki hutumiwa sana kusafirisha watu na mizigo Bujumbura lakini sasa zimekuwa zikitumiwa kutekeleza mashambulio, meya wa Bujumbura Freddy Mbonimpa anasema.

Mtu mmoja aliuawa Jumatatu wiki hii watu waliokuwa wamepaki pikipiki waliporusha guruneti tatu.
Usalama umeimarishwa mjini humo tangu kutoka kwa mashambulio hayo na polisi wanapekua watu na magari, shirika la habari la AFP linasema.

“Polisi wamegundua kwamba wahalifu hubeba guruneti wakitumia mabegu au vikapu,
” Bw Mbonimpa anasema. Mwandishi wa BBC aliyeko Bujumbura Prime Ndikumagenge anasema marufuku hiyo itaathiri sana watu wanaosafiri kutoka eneo moja hadi jingine mjini.

Huwezi kutoka kusini mwa mji hadi kaskazini bila kupitia katikati mwa mji, anasema.
Machafuko yalizuka nchini Burundi Aprili mwaka jana Rais Pierre Nkurunziza, ambaye amekuwa uongozini tangu 2005, alipotangaza kwamba angewania urais kwa muhula wa tatu.
Watu 400 wamefariki na wengine 240,000 kutorokea nchi jirani tangu wakati huo.

Papa Francisko nchini Mexico

Majadiliano ya kiekumene yamechukua sura mpya kwa papa Francisko na Patriaki Kirill wa Moscow na Russia nzima kukutana.
Majadiliano ya kiekumene yamechukua sura mpya kwa papa Francisko kukutana na Patriaki Kirill wa Moscow na Russia nzima.
Mapambazuko mapya ya majadiliano ya kiekumene!
16/02/2016 14:43Baba Mtakatifu Francisko na Patriaki Kirill wa Moscow na Russia nzima wamekutana na kuzungumza pamoja na kutia sahihi Tamko la shughuli za kichungaji kwa Makanisa haya mawili, ili kuanza kuandika ukurasa mpya wa majadiliano ya kiekumene katika Millenia ya tatu ya Ukristo!

 

 
 Baba Mtakatifu akishiriki chakula cha mchana na familia ya Mungu nchini Mexico.
Baba Mtakatifu Francisko akiwa nchini Mexico, Jumatatu tarehe 15 Februari 2016 ametembelea Kanisa kuu la san Cristòbal de las Casa na kusali humo, ameshiriki chakula cha mchana pamoja na wawakilishi wa Familia ya Mungu nchini Mexico pamoja na kuzungumza na  kusali nao!

 

Baba Mtakatifu Francisko akiwa Mexico amesikiliza shuhuda za Injili ya familia.
Baba Mtakatifu Francisko akiwa nchini Mexico amesikiliza shuhuda wa Injili ya familia.

Mashuhuda wa Injili ya familia!

16/02/2016 10:42Baba Mtakatifu Francisko alipokutana na familia nchini Mexico amesikiliza shuhuda za watu waliotelekezwa na familia zao, lakini wakapata fursa ya kuonja huruma na upendo wa Mungu kwa njia ya Kanisa; amesikiliza mashuhuda waliokumbatia utamaduni wa kifo, leo hii wanashuhudia Injili ya uhai!

 


Baba Mtakatifu Francisko anawahimiza wananchi wa Mexico kujikita katika ushuhuda wa tunu msingi za Injili ya furaha!
Baba Mtakatifu Francisko anawahimiza wananchi wa Mexico kuwa ni mashuhuda wa Injili ya familia.

Iweni mashuhuda wa Injili ya familia na huruma ya Mungu!

16/02/2016 10:21Baba Mtakatifu anawaalika wanafamilia kuwa kweli ni mashuhuda wa Injili ya familia na vyombo vya huruma ya Mungu ili kuweza kupambana na changamoto mbali mbali zinazojitokeza katika maisha na utume wa familia; kwa kushinda upweke na kinzani za maisha!
Baba Mtakatifu Francisko akiadhimisha Ibada ya Misa Takatifu na wenyeji wa Chiapas, nchini Mexico
Baba Mtakatifu Francisko akiadhimisha Ibada ya Misa Takatifu na wenyeji wa Chiapas, nchini Mexico.

Onesheni ujasiri wa kuomba msamaha!

16/02/2016 10:02Baba Mtakatifu Francisko akiwa nchini Mexico anasema, umefika wakati wa kujenga na kudumisha udugu, haki, mshikamano na amani; kwa kutambua kwamba haya ni mambo msingi yanayowaunganisha binadamu kama watoto wateule wa Mungu dhidi ya nyanyaso, dhuluma na ubaguzi!
Maskini wanapaswa kujipanga vyema zaidi ili kupambana na ubaguzi kwa kushikamana ili kudumisha utu wao na kupata mahitaji msingi!
Maskini wanapaswa kujipanga vyema kwa kushikamana kutetea utu na heshima yao kwa kupinga ubaguzi na nyanyaso, ili kukuza utu na heshima yao pamoja na kujipatia mahitaji msingi ya maisha.

Changamoto za utunzaji bora wa mazingira nyumba ya wote!

15/02/2016 10:39Kardinali Peter Turkson, Rais wa Baraza la Kipapa la haki na amani anawapongeza wenyeji wa Mexico kwa kuonesha mwanga angavu katika kulinda na kutunza mazingira nyumba ya wote, sanjari na kuendelea kushikamana ili kupambana na changamoto za maisha ili kudumisha utu wao!

 

Baada ya Askofu mkuu Ivan Jurkovic kukamilisha utume wake nchini Russia ameteuliwa kuwa Mwakilishi wa kudumu wa Vatican UN, Geneva.
Baada ya Askofu mkuu Ivan Jurkovic kukamilisha utume wake kama Balozi wa Vatican nchini Russia, ameteuliwa kuwa mwakilishi wa kudumu wa Vatican kwenye ofisi za UN zilizoko Geneva, Uswiss.

Askofu mkuu Ivan Jurkovic ateuliwa kuwa Mwakilishi wa kudumu UN, Geneva

15/02/2016 10:24Askofu mkuu Ivan Jurkovic ameteuliwa kuwa Mwakilishi wa kudumu wa Vatican kwenye Ofisi za Umoja wa Mataifa zilizoko mjini Geneva ili kuchukua nafasi ya Askofu mkuu Silvano Maria Tomasi ambaye amekuwepo huko tangu mwaka 2003. Aliwahi kuwa Balozi wa Vatican nchini Ethiopia na Eritrea.

 

Baba Mtakatifu Francisko ametembelea Hospitali ya "Federico Gomez" Mexico kushukuru kwa huduma na kuwabariki watoto wagonjwa wa saratani!
Baba Mtakatifu Francisko ametembelea Hospitali ya "Federico Gomez" ili kushukuru kwa huduma makini zinazotolewa kudumisha Injili ya uhai pamoja na kuwaombea watoto wagonjwa katika shida na mhangaiko yao!

Papa Francisko kielelezo cha faraja na matumaini kwa wagonjwa!

15/02/2016 10:07Baba Mtakatifu Francisko, Jumapili tarehe 14 Februari 2016 ametembelea Hospitali ya "Federico Gomez" nchini Mexico ili kumshukuru Mungu kwa huduma inayotelewa kwa ajili ya watoto wagonjwa pamoja na kubariki kazi njema inayofanywa na wazazi pamoja na wahudumu wa sekta ya afya!

Pope Francis' prayer intentions for February 2016