
Wakati Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Ismail Aden
Rage akitarajiwa kutua nchini tarehe 22/11/2013 jioni, bodi ya wadhamini ya klabu hiyo
imetangaza kusitisha maamuzi ya kamati yao ya utendaji ya kumwengua
katika nafasi uenyekiti.
Jumanne Kamati ya Utendaji ya Simba iliyokutana Jumatatu bila uwapo kwa mwenyekiti (Rage) aliyekuwa Marekani, ilitangaza kumsimamisha Rage na makocha wa timu yao, Abdallah 'King' Kibadeni na msaidizi wake, Jamhuri Kihwelu 'Julio'.
Kamati hiyo iliamua timu kwa sasa iwe chini ya kocha wa timu ya vijana, Simba B, Seleman Matola ambaye atakuwa pia Msaidizi wa Kocha Mkuu mpya wa kigeni, Zdravok Logarusic, raia wa Croatia atakayetambulishwa Desemba Mosi, mwaka huu.