Week Hot newz


Zitto, Dk. Kitila waeleza siri zao

Zitto Kabwe (kulia) na mwenzake Dk. Kitila Mkumbo, ambao walivuliwa uongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wakizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), jijini Dar es Salaam jana.
Aliyekuwa  Mjumbe wa Kamati Kuu (CC) ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Kitila Mkumbo, amekiri kushirikiana na aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba, kuandaa waraka uliokuwa na mkakati wa kupata Mwenyekiti wa taifa wanayemtaka.

Dk. Mkumbo alitoboa siri hiyo na kusema mtu ambaye kwenye waraka walimtambulisha kama MM kuwa ni Zitto Kabwe na ndiye waliyekuwa wanamuandaa kuwania nafasi ya Mwenyekiti wa taifa.

Wakristu wanao teseka leo hii, ni ushuhuda

Jengeni matumaini kwa Bwana, hata katika hali ngumu, Papa amehimiza wakati wa Ibada ya Misa ya asubuhi Jumatatu hii katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta mjini Vatican. Papa alisisitiza kwamba Wakristo wameitwa kufanya maamuzi thabiti , kama yanavyo fundisha maisha ya mashahidi wa dini wa kila wakati. Hata leo, alibainisha, kuna wake kwa waume wanao teseka kwa sababu ya imani yao kwa Kristu. Na hivyo wao ni mfano kwetu wa kuiga, kwa ajili ya kupata nguvu za kujikabidhi kwa Bwana bila kujibakiza.
Papa aliendelea kufundisha kwamba, kumchagua Kristu, hakuna ukomo. Alieleza hilo akingalisha katika somo la Kitabu cha Nabii Daniel, na Injili : ambamo vijana Wayahudi watumwa katika mahakama ya Nebukadreza na mjane aliyekwenda katika hekalu kumwabudu Bwana. Katika kesi zote, Papa anaona, hapakuwa na ukomo wa hali. Mjane katika hali ya umaskini na vijana katika hali ya utumwa, wote walijikabidhi kwa Bwana . Mjane aliweka vyote alivyokuwa navyo katika hazina ya Hekalu, ambapo kwa vijana walibaki aminifu kwa Bwana, hata katika hatari ya maisha.
Papa aliendelea kusema, katika hali za wote, mjane na vijana – hawakujali hatari za maisha zilizokuwa mbele yao. Walimchagua Bwana kwa moyo moja, bila wasiwasi na bila upungufu. Kwao Bwana alikuwa ni juu ya yote juu. Walitambua Bwana wao ni Mungu na kwake walijikabidhi wenyewe. Na hii hawakufanya kwa sababu za kujitafutia sifa bandia , lakini walifanya hivyo kwa kutambua kwamba, Bwana ndiye mkuu wa yote. Walijua kwamba Bwana ni mwaminifu. Na ndivyo tunavyotakiwa nasi pia kufanya.
Ni kumtegemea Bwana kwa uaminifu na imani kwamba daima yupo, kwa sababu Bwana hawezi kubadilika kubadilika na kujikana mwenyewe. Imani hii katika Bwana Papa Francisko aliongeza, huongoza katika maamuzi thabiti ya kumchagua Yeye kuwa ndiye Bwana wa Yote, Yeye ni mwaminifu, katika katika mambo yote madogo , makubwa na hata magumu.

Papa alieleza na kuitazama historia ya kanisa kwamba, historia yake inaonyesha wanaume, wanawake, wazee, vijana, waliofanya uchaguzi huu, kama tunavyo sikia katika vyombo vya mawasiliano au kusoma katika magazeti juu ya maisha ya mateso yanayokabili hata leo hii, Wakristo katika maeneo mbalimbali duniani.

Wakristu hao wanaoishi nasi katika wakati huu, ni mfano hai kwetu, wenye kutuhimiza pia sisi, kuiweka hazina yetu ndani ya kanisa, ili kwamba, ambamo Bwana yumo ndani mwake. Ushuhuda wa Wakristu hawa wateswa, unashuhudia neema ya ujasiri wa kusonga mbele katika maisha ya Kikristo , katika hali ya kawaida , maisha magumu na hata katika mazingira hatarishi . Ni kuwa na Maamuzi thabiti kwa Bwana.

Marufuku kujisajili kwenye Ufalme wa Shetani!

Wapendwa wanafamilia ya Mungu, karibuni kwa tafakari ya Neno la Mungu, inayotujia tunapoadhimisha leo Sherehe ya Bwana wetu Yesu Kristo Mfalme. Mama Kanisa anatualika tumtafakari Kristo ambaye ni Mfalme wa Ulimwengu na pia kielelezo halisi cha Mfalme wa kweli ambaye ni tofauti na wafalme wa dunia hii.


Tofauti na miaka mingine, kwa mwaka huu adhimisho hili la Sherehe ya Kristo Mfalme linaambatana na hitimisho rasmi la Mwaka wa Imani. Hivyo ni nafasi nzuri kwetu kujikumbusha kuwa Imani ya kweli ni ile ambayo inajengeka katika Kristo Mwenyewe ambaye atatupa tuzo la kushiriki maisha katika ufalme wake wa mbinguni kadiri ile ambavyo tumejibidisha kuiishi imani yetu na kwa jinsi tulivyomruhusu awe Bwana na Mtawala wa maisha yetu.

Wakatekumeni wanaalikwa: kusikiliza kwa makini, kukutana na kutembea na Yesu!

Katika kilele cha Maadhimisho ya Mwaka wa Imani, Jumamosi jioni tarehe 23 Novemba, 2013, Baba Mtakatifu Francisko kwa furaha kuu aliwapokea waketekumeni 500 kutoka katika nchi 47 walioanza safari ya kujenga Fumbo la Mwili wa Kristo yaani Kanisa kwa njia ya Sakramenti ya Ubatizo. Anasema, Neno wa Mungu alifanyika mwili ili kumkomboa mwanadamu kutoka katika lindi la dhambi na mauti na kwa njia ya Ubatizo, mwamini anakufa na kufufuka pamoja na Kristo tayari kuanza hija ya maisha mapya.

Wakatekumeni hao baada ya kumtafuta Mwenyezi Mungu, sasa wako tayari kuonja huruma na upendo wake katika maisha yao na kwamba,

DOMINIKA 34: Sherehe ya Kristo Mfalme wa Ulimwengu

Ninakuleteeni habari njema ya furaha tunapotafakari pamoja ujumbe wa Neno aliyefanyika mwili, Mfalme wa mbingu na nchi. Ni Dominika ya 34 ya mwaka C iliyo pia sherehe ya Yesu Kristu Mfalme.
Kanisa linashangilia na kusherehekea utukufu wa Mwana wa Mungu, Yesu Kristo Mfalme. Kanisa linatangaza daima utawala na enzi ni vya Yesu Kristu Mfalme na hivi lajiweka chini ya uongozi wake aliye kichwa na mwanga katika safari ya kuelekea mbinguni. Pamoja na tangazo hilo Kanisa latuhimiza kumfuata Yesu Kristu Mfalme, kukiri ukuu wake wazi wazi machoni pa mataifa lililo hasa lengo la sherehe hii.
Mpendwa msikilizaji, ufalme wa Kristo kadiri ya prefasio tunayoitumia katika sherehe hii ni ufalme wa ukweli, maisha, utakatifu, neema, haki, upendo na amani. Basi mwaliko kwetu ni kuyaishi haya na hasa kuyatangaza kwa njia ya ushuhuda na si maneno matupu. Oneni jinsi Bwana anavyoishi hayo mpaka pale msalabani.
Mama Kanisa ameweka sherehe hii mwishoni mwa kipindi cha mwaka ili yote yakamilike katika yeye. Tukirudi kidogo katika historia tunaona kuwa sherehe hii iliwekwa katika Kanisa na Baba Mtakatifu Pio XI mnamo mwaka 1925, Kanisa likitaka kujibu tawala za kisiasa, kipagani na kidikiteta ambazo zilikuwa zikikataa utawala wa Mungu na utawala wa Kanisa.
Mpendwa msikilizaji pamoja na kuzaliwa kwa sherehe hii ya Yesu Kristu Mfalme katika mazingira kama hayo, bado kilichomo ndani ya sherehe hiyo ni cha zamani yaani, tangu mwanzo wa ukristu. Wakristu wa kwanza walikuwa katika maisha yao wakitamka kuwa “Yesu ni Bwana” na kwa namna hiyo wengi wakafa mashahidi katika harakati za kutaka kumtukuza Bwana Mfalme wa mbingu na nchi.
Mpendwa msikilizaji Yesu Kristo Mfalme ndiye yule mchungaji mwema ambaye daima tunakutana naye katika sura 10 ya Injili ya Mt. Yohane ambaye ajua sauti ya kondoo wae na walio wake waijua sauti yake. Kumbe ni mfalme wa amani na mapendo.
Nabii Ezekieli anatupa picha halisi ya mfalme aliye pia mchungaji mwema, aliye kinyume na wafalme wa dunia. Mchungaji wa kondoo anayetabiriwa na Ezekieli ni yule ambaye anatafuta kundi lake lililopotea na kulirudisha katika malisho safi na baadaye kulisalimisha pia nyumbani. Kundi hili la kondoo ni wagonjwa, waliopotea waliovunjika moyo na waliofukuzwa.
Picha hii ya mchungaji inajitokeza katika Yesu Kristu Mfalme ambaye kwa Njia ya Msalaba watu wote wamerudishwa nyumbani. Kumbuka maneno yake alipokuwa akizungumza na Nikodemo “kama vile Musa alivyomwinua juu nyoka wa shaba kule jangwani naye mwana wa mtu atainuliwa juu vivyohivyo ili kila anayemwamini awe na uhai wa milele” Yn 3:14-15
Katika somo la pili Mtume Paulo akiwaandikia Wakorintho anatualika kusadiki kuwa Kristu ndiye limbuko letu. Ndiye ambaye amebatilisha kifo kwa njia ya msalaba wa ushindi kama ambavyo walatini wanasema “regnaviti a ligno Deus”. Anaonesha ufalme na ukuu wake kwa kushinda kifo kilicholetwa duniani kwa njia ya Adamu. Kwa ushindi dhidi ya kifo Mungu amemtukuza na kumwadhimisha mno, na hivi mwishoni mwa dunia utawala wa shetani utashindwa kabisa.
Mtume Paulo hatangazi jambo jingine bali kuwa Yesu Kristu ni Mfalme ambaye Kanisa lamshangilia na kumtukuza kwa shangwe na vigelegele. Sisi wanakanisa tunapaswa kufuata mtililiko huohuo pasipo mashaka tukitangaza ushindi wa Bwana, ambaye ametutoa katika ufalme wa giza na kutupeleka katika ufalme wa mwanae ambao kwao tumepata ukombozi na ondoleo la dhambi.
Mwinjili Mathayo anatuonesha mfalme mwenye mamlaka juu ya mbingu na dunia, mwenye uwezo wa kutoa hukumu kadiri ya upendo na haki. Mfalme huyu ameketi katika kiti cha enzi akiwabagua mataifa yote, wengine mkono wa kulia na wengine mkono wa kushoto. Ndiyo kusema kwanza ana enzi na mamlaka lakini pia ni mwenye haki.
Katika hukumu anayotoa yapo mambo msingi ambayo anayatazama. Kama mmoja aliwalisha maskini au hapana, kama mmoja aliwatazama wagonjwa ambao ni kielelezo cha uwapo wa sauti ya Mungu katikati ya jumuiya ya watu. Kigezo kingine ni kile cha kuwatazama wafungwa kifungoni, walio utumwani na wenye njaa. Kwa wale ambao waliwahudumia wahitaji hawa, atawaambia kaeni mkono wa kulia na mkapate kula vilivyo vya Baba yangu maana nilipokuwa mgonjwa mlikuja kuniona hospitali. (Kumbuka kuwa mtu ni sura na mfano wa Mungu).
Kwa hakika ukitazama vema lengo la ainisho hili la watu mbalimbali waliowahitaji, utagundua nguzo kuu, ambayo humwezesha mmoja kuingia katika ufalme wa Mbinguni, nayo ni MAPENDO KWA JIRANI NA KWA MUNGU. Ni kushuhudia kwa dhati IMANI katoliki, imani tendaji, imani inayokuza ubatizo hadi mwisho wa nyakati. Ni kubaki katika pendo la Mwana wa Mungu katika kuhudumu waliowake.
Mpendwa msikilizaji wa Neno la Mungu, kabla ya kumalizia tafakari yetu yafaa pia kutambua hakikisho la kuwa yeye ni Mfalme kadi ya Injili . Mwinjili Matayo anasema akinukuu maneno ya watesi wa Bwana “Huyu ni mfalme wa Wayahudi” na baadaye yanafuata maneno “Kama wewe ni mfalme wa Wayahudi jiokoe mwenyewe”. Bila kutambua, watesi hawa wakidhani wanammalizia na kumpatiliza Mwana wa Mungu, wanatuhakikishia kuwa yeye ni Mfalme wa Mbingu na nchi na ni mfalme wa Wayahudi. Walitarajia afanye miujiza kuhakikisha ufalme wake na badala yake anachagua msalaba wa wokovu kwa watu.
Mpendwa, katika hilo kumbukeni yule mwizi pale msalabani anayesema “Yesu nikumbuke katika ufalme wako….” Na Bwana wetu Yesu Kristu Mfalme anahitimisha katika kumwokoa mtu akisema tutakuwa pamoja mbinguni. Mpendwa unayenisikiliza je, huyu Mfalme Yesu Kristu anatawala moyoni mwako, je sauti yake “tutakuwa pamoja mbinguni unaisikia?” Je, ndugu yangu mpendwa, unaishi kwa ajili ya Bwana au unaishi kwa ajili yako mwenyewe? Kuishi kwa ajili yako mwenyewe maana yake unacho chanzo chako mwenyewe na mwisho wako mwenyewe! Hicho kwa hakika ni kifo!
Mpendwa msikilizaji, leo hii Mama Kanisa anafunga mwaka wa Imani, mwaka ambao Mama Kanisa kwa njia ya Papa Benedikto wa XVI uliwekwa rasmi ili kwao tuchote fadhila ya imani, tukakuze fadhila hiyo na kisha kuieneza kwa mataifa. Imani ni kusadiki kabisa tukiwa na hakika ya mamb tunayoyatumainia, ni kusadiki kabisa mambo tusiyoyaona. Na kwa namna hayo tunaweza kupata kibali cha Mungu kama wazee wetu wa zamani walivyopata kibali cha Mungu kwa njia ya imani. Papa Francesco anasema imani mwanga ambao upo tangu kuumbwa kwetu na mwanga huo huendelea kukua mpaka mwisho wa nyakati, ni Kristu mwanga wa mataifa.
Katika Barua yake hiyohiyo ya kitume LUMENI FIDEI Papa
Francisko kisha anasema, imani si tu huangazia a mambo ya ndani ya Kanisa, au kutumika tu katika kujenga mji wa milele, lakini pia husaidia kujenga jamii yetu katika njia ya uhakika kwa jamii, kutembea vyema kuelekea mustakabali wa maisha yenye matumaini.
Anaendelea kuangalisha katika manufaa ya familia na jamii , kwamba, kuirejesha imani katika familia, inakuwa ni uwasilishaji wa uwezo wa mwanga, wenye kumulikia mahusiano katika jamii nzima. Ni kuiwezesha familia na jamii kufanya majiundo adilifu na manufaa ya wote. Huanzia katika jamii kutembea katika njia ya udugu, kwenye muono kwamba, sisi sote ni wana wa Baba Mmoja wa mbinguni.

Mpendwa msikilizaji, tunaposherehekea Sherehe ya Mfalme wetu na kufunga mwaka wa imani tukumbuke kuwa yeye anapaswa kutawala katika familia zetu zote, katika maneno yetu na matendo yetu. Maneno kama “ mteja ni mfalme” yafaa kuangaliwa vizuri kama kweli yanakuza ufalme wa Kristu au ufalme wetu sisi wenyewe! Yafaa kuangalia ni huduma gani tumefanya katika Kanisa kwa kipindi cha mwaka wa Imani. Ndiyo kusema hatujachelewa bado twaweza kuanza upya safari ya imani. Kumbukeni Bwana anayemwokoa mtu kwa njia ya msalaba anakutaka na wewe uwe chombo cha amani na upatanisho kama tunda la imani.
Tunawatakieni heri na baraka Waamini wote na zaidi wale ambao parokia zao na makanisa yao yako chini ya somo Yesu Kristo mfalme. Mkashike imani na mkawe mfano wa kuigwa mkiongozwa na Yesu Kristo mfalme wa Amani. Tumsifu Yesu Kristo Mfalme.

Tafakari hii imeletwa kwako na Padre Richard Tiganya C.PP.S.

Maadhimisho ya Mwaka wa Imani

Baba Mtakatifu Francisko anawaambia watumiaji wa mitandao ya kijamii kwamba, Ufalme wa mbinguni ni kwa ajili ya watu wanaojiaminisha kwenye upendo wa Mungu na wala si katika mambo ya kidunia.

Katika kilele cha Mwaka wa Imani, Baba Mtakatifu anatarajiwa, Jumamosi jioni kuongoza Ibada ya kuwapokea Wakatekumeni kama kielelezo cha kuvuka Mlango wa Imani, tayari kumpokea Kristo katika hija ya maisha yao ya Kikristo. Ibada hii inatarajiwa kuhudhuriwa na wakatekumeni kutoka sehemu mbali mbali za dunia kama kielelezo cha Ukatoliki wa Kanisa la Kiulimwengu.

Jumapili asubuhi, kwa mara ya kwanza waamini watapata fursa ya kutolea heshima kwa masalia yanayosadikiwa kuwa ni ya Mtakatifu Petro, Mwamba wa Imani, aliyeyamimina maisha yake kwa ajili ya Kristo na Kanisa lake. Ilikuwa ni Mwaka 1971, Papa Paulo VI alipopewa masalia haya yanayohifadhiwa kwenye Kikanisa cha Papa na kila mwaka ifikapo tarehe 29 Juni, Siku kuu ya Watakatifu Petro na Paulo miamba wa imani masalia haya hupelekwa kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican.

Katika Sherehe ya Kristo Mfalme wa Dunia, Baba Mtakatifu Francisko anatarajiwa kuongoza Ibada ya Misa Takatifu kama kilele cha kufunga Mwaka wa Imani, Ibada inayotarajiwa kuanza saa 4:30 kwa saa za Ulaya. Katika Ibada hii, Baba Mtakatifu atawagawia baadhi ya waamini Waraka wake wa kichungaji baada ya Maadhimisho ya Mwaka wa Imani unaojulikana kama "Furaha ya Injili" "Evangelii Gaudium", itakayozinduliwa rasmi, Jumatatu ijayo hapa mjini Vatican.

REPORT NZIMA KUHUSU UJIO WA ADEN RAGE.

MWENYEKITI wa Simba SC, Ahaj Ismail Aden Rage amewasili Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dares Salaam usiku huu akitokea Sudan na kusema kwamba;

“Mimi bado Mwenyekiti wa Simba SC,”.

Rage aliwasili kwa ndege ya shirika la Kenya saa 1:40 usiku na kutokea mlango wa Watu maalum (VIP) ambako alilakiwa na wanachama zaidi ya 200, waliokuwa kwenye mabasi sita aina ya Coaster.

“Umati huu uliokuja hapa ni kielelezo tosha sana kwamba kiasi gani wanachama wa Simba wana imani na Mwenyekiti wao, sasa leo sitasema mengi, nitakuwa na Mkutano na Waandishi wa Habari kesho saa saba mchana makao makuu ya klabu(Msimbazi),”alisema Rage.

Alipoulizwa kuhusu kikao cha Kamati ya Utendaji kilichofanyika Jumatatu na kutangaza kumsimamisha, Rage alisema;

“Kwa mujibu wa Katiba ya Simba, Kamati ya Utendaji haina uwezo wa kumsimamisha Mwenyekiti, usinimalizie utamu njoo kesho mchana Msimbazi,”alisema.

Watu zaidi ya 200 walifika Uwanja wa ndege tangu saa 11 na ushei jioni ya leo kumsubiri Rage wakiimba nyimbo mbalimbali za kumbeza Kaimu Makamu Mwenyekiti, Joseph Itang’are ‘Kinesi’ na kumpamba Rage huku wakicheza ngoma.

NAFASI KAZI


MONITORING AND EVALUATIONTECHNICAL ADVISOR 
Qualifications: Bachelor’s degree in Epidemiology,Biostatistics,Public health, or a related discipline
Apply: HR@thps.or.tz
Details: The Guardian 15
November 2013
Deadline: 27 November, 2013

DRIVER II  - 2 POSITIONS  
Qualifications: Holder of Secondary Education Certificate with Valid class C driving licence and Trade Test/Advanced Driving Course from a recognised institution with not less than one year experience in driving
Apply: Director General,
Fair Competition Commission
Box  7883,Dar es Salaam
Details: Daily News  11 Nov 2013
Deadline: 29 November, 2013

INFORMATION SYSTEMS AND SERVICES OFFICER II    
Qualifications: Holder of Bachelor’s degree in any of the following fields; Information Sciences and/or Library Studies
Apply: Director General,
Fair Competition Commission
Box  7883,Dar es Salaam
Details: Daily News  11
November 2013
Deadline: 29 November, 2013

COMMERCIAL OFFICER - PETROLEUM 
Qualifications: Bachelor degree in Engineering,Petroleum,
Chemical Processing or Mechanical Economics,Accountancy or Marketing from a recongnised university
Apply: The Director General
Energy and Water Utilities
Regulatory Authority (EWURA)Box  72175,Dar es Salaam
Details: Daily News  11 Nov 2013
Deadline: 22 November, 2013
RECORDS MANAGEMENT
OFFICER II     
Qualifications: Holder of a Bachelor’s degree or Advanced Diploma in Records Management from any recognised university
Apply: Director General,
Fair Competition Commission
Box  7883,Dar es Salaam
Details: Daily News  11 Nov 2013
Deadline: 29 November, 2013

HUMAN RESOURCE AND ADMINISTRATIVE OFFICER II    
Qualifications: Holder of Bachelor’s degree in Public Administration,Human resource or Business Administration -HR from any recognised university
Apply: Director General,
Fair Competition Commission
Box  7883,Dar es Salaam
Details: Daily News  11 Nov 2013
Deadline: 29 November, 2013

WATER QUALITY TECHNICIAN    
Qualifications: FTC/Diploma in Water Laboratory from recognised Technical College
Apply: The Managing Director
Mbeya Urban and Sewerage Authority
Box  2932,Mbeya
Details: Daily News  11 Nov 2013
Deadline: 06 December, 2013


PRINCIPAL  INTERNAL  AUDITOR   
Qualifications: Holder of a degree/Advanced Diploma in Accountancy, possession of a Master’s degree in Finance or Accounting and finance from recognised institution
Apply: The Managing Director
Mbeya Urban and Sewerage Authority
Box  2932,Mbeya
Details: Daily News  11
November 2013
Deadline: 06 December, 2013



SENIOR ENGINEER- RENEWABLE ENERGY   


ELECTRICAL  TECHNICIAN
Qualifications: Form IV/VI  with FTC/Diploma in Electrical Engineering from recognised Technician College
Apply: The Managing Director Moshi Urban WAter Supply and Sanitation Authority (MUWSA)
Box  1001 ,Moshi
Details: Daily News  11
November 2013
Deadline: 29 November, 2013

ASSISTANT  OPERATIONS
MANAGER
Qualifications:  Insurance Diploma or Advanced Diploma from CII or equivalent insurance institute);a Bachelor’s degree from a recognised university will be an added advantage
Apply: General Manager MIC Global Risks Tanzania Ltd
Box  10936, Dar es salaam
Details: The Guardian
October 5,2013
Deadline:  30  November, 2013
PLANNING AND CONSTRUCTION TECHNICIAN 
Qualifications: Diploma/FTC Civil from a reputable and recognised technician College
Apply: The Managing Director Moshi Urban WAter Supply and Sanitation Authority (MUWSA)
Box  1001 ,Moshi
Details: Daily News  11 Nov 2013
Deadline: 29 November, 2013

OPERATIONS & MAINTENANCE ENGINEER 
Qualifications: First degree in Water/Mechanical Environmental/Civil Engineering or equivalent qualifications from a recognised institution
Apply: The Managing Director Moshi Urban WAter Supply and Sanitation Authority (MUWSA)
Box  1001 ,Moshi
Details: Daily News  11 Nov 2013
Deadline: 29 November, 2013

MANAGER SEAFARES AFFAIRS,
TRAINING AND CERTIFICATION
Qualifications: University postgraduate degree in Nautical Science, Maritime safety, Maritime Education and Training, Marine Engineering or Master of Chief Engineer or its equivalent
Apply: Director  General,
Sumatra Head Office
Box 3093 Dar es Salaam
Details: Mwananchi  8 Nov 2013
Deadline: 29 November, 2013

RECEPTIONIST
Qualifications:  Diploma in Secretarial Service from a reputable institute, at least 2-3 years working experience plus relevant academic qualifications
Apply: General Manager MIC Global Risks Tanzania Ltd
Box  10936, Dar es salaam
Details: The Guardian
October 25,2013
Deadline:  30  November, 2013

PERSONAL ASSISTANT/ADMINISTRATOR
Qualifications:  Relevant academic qualifications, at least 2-3 years work experience plus relevant academic qualifications
Apply: General Manager MIC Global Risks Tanzania Ltd
Box  10936, Dar es salaam
Details: The Guardian
October 25,2013
Deadline:  30  November, 2013

ACCOUNT EXECUTIVE - 2 POSITIONS
Qualifications:  Insurance Diploma or Advanced Diploma from CII or equivalent insurance institute); a Bachelor degree holder from a recognised university will be an added advantage
Apply: General Manager MIC Global Risks Tanzania Ltd
Box  10936, Dar es salaam
Details: The Guardian
October 25,2013
Deadline:  30  November, 2013

SENIOR ACCOUNT EXECUTIVE Qualifications:  Insurance Diploma or Advanced Diploma from CII or equivalent insurance institute);a Bachelor’s degree from a recognised university will be an added advantage
Apply: General Manager MIC Global Risks Tanzania Ltd
Box  10936, Dar es salaam
Details:The Guardian
October 25,2013
Deadline:  30  November, 2013


Mtindio wa ubongo: Sababu ya watoto wengi kubaguliwa, kunyanyapaliwa




 
  • Kitaalamu, mtindio wa ubongo unaelezwa kuwa ni hali inayompata mwanadamu kwa ubongo wake kushindwa kufanya kazi katika utaratibu wa kawaida. Kimsingi, ni uwezo wa ubongo kutokukua vizuri na kushindwa kufanya kazi yake katika mazingira yake ya kawaida.

Hata hivyo, utafiti uliofanywa na wanasayansi wa Chuo Kikuu cha Emory cha Atlanta, Marekani katika Kitivo cha Dawa, unabainisha kuwa baadhi ya watoto wenye mtindio wa ubongo wanafundishika.
Inaelezwa pia kwamba, watoto hawa wanaweza kubadilika, iwapo tu watafundishwa kwa makini, utulivu na uvumilivu mkubwa.
Mtu anayemfundisha mtoto wa aina hii hatakiwi kamwe kuwa na hasira, na pia inashauriwa sana kuwapongeza wanapofanya vizuri japo kidogo.
Kejo anasema mwalimu anatakiwa awe mpole na ufundishaji wake usiwe wa haraka haraka, aonyeshe mapenzi kwa mtoto, hapaswi kumkemea hata kama anakosea. “Utakuta mwingine hacheki, au anatoka udenda lakini kama akicheza akili inajitengeneza na inaweza kufikia mate yanakatika na hata kucheka na wakati mwingine hurudi katika hali ya kawaida,” anasema.
Watoto wa aina hii inashauriwa wapewe nafasi ya kujenga urafiki na watoto wenzao wa rika lao.
Awali, watoto wenye matatizo ya akili walikuwa wanatengwa na watoto wenzao katika madarasa, kwa kuwekwa kwenye madarasa maalum.
Siku hizi inashauriwa kuwa watoto hao wachanganywe na wanafunzi wenzao wasio na matatizo ya akili, japo hata kwa nusu siku. Utaratibu huu hujulikana kitaalamu, mainstreaming.
Mbali na hayo, inaelezwa pia kuwa wakati mwingine watoto kabla ya kufikwa na hali hiyo ya ulemavu wa akili, wakati mwingine huzaliwa njiti (premature) ambayo mara nyingi mtoto huwa na udhaifu wa viungo.
Matatizo ya uzazi, na uzazi usio salama hufanya mtoto kuzaliwa kabla ya wakati na hiyo husababisha ulemavu wa akili kwani wakati mwingine ukuaji wa ubongo hauwi katika mazingira ya kawaida.
Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Save the Children, Steve Thorn anasema watoto 210,000 huzaliwa kila mwaka na watoto wa kiume ama hufa au kupata ulemavu kwa kuzaliwa kabla ya wakati.
Anasema kwa mwaka jana pekee, watoto wa kiume njiti 114,000 walizaliwa ikilinganisha watoto wa kike 97,000 na kuongeza idadi ya vifo ama wakati mwingine kupatwa na matatizo ya upofu, uziwi na mtindio wa ubongo.    
Dk Daphne Austin wa Mtandao wa Kamisheni ya Afya ya Jamii Uingereza anasema hana shaka kuwa watoto njiti hukua vizuri hadi kufikia wiki 23, 24 na 25 lakini wengi wao hupatwa na ulemavu wa viungo na ubongo.

Walcott uwanjani J`mosi?

Walcot amekuwa akiigua kwa kwaribu miezi miwili
Theo Walcott huenda akaichezea Arsenal siku ya jumamosi ikiwa kwa mara ya kwanza katika kipindi cha zaidi ya miezi miwili baada ya kupona kutokana na majeruhi ya tumbo.
Walcott yumo katika kikosi cha kupambana na klabu yake ya zamani Southampton siku ya Jumamosi.
Walcott mwenye umri wa miaka 24-aliumia katika pambano la ligi dhidi ya Stoke September 22 baada ya kutegua maumivu aliyopata katika pambano la siku nne zilizotangulia dhidi ya Marseille.
"hajachezea hata kikosi cha akiba lakini nitamjumuisha katika kikos ikamili cha Jumamosi '' alisema kocha Arsene Wenger.
"yuko mzima kabisa."
Awali Wenger alimtumia Serge Gnabry kuchezea nafasi iliyoachwa na Walcott, lakini tangu wakati huo safu yake ya kiungo ilimaarishwa na kurejea kwa Mikel Arteta naJack Wilshere.
"Theo ana sifa tofauti na wachezaji wengine na nimefurahi sana kwamba amerejea" alisema Wenger

P- square Live in Dar, Bwana Arusi Pater Okoye ndani



Embedded image permalink
P-square live jijini Dar es salaam kwa show ya kesho picha ya pamoja na wasaniii wa nchini Tanzania.
Pater Okoye akiwa na Diamond Lagosi, Pater Okoye ndio msanii wa P- square ambaye amepata jiko hivi majuzi naye ndio amekuja Dar kwa show.


Wanamuziki wa kundi la P-Square Peter na Paul baada ya kutua jijini Dar usiku wa kuamkia leo. Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Matina Nkrulu ambao ndio wadhamini wakuu wa onesho lao ambalo limeratibiwa na East Africa Radio na EATV.
 
 Hapa wakifanya mahojiano na kituo cha East Africa TV ambao ndio wenyeji wao.
Mahojiano na picha za hapa na pale zikiendelea.


kupagawisha kesho

Nyota wa muziki wa Nigeria, Peter na Paul Okoye wanaounda Kundi la P-Square wamewasili nchini Tanzania.

Nyota wa muziki wa Nigeria, Peter na Paul Okoye wanaounda Kundi la P-Square wamewasili nchini Tanzania juzi usiku majira ya saa 5 kwa ajili ya kutoa burudani kwa Watanzania na wengine wengi kutoka nchi mbalimbali katika tamasha kubwa linalotarajiwa kufanyika kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar es Salaam kesho.

Kundi hilo la wanamuziki mahiri lilikuja nchini kwa mara ya kwanza 2008 katika tamasha lililofanyika kwenye viwanja hivyo hivyo na kuteka maelfu ya Watanzania walioburudika na kufurahi kwa burudani zao.

Kampuni ya huduma za simu ya Vodacom Tanzania ni moja kati ya wadhamini wakuu wa tamasha hilo linalotarajiwa kuwaleta pamoja wateja wake wote na Watanzania kwa ujumla na kuwapa burudani waliyokuwa wakiisubiri kwa muda mrefu.

Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twissa akizungumzia shoo ya wanamuziki hao wenye mafanikio kutoka nchini Nigeria, alisema hilo ni moja ya matamasha makubwa ya burudani kuwahi kufanyika nchini.

“Ujio huu wa wanamuziki wa Kundi la P-Square ulikuwa ukisubiriwa kwa hamu na wapenda burudani wengi nchini. Siku zote kampuni yetu imekuwa mstari wa mbele kuunga mkono shughuli za michezo na burudani nchini na hivyo kuwa chaguo nambari moja na la pekee kwa wateja wetu.

Tunaahidi kushirikiana na wadau mbalimbali wa burudani kuhakikisha tunawaletea kilicho bora wateja wetu, hakuna asiyefahamu kuwa kundi hili ndilo linaloongoza Afrika kwa kuwa na mialiko mingi duniani kutokana na ubora wake,” alisema Twissa.

Wasanii hao wameletwa nchini kwa ushirikiano mkubwa wa udhamini wa Vodacom Tanzania pamoja na East Africa Radio na TV na watatumbuiza pamoja na nyota kadhaa wa muziki wa Tanzania wakiwamo Profesa Jay, Lady Jaydee Ben Pol na Joh Makini.

Alisema kwa ambao hawajanunua tiketi hadi sasa wanachelewa kwani zitakwisha. Alisema kwa sasa tiketi zinapatikana kwa fedha taslimu Sh.35,000 tu kwenye maduka mbalimbali kila wilaya.

Alisema Kinondoni zinapatikana Engine Petrol Station Mbezi Beach, Image View Tegeta, Puma Petrol Station Mwenge, Samaki Samaki, Photo Point – Mlimani City, Hill Park Restaurant – UDSM, Zizzou Fashion Sinza, Rose Garden Mikocheni, Photo Point Mayfair, Best Bite Namanga, Le Tasi Lounge Coco Beach.

Kwa Ilala, alisema tiketi zinauzwa Steers, Samaki Samaki - Samora, Break Point Bar iliyo jirani na Club Billicanas, Photo Point, Ambassador Lounge - Mkapa Towers, Photo Point Quality Centre.

Temeke tiketi zinauzwa TCC Club Chang’ombe, Dar Live Mbagala, Mafuvu Baby Barber Shop Mtoni, na Kisuma (zamani Sugar Ray).
 Photo: Kumekucha.....# press conference at Hyatt #p square live in DAR



P-square wakiwa mbele wa vyombo vya habari . kwa maojiano zaidi  tayari kwa kazi ya kesho



Ghana , Algeria, Nigeria, Ivory Coast na Cameroon zilee Kombe la Dunia


 Team Algeria celebrate victory over Burkina Faso in their World Cup qualifying match on November 19, 2013 in Blida, Algeria. Algeria sealed the fifth and final African zone World Cup qualifying berth, edging their play-off with Burkina Faso on away goals. Algeria got the goal they needed in the 49th minute through skipper Madjid Bougherra off a goal mouth scramble caused by a free-kick. AFP PHOTO/ Farouk BATICHE

Asamoah Gyan mshambuliaji wa Ghana
Ghana na Algeria jumanne zimeungana na timu za Nigeria, Ivory Coast na Cameroon kukamilisha nchi tano zitakazowakilisha bara la Afrika katika fainali za kombe la dunia nchini Brazil mwaka 2014.
Ghana wakicheza ugenini dhidi ya Misri pamoja na kufungwa magoli 2 - 1 walifanikiwa kufuzu kucheza fainali za kombe la dunia kwa vile katika mechi ya awali Ghana iliifunga Misri magoli 6 - 1

South America delivers again


South America delivers again


Regarded by some of its participants as the toughest and most evenly matched of all the qualifying competitions, the South American Zone lived up to all expectations as five contenders battled their way through to the 2014 FIFA World Cup Brazil™.
Their journey to Brazil was lit up by some stellar individual performances and memorable matches, though the tournament will also remain in the memory for other reasons.

Bikira Maria ni Mama wa Matumaini!

Shamrashamra za kufunga Mwaka wa Imani sanjari na Sherehe za Kristo Mfalme zimeanza kutimua vumbi mjini Vatican baada ya Baba Mtakatifu Francisko. Alhamisi tarehe 21 Novemba 2013 kuwatembelea na kusali pamoja na Wamonaki wa Shirika la Wakamadoli mjini Roma. Baba Mtakatifu aliongoza Ibada ya Masifu ya Jioni na baadaye Askofu mkuu Rino Fisichella aliongoza Ibada ya Kuabudu Ekaristi Takatifu, kama changamoto kwa waamini kumkaribisha Kristo katika hija ya maisha yao ya ndani.

Mihadarati;Wema kunyongwa China,

Akiandika katika ukurasa wake wa Histogram, Wema alisema anachukizwa sana na kitendo hicho, kwani kinamfanya asikae kwa amani na watu walio karibu yake, na wengine wanamtenga kupitia vichwa vya habari tofauti vya magazeti, ambavyo kwa asilimia kubwa anasema vinatumika kuuzia magazeti hayo.
“Hivi karibuni kuna gazeti moja limeandika, ‘Ishu ya dawa za kulevya – Wema kunyongwa China,

Poulsen:Silaha za Chalenji hizi hapa



Kocha wa Kilimanjaro Stars, Mdenmark Kim Poulsen ametaja kikosi chake cha wachezaji 23 watakaoshiriki michuano ya Kombe la Chalenji inayofanyika nchini Kenya kuanzia Novemba 27, mwaka huu

Kilimanjaro Stars iliyotwaa kombe hilo mara ya mwisho 2010 chini ya Kocha Mdenmark, Jan Poulsen, na ambayo imepangwa Kundi B katika michuano ya mwaka huu, itacheza mechi yake ya kwanza Novemba 28, mwaka huu dhidi ya Zambia kwenye Uwanja wa Machakos nje kidogo ya Jiji la Nairobi.

Sinema ya msimbazi:Rage kutua Dar kwa Mbwembwe

Wakati  Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Ismail Aden Rage akitarajiwa kutua nchini tarehe 22/11/2013 jioni, bodi ya wadhamini ya klabu hiyo imetangaza kusitisha maamuzi ya kamati yao ya utendaji ya kumwengua katika nafasi uenyekiti.

Jumanne Kamati ya Utendaji ya Simba iliyokutana Jumatatu bila uwapo kwa mwenyekiti (Rage) aliyekuwa Marekani, ilitangaza kumsimamisha Rage na makocha wa timu yao, Abdallah 'King' Kibadeni na msaidizi wake, Jamhuri Kihwelu 'Julio'.

Kamati hiyo iliamua timu kwa sasa iwe chini ya kocha wa timu ya vijana, Simba B, Seleman Matola  ambaye atakuwa pia Msaidizi wa Kocha Mkuu mpya wa kigeni, Zdravok Logarusic, raia wa Croatia atakayetambulishwa Desemba Mosi, mwaka huu.

DONDOO ZA MAPINDUZI NDANI YA SIMBA

Mapinduzi tata Simba

Aliyekuwa Kocha Mkuu wa Simba, Abdallah Kibaden �King� na msaidizi wake Jamhuri Kihwelu �Julio�
Kamati ya Utendaji ya Klabu ya Simba imefanya mapinduzi yenye utata baada jana kutangaza kumsimamisha kwa muda usiojulikana Mwenyekiti wao, Ismail Aden Rage, lakini uamuzi huo ukionekana kwenda kinyume na Kununi za Shirikisho la Soka nchini, TFF.

Kamati hiyo pia imeamua kuwatimua Kocha Mkuu, Abdallah Kibaden “King” na msaidizi wake Jamhuri Kihwelu ‘Julio’ na kumtangaza Kocha mpya kwamba atakuwa ni raia wa Croatia, Zdravok Logarusic ambaye atasaidiwa na nahodha wa zamani wa timu hiyo ambaye kwa sasa anainoa Simba B, Selemani Matola.

Katiba ya TFF
Hata hivyo, Katiba ya TFF ambayo ndiyo Katiba mama inayopaswa kufuatwa na vyama vya soka na klabu zote zilizo chini ya shirikisho hilo lenye mamlaka ya juu kisoka nchini, hairuhusu mapinduzi na wajumbe wote wa kamati za utendaji wa kuchaguliwa wanatakiwa wakae madarakani kwa muda wa miaka minne.

Ibara ya 31 (6) cha Katiba hiyo kinaeleza kwa tafsiri isiyo rasmi; “Mjumbe wa kamati ya utendaji anaweza kuondolewa baada ya yeye mwenyewe kuandika barua ya kujiondoa, kutohudhuria vikao vinne mfululizo vya kamati ya utendaji, kushindwa kufanya kazi za kamati ya utendaji kutokana na kuugua hadi kufikia hatua ya mgonjwa mahututi ndani ya kipindi cha miezi 12 na kupatikana na hatia ya kutenda kosa la jinai au kufungwa pasi na dhamana.”

Babu Seya sasa kufia jela


Nguza Viking na mtoto wake Papii wakitoka mahakamani
Mahakama ya Rufaa nchini Tanzania imetupilia mbali ombi la warufani wawili Nguza Viking na mwanaye, ambao waliomba mahakama hiyo kufanya marejeo ya uamuzi wake wa awali wa kuwapata na hatia kama ambavyo hukumu dhidi yao ilivyotolewa na mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mwaka 2004.
Nguza Viking, maarufu kama Babu Seya na watoto wake watatu walihukumiwa kifungo cha maisha jela kwa makosa ya kubaka na kulawiti watoto.

Askofu: Mtandao umemuua Mvungi

Aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba,Marehemu Dk. Sengondo Mvungi
Aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dk. Sengondo Mvungi, alizikwa jana katika Kijiji cha Chanjale Juu, Wilaya ya Mwanga, mkoani Kilimanjaro huku Askofu Rogath Kimario wa Kanisa Katoliki Jimbo la Same, akiwaeleza waombolezaji kwamba marehemu amekufa kwa kifo cha fedheha kilichotokana na kile alichokiita mauaji ya kimtandao.

20 wauawa kwa shambulio

Moja ya mashambulio nchini Somalia
Karibu watu ishirini wameuawa katika shambulio la kujitoa mhanga kwenye kituo cha polisi nchini Somalia.
Shambulio hilo limetokea katika mji wa Beledweyne karibu na mpaka na Ethiopia. Mashuhuda wameiambia BBC kuwa gari lilipiga lango kuu la kuingia kwenye jengo la polisi na kulipuka kabla ya watu wenye silaha kushuka na kushambulia jengo hilo kwa risasi. Taarifa zinasema wengi waliofariki katika shambulio hilo ni maafisa wa polisi.

Cameroon yazifuata Nigeria, Ivory Coast


Cameroon imekuwa nchi ya tatu kutoka barani Afrika kufuzu kucheza kombe la dunia nchini Brazil mwaka kesho 2014 baada ya kuifunga Tunisia siku ya jumapili kwa magoli 4 - 1 katika mechi iliyopigwa mjini Younde Cameroon.
Cameroon itashiriki fainali hizo za Kombe la Dunia kwa mara ya sita tangu mashindano hayo yalipoanza ambapo sasa itaungana na Nigeria na Ivory Coast ambazo nazo zimefuzu kushiriki mashindano hayo

Tarehe 24 Novemba 2013 Papa kukabidhi Waraka wa "Furaha ya Injili"

Baba Mtakatifu Francisko katika kilele cha Maadhimisho ya Mwaka wa Imani sanjari na Siku kuu ya Yesu Kristo Mfalme wa Ulimwengu anatarajiwa kuwakabidhi waamini Waraka Mpya wa Kichungaji, "Evangelii Gaudium" Yaani "Furaha ya Injili" kama alama ya kudumu ya Maadhimisho ya Mwaka wa Imani. Ibada ya Misa inatarajiwa kuanza saa 4:30 kwa saa za Ulaya.

Hayo yamesemwa na Askofu mkuu Rino Fisichella, Rais wa Baraza la Kipapa la Uhamasishaji wa Uinjilishaji mpya alipokuwa anazungumza na vyombo vya habari mjini Vatican siku ya Jumatatu, tarehe 18 Novemba 2013. Mkutano huu umehudhuriwa pia na viongozi waandamizi kutoka Baraza hili.

Ufoo Saro: Niliokoka kufa kutokana na miujiza ya Mungu

Mwandishi wa habari wa Kituo cha Televisheni cha ITV, Ufoo Saro akisoma somo kwenye biblia wakati wa ibada maalumu ya shukrani kwenye Kanisa la (KKKT ) Usharika wa Kibamba nje kidogo ya Jiji la Dare Salaam jana. Picha na Sanjito Msafiri.


Baba Mtakatifu atoa dawa ya maisha ya kiroho



Jumapili iliyopita tarehe 17 Novemba 2013 wakati wa Sala ya Malaika wa Bwana, kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro, waamini na mahujaji waliokusanyika ili kuungana na Baba Mtakatifu Francisko kwa Tafakari na Sala ya Mchana, walipewa tiba ya maisha ya kiroho, itakayowasaidia katika kumwilisha mafanikio ya Mwaka wa Imani.

Yatakayojiri wakati wa kufunga Mwaka wa Imani:

Mama Kanisa anajiandaa kufunga rasmi Mwaka wa Imani, uliotangazwa na kuzinduliwa na Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto wa kumi na sita na kuendelezwa kwa ari na moyo mkuu na Papa Francisko hapo tarehe 24 Novemba 2013, wakati wa Sherehe ya Kristo Mfalme. Ibada hii inatarajiwa kuongozwa na Baba Mtakatifu Francisko, kuanzia saa 4:00 asubuhi kwa saa za Ulaya. Maadhimisho ya kufunga Mwaka wa Imani yataanza rasmi kwa

Blessing of a New House


Translated by Most Reverend J. H. Schlarman Bishop of Peoria

Mandela hoi awezi kuongea!

Picha ya kale ya Nelson Mandela na Winnie kabla ya kuachana
Mke wa zamani wa Nelson Mandela, amesema rais huyo wa zamani awezi kuzungumza, lakini anatumia uso kuwasiliana na watu.
Winnie Madikizela-Mandela alieleza kuwa Bwana Mandela, mwenye umri wa miaka 95, ni mgonjwa kweli kweli ,lakini alikanusha tetesi kuwa mashini ndio inamsaidia kupumua.
Mwezi wa Septemba Bwana Mandela alirudi nyumbani baada ya kulazwa hospitali mjini Pretoria kwa karibu miezi mitatu akitibiwa ugonjwa wa mapafu.
Serikali ya Afrika Kusini imesema hali yake bado ni ya kutia wasi-wasi na wakati mwengine hubadilika.

Samatta wawania tuzo Mchezaji bora wa Afrika

Mbwana Samatta  na Victor Wanyama (kulia) 
Shirikisho la kandanda barani Afrika CAF limetangaza majina ya wachezaji wa kiafrika watakaowania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa mwaka 2013 na Mchezaji bora wa Afrika anayechezea vilabu vya ndani ya Afrika mwaka 2013.
Katika majina hayo yapo majina mawili ya wachezaji wanaotoka Afrika Mashariki ambao ni Victor Wanyama raia wa Kenya anachezea

GARAMA ZA MATIBABU KUWA JUU: Bacteria sugu ni tishio kubwa


Dawa za antibiotics zinazouzwa Afghanistan
Tume ya wataalamu wa afya imeonya kuwa aina sugu ya vidudu vya bacteria ni moja kati ya tishio kubwa kabisa katika matibabu.
Katika taarifa iliyoandikwa kwenye jarida la kisayansi, The Lancet, wataalamu wanatoa wito mataifa yashirikiane ili kupambana na tishio hilo.

Taasisi ya Kiislamu yachangia damu salama

TAASISI ya Bilal Muslim Mission of Tanzania imewashauri Watanzania kujitolea damu salama ili kuokoa maisha ya wengi wanaohitaji damu hospitalini.
Ombi hilo limetolewa juzi na Mwenyekiti wa taasisi hiyo, Sibtain Meghji, alipozungumza wakati wa utoaji damu salama, tukio lililofadhiliwa na taasisi hiyo jijini Mwanza.

NDOA: habithi katika Uislamu

Mzee wa miaka 80 alirudi nyumbani kutoka msikitini, akabisha mlango wa nyumba yake lakini hakufunguliwa, akasimama kwa mda mpaka akazirai na kuanguka chini, Mke wake akaona mume wake amechelewa, akafunguwa mlango kwenda kumtafuta, akampata amezirai mbele ya mlango, akamwagia maji mpaka akapata fahamu, mke akamuomba msamaha mume wake kwa kuchelewa kumfungulia mlango kwa kuwa hakusikia mlango ukibishwa na akaona yeye ndie sababu ya mumewe kuzirai..
Mume akamwambia mke wake sikuzirai kwa sababu hiyo bali niliposimama mbele ya mlango wangu na nikaona umefungwa, nikawa nafikiria jee kama ningekuwa nimesimama mbele ya Mlango wa Allah subhanahu wata'ala na Allah subhanahu wata'ala hakunifungulia ningekuwaje?
Katika ile hali ya kufikiria hivyo nikajipata sina fahamu;);););)

St. Hugh of Lincoln

St. Hugh of Lincoln
Hugh of Lincoln was the son of William, Lord of Avalon. He was born at Avalon Castle in Burgundy and was raised and educated at a convent at Villard-Benoit after his mother died when he was eight. He was professed at fifteen, ordained a deacon at nineteen, and was made prior of a monastery at Saint-Maxim. While visiting the Grande Chartreuse with his prior in 1160. It was then he decided to become a Carthusian there and was ordained. After ten years, he was named procurator and in 1175 became Abbot of the first Carthusian monastery in England. This had been built by King Henry II as part of his penance for the murder of Thomas Becket.
His reputation for holiness and sanctity spread all over England and attracted many to the monastery. He admonished Henry for keeping Sees vacant to enrich the royal coffers. Income from the vacant Sees went to the royal treasury. He was then named bishop of the eighteen year old vacant See of Lincoln in 1186 - a post he accepted only when ordered to do so by the

Vijana mnapaswa kuwa ni Wamissionari wa Injili, kila siku na kila mahali!

Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii, kwa namna ya pekee, leo anapenda kuwaalika vijana kuwa ni Wamissionari wa Injili, kila siku na kila sehemu.

Itakumbukwa kwamba, Baba Mtakatifu Francisko amechagua tema zitakazoongoza Maadhimisho ya Siku ya za Vijana Duniani kwa kipindi cha Miaka mitatu,

Tujiepushe kula ovyo kujilinda dhidi ya kisukari

DUNIA leo inaadhimisha Siku ya Kisukari. Ni ukweli usiokuwa na chembe ya shaka kuwa katika miaka ya karibuni ugonjwa wa kisukari umekuwa tishio miongoni mwa mataifa mengi kwani wakati zamani ulionekana kuwaathiri zaidi watu walioishi miaka mingi, sasa hata vijana wadogo na watoto wanaathiriwa na ugonjwa huo.

Vatican: Papa Francis hayuko hatarini


MAKAO Makuu ya Kanisa Katoliki Duniani, yamekanusha vikali uvumi ulioenea kwamba Baba Mtakatifu, Francis, yuko hatarini kwa kuwa kundi la kimafia linamuwinda kumfanyia uhalifu kwa kile kilichoelezwa kuhusu uamuzi wake wa kufanya mageuzi katika kanisa hilo.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari wa Vatican, Frederico Kardinali Lombard, alikiambia kituo cha habari cha ABC kwamba hakuna sababu za wazi zinazoweza kuwafanya kuwa na wasiwasi.

Moro wazitaka neema Tamasha la Krismasi

Wakizungumza kwa nyakati tofauti juzi na jana, wadau hao wameelezea kufurahia kufikiwa na tamasha hilo la kimataifa ambalo litapambwa na waimbaji wa ndani na nje ya Tanzania.
Kwa upande wake, Matata Ndizi, kati ya wadau wakubwa wa muziki wa Injili, alisema angependa kumuona muimbaji Edson Mwasabwite katika tamasha hilo.

Roho yenye udadisi mwingi huwa na mwelekeo wa kujitenga na Mungu- Papa .



(Vatican Radio) Roho ya udadisi mwingi, huzaa hali kutatanikiwa na ghasia na fujo ya kujiweka mbali na Roho wa hekima , ambaye huleta amani, alieleza Papa Francis katika homilia yake wakati wa Misa Alhamisi asubuhi katika kanisa dogo la Mtakatifu Marta .

Papa alitoa homilia yake kwa kutafakari masomo ya siku , ambamo somo la kwanza, lilieleza, hali ya kiroho kwa mwanamme na mwanamke, Wakristo wa kweli , wanaoishi katika hekima ya Roho Mtakatifu. Na hekima hii inayowafanya wasonge mbele kwa busara , utakatifu na dhamira safi.

Tafakari ya neno la Mungu, Jumapili ya 33 ya Kipindi cha Mwaka C wa Kanisa

Tunaendelea kama kawaida katika kipindi chetu, tafakari masomo Dominika, na leo tunatafakari masomo Dominika ya 33 ya mwaka C wa Kanisa.

Tayari tunaelekea kumaliza mwaka wa Kanisa, yaani tukiijongea Dominika ijayo iliyo Dominika ya mwisho ambapo tutasherehekea Sikukuu ya Yesu Kristo Mfalme wa ulimwengu. Masomo yote matatu yanachukua sehemu ya tafakari juu ya mwisho wa dunia, ambayo hasa ndiyo tabia ya Dominika zote za mwisho wa mwaka wa Kanisa. Tabia hii kwa kifupi twaiona katika somo la pili ambapo inaonekana katika jumuiya ya kwanza ya kikristu na hasa kati ya Wakristo wa Thesalonike watu walianza kuacha kufanya kazi wakitarajia ujio wa pili wa Bwana kuwa karibu.

Katika hilo Mtakatifu Paulo anawaonya akiwaambia yakuwa yampasa kila mmoja kufanya kazi, uvivu unaojilaza katika subira ya ujio wa Bwana haukubariki. Katika hili tunaweza kuona pia thamani ya kazi katika maisha ya mwanadamu. Kazi iwayo yote iwe ya mikono au ya kiakili au ya kiroho ni ya maana mbele ya Mungu, aliyesema mkaitiishe nchi.

Mpendwa msikilizaji, kama nilivyokwisha dokeza yakuwa masomo yetu, yatupa hali itakavyokuwa wakati wa mapambazuko ya uzima wa milele, tunakutana na hali hiyo katika lugha inayotisha na pengine yaweza kumfanya mtu aogope, na hasa katika ile hali ya kutarajia maneno ya faraja na huruma. Hata hivyo hali hii ya kutisha ina maana yake na baadaye itawekwa sawa na Mungu mwenyewe. Tunajua hilo kwa sababu kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu hata kama ni zito na kali lakini huwekewa mafuta na kugeuka kuwa Neno na tangazo la matumaini kwa mpokeaji aliyeshiba imani!

Mpendwa msikilizaji, kwa sababu hiyo basi yafaa kutenganisha kati ya maneno au lugha itumikayo na ujumbe ambao Mungu apenda kutupatia. Lugha inayojitokeza katika masomo ya Dominika za mwisho za mwaka ni lugha ya kiufunuo, lugha ambayo tunakutana nayo daima katika kitabu cha Ufunuo. Ni wa namna hiyo basi kila mmoja wetu awe makini katika kupembua ujumbe wa Neno la Mungu, asije akaangukia katika shimo la upotoshaji wa Habari Njema.

Mpendwa msikilizaji, tunasema hili kwa sababu ulimwengu wa leo ambao umejaa fitina, ujangili pamoja na ughaidi unaweza kumfanya mtu badala ya kujenga matumaini na kusonga mbele katika kutafuta amani, basi akaona hakuna haja kwa maana ni mikasa tu ndiyo inayotuzunguka! Kuna baadhi ya wenzetu ambao pasipo kutafakari na kuchekesha vema huibuka na mahubiri vitisho kuhusu mwisho wa dunia na huwajengea watu imani ogopeshi ambayo haizaliwi toka upendo wa Kristu msalabani bali katika vionjo vya watu, imani inayosisitiza hukumu badala ya upendo wa Mungu kwa wanadamu.

Mpendwa mwana wa Mungu, tazama upendo wa Mungu pale msalabani, u-wazi anapomwambia yule mwizi tangu leo utakuwa pamoja nami mbinguni! Bwana hapendi tumwogope bali tumpende, kwa maana hakuna atakayepatilizwa kumbuka anasema “walakini hautapotea hata unywele mmoja wa vichwa vyenu! Inatosha tu pasipo kuogopa kusubiri na katika subira hiyo basi tutaziponyesha nafsi zetu. Upendo wa Mungu haurudi nyuma, jicho alilomtazama Zakayo ndilo hilohilo jicho la milele ambalo atatutazama nasi katika nyakati za mwisho na sasa. Katika hii basi Mungu anatudai kutumaini daima kama ambavyo yeye ni tumaini la kweli.

Kwa nini jambo hili? Jambo hili linakuja katika tafakari kwa maana katika maisha yetu kuna kishawishi kikubwa cha kuacha njia ya Bwana, njia nyembamba, njia ya maisha na kufuata njia pana, njia ya kupoteza, njia ya kifo wakati wa taabu na shida katika maisha yetu ya kila siku. Kumbukeni daima njia ya wokovu ni ndefu, ni siri ya Mungu ambayo hufunuliwa kwa kila mmoja wetu katika tumaini la kweli. Ndiyo kusema nabii Malaki anasema kwenu ninyi mnaolicha jina langu, jua la haki litawazukia lenye kuponya katika mbawa zake. Kumbe siri ya Mungu tunaigundua katika kulicha jina lake na kutumaini wokovu pasipo kusita.

Mpendwa mwana wa Mungu, wanaolicha jina la Mungu ni wale ambao kila siku ya maisha yao hutekeleza nyajibu zao katika familia na mahali pa kazi kwa upendo usiodai faida bali unaolala na kujisimika katika matumaini na upole wa moyo. Katika kujenga tumaini basi ni rahisi yatakapojitokeza matukio ya kutisha tunayoyasikia katika Injili, mwamini kusima na kusonga mbele katika subira pasipo woga na kulicha jina la Bwana.

Hili lina maana ya kwamba tusihangaike kutafuta namna ya ajabu ya kuishi ukristu wetu bali namna ya kawaida iliyojaa mapendo thamini kwa ndugu na jirani kama alivyofanya Msamaria mwema. Tukitenda kile cha kawaida kama Mtakatifu Thereza wa Mtoto Yesu, basi tutakuwa na uhakika wa kujipatia njia nyembamba hata katika mateso tunayokumbana nayo kila siku ya maisha yetu.

Basi mpendwa, tunapoelekea kufunga mwaka wa Kanisa tunaalikwa kuwa na kitu cha kuweka mbele ya Mungu kama tiketi yetu ya kuonana naye, na hivi basi usisahau kabisa yakwamba tumaini lako na imani yako tendaji inayojenga familia ya Mungu ndizo tiketi mwafaka kwa ajili ya sherehe hiyo.

Mpendwa msikilizaji, Baba Mtakatifu Francisko katika barua yake ya Kitume Mwanga wa Imani , anatufundisha kuwa mwanga wa imani unadai kuwekwa katika huduma ya sheria ya haki, na amani, mwanga huo unakuwa ni uwezo unaoongeza nguvu katika mahusiano ya binadamu, na katika kuboresha maisha ya pamoja na mshikamano wa kijamii. Imani inafanya sisi kufahamu usanifu wa mahusiano kati ya binadamu kwa sababu imani huzingatia msingi ya adilifu katika muono wa sheria za Mungu. Na hivyo imani inakuwa huduma kwa manufaa ya wote.


Mpendwa, imani ni zawadi ambayo inadai kutunzwa pia ili isipotee na haipaswi pia kutunzwa tu katika moyo wetu bali lazima ijitokeze nje ili kuweza kushirikisha wengine tumaini la kweli na upendo wa Mungu kwa ajili ya wote. Imani huimarisha wengine na hivi tukaweza sote kuwa tayari kuisubiria siku ya mwisho kwa furaha.

Nikutakie furaha na tumaini la kweli katika Mungu Mkuu, mpaji wa mapaji na zawadi zote za mbinguni. Tumsifu Yesu Kristo.
Tafakari hii imeletwa kwako na Pd Richard Tiganya, C.PP.S.

St. Albert the Great

St. Albert the Great
St. Albert the Great
Feastday: November 15
Patron of Scientists

Albert the Great was one of the Church's greatest intellects. He studied at the University of Padua and later taught at Hildesheim, Freiburg-im-Breisgau, Regensburg, and Strasbourg. He then taught at the University of Paris, where he received his doctorate in 1245. He was among the first and greatest of the natural scientists, gaining a reputation for expertise in biology, chemistry, physics, astronomy, geography, metaphysics, and mathematics. He was also very learned in biblical studies and theology.

Daily Reading for Friday, November 15th, 2013


Reading 1, Wisdom 13:1-9

1 Yes, naturally stupid are all who are unaware of God, and who, from good things seen, have not been able to discover Him-who-is, or, by studying the works, have not recognised the Artificer.
2 Fire, however, or wind, or the swift air, the sphere of the stars, impetuous water, heaven's lamps, are what they have held to be the gods who govern the world.
3 If, charmed by their beauty, they have taken these for gods, let them know how much the Master of these excels them, since he was the very source of beauty that created them.
4 And if they have been impressed by their power and energy, let them deduce from these how much mightier is he that has formed them,
5 since through the grandeur and beauty of the creatures we may, by analogy, contemplate their Author.
6 Small blame, however, attaches to them, for perhaps they go astray only in their search for God and their eagerness to find him;
7 familiar with his works, they investigate them and fall victim to appearances, seeing so much beauty.
8 But even so, they have no excuse:
9 if they are capable of acquiring enough knowledge to be able to investigate the world, how have they been so slow to find its Master?

Responsorial Psalm, Psalms 19:2-3, 4-5

2 day discourses of it to day, night to night hands on the knowledge.
3 No utterance at all, no speech, not a sound to be heard,
4 but from the entire earth the design stands out, this message reaches the whole world. High above, he pitched a tent for the sun,
5 who comes forth from his pavilion like a bridegroom, delights like a champion in the course to be run.

Gospel, Luke 17:26-37

26 'As it was in Noah's day, so will it also be in the days of the Son of man.
27 People were eating and drinking, marrying wives and husbands, right up to the day Noah went into the ark, and the Flood came and destroyed them all.
28 It will be the same as it was in Lot's day: people were eating and drinking, buying and selling, planting and building,
29 but the day Lot left Sodom, it rained fire and brimstone from heaven and it destroyed them all.
30 It will be the same when the day comes for the Son of man to be revealed.
31 'When that Day comes, no one on the housetop, with his possessions in the house, must come down to collect them, nor must anyone in the fields turn back.
32 Remember Lot's wife.
33 Anyone who tries to preserve his life will lose it; and anyone who loses it will keep it safe.
34 I tell you, on that night, when two are in one bed, one will be taken, the other left;
35 when two women are grinding corn together, one will be taken, the other left.'
36
37 The disciples spoke up and asked, 'Where, Lord?' He said, 'Where the body is, there too will the vultures gather.'

Meno ya tembo: Maafisa TRA na Bandari mbaroni...


Meno ya tembo yaliyokamatwa
POLISI nchini Tanzania wamesema shehena ya meno ya tembo yaliyokamatwa katika bandari ya Zanzibar ni sawa na tembo mia tatu na watano, yakiwa na thamani ya karibu shilingini bilioni nane, sawa na karibu dola milioni tano za Kimarekani.
Watu wawili wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuhusika na meno hayo, huku maafisa wawili wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, TRA, na mmoja wa Mamlaka ya Bandari pia wamekamatwa kuhusiana na tukio hilo.